quinta-feira, 17 de dezembro de 2015

MUNGU ALICHUKUA BINAFSI HISTORIA YA WATU WAKE


Kutafakari kutoka Mt 1, 1-17

Kutokana na siku hii ya leo tunalianza juma maalum katika maandalizi yetu ya Krismasi. Kwa hivyo injili inatuletea ukoo wa Yesu. Majina haya mengi yaliyojulishwa na Mathayo yanatusaidia kufahamu mwelekeo wa binadamu wa Mwana wa Mungu. Ni ushahidi kwamba Yesu hakuonekana ghafla wala ni mgeni katika historia ya binadamu, bali tukio lake lilitokea polepole, hatua kwa hatua na kwa muda mrefu. Mungu aliwaandaa watu wake kwa uvumilivu kupitia Mwana wake ili historia hii ilikuwe na uwezo wa kumpokea katika wakati muafaka. Yesu Kristo anakamilisha ahadi aliyoitoa Mungu katika Agano la Kale. Kwa sababu hii, Yesu anatambulishwa kuwa ni mwana wa Mfalme Daudi na pia mzao wa Abrahamu. Mathayo anatumia mifano mingi kutoka katika unabii uliotolewa na manabii wa Agano la Kale, kueleza maisha ya Yesu ambaye alikuja kuwa Mwokozi wa Wayahudi (huu ni ufahamu wa kwanza kuhusu utume wake). Lakini mpango na lengo la Maandiko Matakatifu ni kuwasaidia watu kufahamu ufundishaji wa Mungu mwenyewe ambaye anatumia watu fulani kwa kufikia wote. Kama hii Mwanao hakutumiwa ili awe mali ya Wayahudi, bali Mwokozi wa ulimwengu wote.
Kwa nini yeye ni Mwokozi wa ulimwengu wote? Ni muhimu sana kujipatia nia ya Mungu kuhusu ubinadamu tangu uumbaji. Kwanza kabisa ulikuwa uamuzi wa Mungu kumwumba binadamu kushiriki naye uzima wake mwenyewe. Upinzani asili kupitia dhambi haukumzuia Mungu kuendelea mpango wake. Na, halafu aliamua kumwokoa binadamu mpotevu. Mungu mwenyewe aliwaandaa watu wake kwa muda mrefu akiifanya historia yao kuwa historia ya wokovu. Kwa sababu ya nia na matendo ya Mungu hatuwezi kuongelea historia mbili, bali historia ya Mungu na binadamu, yaani Historia ya wokovu. Mungu anamtafuta binadamu kumpa uzima wa milele ambao ni uhai wake mwenyewe. Historia hii inatokea polepole kati ya mwanga na vivuli. Kizazi cha Daudi kinaitwa kizazi cha mwanga kwa sababu ya mwelekeo wake kuelekea kwa Yesu. Kizazi cha utumwa wa Babeli kinafikiriwa kizazi cha vivuli kwa sababu upinzani wa watu dhidi ya mwongozo wa Mungu uliwazuia kuishi kama Watu wa Mungu. 

Tunaweza kuongelea njia maalum ya kuingia katika historia ya binadamu. Mungu anaingia katika maisha ya watu kwa wakati halisi. Yeye aliongea kwa namna mbalimbali kupitia manabii na mababu zetu ya zamani na siku hizi anaongea kupitia Mwanae mwenyewe. Yeye huongea kila wakati, lakini  haongei hewani bali hupitia katika matukio mazuri au mabaya  katika historia ya watu. Mungu alijifanya mmoja wetu na bado yuko nasi kwa namna mbali mbali. Kwa kivyo hakuna tukio lolote la historia lisilokuwa na maana. Angeweza kufanya kila kitu peke yake bali hakutaka. Alichagua Maria, Yosefu, Yohane na viongozi wengi kama washirika, akiingia katika historia kwa namna ya pekee na inabidi watu watayarishwe kumkaribisha Masiya wake kwa wakati wote. Sisi ni sehemu ya mwendo huu na kualikwa kumsaidia Mungu kwa mafanikio ya mipango yake kwa ubinadamu wote. Tumshukuru Mungu kwa matendo yake makuu katika historia yetu na kwa wito wetu kama washirika wake.

Fr Ndega
Mapitio: Sara

Nenhum comentário: