domingo, 27 de dezembro de 2015

FAMILIA TAKATIFU, YESU, MARIA NA YUSUFU


Kutafakari kutoka YbS. 3,2-6, 12-14; Wak 3, 12-21; Lk 2: 41-52


   Tunasherehekea Jumapili ya Familia Takatifu Yesu, Maria na Yosefu. Sikukuu hii inatukumbusha kwanza kuhusu mkutano wa wachungaji na Maria Yusufu, na Mtoto mchanga amelala horini. Hakika kutembelea huku kulisababisha kutafakari kubwa mioyoni mwa Maria. Sikukuu hii inataja pia ushiriki wa familia takatifu katika hekalu ya Yerusalemu. Tukio hili liliwasaidia wazazi wa mtoto Yesu kujua kidogo zaidi kuhusu hazina kubwa ambayo aliwakabidhi Mungu. Hasa kwa upande wa Mama Maria hii ilikuwa nafasi maalum ya kutafakari kuhusu mpango wa Mungu. Hii ni nafasi pia ya kutafakari kusuhu maana ya familia za binadamu na mahitaji ya kuishi thamani nyingi za Familia takatifu ambazo zinampendeza Mungu na kuisaidia jamii.       
        Ushiriki wa Familia takatifu (Yesu, Maria na Yosefu) katika jumuiya yake ni kielelezo/hamasa kwa Ushiriki wetu katika jumuiya/kanisa. Kulingana na andiko hili la Luka ushiriki wa familia hii ulikuwa desturi. Miongoni mwa Wayahudi kila Myahudi anapaswa kwenda Yerusalemu angalau mara moja kwa mwaka kwa sababu ya sherehe ya pasaka pamoja na wengine. Yesu alikuwa kijana wa umri wa miaka kumi na miwili, na ilionekana alipotea hekaluni, lakini kwa kweli yeye alijikuta mwenyewe kwa sababu inampendeza kuhusishwa na kushughulika kuhusu hali ya Baba yake. Hali hii ilikuwa ngumu sana kwa Maria na Yosufu wafahamu. Hasa Mariamu, ingawa hakufahamu hali hii, alikuwa na tabia nzuri ya kuweka moyoni mwake matukio muhimu, akitafakari na kutafsiri ili atende mapenzi ya Mungu. Maria alikuwa makini sana kwa matendo ya Mungu katika historia ya watu wake. Moyo wake ulikuwa makao ya Mungu, mahali pa kwanza, ambapo Yesu alizaliwa. Kwa hivyo haikuwa ngumu sana kwa yeye kuishi ushirika wa ndani na moyo wa mwana wake Yesu.
       Sehemu ya mwisho ya injili hii inasema kwamba Yesu alirudi Nazareti pamoja na wazazi wake na alikuwa akiwatii. Hii ilikuwa njia yake ya kuishi ambayo inampendeza Mungu na ni mfano kwa wanadamu wote. Kuhusu hayo somo la kwanza pia linathibitisha umuhimu wa uhusiano wa ndani kati ya wana wa familia, kufikiria watoto kama baraka kwa wazazi. kuwatii na kuwaheshimu wazazi kunayahusu mapenzi ya Mungu na kunazivutia baraka nyingi kwa familia. Kulingana na Mt Paulo mifano ya Kristo ya utii na upendo lazima kuwa kipimo cha uhusiano kati ya wanandoa kwa sababu thamani hizi zinampendeza Mungu na zinawahamasisha watoto katika safari yao. Familia inampedeza Mungu ambaye, tangu mwanzo, alimpanga binadamu kwa mfano wake, akisema: “Si vizuri huyu mwanamume kuwa peke yake. Nitamfanyia msaidizi wa kumfaa”. Basi Uumbaji wa wanadamu ulikuwa mwaliko kwa kuishi katika familia. Ni mapenzi ya Mungu waweze kuwa pamoja, kupendana na kusaidiana. Kwa nini familia ni muhimu sana? Kwa sababu familia ni msingi wa uzoefu wa binadamu; Kwa sababu pasipo familia uimara wa jamii hauwezekani. Kwa sababu bila familia mawasiliano ya thamani ya jamii kizazi kwa kizazi hayawezekani. Kwa maana uhusiano kati ya wazazi na watoto unawafanya kuwajibika na kukomaa zaidi. Kwa sababu bora kuliko chochote, familia inayaridhisha mahitaji ya hisia na fizikia/mwili, kuwapa watoto utoto salama na imara.
      Yesu anapenda sana kushiriki katika maisha ya familia. Yeye alizaliwa katika familia moja na kutokana na makao ya Nazareti alibariki familia zote za ulimwengu. Uwepo wake ni ufanisi ili familia  zetu zifikie lengo lao kulingana na utambulisho asili. Kumheshimu Maria, mama yake, kunatusaidia kutambua uwepo na matendo ya Mwanawe katika familia ili ishinde hofu, changamoto taabu na majaribio mengi, hasa majaribio ya uzinzi na talaka. Jukumu la Yosefu pia ni chanzo cha msukumo kwa akina baba wote ili wawe ishara za ulinzi na utunzaji wa Mungu, kuzaa hali ya usalama na utulivu katika familia. Uwepo wa Yesu, Maria na Yusufu unaiweka wakfu familia ukiifanya takatifu. Familia ni mahali pa kumcha Mungu; basi, ni mahali patakatifu. Baba Mt Yohane Paulo II alisema kwamba ni lazima kuiokoa familia. Nasi tunaweza kufanya hivyo hasa kwa kuziheshimu na kuzisaidia thamani ambazo zinaishiwa katika familia na zinatufanya binadamu wa kweli.
Fr Ndega

Mapitio: Sara 

SIKUKUU YA KUZALIWA KWAKE BWANA


Kutafakari kuhusu Luka 2, 1-14

Kulingana na liturujia ya siku hii takatifu, ujumbe kuhusu kuzaliwa kwa Yesu ni ujumbe wa furaha kubwa kwa wote, kwa sababu Mwokozi amezaliwa kwa wote. Tufurahi kwa sababu Mungu anatupenda, yeye yupo kati yetu na analeta wokovu kwetu. Wokovu ni kazi ya Mungu, lakini unatendeka duniani na ushiriki wa binadamu. Basi tuchukue Mariamu na Yusufu kama mifano. Katika tukio hilo la ajabu na unyenyekevu wa watu waliohusishwa, Mungu alidhihirisha njia yake yenyewe ya kutenda. Hali hii inathibitisha msemo wa Afrika ambao husema, “watu wanyenyekevu, kufanya vitu rahisi na katika mahali rahisi wana uwezo wa kubadilisha ulimwengu.” Mabadiliko makubwa ambayo jamii yetu inahitaji lazima kutokea ndani ya mwanadamu. Jamii mpya itatokea wakati kila mtu atatambua mahitaji ya kujibadilisha mwenyewe zaidi kuliko ajaribu kubadilisha wengine. Kulingana na Baba Mtakatifu Francisco, “Dunia itabadilika ikiwa tuanze kubadilisha matendo yetu kupitia tabia zetu na chaguzi zetu.” Kwa hiyo, Krismasi ni wakati wa kubadilisha tabia na chaguzi zetu.
Katika Yesu, Mungu amekuwa mmoja wetu, kuchukua hali halisi yetu ya binadamu na kulitoa pendekezo mpya la maisha. Kwa hivyo haitoshi kukiri katika Yesu wokovu wa Mungu; ni muhimu turuhusu kuongozwa na ujumbe wake wa amani na upendo. Kuzaliwa kwa Yesu kuliwabadilisha binadamu wote katika familia kwa njia ya kipekee, kujaza mioyo ya watu kwa furaha na matumaini. Kwa kweli, Mungu anajifunua kama jirani, maskini na anayekataliwa, kualika tutambue thamani ya ishara ndogo na miradi midogo. Bila shaka chaguo hili la Mungu linatuaibisha, kutualika kufikiri na kutenda tofauti. Kupitia udogo Mungu hufanya makuu. Hivyo, Krismasi ni wakati wa kubadilisha mawazo wetu.
Kipengele kingine cha kutafakari kwetu katika usiku huu ni kuhusu wachungaji, waliokuwa watu wa kawaida wadharauliwa katika jamii. Wachungaji walikuwa watu waangalifu ambao walichunga wanyama wao karibu na Bethlehem wakati wa usiku. Walikuwa kweli waangalifu kwa sababu ndani yao hisia kuhusu Mungu na ukaribu wake ulikuwa hai sana. Wachungaji walikuwa watu wa kwanza kuupokea ujumbe mkubwa wa furaha kwa sababu mioyo yao ilikuwa macho. Yeyote tu aliye na moyo makini ana uwezo wa kuamini katika habari njema na kutarajia hali nzuri katika kila alfajiri mpya. Mtu tu aliye na moyo makini ana ujasiri wa kuanza safari kwa kukutana na Mungu katika mahali pasipotarajiwa, yaani katika hali ya mtoto mdogo na mahali maskini sana. Hivyo, Krismasi ni wakati wa kuangalia tofauti ili kuona zaidi na kufanya tofauti katika maisha ya watu wengi.
Mungu Mwenyezi anakubali hali ya mtoto mdogo, katika utegemezi kabisa na utunzaji na upendo wa binadamu. Imani inatuongoza kumtambua mtoto huyu mdogo wa Bethlehemu katika kila mtoto ambaye sisi hukutana katika safari yetu ya kila siku. Kila mtoto anaomba upendo wetu. Tufikiri leo, kwa njia maalum, kuhusu baadhi ya watoto ambao hawana uzoefu wa upendo wa wazazi wao; kuhusu pia watoto wa mitaani ambao hawana mahali pa kuishi; kuhusu watoto ambao wanatumika kama askari, wanaobadilishwa katika vyombo vya vurugu, badala ya kuwa vyombo ya upatanisho na amani; tena kuhusu watoto ambao ni waathirika wa unyanyasaji wa kijinsia, na kuhusu watoto maskini waliolazimishwa kuziacha ndoto zao kwa sababu ya hali mbaya ya kiuchumi. Mtoto mdogo wa Bethlehemu ni mapitio mapya ili tuweze kujitoa ili dhiki ya watoto hawa ikomeshwe. Mwanga wa Bethlehemu uguse mioyo yetu, kuifanya yenye unyeti kwa hali hii. Hivyo, Krismasi ni wakati wa utunzaji na upendo kwa walio na mahitaji mengi.
Ingawa sisi huishi katika jamii ya ulaji ambayo inatuzuia kushughulika kwa thamani muhimu sana, tunapaswa kuwa macho. Krismasi si ulaji. Ni sikukuu ya ufunuo wa Fumbo la upendo wa Mungu unaobadilisha moyo wa binadamu na kuufanya wenye unyeti kwa mapitio ya Mungu. Mungu anatupenda bure na kwa ukarimu, bila astahili kwa upande wetu. Uzoefu huu lazima kutuongoza tufanye vile vile anavyofanya. Kama hii, Krismasi itakuwa zaidi kuliko kipindi kimoja kwa mwaka. Itakuwa Krismasi daima ikiwa tujifunze kupenda kweli na kuweka juhudi zaidi kwa kujenga jamii ya ndugu na haki kwa wema wa wote.

Fr Ndega

Mapitio: Sara

domingo, 20 de dezembro de 2015

UTUMISHI NA UKARIMU WA BIKIRA MARIA


Kutafakari kuhusu 5,2-4; Waebrania 10, 5-10; Luka 1:39-45

      Liturujia ya jumapili hii inatujulisha mtu muhimu sana kama kielelezo cha matayarisho na makaribisho kwa Yule atakayekuja, yaani Bikira Maria. Mkutano wake na dada yake Elizabeti ni alama ya mambo makuu ya Mungu ambaye ana mtazamo maalum kwa hali ya wanyenyekevu na maskini. Kutokana na hali hii alidhihirisha fumbo la mapenzi yake. Anawatumia waliopatikana ili mipango yake yatimize. Katika somo la kwanza nabii Mika anatangaza kuzaliwa kwa mkombozi mmoja kwa Waisraeli atakayetawala milele kwa nguvu za Bwana. Yeye ni mfano wa mwokozi wetu Yesu Kristo aliyekuja kwa ajili ya ulimwengu wote akifanya mapenzi ya Mungu, kulingana na ujumbe wa Waraka kwa Waebrania. Kupitia kujisalimisha kwake mara moja tu tumepata utakaso na wokovu. 
    
     Alipoelewa mpango wa Mungu katika maisha yake Maria alijibu: “Mimi ni mjakazi wa Bwana, nitendewe kulingana na neno lako”. Hili lilikuwa jibu la ajabu la Bikira Maria mbele ya tangazo la Malaika Gabrieli. Wito wa Maria ni maonyesho ya ukarimu wa Mungu. Ukarimu wa Bwana ulihamasisha ukarimu wa mtumishi wake aliyeenda kwa haraka kutembelea dada yake Elisabeti ambaye pia alikuwa amepata mimba na alikaribia kuzaa kwani ilibaki miezi mitatu. Mkutano wa wanawake wawili ni mkutano wa agano, yaani Agano la Kale linalikaribisha Agano Jipya. Kuna pia mkutano wa vizazi, yaani mzee anamkaribisha kijana na kijana anamtumikia mzee. Mpango wa Mungu unajumuisha vizazi vyote na kila kizazi kinaalikwa kuchukua ujumbe wake kulingana na mwendo wake wenyewe. Tukio hili la wanawake hawa wawili linaonyesha njia maalum ya Mungu ya kutenda, dhidi ya matarajio ya binadamu, ni kwamba, mwanamke asiyezaa anakuwa mwenye rutuba na mwanamke bikira anapata mimba kwa njia ya ajabu.

    Maria alitaka kushiriki furaha ya Elizabeti kwa kuwa Mungu alikuwa ameingia katika maisha yake. Elizabeti na Yohana Mbatizaji ambaye alikuwa bado hajazaliwa wanashiriki pia furaha ya Maria na Yesu ambaye hajazaliwa. Wanawake wawili kukutana, watoto wao pia wanakutana. Maria anatukumbusha kwamba ni lazima kuondoka na kuenda kukutana na wengine na kuyatambua matendo ya Mungu maishani mwao. Maria anatusaidia kuamini kwamba matendo makuu ya Mungu katika historia ni ishara ya uaminifu wake. Tunaalikwa kuchukua ahadi ya kuondoka na kuenda kwa wengine kuona walivyobarikiwa na Mungu. Wengi wanangojea kutembelea kwetu na mshikamano wetu. Kwa kufanya hivyo tunahitaji kushinda baadhi ya vikwazo vinavyotuzuia kushirikiana na baadhi ya watu katika jamii au kabila jingine.


      Basi, ni mwenye furaha aliyeamini katika ahadi ya Mungu, kwa maana Yule anayeahidi ni mwaminifu. Imani inakuwa kigezo/kipimo cha msingi wa furaha. Maria anakuwa ishara ya ubinadamu mpya, uliobadilishwa na kuokolewa na Mwanae. Maria ni mmoja wetu ambaye alijihisi aliyeangaliwa kwa huruma na akaishi kwa shukrani. Aliyeangaliwa kwa huruma kwa sababu Mungu alitenda makuu maishani mwake. Yeye aliishi kwa shukrani kwa sababu aliyapatikana maisha yake ili, kupitia jibu lake, Mungu atende makuu maishani mwa watu hasa maskini. Kwa kiwangu kidogo sisi pia tunapitia tabia hizi, ni kwamba, tumeangaliwa kwa huruma kupitia zawadi kubwa ya wito. Tabia ya shukrani ndani yetu inaonyeshwa nje kupitia utumishi kwa furaha na ukarimu. Hali ya kuwa walioangaliwa kwa huruma haitutegemei sisi, bali inamtegemea Mungu ambaye anatujalia baraka nyingi; hali ya kuwa kama walio na shukrani inatutegemea sisi peke yetu. Mbele ya majaribio ya kufa moyo au kukata tamaa Maria ni kielelezo kwetu kwa upatikanaji kabisa kwa mipango ya Mungu. Kama yeye tunaalikwa pia kuishi kama wamebarikiwa na kumchukwa Yesu kwa wengine katika mahali po pote tuendako.   

Fr Ndega
Mapitio: Sara

quinta-feira, 17 de dezembro de 2015

MUNGU ALICHUKUA BINAFSI HISTORIA YA WATU WAKE


Kutafakari kutoka Mt 1, 1-17

Kutokana na siku hii ya leo tunalianza juma maalum katika maandalizi yetu ya Krismasi. Kwa hivyo injili inatuletea ukoo wa Yesu. Majina haya mengi yaliyojulishwa na Mathayo yanatusaidia kufahamu mwelekeo wa binadamu wa Mwana wa Mungu. Ni ushahidi kwamba Yesu hakuonekana ghafla wala ni mgeni katika historia ya binadamu, bali tukio lake lilitokea polepole, hatua kwa hatua na kwa muda mrefu. Mungu aliwaandaa watu wake kwa uvumilivu kupitia Mwana wake ili historia hii ilikuwe na uwezo wa kumpokea katika wakati muafaka. Yesu Kristo anakamilisha ahadi aliyoitoa Mungu katika Agano la Kale. Kwa sababu hii, Yesu anatambulishwa kuwa ni mwana wa Mfalme Daudi na pia mzao wa Abrahamu. Mathayo anatumia mifano mingi kutoka katika unabii uliotolewa na manabii wa Agano la Kale, kueleza maisha ya Yesu ambaye alikuja kuwa Mwokozi wa Wayahudi (huu ni ufahamu wa kwanza kuhusu utume wake). Lakini mpango na lengo la Maandiko Matakatifu ni kuwasaidia watu kufahamu ufundishaji wa Mungu mwenyewe ambaye anatumia watu fulani kwa kufikia wote. Kama hii Mwanao hakutumiwa ili awe mali ya Wayahudi, bali Mwokozi wa ulimwengu wote.
Kwa nini yeye ni Mwokozi wa ulimwengu wote? Ni muhimu sana kujipatia nia ya Mungu kuhusu ubinadamu tangu uumbaji. Kwanza kabisa ulikuwa uamuzi wa Mungu kumwumba binadamu kushiriki naye uzima wake mwenyewe. Upinzani asili kupitia dhambi haukumzuia Mungu kuendelea mpango wake. Na, halafu aliamua kumwokoa binadamu mpotevu. Mungu mwenyewe aliwaandaa watu wake kwa muda mrefu akiifanya historia yao kuwa historia ya wokovu. Kwa sababu ya nia na matendo ya Mungu hatuwezi kuongelea historia mbili, bali historia ya Mungu na binadamu, yaani Historia ya wokovu. Mungu anamtafuta binadamu kumpa uzima wa milele ambao ni uhai wake mwenyewe. Historia hii inatokea polepole kati ya mwanga na vivuli. Kizazi cha Daudi kinaitwa kizazi cha mwanga kwa sababu ya mwelekeo wake kuelekea kwa Yesu. Kizazi cha utumwa wa Babeli kinafikiriwa kizazi cha vivuli kwa sababu upinzani wa watu dhidi ya mwongozo wa Mungu uliwazuia kuishi kama Watu wa Mungu. 

Tunaweza kuongelea njia maalum ya kuingia katika historia ya binadamu. Mungu anaingia katika maisha ya watu kwa wakati halisi. Yeye aliongea kwa namna mbalimbali kupitia manabii na mababu zetu ya zamani na siku hizi anaongea kupitia Mwanae mwenyewe. Yeye huongea kila wakati, lakini  haongei hewani bali hupitia katika matukio mazuri au mabaya  katika historia ya watu. Mungu alijifanya mmoja wetu na bado yuko nasi kwa namna mbali mbali. Kwa kivyo hakuna tukio lolote la historia lisilokuwa na maana. Angeweza kufanya kila kitu peke yake bali hakutaka. Alichagua Maria, Yosefu, Yohane na viongozi wengi kama washirika, akiingia katika historia kwa namna ya pekee na inabidi watu watayarishwe kumkaribisha Masiya wake kwa wakati wote. Sisi ni sehemu ya mwendo huu na kualikwa kumsaidia Mungu kwa mafanikio ya mipango yake kwa ubinadamu wote. Tumshukuru Mungu kwa matendo yake makuu katika historia yetu na kwa wito wetu kama washirika wake.

Fr Ndega
Mapitio: Sara

MAANA YA UWEZO WA YOHANA WA KUWATHIBITISHIA WASIKILIZAJI WAKE


Kutafakari kuhusu Sef 3, 14-18; Wap 4, 4-7; Lk 3, 10-18

       Liturujia ya jumapili hii tatu inaleta mwaliko kwa furaha kwa sababu ya ukaribu wa ujio wa Bwana wetu. Hali hii tunaweza kutambua kupitia ujumbe wa nabii Sefania ambaye waliwahamasisha waisraeli wafurahi na kumshangilia Mungu mfalme wao. Maana ya furaha kubwa ni kwa sababu uwepo wa Mungu katikati yao ulileta ukombozi ukidhamini usalama na ulinzi dhidi ya maadui yao. Ujumbe wa furaha unaendelea pia kupitia waraka wa Paulo kwa Wafilipi kwa sababu Mungu yu karibu na neno lake ni alama ya ukaribu wake. Ukaribu wa Mungu ni uwepo wake kwa wakati sawa na uwepo wake ni ufanisi, yaani ni nafasi ya wokovu.
        Kuhusu injili tuna vipengele vingi kwa kutafakari kwetu. Andiko hili ni mwendelezo wa injili ya jumapili iliyopita. Luka anaendelea kueleza kuhusu kazi ya Yohane Mbatizaji na kipengele cha kwanza ni kuhusu uwezo wa Yohana wa kuwathibitishia wasikilizaji wake. Kama ilitokea na manabii wa zamani, tunaamini kwamba uwezo huu unatokana na uzoefu wa kweli wa Neno la Mungu. Yohane alifikiwa na Neno la Mungu jangwani. Yeye aliishi katika upweke wa jangwa, aliyefunguliwa kabisa kwa msukumo wa Mungu. Alijifunza kutokana na Neno la Mungu jinsi ya kuwa shahidi wa habari njema ya wokovu. Miongoni mwa wasikilijazi wa Yohane, Luka anawataja watoza ushuru na askari ambao walitaka kubatizwa. Hasa watoza ushuru walichukiwa na Wayahudi wenzao kwa sababu walikuwa washirika wa Roma. Wakati wa Yesu, watoza ushuru waliwekwa katika kundi maalum la wenye dhambi. Kuchanganyika nao kulimfanya mtu apate dhambi yao pia. Yesu alichanganyika nao, akivuka mipaka iliyowekwa na watu. Kikundi hiki pamoja na askari walitambua ukweli wa hali yao na hivyo wakaomba msamaha. Lakini nia njema pekee haitoshi. Yohane anawataka watende haki.  Kwa hivyo aliwaalika washiriki mali yao.
       Ukuu wa Yohane Mbatizaji ulikuwa kutambua ukuu wa Bwana, akijifikiria mwenyewe kama sauti tu na asiyestahili kuulegeza ukanda wa viatu vyake. Yesu mwenyewe alitambua ukuu wa Yohane akiweka unyenyekevu wake kama rejea. Hatuhitaji kumlinganisha Yesu na Yohane Mbatizaji ili tugundue ni nani kati yao ni mtu mkuu. Bila shaka Yesu ni mkubwa zaidi kuliko Yohane. Lakini ni vizuri sana kutambua uhusiano huu wa ajabu kati ya wote wawili. Ikiwa Yohane anaongea kuhusu Yesu anamsifu; ikiwa Yesu anaongea kuhusu Yohana anafanya vivyo hivyo. Tunahitaji kujifunza sana kutokana na uhusiano huu, kwa manufaa ya Kanisa na kwa wema wa uhusiano wetu kama wakristo, watumishi wa mwili wa Bwana.
         Basi, ni kazi ya Yohane kutangaza mwisho wa wakati wa kumgojea Masiya na mwanzo wa historia mpya, ambayo ilifanywa na watu wapya waliofanywa upya katika Roho wa Kristo. Kama huu ni uzoefu wa ubatizo. Lakini ni lazima kukumbuka baadhi ya tofauti kati ya ubatizo uliotolewa na Yohane na ule atakaotoa Masiya. Yohana aliwabatiza watu kwa maji kama kielelezo cha kugeuka kwao. Uzoefu huu ulikuwa hatua muhimu, bali haikufikia mabadiliko kamili ya ndani. Ubatizo wa Roho Mtakatifu na moto una nguvu ya kufanya mabadiliko kwa sababu unamfanya mtu kuzaliwa katika familia ya Mungu. Alama yetu kama watoto wa Mungu haiwezi kufutika. Hii ni chapa ya ubatizo wetu. Ipo daima!

        Wakati wa Yohane Mbatizaji unaomhusu Kristo ni mwendelezo, lakini unaushinda wakati wa maandalizi wa zamani. Huu ni wakati wa kutangaza kuhusu mahitaji ya kumkaribisha Bwana aliyetaka kukutana na binadamu. Basi kwa upande wa Mungu, mwendo wa mkutano uko tayari. Kwa upande wa binadamu ni lazima imani na kukubalika kwa uhuru na binafsi. Ikiwa ukuu wa Yohana ulikuwa kutambua ukuu wa Bwana, ukuu wa kila mtu katika ufalme wa Mungu ni kuyakubali mapendekezo ya Yesu na kuzifuata nyayo zake. Kielelezo cha Yohane kiwe daima rejea kwa safari yetu ya kukubalika kwa mipango ya Mungu na kuutangaza wakati wa kutembelea kwake kwetu daima. 

Fr Ndega

terça-feira, 8 de dezembro de 2015

RESULT OF THE TRUE EXPERIENCE OF THE WORD OF GOD


Reflection from Bar 5, 1-9; Phil 1: 3-6, 8-11; Lk 3, 1-6


     The liturgy of this Sunday continues inviting us to welcome the Lord who is coming to bring salvation to us. It is necessary to prepare ourselves in order we can receive the Messiah in any time. The Advent season helps us to recognise that the right preparation needs transformation total of the heart. The words of the prophet Baruch motivated the people in the Babylon’s exile, proclaiming the nearness of their liberation. After all that sufferings they could go back home Jerusalem with great joy because God remembered them and guided them in his light and glory. Paul recognises that the faith and communion of the Philippians are extension of the gospel which they received with enthusiasm and willingness. Through Jesus Christ and his gospel they can bear good fruits for the glory and honour of God.     
      The gospel speaks about John the Baptist whom was reached by the Word of God in the desert. In the bible, the desert is special place for the experience of the Word of God’s. In that place many people were transformed in strong leaders in order to lead the People of God according to his guidelines. John the Baptist is considered the last and the greatest of all prophets. The Luke’s version mentions priests and politics leaders in order to show that through his messenger, God enters in the concrete life of the people in a specific time. God doesn’t speak in the ear, but through good and bad events in the history of the people. God made himself one of us and continues with us in different ways. For that there is no event in the history without meaning. In order to show the vocation of John in the events of his time, Luke shows that the greatest event was very near. God enters in the history with very particular way and requests that the people should be prepared to welcome the Messiah whom was expected for long time.
The coming of John the Baptist has a great meaning and follows the plan of God who has right time for everything. His Word transforms the life of John in instrument of salvation. As John is link between the Old and the New Testaments, his mission announces that the time of the Messiah is near to start. He is only the voice which prepares the ways of the Lord. John prepared the people to receive the Messiah using the baptism. Through this sign he proclaimed the mercy of God available for each person because it is plan of God that his salvation should reach all. So, the gesture of John was condition to pass from life of sin and dearth to grace and the new life of God. Important aspect in this action of John is that he baptized those who were in need of the mercy of God and repented their sins. John and that people believed that it is God whom forgives their sins.   
The Baptism of John is different of ours, but both are opportunity to live new life. For us Christians the new life is gift of Christ and result of his mission. The Christian baptism, besides the forgiveness of sins, guarantees participation in the life of the own God. The baptism is the first of the three sacraments of initiation followed by Chrism and Eucharist. Our baptism is external sign of the death to life of sins and sign also of the resurrection in Christ who is victorious against the sin and the dearth. He is the true light which enlightens each person. Through this process we become sons and daughters of the light in order to walk in the light of God each day of our life.

The Advent season helps us to prepare ourselves to celebrate the birth of Jesus. While the world of business advice the people to prepare themselves to Father Christmas buying something, Advent season proposes inner spiritual preparation and the effort for reconciliation with God and others. There are obstacles to remove with the help of the forgiveness of God. For that let us assume this good time to celebrate the sacrament of Reconciliation and to live in new way the relationship with God and others. 

Fr Ndega

MATOKEO YA UZOEFU WA KWELI WA NENO LA MUNGU


Kutafakari kuhusu Bar 5, 1-9; Wafil 1: 3-6, 8-11; Lk 3, 1-6

      Liturujia ya jumapili hii inaendelea kutumwalika kumkaribisha Bwana anayekuja kutuletea wokovu. Tunapaswa kujiandaa vizuri ili tuweze kumpokee Masiya wakati wowote. Wakati wa Majilio unatusaidia kutambua kwamba kwa matayarisho kamili ni lazima mabadiliko ya moyo, kwa njia mpya kabisa.  Maneno ya nabii Baruku yalihamasisha watu utumwani Babeli yakitangaza ukombozi karibu. Baada ya mateso hayo yote wataweza kurudi nyumbani Yerusalemu kwa furaha kubwa kwa sababu Mungu aliwakumbuka na kuwaongoza katika mwangaza na utukufu wake. Huu ni mfano wa wokovu wetu katika Kristo. Paulo anatambua kwamba imani na ushirika wa Wafilipi ni uenezi wa injili waliyochukua kwa shauku na utayari. Kwa njia ya Kristo na injili yake wanaweza kuzaa mazao mazuri kwa utukufu na sifa ya Mungu.  

       Injili inaongelea Yohane Mbatizaji anayefikiwa na Neno la Mungu jangwani. Katika biblia jangwa ni mahali maalum kwa uzoefu wa Neno la Mungu. Katika mahali huko watu wengi walijibadilisha kuwa viongozi wenye nguvu kwa kuwaongoza Watu wa Mungu kulingana na mwongozo wake. Yohane Mbatizaji anafikiriwa kuwa nabii wa mwisho na mkuu wa manabii wote. Toleo la Luka linataja makuhani na viongozi wa kisiasa ili kuonyesha kwamba kupitia mjumbe wake, Mungu huingia katika maisha halisi ya watu kwa wakati fulani. Mungu haongei hewani bali hupitia katika matukio mazuri au mabaya  katika historia ya watu. Mungu alijifanya mmoja wetu na bado yuko nasi kwa namna mbali mbali. Kwa kiyo hakuna tukio lolote la historia lisilokuwa na maana. Kwa kuonyesha wito wa Yohane katika matukio ya wakati wake, Luka anaonyesha kwamba tukio kubwa liko karibu. Mungu anaingia katika historia kwa namna ya pekee na inabidi watu watayarishwe kumkaribisha Masiya aliyetarajiwa kwa muda mrefu.

Kuja kwake Yohane Mbatizaji kuna maana na kuufuata mpango wa Mungu ambaye ana wakati kamili kwa kila kitu. Neno lake linayabadilisha maisha ya Yohane katika chombo cha wokovu. Kama Yohane ni kiungo kati ya Agano la kale na Jipya, kazi yake inatangaza kwamba nyakati za Masiya ziko karibu kuanza. Yeye ni sauti tu ambayo inatayarisha njia za Bwana. Yohane aliwatayarisha watu kumpokea Masiya kwa ubatizo. Kupitia ishara hii alitangaza huruma ya Mungu iliyopatikana kwa kila mtu kwa sababu ni mpango wa Mungu kwamba wokovu wake ufikie wote. Basi ishara ya Yohane ilikuwa kielelezo cha kupita kutoka katika dhambi na mauti kwenda katika neema na maisha mapya ya Mungu. Kipengele muhimu katika tendo hili la Yohana ni kwamba aliwabatiza wale waliomhitaji Mungu na kutubu dhambi zao. Yohane na watu hao waliamini kwamba ni Mungu anayesamehe dhambi zao.

Ubatizo wa yohane ni tofauti na ubatizo wetu, lakini yote mbili ni nafasi ya kuishi maisha mapya. Kwa upande wetu maisha mapya ni zawadi ya Kristo na matokeo ya utume wake. Ubatizo wa kikristo, pamoja na maondoleo ya dhambi, unadhamini ushiriki katika uzima wa Mungu mwenyewe. Ubatizo ni wa kwanza katika sakramenti tatu za mwanzo ukifuatiwa na Kipaimara na Ekaristi. Ubatizo wetu ni alama ya nje ya kufa katika dhambi, na pia ni ishara ya ufufuko wa maisha mapya katika Kristo aliye mshindi dhidi ya dhambi na mauti. Yeye ni mwanga wa kweli ambao unamtia nuru kila mtu. Kupitia mwendo huu tumekuwa wana wa nuru ili tutembee katika nuru ya Mungu kila siku ya maisha yetu.


Kipindi cha Majilio kinatusaidia kujiandaa kusherehekea kuzaliwa kwa Yesu. Wakati ulimwengu wa biashara unashauri watu wajiandae kwa Noeli kwa kununua vitu, kipindi cha Majilio kinatupendekezea matayarisho ya ndani kiroho, na hamu ya kutaka kutupatanishwa na Mungu na wenzetu. Kuna vikwazo vya kuondoa katika maisha yetu kwa msaada wa neema ya msamaha wa Mungu. Kwa hivyo tuchukue wakati mzuri huu kuadhimisha msamaha wa Mungu kwa sacramenti ya Upatanisho na kuishi kwa njia mpya uhusiano wetu na Mungu na wengine.


Fr Ndega
Mapitio: Sara

domingo, 29 de novembro de 2015

KUWA MACHO KWA KUJA KWAKE MWANA WA MTU


Kutafakari kuhusu Lk 21, 25-28, 34-36

   Tumeanza wakati mpya katika liturujia ya kanisa uitwao Majilio. Wakati huu unayahamasisha matumaini yetu katika matarajio ya Kuja kwake Bwana mara ya pili katika mwisho wa nyakati na unakumbuka pia Kuja kwake kwa kwanza, kutuandaa tusherehekee sikukuu ya kuzaliwa kwake katika Krismasi. Basi, Liturujia ya msimu huu ni mwaliko kwa kukesha ili tutambue na kuzikaribisha ishara za uwepo wa Bwana katika hali yetu ya kila siku. Ni mwaliko pia kwa shukrani kwa sababu Bwana anakuja daima kukutana na sisi, kutupa wokovu wake. Matukio yote makuu yanahitaji maandalizi mazuri ili yaweze kusherehekewa vizuri. Kama hii ni Majilio kwa uhusiano na tukio kubwa la Krismasi.

         Mwanzoni mwa sura ya kumi na tatu ya injili ya Luka Yesu anaongea kuhusu uharibifu wa Yerusalemu. Ufunuo huu uliwahamasisha baadhi ya wanafunzi wake wamwulize swali kuhusu ishara gani, siku na saa gani ya uharibifu huu. Yesu anatumia nafasi hii kutabiri kuhusu mambo mengi akiiandaa mioyo ya wafuasi wake kwa wakati ujao. Aliwaambia kuhusu ishara nyingi mbinguni, taabu, mateso, dhiki kuu na kuja kwake, kulingana na unabii wa Danieli, yaani, juu ya mawingu ya angani mwenye nguvu na utukufu mwingi. Kanisa katoliki hutafsiri tukio hili kama kuja kwake Yesu mara ya Pili ili kuwahukumu wazima na wafu. Hiyo ndiyo imani yetu ambayo sisi hutangaza kila jumapili. Kuhusu siku na saa hii hakuna mtu ajuaye. Hii ni sehemu ya mpango wa hekima na wema wa Baba. Kwa hivyo huu ni pia mwaliko kwa kukesha.

        Ingawa uharibifu wa mji wa Yerusalemu ulitokea katika mwaka wa 70 B.K., nia ya Yesu haikuwa kuwajulisha kuhusu tukio hili, bali kuhusu matokeo ya tukio hili katika maisha ya wafuasi wake. Alitabiri kwamba “nguvu za mbingu zitatikiswa” akifikiria imani na ushuhuda wa wanafunzi wake kama nguvu za mbingu zipo ulimwenguni. Wanafunzi wa Yesu wataishi kipindi cha machafuko na watajaribiwa kuiacha imani katika Kristo na kukata tamaa kuhusu utambulisho wao wa wanafunzi kwa sababu ya matusi, majaribio, matatizo na mateso mengi. Ilionekana kwamba walikuwa peke yao mbele ya machafuko hayo yote. Lakini Yesu mwenyewe alikuwa amewaahidi uwepo wake daima kupitia maneno haya, “mimi nipo pamoja nanyi sikuzote, hata ukamiliifu wa dahari.” Maneno haya ni mwaliko kwa ushuhuda na kusali kama njia ya kukesha. Hao wana jukumu la kuendelea utume wa Mwalimu, wakiwa makini kwa ishara za kuja kwake ili akutane nao na kuwatuza kwa maana ya uaminifu wao.

Andiko hili linatuambia kwamba Kristo ni mshindi na ujio wake unaanzisha wakati mpya anaoshiriki na wanafunzi wote wanaobaki wamesimama na kuinua vichwa vyao kupitia imani na ushuhuda kwa uaminifu. Tunapaswa kuishi imani yetu ya kikristo kwa uhusiano na kila kitu ambacho kinatokea kandokando yetu. Jamii inatarajia imani yenye maana na iwe jibu kwa hali iliyopo na binadamu anayoiishi. Je, imani yetu ni gani? “Je, tena wakristo wanapaswa kuwa na tabia gani wakati wa mazingira magumu? Kama aliwaambia wafuasi wake wa zamani, Yesu anatuhakikishia kuwa mazingira magumu ni sehemu ya safari ya wale ambao wanamfuata katika nyakati zote, lakini Yeye anatukumbusha pia kwamba ni katika machafuko haya ya dunia hii tunapojiandaa kukutana naye mwishoni mwa maisha yetu binafsi hapa duniani. Kwa hivyo kila hatua ya safari yetu ni maandalizi kwa mkutano wa mwisho na Bwana wetu.


         Liturjia linataka kuimarisha imani yetu na kufufua tumaini letu kwa tendo la wokovu wa Mungu ndiye mkuu katika nyakati zote, zilizopita na zijazo. Hali hii inatualika kuishi wito wetu wa wafuasi kwa uaminifu katika nyakati zote pia, hata wakati wa mateso makali. Baada ya machafuko yote tutakuwa washindi pamoja na Bwana wetu mshindi. Kulingana na mithali fulani, “hakuna usiku hata wa muda mrefu pasipo mapambazuko”. Basi, kwa wale wanaomfuata Kristo, mazingira magumu si ishara za mwisho wa nyakati bali ni wakati mpya, wakati wa kuishi wito wetu kwa shauku zaidi, furaha na tumaini, kuushuhudia kwa uaminifu uwepo wa Bwana miongoni mwetu. Anakuja kwa upendo na kutuokoa. Tukaribishe ishara za nyakati kama msaada tutambue uwepo wa Bwana na kuishi mafundisho yake kwa njia mpya.

Fr Ndega
Mapitio: Sara

quarta-feira, 25 de novembro de 2015

UFALME WA YESU NI TOFAUTI KABISA


Kutafakari kuhusu Yoh 18, 33-37

            Tunasherehekea sikuku ya Bwana Wetu Yesu Kristu Mfalme. Yeye ni Mfalme wa mbingu na dunia; enzi na utawala wote ni wake. Liturjia hii inatualika kumfuata Mfalme huyo ambaye ni njia, ukweli na uzima. Kuutafuta kwanza ufalme wake ni maana ya kweli ya maisha yetu.

Mbele ya Pilato, Yesu hakukanusha juu ya ufalme wake,  bali anafafanua zaidi maana ya ufalme huo. Swali la Pilato kwa Yesu ya kwamba: “Wewe ni Mfalme wa Wayahudi?”, lilikuwa limewaza kuwa Yesu alikuwa mmoja wa wazalendo ambaye alitaka kuupindua utawala wa Roma na kuanzisha utawala mpya wa kisiasa kwa wayahudi. Wayahudi wengine walitumaini kuwa Masiha angewarudishia tena utawala wa Daudi. Wote, Pilato na Wayahudi, wana wazo ambalo sio kamili kuhusu ufalme wa mbinguni na kuhusu pia Yule aliyechaguliwa na Mungu adhihirishe ufalme huu. Yesu anakubali kuwa yeye ni mfalme, lakini siyo mfalme wa wayahudi tu. Yeye ni Mfalme wa wote na Ufalme wake ni tofauti. Kumbe ufalme wa Yesu si wa dunia hii lakini unawahusu wote waishio hapa duniani.

      Ufalme ni mapenzi ya Mungu ambayo Yesu aliishi na ufalme huu ni pia hali mpya aliyoanzisha ulimwenguni. Uwepo wake unaanzisha wakati mpya, yaani, wakati wa wokovu wa Mungu. Msingi wa ujumbe wa Yesu ni tangazo la wokovu wa Mungu ambalo ni sawa na tangazo la ufalme pia. Kwa kweli Yesu hajitangazi mwenyewe, bali anautangaza Ufalme. Katika Yesu mwenywe ufalme ulikuwa hali halisi ukisababisha mabadiliko ulimwenguni kwa wema wa wote hasa kwa walio na mahitaji mengi, yaani, wagonjwa wanapona, bubu wanaongea tena, vipofu wanapata kuona tena, maskini wanaipokea habari njema na wenye dhambi wanaondolewa dhambi zao. Kuna wengi ambao wanalitambua tendo la wokovu wa Mungu katika ishara za ukombozi za Yesu na wanajiruhusu kubadilishwa, lakini kuna wengine pia ambao wanajifunga wenyewe na hawawezi kutambua kile ambacho kinatokea kandokando yao. Upinzani dhidi ya Yesu ni upinzani dhidi ya mafanikio ya Ufalme wa Mungu. Katika maana hii ni ngumu sana kumfuata nyayo zake na kutangaza ufalme wake.

        Sio kwa Pilato tu, bali kwa wengine pia ilikuwa ngumu kufahamu kwamba Ufalme wa Yesu ni tofauti na wa dunia hii. Ufalme wake ni wa kuushuhudia ukweli na kuwaongoza watu katika njia ya kweli. Ufalme ambao Yesu anatangaza upo ndani yake na unaonyeshwa kupitia matendo yake miongoni mwa watu. Yesu hakufasili Ufalme lakini aliuonyesha upo ulimwenguni kupitia ishara nyingi. Hii si hali kwa kutazama bali kwa kuhisi na kutangaza. Hili ni fumbo la imani. Ingawa hatuna ufafanuzi kuhusu ufalme kutokana na injili, ibada ya Ekaristi ya siku hii inatujulisha baadhi ya thamani ambazo zina uhusiano wa ndani na ufalme ambao Yesu alikuja kutangaza, yaani, “Huu ni ufalme wa milele na ulimwengu wote, ufalme wa kweli na uzima, ufalme wa utakatifu na wa neema, ufalme wa haki, mapendo na amani.”


        Ni lazima kuwa makini sana kwa ishara za ufalme huu, kwa sababu, ingawa ufalme huu ni hali inayochanganyika na hali za binadamu, zipo ishara nyingi zinazoonekana kuwa wa Ufalme wa Mungu, lakini zinaweza kutudanganya. Yesu ni ishara ya ufalme kwa namna ya ajabu. Hatuhitaji nyingine. Msingi wa ufalme wa Yesu ni ushuhuda katika kweli unaoweza kubadili maisha ya watu, ikiwa tumkubali. Tunapomkubali Yesu na kumsikiliza na kisha kumruhusu awe kiongozi wa maisha yetu, tutakuwa tukiishi katika kweli. Kila aliye wa hiyo kweli humsikia sauti ya Yesu anayesema kuamba ndiye njia, ukweli na uzima. Ukweli huu utawapeni uhuru. Ufalme wa Yesu hupingana na uongo, uonevu na ukandamizaji na kila namna. Ufalme wa Yesu hautokani na nguvu au vita. Hivyo kila mmoja wetu ni budi aisikie sauti ya ukweli na kuamua kwa hiari yake kuifuata. Tuchukue pamoja na Mtakatifu Yohana Calabria ahadi ya kutafuta kwanza Ufalme wa Mungu kuiimarisha imani duniani katika Mungu Baba Mtoaji.

Fr Ndega
Mapitio: Sara

quarta-feira, 18 de novembro de 2015

WAKATI WA MAZINGIRA MAGUMU

Kutafakari kuhusu Dan 12: 1-3; Heb 10: 11-14; Mk 13: 24-32

Tunaweza kuanza kutafakari huku kujiuliza maswali sisi wenyewe: “Je, wakristo wanapaswa kuwa na tabia gani wakati wa mazingira magumu? Liturgia hii ni hamasa Kwetu ambao tunaalikwa kuishi imani yetu katika Kristo kama maana ya utambulisho. Kwa sisi ujumbe kuhusu miisho ya nyakati si ishara kwa kukata tamaa, bali mwaliko kwa tumaini. 

Somo la kwanza kutokana na kitabu cha nabii Danieli ni ufunuo kuhusu hukumu na ufufuko. Ni mara ya kwanza ambayo tangazo la ufufuko linaonekana katika biblia kabla ya Kristo. Watu wa Israeli walitumwa na wagiriki na kuteseka sana. Wengi miongoni mwao waliacha kumwamini Mungu, lakini wengine waliendelea katika imani yao kwa uvumilivu. Kwao Mungu alituma malaika Mikaeli awalinde na kuwahamasisha wakabili wakati wa taabu bila kukata tamaa. Uwepo wa malaika Mikaeli ni dhamana ya ukombozi na ufufuko kwa wale ambao walikuwa waaminifu kutenda mema hadi upeo. Kulingana na somo la pili sadaka ya Kristo ilishinda sadaka za makuhani wa Agano la Kale kwa sababu sadaka zao zilikuwa hafifu, haba na hazikuweza kuondolea dhambi za watu wote. Lakini sadaka ya Kristo iliyotolewa mara moja tu iliweza kuwatakasa watu wote kwa nyakati zote. Katika kila misa takatifu tunasherehekea fumbo la sadaka hii, kuuhisi na kuusaidia wokovu wa Kristo kwa wote. Ni Kristo mwenyewe ambaye anatuhusisha katika mwendo huu.

         Mwanzoni mwa sura ya kumi na tatu ya injili hii ya leo Yesu anasema kuhusu uharibifu wa Yerusalemu. Ufunuo huu uliwahamasisha baadhi ya wanafunzi wake wamwulize swali kuhusu ishara gani, siku na saa gani ya uharibifu huu. Yesu anatumia nafasi hii kuongelea mambo mengi ambayo yatatokea baadaye ili kuiandaa mioyo ya wafuasi wake, ni kwamba, ishara nyingi mbinguni, taabu, mateso, dhiki kuu na kuja kwake kulingana na unabii wa Danieli, yaani, juu ya mawingu ya angani mwenye nguvu na utukufu mwingi. Kanisa katoliki hutafsiri tukio hili kama kuja kwake Yesu mara ya Pili ili kuwahukumia wazima na wafu. Hiyo ndiyo imani yetu ambayo sisi hutangaza kila jumapili. Kuhusu “Siku ya Bwana”, katika Agano la Kale manabii walikwisha wajulisha Waisraeli kuwa siku hii haingekuwa ya adhabu kwa mataifa mengine tu, bali pia kwa Waisraeli kwa kutokuwa waaminifu katika agano walilolifanya na Mungu. Kuhusu siku na saa hii hakuna mtu ajuaye. Hii ni sehemu ya mpango wa hekima na wema wa Baba. Kwa hivyo huu ni pia mwaliko kwa kukesha. Kwa wale ambao wanamfuata Yesu, kukesha lazima kuwa tabia daima kwa sababu ikiwa tunamjua mwalimu wetu, tutakuwa tayari daima ili kumkaribisha.


    Katika utume wake, Yesu aliwaonya wafuasi wake kuwa, mwisho wa nyakati utatanguliwa na matukio mengi magumu, lakini Yesu hataki kutuogopesha. Anatuambia tutarajie kuja kwa pili kwa mwana wa mtu atayekuja kuwachukua wana wa Mungu. Lengo ni kuimarisha imani yetu na kufufua tumaini letu kwa tendo la Mungu ndiye mkuu katika nyakati zote, zilizopita na zijazo. Anatufundisha kuishi wito wetu wa wafuasi kwa uaminifu katika wakati zote pia, hata wakati wa mateso makali. Ushuhuda wa Yesu ni kwamba Mungu huingia katika historia yetu kwa upendo na anajionyesha tofauti kabisa nasi na hata historia yake ni tofauti na yetu.  Baada ya majaribu yote Mungu atakuwa ndiye mshindi. Ni mwaliko tuwe na imani kwa Mungu na kuacha kutabiri mambo, kushinda hofu na mashaka yote. Kulingana na mithali fulani, “hakuna usiku hata wa muda mrefu pasipo mapambazuko”. Basi, kwa wale ambao wanamfuata Kristo, mazingira magumu si ishara za mwisho wa nyakati bali ni wakati mpya, wakati wa kuishi wito wetu kwa shauku zaidi, furaha na tumaini, kuushuhudia kwa uaminifu uwepo wa Bwana miongoni mwetu. Anakuja kwa upendo na kutuokoa. Tukaribishe ishara za nyakati kama msaada tutambue uwepo wa Bwana na kuishi mafundisho yake kwa njia mpya. 

Fr Ndega
Mapitio: Sara

segunda-feira, 2 de novembro de 2015

THE DEATH OF CHRIST IS ALREADY OUR VICTORY

Reflection from John 11: 11-27

When we celebrate the life, we celebrate a great mystery, a precious gift which comes from God. In Christ this gift receives a character of fullness and it is through him that we can understand that the life doesn’t finish here in this world. The inheritance of life of the people who advanced us has a great value for us who are called to continue in the faith to live with meaning. If we cannot see any more the people who advanced us, the true values lived and left by them are the evidence that their passage among us wasn’t in vain. Saint John Calabria used to say: “If we have God in us, we shall do the good only with our passing”. Celebrating the dead is fraternal manifestation of our recognition of how they continue being important for us all, because the death is not an absolute end; it only concludes one stage of the life.  In moments of sorrow, of sadness and nostalgia, let ourselves be helped by the prayers of the friends and enlightened by the Word of God, which strengthen us in the faith and commit us in the life.

As Christians, our main characteristic is the hope. Thus expresses S. Paul: “If Christ didn’t rise our faith is vain and our hope is without sense”. The God in whose we believe is the God of life and when gave the life to us he bound us to himself, making us his beloved sons and daughters. For much we suffer while we are in this life, nothing is compared to the joy to be experienced with the glory that will be revealed to us. In this sense, let us learn from Jesus that, although the situation of so great sorrow and suffering which he experienced on the cross, he maintained his unshakable trust in the providential action of God: “Father,In your hands I commend my spirit.” This should be the confident and constant cry of our spirit, raising the assurance that God neither abandons us and nor keeps quiet before what happens with us. The response from God before the death of Jesus comes right away with the resurrection, that is anticipation of our own resurrection and so, guarantee of our full life, for he is not God of dead but of living. In other words, God doesn’t want the death. In Jesus he reveals himself as resurrection and life.


         Why do people die? Jesus taught us to cultivate the faith in God Abbá, who is turned to us with all strength an activity of his compassionate and liberator love. He attracts us to himself with bonds of tenderness and he desires to keep us bound to him. At the same time, he is always coming in our direction and he expects being welcomed. Our life on earth passes only for one stage. It should continue her journey in other stage, because we are called to the fullness. Conscious of this reality, said the wise Augustine: “O God you made us to you and our heart are restless until they rest in you”. For the one who has Faith, the death is therefore, repose in God, through which all of us have to pass to become full. The fundamental moment of our life will come in which we shall meet definitively with God, before whom we won’t be asked if we belonged to some religion or how many times we went to church, but how much we were able to love. The choices which we do in the course of the journey will determine the direction our life. Through Christ’s will, our life should attain the fullness, which starts in the daily care, in the small gestures of affection at home, in the school, in our work and in our community commitment. We are invited to maintain the communion with God who is the primordial and infinite source of life.  

Fr Ndega

KIFO KWAKE KRISTO NDICHO USHINDI WETU

Kutafakari kutoka Yoh 11: 11-27

        Tunaposherehekea uzima, tunasherehekea fumbo kuu ambalo ni zawadi itokayo kwa Mungu. Katika Kristu zawadi hii inapata ukamilifu na vile vile tunapata kuelewa kwamba maisha hayafikii mwisho hapa duniani. Urithi wa maisha ya wale waliotuacha ina thamani kuu kwetu tunaoitwa kuendelea katika imani  kuishi maisha yenye maana. Ikiwa hatuwezi kuwaona tena wale ambao walitutangulia, yale maadili waliyoishi na kutuachia ndiyo ushuhuda wa kwamba uwepo wao kati yetu haukuwa utupu. Mtakatifu John Calabria alikuwa na mazoea ya kusema, “Ikiwa tuna Mungu ndani yetu, tutafanya yale mazuri hata kwa kupita kwetu tu”. Kusherehekea wafu ni alama kuu ya jinsi wanavyoendelea kuwa muhimu kwetu sote, kwa hivyo kifo sio mwisho wa maisha: hiki kinadhihirisha tu mwisho wa sehemu moja ya maisha. Katika nyakati za sorrow na huzuni, tujiruhusu kusaidiwa na maombi ya marafiki na kuhamasishwa na neno la Mungu linaloimarisha imani yetu na uwezo wetu wa kujitolea .
           Kama Wakristo, tabia yetu kuu ni tumaini. Kwa hivyo, Mt. Paulo akasema: “Na kama Kristo hakufufuka, imani yenu ni bure na tumaini letu pasipo maana”. Mungu ambaye tunaamini ni Mungu wa uhai na anapotupa uzima, yeye hujiunganisha nasi na kutufanya wanawe wapendwa. Kwa kuwa mateso katika maisha haya, hayawezi kulinganishwa na furaha tutakayohisi na utukufu utakaotufunuliwa. Vilevile, tujifunze kujisalimisha kutoka kwa kielelezo cha Yesu ambaye hata katika wakati wa huzuni na mateso, aliyohisi kupitia msalaba, aliilenga imani yake katika tendo la riziki ya Mungu: “Ee Baba, mikononi mwako naiweka roho yangu”. Hili lazima kuwa kilio cha roho zetu ili tuhakikishie kwamba Mungu hawezi kutuacha wala kunyamaza mbele ya kinachotufanyikia. Mbele ya kufa kwake Yesu Jibu la Mungu ni ufufuko wa Mwanawe. Hilo linatupa matarajio ya kufufuka kwetu na hivyo, yatuhakikishia maisha kamili kwani yeye si Mungu wa wafu bali wa wanaoishi. Hivyo ni lazima kutangaza kwamba Mungu hataki kifo. Katika Yesu anajifunua kama ufufuko na uhai.
            Kwa nini watu  hufa? Yesu alitufundisha kulenga imani yetu katika Mungu Baba, ambaye anatujali kwa nguvu yote ya pendo lake lenye huruma na ukombozi. Yeye hutuvuta kwake kwa dhamana za huruma na anatamani kuwa mmoja nasi. Kwa wakati huo huo, yeye huja kwetu daima na hutarajia kukaribishwa. Maisha yetu duniani hupitia sehemu moja tu. Yanapaswa kuendelea safari yake katika sehemu nyingine, kwa sababu twaitwa kwa ukamilifu. Katika maana hii, Agostino asema: “Ee Mungu ulituumba tuwe wako na mioyo yetu inahangaika hadi tunapopumzika kwako”. Kwa Yule mwenye imani, kifo ni pumziko katika Mungu ambako sisi sote lazima kupitia ili tukuwe wakamilifu. Wakati muhimu sana maishani mwetu  utakuja na tutakutana na Mungu kwa njia ya kipekee. Tutakapokuwa mbele yake hatutaulizwa iwapo tulishiriki katika dini yoyote wala mara ngapi tulienda kanisani bali kiasi cha tulivyoweza kupenda. Chaguo tunayochagua katika mkondo wa safari yetu itadhihirisha mwelekeo ambao maisha yetu yatachukua. Kulingana na mapenzi ya Mungu, maisha yetu yanafaa kupata ukamilifu uanzao na uangalifu wa kila siku katika ishara za upendo nyumbani na kujitolea kwa jumuiya. Kwa hivyo tupate kuunganishwa na Mungu aliye mwanzo na chanzo cha uzima na asiyepungukiwa kamwe.


Fr Ndega

domingo, 1 de novembro de 2015

UTAKATIFU KAMA WITO WETU NA MATARAJIO YA MUNGU

Kutafakari kutoka Ufu 7: 2-4, 9-14; Mt 5, 1-12

    Tunaadhimisha sikukuu ya Watakatifu wote. Ni nafasi maalum ya kutafakari kuhusu mwito wa Mungu tangu ubatizo wetu. Utakatifu ni wito wa mkristo: “Muwe watakatifu kama Baba yenu alivyo”, asema Bwana. Mpango wa Mungu ni kutufanya washiriki katika utakatifu wake. Watakatifu ni rafiki za Mungu. Wanatupenda na kutamani tufikie huko walikotutangulia, na Mungu hawezi kuwanyima kitu. Basi, wakati tunawaheshimu watakatifu wote, tukaribishe njia ya utakatifu ya liturujia siku ya leo kama iliyowezekana na iliyotarajiwa na Mungu kwa wote.

     Kulingana na somo la kwanza, ushindi wa Mwana-kondoo ulibadilisha njia ya mauti katika njia ya uzima kwa wale wanaozifuata nyayo zake kwa uaminifu na kujiruhusu kuuawa kwa ajili yake. Wanashiriki furaha milele ya Bwana wao. Hiyo ni njia mno ya utakatifu. Kuuawa ni zawadi maalum ya Roho Mtakatifu: zawadi kwa ajili ya Kanisa nzima. Katika mashahidi, Kristo anaonyeshwa kwa njia maalum: utajiri wa Fumbo la Pasaka yake, Msalaba wake na Kufufuka kwake. Kristo, Mwana-kondoo ni shahidi wa kwanza, Shahidi kwa namna ya ajabu. Ni yeye ambaye kuwahamasisha wanaume na wanawake kujikataa, kuuchukua msalaba wao na kuzifuata nyayo zake. Tabia hii ya kujisalimisha kabisa kwa ajili ya Yesu ni tangazo la thamani kweli ambazo zinadumu milele. Mashahidi wanahisi kama mali ya Kristo na kugundua kwamba maana ya maisha yao ni kujitolea wenyewe kwa ajili ya wengine, kulingana na Mt. Paulo aliyesema, “Mimi ni radhi kabisa kujitolea mimi kabisa kwa ajili ya roho zenu” (2Wko 12:15).

        Injili ya leo inatuonyesha furaha ya watakatifu na njia inayotuwezesha kufika mbinguni. Andiko hili ni mwanzo wa iliyojulikana kama “Hotuba mlimani” ya Yesu (hii inajumuisha sura tatu 5-7). Kwanza kabisa ni muhimu sana kuifahamu nia ya Mathayo. Yeye anamjulisha Yesu kama “Musa Mpya” na kila kitu kuhusu Kristu kinaleta chapa ya upya, yaani, Mlima wa “wenye heri wanane” ni Mlima wa Sinai mpya; “Heri nane” ni mafundisho mapya kuhusu Amri; udugu ni haki mpya, inayoshinda haki ya Waalimu wa Sheria na Mafarisayo; Mwili wake ni Hekalu jipya. Utakatifu si utambulisho ya baadhi ya watu tu, bali pendekezo jipya kwa wote: “Muwe watakatifu kama Baba yenu alivyo”. Wakati Yesu alianza tangazo la Ufalme wa Mungu aliamua kuhubiri kwa maskini waliowakilishwa kupitia nyuso nyingi, yaani: walio maskini wa roho ambao ni wasio na tamaa ya makuu; wenye huzuni ni wenye unyeti mbele ya uchungu wa wenzao; nguvu za wenye upole zinatoka kwa Mungu; wenye njaa na kiu ya haki ni waliojitolea kwa kujenga jamii nzuri; wenye rehema ni walio karibu na Mungu nao ni wenye unyeti mbele ya mahitaji ya watu; wenye moyo safi ni waliomtambua Mungu yupo katika kila mtu; wapatanishi ni waliosaidia upatanisho katika jumuiya zetu; wanaoteswa maana ya haki ni walio mashahidi wa wema wa Mungu kati yetu.   


     Hali hizi zinazojulishwa na Yesu si mbali nasi, bali ni sehemu ya maisha yetu. Yeye anatambua vitu vizuri miongoni mwetu na kwa hivyo anavijulisha kama njia kamili kuingia katika Ufalme wake. Hii ni njia iliyochukuliwa na watakatifu wote kwa sababu walimwamini Yesu na mapendekezo yake. Walitambua kwamba maisha yao hayana lengo lingine ila utakatifu. Kama Mt. Yohana Calabria, waliamini kwamba mtu halazimu kufanya vitu vya ajabu ili awe mtakatifu, bali anaweza kuwa mtakatifu kupitia shughuli za kila siku. Kwa hivyo watakatifu si watu wa zamani tu, bali ni pia wengi miongoni mwetu ambao wanajitolea daima kwa ajili ya jumuiya, kwa ajili ya dunia nzuri. Kupitia uzoefu wa utakatifu wa Yohana Calabria tunajifunza kwamba ikiwa tunataka kuwasaidia wengine kuwa watakatifu, tunapaswa kuutafuta utakaso wetu wenyewe kupitia juhudi ya kila siku kwa kufanya mapenzi ya Mungu. Mtu hawezi kutoa kile ambacho yeye hana. Sikukuu hii ni hamasa kwa kuyaamsha matumaini makubwa mioyoni mwetu ili tuwe watakatifu. Kupitia msaada wa neema ya Mungu, tuweze kuchukua “Heri Nane” kama mpango wa maisha na njia kamili ili “tuwe watakatifu kama Baba yetu wa mbinguni alivyo”. 

Fr Ndega
Mapitio: Sara

quinta-feira, 29 de outubro de 2015

MTAKATIFU YOHANA CALABRIA NA WAGONJWA

Kutafakari kuhusu Is 49: 14-15; Mt 6: 24-34

        Liturujia inatujulisha mifano miwili yenye nguvu kuhusu Mungu. Katika Somo la kwanza Mungu analinganishwa kwa mama na katika injili Mungu analinganishwa kwa baba. Mungu anawapenda watu wote na hamsahau yeyote wa wana wake. Yeye anakijali kila kitu ambacho wana wake wanahitaji. Mtakatifu Yohana Calabria aliishi kwa uzoefu huu kwa mkazo na aliweza kuushuhudia kwa wengine. 

   Watu wa Israeli walikuwa watumwa katika Babeli na wakajihisi walioachwa na kusahauliwa. Nabii Isaya aliwasaidia kutambua kwamba Mungu alikuwapo miongoni mwao na hakuwasahau. Yeye ni Mungu mpole ambaye anawapenda na kuwalinda watu wake zaidi kuliko mama ampendaye mtoto wake anyonyaye. Basi, uwepo wake ni dhamana ya utunzaji na ulinzi. Katika injili Yesu anawafundisha wanafunzi wake kuhusu umuhimu zaidi wa maisha. Anaongea kuhusu hatari ya utajiri na miliki yote ambayo inaweza kumshika mtu hivi hata asiweze kifikiria mambo yanayomhusu Mungu. Nia kuu ya Yesu ni kuongea kuhusu Mungu kama Baba aliye na wasiwasi kwa utunzaji wa upendo kwa kila kitu. Baba huyu anatarajia jibu la ukarimu kutoka kwa wanadamu ambao wana thamani zaidi kuliko viumbe vingine vyote. Kuwa mwanafunzi wa kweli wa Yesu ni kutafuta kwanza Ufalme wa Mungu Baba na haki yake kama rejea ya maisha. Kwa maneno mengine, anatualika kujisalimisha mikononi mwa Mungu ambaye anayajua mahitaji yetu na yuko tayari daima kutusaidia.

       Injili hii inafikiriwa msingi wa kiroho ya Mt. Yohane Calabria kwa sababu kupitia injili hii aliufanya ugunduzi mkubwa. Aligundua jinsi ya kuishi kwa njia halisi ubaba wa Mungu na kuwa ishara ya riziki yake kwa watu. Kutokana na andiko hili alichukua mistari 33 kama ahadi kwake: “Mtafuteni kwanza Ufalme wa Mungu na haki yake; na hayo yote mtapewa kwa ziada.” Kulingana naye “Injili anatuongelea kwamba Mungu ni Baba, anatujali zaidi kuliko ndege wa angani na maua ya mashamba hata atatujalia kile ambacho tunahitaji kwa chakula na kwa mavazi, lakini tunapaswa kuutafuta kwanza Ufalme wake na haki yake”. Mt Calabria alifahamu kwamba ililazimu kuifufua imani duniani kwa Mungu Baba wa wanadamu wote, kupitia kujisalimisha kabisa kwa Riziki yake. Kwake imani kweli na asili inafikiria Mungu si kama Muumba na Bwana tu, bali kwanza kama Baba”. Mungu ni Baba, hutujali na wote ambao tunawapenda; macho yake ni makini sana kwa kila kitu na kila kitu kinapangwa na kuongozwa na hekima, nguvu na wema wake pasipo mwisho.

      Mt. Yohana Calabria alikuwa mtu mwenye unyeti mno kuuhusu ugumu na mateso ya wengine.  Aliweza kuweka matendoni maneno yake kuhusu wema na utunzaji wa Mungu katika Riziki yake, akisema, “Riziki ni Mama mpole ambaye hupatia kila kitu kwa wema wetu, hata kwa wema wetu mkubwa. Tunapaswa kuhisi tumebebwa kwa mikono yake ya mama”. Yohana Calabria aliamini katika ukweli huo na hata aliyapanga maisha na kazi zake zote kulingana na hali hii. Kama ishara ya utunzaji wa Mungu alikuwa na unyeti mkubwa kwa uhusiano na wagonjwa. Alimwona Kristo mwenyewe katika walio wagonjwa. Alifikiria mateso ya wagonjwa kama thamani na msaada mkubwa kwa mtume wa kanisa. Aliwahamasisha na kuwaonya wagonjwa kuukaribisha ugonjwa na mateso kwa utulivu na sala. magonjwa kwao yana maana kwa wokovu wao na wokovu ulimwenguni. Kristu mwenyewe aliwapenda wagonjwa na wakati wa maisha yake alikwenda mara nyingi kuwatembelea na kuwaponya. Kwa njia Mtakatifu Yohana Calabria, tumwombe Mungu kwa ajili ya wagonjwa wote, hasa kwa hawa ndugu zetu wapo katika misa hii ili neema ya Mungu iimarishe imani na nguvu zao. Maisha yenu yawe ushuhuda wa wema wa Mungu kwa sisi sote.

Fr Ndega
Mapitio: Sara

IMANI YA KWELI NA HALISI

Kutafakari kutoka Mk 10, 46-52

     Yeriko ni mmoja miongoni mwa miji ya zamani ulimwenguni. Hii nieneo ya baadhi ya matukio makuu ya biblia; hata katika muda wa Musa ilikuwa tayari kuongelewa kuhusu mji huu. Tukumbuke “kuzingirwa na kuchukuliwa kwa Yeriko” na Waisraeli katika wakati wa Yoshua (Yoshua 6, 1-27). Tukumbuke pia Zakayo; mabadiliko ya maisha yake yalitokea katika Yeriko. Mji huu ni karibu na mto Yordano na Yesu alipita mahali huko mara nyingi. Andiko siku ya leo linaongea kuhusu mkutano wa Yesu na kipofu Bartimayo, aliyeketi kando ya barabara ya mji. Hakika alikuisha amesikia kuhusu Yesu na alitaka sana nafasi ili kukutana naye. Lakini hakujua kwamba Yesu pia alitaka kukutana naye ili kumwongozea njia mpya ya kuishi. Kisha, nafasi imefika! Shauku ya kipofu ilikuwa kubwa sana kwamba hakuna kitu au mtu kumfanya  anyamaze.

    Kilio cha kipofu ni kilio cha kila binadamu mwenye dhamiri kuhusu udhaifu wake na mahitaji ya huruma ya Mungu. Kipofu ni ishara ya kivuo dhahiri cha ndugu zetu wengi. Ni nafasi ya kutambua kwamba watu wengi wanaanguka au wameachwa barabarani. Wanapaza sauti kwa huruma na kwa nafasi kwa sababu wanaamini kwamba wale ambao wanajiita wafuasi wa Yesu wanaweza kusikiliza sauti yao na kuwatendea mema. Yesu alisikia si kilio cha kipofu tu, bali pia kilio cha wale ambao walimwambia kipofu “anyamaze”! jibu la Yesu linaonyesha mchanganyiko wa huruma na hasira, kwa sababu alikuwa kushughulika kwa upofu wa aina mbili tofauti, yaani, upofu wa Bartimayo na upofu wa umati wa watu ambao walikuwa wakimfuata Yesu bila ushirika na hisia zake. Je, ni nani ana upofu zaidi, yule aliye kipofu asili au wale ambao hawapati kuona walio na mahitaji kandokando yao? Hata hivyo kuna tumaini, kwa sababu miongoni mwa wale ambao walimwambia kipofu “unyamaze!” walikuwapo wengine ambao walimwambia “jipe moyo, anakuita! Yeye hajamsahau na hawaachi wale ambao wanamwamini”. Sauti hizi ni za watu ambao wanachukua ujumbe wa unabi na wanapata kuwahamasisha wenye kukata tamaa. Ni ishara pia ya walio upatanishi wa Mungu katika maisha ya yeyote anayegundua wito wake ili aweze kumjibu Mungu kulingana na matarajio yake.


     Yesu ambaye tunamfuata ni mwenyeunyeti sana. Ana macho na masikio makini sana kwa hali halisi ya watu. Anatualika kuwa na unyeti sawa. Kwa kawaida sisi ni kama kipofu huyo, tunahitaji mkutano wa mabadiliko ya maisha ili kuona bora nini inatokea kandokando yetu na kumfuata yesu ambaye anatuleta maana mpya kwa maisha yetu. Sisi ni pia kama wengine karibu na Yesu, lakini mbali sana na ndugu zetu, waliofungwa kabisa kwa hali halisi kandokando yetu na hata tunafikiri kwamba tuna mamlaka ya kuwaambia wengine: “mnyamaze”. Sisi  tuko na kosa kubwa. Sisi lazima kuwamakini sana kuhusu baadhi ya uzoefu ambao unatufungua kwa Mungu lakini unatufunga kwa wengine. Ikiwa imani yetu haituongozi kukutana na wengine na haitufanyi wenye huruma, imani hii ni udanganyifu. Kupitia Ekaristi hii, tumwombe Mungu neema ya imani ya kweli na halisi.

Fr Ndega
Mapitio: Nikoletee

quarta-feira, 7 de outubro de 2015

MUNGU BABA YETU KATIKA BIBLIA NA KATIKA MAWAZO WA Mt. YOHANE CALABRIA

katika siku hii ya maadhimisho ya sikukuu ya Mtakatifu Yohana Calabria nataka kupendekeza kutafakari kuhusu UBABA WA MUNGU. Tunamshukuru Mungu Baba ambaye ametupa Yohane kama nyota mbinguni na nuru karibu nasi. 
YOHANA WA MASKINI (M: Jorge Trevisol – Translation to Kiswahili: Fr Ndega)
- Imba viumbe vyote! Hii ni siku kwa wote/ Mungu alitupa Yohana, nyota mbinguni, nuru karibu nasi/ imba viumbe na watu!/ imbeni kwa furaha kubwa!/ uhai unapendeza Mungu/ ana upendo wa Baba kwa maskini wake/ Ref: /: Imba Yohana wa maskini, kwamba dunia itakusikiliza/ Mungu aliyefanya mvua, jua, bahari na ni Baba yetu pia.:/ 2. Ninahisi upo karibu/ naimba na unaimba nami/ unasema kwa nyuso za wengi kwa uhai dhaifu ndani yangu unakutafuta/ ufukuze hofu yetu/ kila wakati una nguvu/ Kuishi sasa kwa muda ni kuhisi kwamba wewe ni yote milele/ 3. kwa sababu uliishi hayo/ kwa sababu ulituambia/ vivyo hivyo tutaishi/ pamoja na wewe/ kamwe bila na wewe/
MPANGO WANGU WA KUTAFAKARI
Utangulizi
1 Ubaba wa Mungu katika Biblia
            1.1 neno Baba kwa uhusiano na Mungu katika Agano la Kale
            1.2 neno Baba katika Injili
            1.3 maneno Mungu Baba ni yenyewe ya Waraka wa Mitume
            1.4 Yesu anamdhihirisha Mungu kama Baba
            1.5 “Sala Baba yetu ni awali ya Injili” (Mt. Yohane Calabria)  
2 Uzoefu wa Ubaba wa Mungu kwa Mtakatifu Yohana Calabria na Familia yake ya Kiroho
Hitimisho

Utangulizi
Msomo wa kutafakari kwetu ni kuhusu Mungu Baba au ubaba wa Mungu. Bila shaka kwamba baada ya tutafute maana ya maneno haya katika Biblia, rejeo kwa kutafakari kwetu itakuwa maandiko, mawazo na mtazamo wa Mtakatifu Yohana Calabria. Msomo huu kuhusu ubaba wa Mungu ni jambo la msingi la kiroho ya Calabria. Ni vizuri sana kujua kwamba Yohana Calabria aliwekwa mtakatifu katika mwaka wa Mungu Baba ambao ulikuwa sehemu ya mwisho katika maandalizi kwa sherehe ya yubilei ya Miaka elfu mbili ya kuzaliwa kwake Bwana Yesu Kristu.
Mwanaume huyo mkuu anayeitwa Yohana Calabria alizaliwa terehe nane mwezi wa kumi mwaka wa elfu moja mia nane sabini na tatu. Alikuwa maskini sana kwa mtazamo wa kibinadamu na tajiri sana kwa upande wa Mungu. Kulingana na uzoefu wake tunajifunza kwamba hatuweze kuongea kuhusu Mungu ikiwa hatupitii hayo. Na huu ulikuwa uzoefu wake, yani, Mungu ni Baba na Mtoaji. Ingawa hali mbili inatokea pamoja katika Mungu, tutatafakari kuhusu ubaba peke yake.

1 Ubaba wa Mungu katika Biblia

1.1 neno Baba kwa uhusiano na Mungu katika Agano la Kale
Maneno Baba yetu si maneno ya Yesu tu, kwa sababu kabla yeye yalitumika katika maandiko ya manabii ya Agano la Kale. Bila shaka Yesu hakuyatumia maneno haya tu, bali alianzisha uhusiano mpya na Mungu, akileta maana mpya kabisa kwa maneno Baba yetu. Neno Baba kwa uhusiano na Mungu, tunaweza kukuta katika: Isaya 9:6 (Baba milele); Is 63:16 (wewe ni Baba yetu - mara mbili); Is 64:8 (wewe ni Baba yetu); Yeremia 3:4.19 (Baba yangu – mara mbili); Malaki 2:10 (Tuna Baba mmoja)

1.2 neno Baba katika Injili
Kuhusu injili hali ni tofauti sana kwa sababu neno hili lilikuwapo midomoni mwa Yesu daima, yaani, Baba, Baba yangu, Baba yenu, Baba yake, Baba Yako, Baba yao, Baba yetu,etc. Katika Mathayo - mara 42; Marko – mara 5; Luka - mara 16; Yohane – mara 114. Tunaweza kusema kwamba Yohane ni “Injili ya Baba” kwa sababu inaongea sana kuhusu uhusiano wa Yesu na Baba yake. Tena tunatambua kwamba katika toleo hili peke yake tunaweza kufanya maneno kama Baba mtakatifu, Baba mwenye haki, Baba yangu na yenu pamoja, etc. Katika matoleo ya Mathayo, Marko na Luka tunakuta uzoefu wa ubaba kwa uhusiano na huruma na kujua, kwa nfano, Baba atawasamehe, Baba yenu anajua,etc.  Lakini sala ya Bwana inayojulikana kama Baba yetu, tunaweza kukuta katika Mathayo na Luka peke yao.

1.3 maneno Mungu Baba ni yenyewe ya Waraka wa Mitume
Maneno mawili pamoja, yaani, Mungu Baba, tunakuta katika Agano Jipya peke yake na hasa katika Waraka: Wagalatia 1,1; Waefeso 6,23; Wafilipi 2,11; Wakolosai 3,17; 1Wathesalonike 1,1; 2Wathesalonike 1,2; 1Timotheo 1,4; 2Timotheo 1,4; Tito 1,4; 1Petro 1,2; 2Petro 1,17; 2Yohane 1,3; Yuda 1,1. Mara nyingi maneno haya Mungu Baba yanatumika kuonyesha shukrani au utambulisho kuhusu zawadi za Mungu katika jumuyia. Yanaonyesha pia matakwa ya mtume mwandishi kuhusu safari ya imani ya jumuiya fulani.

1.4 Yesu anamdhihirisha Mungu kama Baba
Yesu anapoongea na Mungu na kuhusu Mungu, anatumia neno Baba. Hali hii inatafisiri uzoefu wa ndani, ushirika wa upendo na uhai kati ya Mwana na Baba yake. Maisha yake na uzoefu wake na Baba ni mwaliko kwa wasikilizaji washiriki katika ushirika sawa, wakiishi kwa uzoefu wa ndani na Mungu. Yesu anatuletea ufunuo wa uso kweli wa Mungu: wa kwanza - Mungu aliye na wasiwasi kwa utunzaji wa upendo kwa kila kitu, “hata nywele moja ya kichwa chetu” (Lk 21,18); wa pili - Mungu Baba, ambaye ana watoto tofauti na anashiriki zawadi zake na wote kwa njia sawa. Anawapenda wote na anataka kwamba watu wote wajihisi kuishi katika familia, washiriki furaha yake kama Baba. Katika familia hii anautoa utunzaji na ulinzi ambao ni maonyesho ya upendo wake wa Baba. Tuko katika ushirika wa ndani naye ikiwa tunashiriki hisia zake kuhusu wengine. Kwa hivyo Yesu alitufundisha kusali, akishiriki nasi njia yake yenyewe ya kusali. Alitujulisha kujua huyo ambaye ni Baba yake na Baba yetu pia.

1.5 “Sala Baba yetu ni awali ya Injili” (Mt. Yohane Calabria)

Mantra: Baba sikia wanao, sikia sauti zao, sikia dunia nzima...
Yesu anapowafundisha wanafunzi wake kusali, aliwakumbusha kuhusu mahitaji ya tabia ya mwana anayemwomba Baba kwa imani. Kama yeye alivyoishi, tabia kamili ya wanafunzi lazima kuwa kujisalimisha mikononi mwa Huyo anayejua mahitaji ya wana kabla ya wamwulize kitu. Sala ya kweli ni kitendo cha kujisalimisha. Sehemu ya kwanza ya sala ambayo Yesu anawafundisha wanafunzi wake ni utambulisho wa ubaba wa Mungu, ambaye ni mwema na mtoaji. Katika sala hii, kila kitu ambacho kinaja baada ya Baba kinategemea kwa neno hili/mwelekeo/hali. Ni lazima kufanya mapenzi ya Mungu ili Ufalme wake utokee duniani kama mbinguni. Mapenzi ya Baba huyu lazima kuwa chakula cha watoto wake kama kilichotokea na uzoefu wa Yesu miongoni mwa wanadamu.  
Kwa Baba huyu sisi lazima kuhutubia kwa imani, wenye uhakika kwamba tumepokea sana. Tunaomba kwa mkate, msamaha na upatanisho. Kulingana na Maandiko matakatifu, “kutokana na wema wake tumepokea neema juu ya neema”. Sala hii inathibitisha utunzaji wa upendo wa Mungu anayeshiriki zawadi zake na wana wake, akitarajia kwamba tufanye vivyo hivyo na wengine ili udugu uwe maonyesho ya kweli ya ubaba wake na chombo cha huruma yake. Maombi Baba yetu yanatufundisha kufikiri kuhusu mahitaji ya wengine na si kwa mahitaji ya kibinafsi tu. Kupitia sala hii tunaomba muhimu zaidi, yaani, “mkate wa kila siku” kwa sababu sisi lazima kupinga dhidi ya aina yote ya ukusanyaji na ubadhirifu ambao unaharibu udugu, kufanya maskini na wenye njaa wateseke. Kuhusu mambo haya Baba Mtakatifu Francisco asema: “Ulaji umetuongoza kutumia chepesi pamoja na ubadhirifu wa chakula cha kila siku... sisi lazima kukumbuka kwamba chakula ambacho sisi hutupa takatakani ni kama ikiwa tulikuwa tumeiba kutoka meza ya walio maskini na wenye njaa.”
Kwa Mt. Yohana Calabria, “sala Baba Yetu ni awali ya Injili. Matatizo lazima kufikiriwa na kusomwa kwa uhusiano na maelewano kwa ubaba wa Mungu.” Ikiwa tunasema “Baba Yetu” ni kwa sababu tunasadiki kwamba sisi ni ndugu wa wengine wengi. Mungu hawabagui watu na hamsahau yeyote wa wana wake. Hapendezwi na sala ambayo haifikirii ndugu wengine. Mungu si daima anatupa vitu ambavyo tunamwomba, bali anatupa daima vitu tunavyohitaji kwa sababu anajua kila kitu. Ikiwa mara nyingi hatupokei vitu ambavyo tunamwomba ni kwa sababu hatuombi ipasavyo. Labda kutokuwa na tabia na nia kamili iliyodaiwa na Yesu wakati aliwafundisha wafuasi wake kusali. Tunaalikwa kuishi kwa udugu kutokana na ubaba wa Mungu na kuwa na mioyo ya wana, kwa sababu mtu asiyeishi kama mwana hajifunzi kuwa ndugu.

2 Uzoefu wa Ubaba wa Mungu kwa Mt. Yohana Calabria na kwa Familia yake ya Kiroho
Mantra: Baba yetu sisi ni wanawe, Baba yetu sisi ni ndugu...
Mt. Yohane Calabria alikuwa mwenye unyeti daima kwa ishara za utunzaji wa Mungu ulimwenguni. Lakini usiku mmoja wakati yeye hakupata kulala usingizi, alichukua injili na aliufanya ugunduzi mkubwa. Aligundua jinsi ya kuishi kwa uhalisi ubaba wa Mungu. Kifungu ambacho kiliichukua uangalifu wake zaidi kilikuwa Mt 6,24-34. Kutokana na kifungu hiki alichukua ahadi kwake na kwa familia yake ya kiroho, yaani, “Mtafuteni kwanza Ufalme wa Mungu na haki yake; na hayo yote mtapewa kwa ziada.” Kulingana naye kwa kushuhudia duniani kwamba Mungu ni Baba, Mama, Kila Kitu, tunahitaji kwanza kufanya sisi wenyewe uzoefu wa ubaba wa Mungu na kulima hisia ya miliki ya Baba huyu. Kama hivyo alimwambia mama fulani: “Sisi ni wa Mungu, Mungu ni Baba, Mama Kila kitu chetu. Upende Bwana na atakuwa heri (mwenye furaha)” (24-1-1930).
Kwa yeye, “Mungu ni Baba na Baba mwema. Hakuna mama ambaye anawapenda sana watoto wake kama Mungu anawapenda watu wote na kila mmoja wetu”. Calabria anaongea pia kuhusu Mungu kama Riziki, kwa sababu kulingana naye, haiwezekani kutenga Ubaba wa Mungu na Riziki yake. Kwa hivyo, asema, “Riziki ni Mama mpole ambaye hupatia kila kitu kwa wema wetu, hata kwa wema wetu mkubwa. Tunapaswa kuhisi tumebebwa kwa mikono yake ya mama”. Yohana Calabria aliamini katika ukweli huo na aliyapanga maisha na kazi zake zote kulingana na hali hii. Katika mwanzo mwa kazi yake, alipoonekana mtoto wa kwanza, Yohana alifahamu kwamba Mungu akatarajia kutoka kwake imani maalum ambayo huonyeshwa kupitia matendo mema kwa masikini wapendelewa na Mungu. Baada ya mtoto wa kwanza, wengine wengi walikuja nyumbani. Nyumba hiyo iliitwa “Nyumba ya wavulana wema”. Kama hii, ishara ya mapenzi ya Mungu ilikuwa wazi sana kwa Yohana Calabria.
Kupitia uzoefu ambao Mt. Calabria aliishi kuhusu ubaba wa Mungu, akawa mshahidi na mhubiri wa ubaba huu. Kama hivyo asema, “Injili anatuongelea, kwa mfano, Mungu ni Baba, anatujali zaidi kuliko ndege wa angani na maua ya mashamba hata atatujalia kile ambacho tunahitaji kwa chakula na kwa mavazi, lakini tunapaswa kuutafuta kwanza Ufalme wake na haki yake. Basi, je, imani yetu katika ubaba wa Mungu ni nzuri? Je, tena ni nzuri imani yetu katika Riziki yake takatifu na wema?” 
Imani kweli na asili inafikiria Mungu si kama Muumba na Bwana tu, bali kwanza kama Baba”. Mungu ni Baba, hutujali na wote ambao tunawapenda; macho yake ni makini sana kwa kila kitu; hakuwezi tokea chochote kisichotarajiwa kama mshangao (bila maana); kila kitu kinapangwa na kuongozwa na hekima, nguvu na wema wake pasipo mwisho. Juu ya yote tunaweza kusema kwamba ni kwa wema wake.

Hitimisho
Uzoefu wa ubaba wa Mungu ulimhamasisha Yohane Calabria kuanza Kazi kubwa. Katika mwanzo, padre Yohane alisaidiwa na mama yake. Lakini, baada ya wakati mchache, walikuja Mabruda, Mapadre, Masister, makundi mengi ya watu wasio watawa. Pamoja na padre Yohana, sisi ni Familia ya Kiroho ya Calabria inayoitwa “Poor Servants of Divine Providence” na kazi yetu ni kutafuta Ufalme wa Mungu. Hali hii inatokea katika ahadi ya kuifufua imani duniani kwa Mungu Baba wa wanadamu wote, kupitia kujisalimisha kabisa kwa Riziki yake. Kiroho yetu ni Injili. Kulingana na Mtakatifu Yohana Calabria, tunahitaji kurudi kwa Injili daima ili maisha yetu yabadilike na hali kandokando yetu pia.
Maandiko ya Mt. Yohana Calabria yanadhihirisha jinsi alivyokuwa na ubinadamu mno, akifahamu ugumu wa wengine, lakini kwa wakati sawa, alijua kuonyesha njia kamili kwa ufumbuzi wa matatizo yao. Kutokana na uzoefu wa Mt. Calabria tunajifunza kwamba Mungu ni Baba mwema na mtoaji bila mwisho, na sisi sote ni ndugu katika Kristo. Tunaalikwa kuishi kama ndugu kutokana na ubaba wa Mungu na kuwatendea mema wengine vivyo hivyo tungependa wao watutendee. Kulingana naye, “Tunapaswa kuwa na kujihisi watumishi, bali kwa utumishi wa Mwenyeji fulani ambaye ni pia, na kwanza kabisa, Baba. Basi utumishi wetu ni wa wana, utumishi wa huria na upendo... kama alivyotumika Bwana wetu Yesu Kristo, mtumishi wa Baba kwa namna ya ajabu, ambaye wakati wa maisha yake ya kibinadamu alifanya tu kutimiza amri zako: “Ninafanya kama Baba alivyoniamuru kufanya.”

Tumsifu na tumshukuru Mungu Baba kwa kielelezo cha imani ambacho ni Yohane Calabria na mtume wake duniani kupitia Familia yake ya Kiroho. 

Fr Ndega
Mapitio: Sara