domingo, 25 de dezembro de 2022

MUNGU ALIYAJENGA MAKAO YAKE KATI YETU

 

Kutafakari kuhusu Is 52. 7-10; Eb 1. 1-6; Yoh 1. 1-18




 

    Sisi tunaishi wakati wa furaha na shukrani, yaani wakati wa Krisimasi. Kila kitu kinaonekana kuwa na rangi zaidi, mwanga zaidi na maana zaidi. Haya ndiyo matokeo ya uwepo wa Mungu miongoni mwetu; yeye aliyachukua mazingira yetu na kutualika kujifunza kutoka kwake ili tuweze kuishi vizuri. Tumshukuru Mungu kwa kuendelea kutupa sisi nafasi ya kuwa watu wapya. Ujumbe wa kuzaliwa kwa Yesu ni ujumbe wa furaha kubwa kwa wote, kwa sababu Mwokozi alizaliwa kwa wote. Tufurahi kwa sababu Mungu aliamua kuyajenga makao yake kati yetu na kutuletea wokovu.

    Kulingana na somo la kwanza, baada ya uzoefu wa utumwa Watu wa Israeli waliishi hali mpya na kugundua tena wito wao kama watu wa Mungu. Wito huu sio kutumia kisasi dhidi ya maadui yao, bali kutangaza habari njema ndiyo habari ya amani. Habari hii ni ujumbe wa faraja unaotoka kwa Mungu na kutia moyo wa watu. Kwa hivyo unapaswa kutangazika kwa wote. Miguu yetu ni ishara ya upatikanaji wetu, hamu yetu kwa ajili ya mpango wa Mungu. Yote ambayo Mungu amefanya maishani mwetu ni lazima kutangazika. Furaha iliyo matokeo ya tendo hili itakuwa kamili maishani mwetu tu ikiwa tunatangaza kwa wengine.

  Somo la pili linatuanzisha kwenye siri ya neno la Mungu kwa kushuhudia kwamba Mungu wetu ndiye Mungu wa neno. Aliviumba vyote kwa nguvu ya neno lake. Yeye aliongea zamani kwa kupitia mababu zetu, anaongea leo na kuendelea kuongea kwa sababu huyo Neno alikuwako kwake milele. Neno hili ni Mwanawe Yesu Kristo aliye mpatanishi wa Agano Jipya. Yeye ni utimizaji wa ahadi zote za Mungu kwa watu wa Agano la Kale. Mambo yote yalifanyika kwa sababu yake na kwa ajili yake. Tena mambo yote yanazunguka kandokando yake na kuikuta maana katika yeye. Hivyo hakuna yeyote ambaye anaweza kutupatia wokovu ila yeye peke yake aliye Neno la milele la Baba.   

    Kuhusu injili tuko na mwendelezo wa ujumbe huu lakini kwa kiini zaidi. Neno la Mungu ambaye alikuwako milele ni Mwana wa Mungu. Huyo ni maana ya vyote vilivyofanyika. Huyo Neno alifanyika mwili tumboni kwa Bikira Maria akija ulimwenguni amejaa neema na ukweli akifunua sura ya Mungu kama Baba aliyejaa wema na huruma. Mwana Yesu alitufanya watoto wa Mungu na kutuangaza kwa mwanga wake ili tuwe mashahidi wa nuru na ukweli kama vile Yohana Mbatizaji. Mambo yote ambayo Mungu anafanya ni mazuri na kamili kwa sababu hii ni njia yake ya kutenda.

    Basi, “Neno alifanyika mwili na akakaa kwetu”. Katika Yesu, Mungu ni mmoja wetu. Yeye ni huruma ambaye alijiruhusu kukuta na kuguswa akituletea pendekezo mpya la maisha. Kwa hivyo, haitoshi kuitambua huruma ya Mungu katika Yesu; ni muhimu pia tujiruhusu kuguswa na huruma hii na tena kuongozwa na ujumbe wake wa amani na upendo. Kuzaliwa kwake Yesu kuliwafanya wanadamu wote wawe familia moja ya kipekee. Kweli, Mungu alijidhihirisha kama jirani, maskini na aliyekataliwa, akitualika sisi sote tutambue thamani ya ishara ndogo na mipango midogo. Bila shaka chaguo hili la Mungu linatualika kufikiri na kutenda kwa njia tofauti, yaani kuwa wanadamu bora.

Mungu Mwenyezi anakubali hali ya mtoto mdogo, kwa utegemezi kabisa wa utunzaji na upendo wa binadamu, kwa mfano Mariamu na Yusufu. Ndiyo imani inayotuongoza kutambua mtoto huyu mdogo wa Bethlehemu katika kila mtoto ambaye sisi hukutana katika safari yetu ya kawaida. Kila mtoto anaomba upendo wetu. “Tufikiri kuhusu watoto ambao hawana uzoefu wa upendo wa wazazi wao; pia kuhusu watoto wa barabara ambao hawana mahali pa kuishi; tena kuhusu watoto wanaotumika kama askari, wakibadilishwa kuwa vyombo vya ukatili badala ya kuwa vyombo vya amani; pia kuhusu watoto ambao ni waathirika wa unyanyasaji wa kijinsia, na kuhusu watoto waliolazimishwa kuacha ndoto zao kwa sababu ya hali ya kiuchumi siyo nzuri”. Mtoto ndogo ya Bethlehemu ni mwaliko ili tuweze kusaidia kwa hali tofauti maishani mwa watoto wetu.

Ingawa tunaishi katika jamii ya ulaji, inayotuzuia kulenga muhimu katika maisha yetu, tunapaswa kuwa macho. Krismasi ni zaidi ya ulaji. Ni sikukuu ya ufunuo wa fumbo la upendo wa Mungu unaobadilisha moyo wa binadamu kuwa makao ya thamani za kweli. Mungu anatupenda kwa hiari na ukarimu, bila astahili kwa upande wetu. Uzoefu huu unatuongoza kutenda vivyo hivyo ili Krismasi iwe zaidi ya wakati mmoja tu kwa mwaka. Itakuwa Krismasi daima ikiwa tuweze kujifunza jinsi ya kupenda kwa kweli na kuweka juhudi kwa kujenga jamii ya undugu na ya haki kwa wema wa wote.


Fr Ndega

sexta-feira, 16 de dezembro de 2022

KUWA WASHIRIKA WA MUNGU

 

Tafakari kutoka Is 7: 10-14; Rm 1: 1-7; Mt 1: 18-24




 

    Katika safari yetu kuelekea Krismasi, ni muhimu sana kutafakari kuhusu Mtakatifu Yosefu aliyekuwa mtu mkimya bali alikuwa na ushiriki mkubwa katika kuhakikisha usalama na ulinzi kwa Mwana wa Mungu aliyekuja ulimwenguni, dhaifu na mhitaji. Ingawa Mungu angeweza kuwaokoa wanadamu peke yake, alitaka kuchagua washirika kwa kutekeleza mpango wake kama alivyosema Mtakatifu Augustino, “Mungu alituumba bila sisi lakini hakutaka kutuokoa bila sisi”.

    Katika somo la kwanza nabii Isaya halikukataa uamuzi wa mfalme wa Yuda, yaani Ahazi ambaye akihisi kutishwa na uvamizi unaowezekana na uliokuwa karibu, aliamua kufanya mapatano ya kisiasa na kijeshi pamoja na Ashuru badala ya kumwomba Bwana ishara kama maonyesho ya imani katika uwepo na ulinzi wake. Lakini Mungu, hata akikataliwa, hajiachi kuzuiwa kuhusu mpango wake wa kuwaokoa watu wake na kwa sababu hiyo anatoa kuzaliwa kwa mtoto ambaye ataufanya ufalme huu kuwa imara, na kutoa mustakabali wa tumaini kwa watu wote. Tunaona katika mtoto huyo sura ya Yesu, ambaye anatuletea wokovu, akihakikishia kwamba uthabiti wa kweli hautokani na ulinzi wa kibinadamu bali kwa kumtumaini Mungu.

    Katika somo la pili, Paulo anahutubia Wakristo wa Rumi kwa kujijulisha mwenywe si kwa kutumia data yake binafsi ya masjala bali kutokana na utambulisho wake mpya uliozaliwa kutokana na mkutano na Yesu Kristo aliyemfanya kuwa mtume wa Mataifa. Utambulisho wake huu hautokani na sifa zake bali ni uchaguzi unaofanywa kwa upendo, zawadi ya neema ya Mungu. Ufahamu huu wa Mtume Paolo unatuimarisha katika safari yetu na kutufanya tuelewe kwamba sisi pia tunapendwa na Mungu nasi tu watakatifu kwa wito kwa ajili ya kuwa washirika wake katika kazi ya wokovu kama mashahidi wa upendo wake na uhuru wake.

    Injili inatujulisha mfano wa Yusufu ambaye anaitwa mtu mwenye haki, yaani, “aliyekuwa na sheria yote ya Bwana moyoni mwake”. Kwa sababu ya pendekezo la Mungu lenye changamoto kwa Mariamu, anaongozwa kufanya uchaguzi wa ajabu. Maria anapomweleza kuhusu hali aliyokuwa akikabili, anamhakikishia kwamba ilikuwa ni uingiliaji wa kimungu. Kisha, Yosefu alikuwa mbele yake si tu sheria ya Mambo ya Walawi, ambayo iliamuru kushutumu wanawake kama kwahali hii ya Mariamu, bali pia upendo aliokuwa nao kwa msichana huyo na uaminifu wa maneno yake, akikubali kuweka maisha yake hatarini ili mpango wa Mungu ukatimize kwa ajili ya wokovu wa watu wake.

    ‘Ndiyo’ ya Maria aliye huru na mkarimu ilikuwa imesubiriwa na Mungu ambaye alimtaka awe mtumishi wake na alikuwa amemwandaa kwa hili, lakini tunapaswa kukubali kwamba ili aishi ndiyo hii yake, zaidi ya neema ya Mungu, Mariamu pia alisaidiwa na ndiyo ya Yusufu. Kwa busara na ukimya wake, anafanya ndoto ya wanandoa itimie kwa wakati zaidi na kumpa Mungu nafasi sahihi ya kutenda. Kwa hakika, pamoja na Yusufu Mungu hatoi Mariamu tu bali pia malaika wa kumsaidia “kuifuata njia ya upendo na kuiacha ile ya Sheria”. Hivyo toleo la Maria kuhusu ukweli wa lililotokea limethibitishwa. Wote wawili wameongozwa katika njia ifaayo ili kazi hii iliyozaliwa na mpango wa kimungu isishindwe kwa sababu ya magumu ya kibinadamu.

    Watu hawa wawili wanaotembelewa na Mungu, katika unyenyekevu na udogo wao hufanya maisha yao ya kila siku kuwa yenye kuzaa matunda, wanakuwa vyombo vya heshima vilivyotumiwa na Mungu kwa hiari katika kazi kuu ya wokovu. Ushuhuda wao unatusaidia kuelewa ni nini njia ya Mungu na ni nini hasa kinachompendeza. Hata kama hawakuelewa kazi yao ingekuwaje hapo mwanzo, hawakuweka vikwazo katika njia ya mipango ya Mungu.Vivyo hivyo lazima iwe mwitikio wetu wa kila siku kwa wito wa Mungu. Hatuhitaji kuelewa mara moja kazi yetu inapaswa kuwa nini. Tunahitaji kupatikana na kuwa tayari kwa kila kitu, tukimwaminia Mungu kama Mariamu, Yusufu na wengine wengi walivyofanya.


Fr Ndega

ESSERE COLLABORATORI DI DIO

 

Riflessione a partire da Is 7, 10-14; Rm 1, 1-7; Mt 1, 18-24



 

    Nel nostro cammino verso il Natale non poteva mancare la figura di San Giuseppe, un uomo silenzioso ma di forte partecipazione nel garantire sicurezza e protezione al Figlio di Dio venuto nel mondo, fragile e bisognoso.  Anche se Dio poteva salvare gli uomini da solo, ha voluto scegliere collaboratori per portare a compimento questo suo piano. Su questo diceva St Agostino, “Dio ci ha creato senza di noi ma non ha voluto salvarci senza di noi”.

    Nella prima lettura il re di Giuda, Acaz viene rimproverato dal profeta perché, sentendosi minacciato da una possibile ed imminente invasione, decide di fare una alleanza politico-militare con l’Assiria, invece di chiedere un segno al Signore, esprimendo fiducia nella sua presenza e protezione. Ma Dio anche se rifiutato, non si lascia fermare nel suo piano di salvare il suo popolo e per questo suscita la nascita di un discendente che renderà questo regno stabile, offrendo un futuro di speranza a tutto il popolo. Vediamo in questo discendente l’immagine di Gesù, che ci porta la salvezza, assicurando che la vera stabilità non viene dalle protezioni umane ma dalla fiducia in Dio.

    Nella seconda lettura Paolo si rivolge ai cristiani di Roma presentando se stesso non a partire dai dati anagrafici ma dalla sua nuova identità nata da un incontro con Gesù Cristo che lo ha costituito apostolo delle genti. Questa sua identità non viene dai suoi meriti ma da una scelta fatta per amore, un dono dalla grazia di Dio. Questa consapevolezza dell’Apostolo ci motiva nel nostro cammino e ci fa capire che anche noi siamo amati da Dio e santi per vocazione per diventare i suoi collaboratori nell’opera della salvezza, come testimoni del suo amore e della sua gratuità.

    Il vangelo ci introduce la figura di Giuseppe che è chiamato uomo giusto, cioè, “uno che aveva nel cuore tutta la legge del Signore”. Lui, a motivo della proposta sconcertante di Dio fatta a Maria, viene portato a fare una scelta drammatica. Quando Maria gli racconta la situazione che stava vivendo, gli assicura che si tratta di uno intervento divino.  Davanti a sé Giuseppe aveva non solo la legge del Levitico, che richiedeva di denunciare donne nella situazione di Maria, ma anche l’amore che sentiva per quella fanciulla e la sincerità delle sue parole, accettando di mettere la sua vita in gioco affinché il sogno di Dio venisse concretizzato per la salvezza del suo popolo.

    Il ‘Sì’ libero e generoso di Maria era già atteso da Dio che l’ha voluta come sua serva e l’aveva preparata per questo, ma dobbiamo ammettere che per vivere questo suo sì, a parte la grazia di Dio, Maria è stata aiutata anche dal sì di Giuseppe. Con la sua prudenza e silenzio, fa che il sogno della coppia guadagni in tempo e dà a Dio la giusta opportunità d’agire. Infatti, accanto a Giuseppe Dio provvede non solo Maria ma anche un angelo per aiutarlo a “seguire la via dell’amore e abbandonare quella della Legge”. Così viene confermata la versione di Maria sulla verità dei fatti. Entrambi sono stati guidati nella via giusta affinché quest’opera nata da una iniziativa divina non venga meno a motivo delle difficoltà umane.

    Queste due persone visitate da Dio, nella loro semplicità e piccolezza fanno della loro quotidianità una esistenza feconda, diventano nobili strumenti usati volentieri da Dio nella grande Opera della salvezza. La loro testimonianza ci aiuta a capire ciò che è lo stile di Dio e ciò che veramente piace a lui. Anche se non hanno capito quale sarebbe stato il loro compito all’inizio, non hanno messo ostacoli ai piani di Dio. Così deve essere la nostra risposta quotidiana alla chiamata divina. Non bisogna capire subito qual deve essere il nostro compito. Bisogna essere disponibili e mettere la nostra vita in gioco, fidandoci di Dio come hanno fatto Maria, Giuseppe e tanti altri.

 

Fr Ndega

Revisione dell'italiano: Giusi

sexta-feira, 2 de dezembro de 2022

LET US PREPARE THE WAYS FOR THE LORD

 

Reflection on Is 11: 1-10; Rom 15: 4-9; Mt 3: 1-12




     This liturgy continues to invite us to welcome the Lord who comes to bring us salvation. We are invited to prepare ourselves well so that we can receive the Messiah at any time. The Advent season helps us to realize that for a very good preparation a change of heart is necessary, in a completely new way. The words of the prophet Isaiah fill people's hearts with great hope because they announce the wonderful situation that their Lord is preparing for their lives. God leads his people in his light and glory. He promised them a saviour who will bring them peace and act with justice and love, especially regarding the poor and the suffering. This redeemer is Christ, who is God with us.

    Paul writing to the Romans confirms that Christ fulfilled the promises made to the ancestors as the faithful servant of God. His presence on earth has been an expression of God's mercy to all, even to the Pagans who were considered as the ones who have no chance of salvation. Anyone who identifies himself with Christ as his follower should have the same his feelings. Thus, the faith and fellowship of the Romans and all Christians become a concrete way of propagation of good news of the gospel by producing good crops for the glory of God. This is the truth of our identity.

    The Gospel speaks of John the Baptist who appears in the desert proclaiming the Word of God. John's ability comes from the experience of this Word because no one can give evidence of something without having the opportunity to experience this thing. John begins his work in the desert. In the Bible the desert is a special place to experience of the Word of God. In that place, many leaders lived an inner experience of God to prepare themselves for the work of leading God's people according to his guidance and his will. John the Baptist is the last prophet and considered the greatest of all prophets.

    The coming of John the Baptist follows the plan of God who has a perfect time for everything. As John is the link between the Old and New Testaments, his work announces that the Messianic times have begun. He is just a voice that prepares the ways of the Lord. First of all, he announced the penance to the people in order to welcome the kingdom of God that is near us. This kingdom means the presence of God among his people in Jesus’ person and the welcome to this kingdom happens when we give permission to God's work in our lives.

    Besides the words, John used also the baptism to prepared the people to receive the Messiah. Through this sign he announced God's mercy available to everyone because it is God's plan that his salvation can reach all. John's baptism could not remove people's sins and John realized that well. So, if this baptism did not have the power to remove sins, why did John use this sign? It is because he wanted to help the people to recognise their sins and open their hearts to God’s mercy. It was a preparation to the new baptism that the Messiah will use as the external gesture of the passage from sin to grace and from death to new life.

    The baptism of John is different from the baptism of Jesus, but both are opportunities to live a new life. In our case, new life is the gift of Christ and the result of his mission. Christian baptism, beyond of the remission of sins, guarantees participation in God's own life. Baptism is the first of the three sacraments of initiation followed by Confirmation and the Eucharist for a complete Christian initiation. Our baptism is an outward sign of death to sinful life, and of resurrection to new life in Christ who is victorious over sin and death. He is a true light that enlightens everyone. Through this process we have become children of light so that we walk in the light of God every day of our lives.

    The Advent season helps us to prepare ourselves to celebrate the birth of Jesus. John's humble life is an invitation to us to do the same so that our lives can please God. The things John said to the Pharisees and Sadducees are also important for us: about repentance, words are not enough; we have to show the real signs of our change, otherwise we will not be able to prepare ourselves properly to welcome Jesus. There are many obstacles to remove from our lives with the help of God's mercy. So, let's take this good opportunity to celebrate the sacrament of Reconciliation (and penance) and live in a new way our relationship with God and others.


Fr Ndega

TUTENGENEZENI NJIA YA BWANA

 

Kutafakari kuhusu Is 11: 1-10; Rm 15: 4-9; Mt 3: 1-12




     Liturgia hii inaendelea kutumwalika kumkaribisha Bwana anayekuja kutuletea wokovu. Tunaalikwa kujiandaa vizuri ili tuweze kumpokea Masiya wakati wowote. Wakati wa Majilio unatusaidia kutambua kwamba kwa matayarisho kamili ni lazima mabadiliko ya moyo, kwa njia mpya kabisa. Maneno ya nabii Isaya yanaijaza mioyo ya watu kwa matumaini makubwa kwa sababu yanatangaza hali ya ajabu ambayo Bwana wao anaandaa kwa maisha yao. Mungu anawaongoza watu wake katika mwangaza na utukufu wake. Anawaahidi mkombozi ambaye atawaletea amani na kutenda kwa haki na upendo hasa kuwahusu maskini na wanaoteseka. Mkombozi huyo ndiye Kristo, aliye Mungu pamoja nasi.

    Paulo akiwaandikia Waroma anathibitisha kwamba Kristo alitimia ahadi zilizowafanyiwa mababu kama mtumishi mwaminifu wa Mungu. Uwepo wake duniani umekuwa maonyesho ya huruma ya Mungu kwa wote hata kwa Wapagani ambao walichukuliwa kama wasio na nafasi ya wokovu. Yeyote anayejitambulisha na Kristo kama mfuasi wake anapaswa kuwa na hisia sawasawa na yeye. Hivyo imani na ushirika wa Waroma na Wakristo wote wakuwa uenezi wa habari njema kwa kuzaa mazao mazuri kwa utukufu wa Mungu. Huu ndio ukweli wa utambulisho wetu.  

    Injili inaongelea Yohane Mbatizaji anayeonekana jangwani kwa kutangaza Neno la Mungu. Uwezo wa Yohane unatokana na uzoefu wa Neno hili kwa maana hakuna mtu hata mmoja aweze kutoa ushahidi wa jambo fulani bila kupata nafasi ya kufanya uzoefu wa jambo hili. Yohane anaanza kazi yake jangwani. Katika biblia jangwa ni mahali maalum pa uzoefu wa Neno la Mungu. Katika mahali huko viongozi wengi waliishi uzoefu wa ndani wa Mungu ili kujiandaa kwa kazi ya kuwaongoza Watu wa Mungu kulingana na mwongozo wake na tena kwa matakwa wake. Yohane Mbatizaji ndiye nabii wa mwisho na kufikiriwa kama mkuu wa manabii wote.

Kuja kwake Yohane Mbatizaji kunaufuata mpango wa Mungu ambaye ana wakati kamili kwa kila kitu. Kama Yohane ni kiungo kati ya Agano la kale na la Jipya, kazi yake inatangaza kwamba nyakati za Masiya zimeanza. Yeye ni sauti tu ambayo inatayarisha njia za Bwana. Kwanza kabisa aliwatangazia watu watubu ili kuukaribisha ufalme wa Mungu ulio karibu nasi. Ufalme huu unamaanisha uwepo wa Mungu miongoni mwa watu wake kupitia nafsi ya Yesu na makaribisho kwa ufalme huu yatokea tunapotoa ruhusa kwa tendo la Mungu maishani mwetu.

Zaidi ya maneno, tena Yohane aliwatayarisha watu kumpokea Masiya kwa ubatizo. Kupitia ishara hii alitangaza huruma ya Mungu iliyopatikana kwa kila mtu kwa sababu ni mpango wa Mungu kwamba wokovu wake ufikie wote. Ubatizo wa Yohane haukuweza kuziondoa dhambi za watu naye Yohane alitambua hilo vizuri. Basi, je ikiwa ubatizo huu haukuwa na uwezo wa kuziondoa dhambi, kwa nini Yohane aliitumia ishara hii? Ni kwa sababu alitaka kuwasaidia watu kukiri dhambi zao na kufungua moyo kwa huruma ya Mungu. Ubatizo huu ulikuwa maandalizi kwa ubatizo mpya na kamili atakaotumia Masiya kama ishara inayoonekana mapito kutoka dhambi kwenye neema na kutoka mauti kwenye maisha mapya.

Ubatizo wa Yohane ni tofauti na ubatizo wa Yesu, lakini yote mbili ni nafasi ya kuishi maisha mapya. Kwa upande wetu maisha mapya ni zawadi ya Kristo na matokeo ya utume wake. Ubatizo wa Kikristo, pamoja na maondoleo ya dhambi, unadhamini ushiriki katika uzima wa Mungu mwenyewe. Ubatizo ni wa kwanza kati ya sakramenti tatu za mwanzo ukifuatiwa na Kipaimara na Ekaristi kwa uzoefu wa mwanzo katika safari ya kikristo. Ubatizo wetu ni ishara ya nje ya kufa kwa maisha ya dhambi, na ya kufufuka kwa maisha mapya katika Kristo aliye mshindi dhidi ya dhambi na mauti. Yeye ni mwanga wa kweli unaomfafanua kila mtu. Kupitia mwendo huu tumekuwa wana wa nuru ili tutembee katika nuru ya Mungu kila siku ya maisha yetu.

Kipindi cha Majilio kinatusaidia kujiandaa kusherehekea kuzaliwa kwa Yesu. Maisha ya unyenyekevu ya Yohane ni mwaliko tutende kama yeye alivyo ili maisha yetu yaweze kumpendeza Mungu. Mambo Yohana aliyowaambia mafarisayo na masadukayo ni muhimu pia kwetu: kuhusu kutubu hayatoshi maneno; tunapaswa kuzionyesha ishara halisi za mabadiliko yetu, vinginevyo hatutapata kujitayarisha ipasavyo kwa kumkaribisha yesu. Kuna vikwazo vingi vya kuondoa katika maisha yetu kwa msaada wa huruma ya Mungu. Basi, tuchukue nafasi hii nzuri kuadhimisha sacramenti ya Upatanisho (na kitubio) na kuishi kwa njia mpya uhusiano wetu na Mungu na wengine.


Fr Ndega