sábado, 29 de setembro de 2018

WANAFUNZI WENGINE WA YESU



Kutafakari kutoka Hes 11:25-29; Mk 9:38-43, 45, 47-48

Mungu hawabagui watu kwa maana anapenda na katika upendo hakuna ubaguzi. Matarajio yake ni watu wake wote wawe manabii, wakisikiliza neno lake na kuongea katika jina lake. Kupitia Roho wake Mtakatifu, anatuimarisha tuwatendee wote mema kulingana na mapenzi yake, akidhibitisha kwamba upendo wake hauna mpaka. Mbele ya Mungu hakuna mtu wa heshima kuliko wengine. Yeye hakubali umaarufu au ubaguzi, bali anatarajia ahadi kwa njia yake ya kufikiri na kutenda. Anatenda hivyo kwa sababu ya upendo Wake mkubwa.

Mtakatifu Yakobo anakosoa kwa nguvu watu wanaokuwa tajiri kwa njia ya udhalimu kwa kukanusha mishahara kwa wafanya kazi. Mungu anapinga hali ya udhalimu na kosa la usawa kati ya watu. Yeye ndiye tayari kutenda kwa ajili ya walio waathirika wa udhalimu na kumwomba kwa imani. Ukosoaji huu unatumika pia kwa wote ambao wajikabidhi katika mali ambayo anayo kuliko riziki ya Mungu. Mtu anapokufa hawawezi kuchukua mali chochote pamoja naye; kwa hivyo tabia ya kuongeza mali kwa nafasi yake mwenyewe haina maana.

Wanafunzi wa kwanza walijaribu kumkataza mtu fulani ya kufanya mwujiza kwa jina la Yesu kwa sababu hakuwa mmoja wao. Walifanya hivyo kwa mamlaka gani? Yesu hakukubaliana na tabia hii na kuwaambia kwamba mtu anayetenda mema kwa jina lake (Yesu) hawezi kumtendea vibaya. Kisha akiendelea kwa mafundisho yake, alisema kwamba watu wanaosaidia wafuasi wake watapokea tuzo kwa sababu ya utambulisho wake na wale waliotumiwa kwa jina lake. Yesu anawakumbusha pia kwamba mambo yote wanayofanya wale wanaomfuata yapaswa kuwaimarisha watu kumwamini Kristo. Ni lazima kuepuka Kashfa kwa sababu tabia hii inavuruga imani na kukana utambulisho wa wanaomfuata Yesu.

Tumetafakari kuhusu ugumu wa wanafunzi wa Yesu kuelewa na kuyapokea mafundisho yake. Kujaribu kumkataza mtu fulani ambaye alifanya mema kwa jina la Yesu ni ishara ya ugumu ya kumfahamu Yesu na mapendekezo yake. Maana ya kuwa mfuasi wa kweli wa Yesu siyo maneno tu, bali ni matendo mema hata kama yeyote hahudhurii kikundi. Badala ya kuwakataa wengine ambao wanatenda mema kwa jina la Yesu, wanafunzi wake wanapaswa kujikataa wenyewe. Kuwa mwanafunzi wa Yesu kunamaanisha kuishi imani iliyoonyeshwa kwa matendo. Kwa Yesu wale wanaosikiliza Neno la Mungu na kuweka vitendoni ndio mama na ndugu zake na wanafunzi wake. Hivyo yule aliyetenda mema kwa jina la Yesu anaweza kufikiriwa kama mwanafunzi wake. Mtazamo wa wanafunzi ndio tofauti na ule wa mwalimu wao kwa sababu lengo lao sio kukaribisha bado bali ubaguzi.

Kitu muhimu katika dini au imani ni matendo na siyo maneno tu. Matendo husema zaidi kuliko maneno. Wakristo wa kwanza ndio mfano halisi kwa sababu waliweza kuwavutia wengine si kwa maneno, bali kwa njia yao ya maisha. Kuhusu hao watu walisema: “Mwone kama wanavyopendana”! hali hii iliwezekana kwa sababu ya upendo wao ulionyeshwa kupitia ridhaa wao kwa wao, kushiriki pamoja, uvumilivu katika maombi pamoja na unyenyekevu wa moyo. Kuhusu hayo Sinodi ya Afrika imesema: “Sharti muhimu la kuhubiri ni ushuhuda wa maisha”. Mwanafunzi wa kweli wa Yesu hawezi kuwa na ubaguzi na kuamini kuwa watu wa kundi lake pekee ama kanisa lake ndiyo wanafunzi pekee wa Yesu na kwamba ndio hao peke yao ambao wameokolewa.

Hatuwezi kufikiri kwamba Yesu ni mali yetu. Ikiwa tunahisi karibu na Yesu, hatuwezi kuishi mbali sana na ndugu zetu, kufungwa kabisa kwa hali kandokando yetu na hata kufikiri kwamba tunakuwa na mamlaka ya kuwazuia wengine watende kwa jina la Yesu. Tuko mbele ya kosa kubwa. Tuwe macho kuhusu baadhi ya uzoefu ambao unatufungua kwa Mungu lakini unatufunga kwa wengine. Ikiwa imani yetu haituongozi kukutana na wengine na kutambua mema ambayo wanaweza kufanya imani yetu ni utenganisho. Basi, ili Mungu atufundishe kutambua mwendelezo wa kazi zake mbele ya matendo mema ya Wakristo na kusaidiana kwa wema wa wote.

Fr Ndega

sábado, 22 de setembro de 2018

YATOSHA KUWA KAMA WATOTO WADOGO



Hek 2:12.17; Yak 3: 16-4:3; Mk 9,30-37



         Andiko la kitabu cha Hekima ya Sulemani linaongea kuhusu ushuhuda muhimu wa mtu mwenye haki na upinzani wa wale ambao hawaukubali ushuhuda wake na kumtendea vibaya, hata kwa kupanga kifo chake. Hali hii inatokea kwa sababu ya uaminifu yake kwa Mungu. Mambo yote ambayo washtaki wanasema dhidi ya mwenye haki yanakuwa uthibitisho wa utambulisho wa mtu huyo aliye mwana wa Mungu naye Mungu mwenyewe atamtegemeza na kumtetea dhidi ya adui zake. Huu ndio mfano wa Kristo ambaye aliteseka sana kwa sababu ya uaminifu wake kwa mpango wa Mungu na kwa kujisalimisha kwake aliupata wokovu hata kwa wale waliomkandamiza.  

         Andiko la pili linasema kuwa hekima ambayo inasababisha kujua kamili inatoka kwa juu kwa sababu ni Mungu mwenyewe chanzo cha hekima ya kweli. Mtu anayeongozwa na hekima hii anaweza kuchagua vizuri na kuwa chombo cha amani, cha umoja na cha ushirika katika jumuiya, na kuwa tayari kusikiliza maneno ya wengine na kutenda mema kwa ajili yao.

         Injili ni mwendelezo wa tangazo la Petro kuhusu utambulisho wa Yesu na mwaliko wa Yesu mwenyewe ili wafuasi wake wamfuate katika kujisalimisha kwake ili wapate uzima. Yesu alitambua kwamba walihitaji kujua maana kamili ya utambulisho wake kama Masihi na kuyafahamu vizuri mapendekezo yake. Kwa hivyo alitumia nafasi maalum katika mahali pa faragha ili kuwafundisha. Kwa nini hakutaka watu wafahamu alipo pamoja na wanafunzi wake? Kwa sababu wazo wa Masihi ambao watu walikuwa nao ulikuwa mbali sana na utambulisho wake na kwa hivyo lilikuwa hatari kwa malezi ya wanafunzi wa Yesu.  

     Basi, bila kusukumwa na uwepo wa watu, Yesu alijiona mwenye heri kabisa ili kuwaongelea kwa uwazi kuhusu mateso, kifo na ufufuko wake, lakini walionekana mbali sana na mwalimu. Hawakuelewa tena kwa sababu walishughulika kwa mawazo na nia tofauti. Kwao ilikuwa muhimu kujadili juu ya msimamo na upendeleo kuliko kuandamana na mwalimu wao kwenye kujisalimisha. Kwa uvumilivu na kwa kutumia mtoto kama mfano, yeye aliwasaidia kufahamu ufunuo wake na masharti ya kumfuata. Yule anayeamua kumfuata Yesu anapaswa kuongoza maisha yake kulingana na mantiki tofauti na mawazo wa dunia. Ikiwa katika nafasi iliyopita Yesu aliwaomba kuyatoa maisha ili kuyaokoa, hapo aliwaomba kuwa wa mwisho na mtumishi ili kuwa wa kwanza.

          Yesu anadhihirisha utambulisho wake kama Mwana wa Adamu (mtu). Katika Agano la Kale tunakuta maneno haya katika vitabu vya nabii Danieli na Ezekieli. Kulingana na Danieli maneno haya yaongea kuhusu hali ya utukufu wa yule ambaye atakuja siku ya mwisho (Dan 7:13). Kulingana na toleo la Ezekieli maneno Mwana wa Mtu yanatumiwa na Mungu kwa uhusiano na nabii wake na kuonyesha hali ya udhaifu na kifu cha binadamu (Ezk 2:1, 3:1.25, 17:2). Basi, hii ni maana iliyotumiwa na Yesu ili kuongea kuhusu utambulisho wake kwa uhusiano na hali ya binadamu na fumbo la mateso, kifo na ufufuko wake ambalo lilisababisha ubinadamu mpya. Hivyo, tunafahamu maana ya ufundishaji wa uvumilivu  wa Yesu ili kuwasaidia wanafunzi wake walio na ujinga na udhaifu wa akili.

        Watoto wadogo wana nafasi maalum moyoni mwa Yesu. Alisema kwamba Ufalme ni wao naye mtu anayetaka kuingia katika Ufalme huu anapaswa kuwa kama watoto. Basi,  Yesu anatuongelea kwamba ni lazima mabadiliko ya mawazo na tabia ili tuweze kumfuata kwa kweli. Mfano wa watoto wadogo ni maalum kwetu kwa sababu hao wanatusaidia kutafuta muhimu zaidi ya maisha, yaani ukweli, unyenyekevu wa moyo, kuamini, n.k. Kama vile wanafunzi wa kwanza sisi pia tuko na ugumu wa kufahamu mambo yote kumhusu Yesu na mapendekezo yake, lakini tukimruhusu, yeye anaweza kufungua akili zetu na kubadilisha moyo wetu ulingane na matarajio yake. Siku ya leo yeye anatualika kwa uhusiano wa kibinafsi naye. Kupitia uhusiano huu peke yake tunaweza kuingiza utambulisho wake na kufahamu maana ya ushiriki wetu katika kazi yake ya ukombozi. Mfano wa watoto wadogo utusaidie kufahamu nia ya Yesu kuhusu maisha yetu na kukubali mapendekezo yake kwa kutumia nguvu zetu kwa ajili yake “mpaka kifo, mpaka uzima”.

Fr Ndega


É SUFICIENTE SER COMO AS CRIANÇAS



Sab 2, 12,17; Tiago 3, 16-4.3; Mc 9:30-37


      O texto do livro da sabedoria fala sobre o testemunho da pessoa justa e a oposição daqueles que não aceitam o seu testemunho e lhe tratam mal, inclusive tramando a sua morte. Isso acontece por causa de sua fidelidade a Deus. Tudo o que os adversários dizem torna-se uma confirmação da identidade daquele que sente filho de Deus e o próprio Deus virá em seu socorro, salvando-o de seus inimigos. Esta é uma imagem de Cristo que sofreu muito por causa de sua fidelidade ao plano de Deus e com o seu sacrifício trouxe a salvação até para aqueles que o oprimiam.

       O segundo texto nos fala que a sabedoria que traz o conhecimento perfeito vem do alto porque é o próprio Deus a fonte da verdadeira sabedoria. A pessoa que se deixa conduzir por essa sabedoria é capaz de fazer bem suas escolhas, tornando-se um instrumento de paz, unidade e comunhão na Comunidade; será sempre disposta a escutar os outros e a se doar pelo bem deles.

        O Evangelho continua a mensagem do domingo passado sobre a identidade de Jesus e o convite para segui-lo para obter a vida plena. Jesus percebeu que os seus discípulos precisavam conhecer o verdadeiro significado de sua identidade como Messias de Deus e entender bem suas propostas; Por esta razão, ele decidiu leva-los para um lugar longe do povo para ensiná-los. Jesus deseja estar a sós com os seus discípulos. Por que ele não queria que as pessoas soubessem onde ele estava com seus discípulos? Porque a ideia de Messias que as pessoas tinham era longe daquilo que era sua identidade e isso era perigoso para a formação de seus discípulos.

       Finalmente, sem a presença da multidão, Jesus se sente mais livre para falar a eles com a sinceridade do seu coração sobre o mistério do seu sofrimento, morte e ressurreição, mas eles pareciam distante do mestre. Eles não entenderam porque não estavam atentos; tinham outras motivações e pensamentos. Era mais importante para eles discutir posições e privilégios do que acompanhar o mestre para a total entrega de si. Pacientemente e pegando uma criança como exemplo, Jesus os ajudou a compreender a sua revelação e as condições para segui-lo. Quem decide seguir Jesus deve conduzir a sua vida segundo uma lógica diferente da mentalidade deste mundo. Se na última vez, ele disse que é doando a vida que se pode salvá-la, desta vez diz que é preciso ser o último e servo dos demais para poder ser o primeiro.

         Esta realidade revela a identidade do Mestre Jesus que se fez servo por amor. Ele se revela como Filho do homem por causa de seu envolvimento com a realidade humana. No antigo testamento encontramos esta expressão nos livros de Daniel e Ezequiel. De acordo com Daniel, este "Filho do homem" refere-se à glória daquele que virá no fim dos tempos (Dan 7:13). De acordo com a versão de Ezequiel, "filho do homem" é o título usado por Deus no relacionamento com seu profeta e expressa a condição frágil e mortal do ser humano (Ezek. 2,1, 3:1.25, 17,2). Assim, este é o sentido usado por Jesus para falar sobre sua identificação com a condição humana e o mistério da sua paixão, morte e ressurreição a partir do qual surge uma nova humanidade. Assim, entendemos a razão da pedagogia o paciente e criativa de Jesus em relação aos seus discípulos, "duros de coração lentos para crer".

        As crianças têm um lugar especial no coração de Jesus. Ele disse que o Reino de Deus pertence a eles e aqueles que querem entrar neste reino devem tornar-se como as crianças. Então, Jesus nos fala sobre a necessidade de mudança de mentalidade e atitude para que possamos segui-lo verdadeiramente. O exemplo das crianças é especial para nós porque nos ajudam a buscar o que é mais importante na vida, isto é, a verdade, a simplicidade de coração, a confiança, etc. Como os primeiros discípulos, nós também não compreendemos tudo sobre Jesus e suas propostas, mas se lhe damos permissão, ele pode abrir nossas mentes e transformar nossos corações para que sejam de acordo com suas expectativas sobre nós. Jesus nos chama para uma relação pessoal com ele e é somente através de uma relação assim que podemos assimilar sua pessoa e entender o que ele quer de nós, isto é, o sentido de nossa participação como seus colaboradores em sua missão Redentora. O exemplo dos "pequeninos" nos ajude a entender a intenção de Jesus sobre a nossa vida e a acolher a sua proposta, usando todas as nossas energias pela sua causa, "até à morte, até à vida".

Fr Ndega


BASTA ESSERE COME I BAMBINI



Riflessione su Sap 2, 12.17; Giac. 3, 16-4,3; Mc 9,30-37


       Il brano della Sapienza parla sulla testimonianza del giusto e della opposizione di coloro che non accolgono la sua testimonianza e lo trattano in modo cattivo, anche tramando la sua morte. Questo succede a causa della sua fedeltà a Dio. Tutto quello che dicono gli avversari diventa una conferma dell’identità di colui che si sente figlio di Dio e il proprio Dio verrà in suo soccorso, salvandolo dai suoi nemici. Questa è una immagine di Cristo che ha sofferto molto a causa della sua fedeltà al progetto di Dio e con il suo sacrificio ha portato salvezza anche per coloro che lo opprimevano.

        Il secondo testo ci comunica che la sapienza che porta la perfetta conoscenza viene dall’alto perché è Dio stesso la sorgente della vera sapienza. La persona che si lascia condurre da questa sapienza può fare bene le sue scelte, diventando strumento di pace, di unità e comunione nella comunità; sarà sempre disposta ad ascoltare gli altri e a donare se stessa per il loro bene.

     Il vangelo continua il messaggio della volta scorsa sull’identità di Gesù e l’invito a seguirlo per ottenere vita piena. Gesù ha percepito che i suoi avevano bisogno di conoscere il senso vero della sua identità come Messia di Dio e capire bene le sue proposte; per questo ha deciso di usare una opportunità speciale in un posto in disparte per insegnare loro. Perché non ha voluto che la gente sapesse dove era lui con i suoi? Perché l’idea di messia che la gente aveva era lontano dalla sua identità e per questo era anche pericolosa per la formazione dei suoi discepoli.

        Senza la presenza della folla, Gesù si sente più libero per parlare ai suoi con sincerità sulla sua sofferenza, morte e risurrezione, ma loro sembrano lontani dal loro maestro. Non capivano perché non erano attenti, avevano altre motivazione e pensieri. Per loro era più importante discutere circa posizioni e privilegi che accompagnare il maestro verso la totale consegna di sé. Con pazienza e prendendo un bambino come esempio, Gesù li ha aiutati a capire la sua rivelazione e le condizioni per seguirlo. Chi decide di seguire Gesù deve condurre la sua vita secondo una logica diversa dalla mentalità di questo mondo. Se nella volta scorsa, egli ha detto che è donando la vita che si può salvarla, questa volta dice che bisogna essere l’ultimo e servo degli altri per essere il primo.

        Questa realtà rivela l’identità propria del Maestro Gesù che si è fatto servo per amore. Lui si rivela come Figlio dell’uomo a causa del suo coinvolgimento con questa realtà. Nel Vecchio Testamento troviamo questa espressione nei libri di Daniele e di Ezechiele. Secondo Daniele questo “Figlio dell’uomo” riferisce alla gloria di colui che arriverà alla fine dei tempi (Dan 7:13). Secondo la versione di Ezechiele, “Figlio dell’uomo” è il titolo usato da Dio nei confronti del suo profeta ed esprime la condizione fragile e mortale dell’essere umano (Ez. 2,1, 3:1.25, 17,2). Quindi, questo è il senso usato da Gesù per parlare della sua identificazione con la condizione umana e il mistero della passione, morte e risurrezione da cui sorge una nuova umanità. Così, possiamo capire il senso della pedagogia paziente e creativa di Gesù nei confronti dei suoi discepoli, “stolti e lenti di cuore”.

       I bambini hanno un posto speciale nel cuore di Gesù. Egli ha detto che il Regno di Dio appartiene a loro e chi vuole entrare in questo regno deve diventare come loro. Quindi, Gesù ci parla sulla necessità di cambiamento della mentalità e atteggiamento affinché possiamo seguirlo veramente. L’esempio dei bambini è speciale per noi perché loro ci aiutano a cercare ciò che è più importante nella vita, cioè, la verità, la semplicità di cuore, il fidarsi, ecc. Come i primi discepoli anche noi non riusciamo a capire tutto su Gesù e le sue proposte, ma se gli diamo il permesso, egli può aprire la nostra mente e cambiare il nostro cuore perché sia secondo le sue aspettative su di noi. Gesù ci chiama a una relazione personale con lui ed è solo all’interno di una relazione che possiamo assimilare la sua persona e capire cosa vuole da noi, cioè, il senso della nostra partecipazione come suoi collaboratori nella sua opera redentrice. L’esempio dei “piccoli” ci aiuti a capire l’intenzione di Gesù sulla nostra vita e ad accettare le sue proposte, spendendo tutte le nostre energie a causa sua, “fino alla morte, fino alla vita”.

Fr Ndega

sábado, 15 de setembro de 2018

UAMINIFU WA MUNGU NI NGUVU YETU


Kutafakari kuhusu Isa 50:5-9; Yak 2,14-18 Mk 8:27-35


     Mtumishi wa Bwana anajiona kuimarishwa kwa sababu ya uhakika wa upendo na utunzaji wa Mungu daima maishani mwake. Uhakika huu unamfanya imara mbele ya mateso mengi. Yule ambaye anamtumainia Bwana habaki kuchanganyikiwa na mwenye udanganyifu kwa sababu “uaminifu wa Bwana ndio nguvu yetu”. Mtakatifu Yakobo anawaomba Wakristo wawe walio halisi katika njia ya kuamini. Imani inayoonyeshwa kwa maneno peke yake siyo kweli. “Maneno yatoweka hata ikiwa yanaonekana yawe na imani. Matendo yanaiweka halisi kwa kuifanya iwe iko na sasisha”. Basi, ndiyo matendo mema ambayo yadhihirisha ukweli wa imani yetu. Madre Teresa wa Kaukuta alikuwa na haya ya kusema: “Kila tendo la upendo linalofanyika kwa moyo linaweka halisi imani kwa kumkaribia Mungu”.

      Yesu alikuwa anatembea pamoja na wanafunzi wake. Walipofika karibu na Kaisaria Filipi aliwauliza maswali kuhusu utambulisho wake kulingana na mtazamo wa watu. Majibu yalikuwa ishara ya kwamba mawazo kuhusu Yesu hayakuwa wazi sana kwa upande wa watu. Ingawa hayakuwa wazi kwa watu, ni lazima kuwa tofauti kwa mitume kumi na wawili, kwa sababu kwa Yesu haikuwa muhimu sana yale ambayo watu walifikiri, bali imani na kukiri kwa wafuasi wake. Petro alidhihirisha yale ambayo wanafunzi wengine kumi na mmoja walijua pia: Yesu ni Masiya wa Mungu. Lakini hawakuweza kuitangaza habari hii kwa sababu ya kosa la maana kamili. Yesu alitambua kwamba wafuasi wake walihitaji kujua kwa kina maana ya utume wake kama Masiha na masharti kwa kumfuata kwa kweli.

        Mawazo ya wafuasi wa Yesu kuhusu Masiya yalifuata matarajio ya Wayahudi wengine, yaani, Masiya wa kisiasa atakayetumia nguvu zake za kimungu ili kuwakomboa Wayahudi toka ukoloni wa Warumi. Bila shaka Yesu alikataa mawazo hayo kwa kuonyesha njia tofauti ya kutimiza mpango wa Mungu, yaani kupitia mateso, kifo na kufufuka. Njia aliyochagua Yesu ni ile ya mtumishi wa Bwana wa nabii Isaya. Utambulisho wa mtumishi huyo ni kuwa makini kwa sauti ya Mungu ili aweze kufanya mapenzi yake kwa kutumikia kabisa. Kwa kufanya mapenzi ya Mungu mtumishi huyo alipaswa kuteseka na kufa, lakini alisimama upande wa Mungu ambaye alimsaidia akimfanya mshindi. Itikio la Petro lilidhihirisha upinzani dhidi ya njia ya maisha Yesu aliyochagua ili atimize mapenzi ya Mungu. Uamuzi wa Yesu ulikuwa katika ushirika na Baba yake na upinzani dhidi ya njia hii ni upinzani dhidi ya mapenzi ya Mungu.

        Wanafunzi wa kwanza walihitaji mwendo wa muda mrefu ili kujifunza kumhusu Yesu na kuyafahamu mapendekezo yake sawasawa. Yesu alimkemea Petro lakini alimwalika afuate mtazamo wa Mungu ili awe mwanafunzi wa kweli. Kidogo kidogo wote walitambua kwamba kwa kujitoa kama Yesu alivyo, walipaswa kuzifuata hatua tatu, yaani, kujikana wenyewe, kuichukwa misalaba yao na kumfuata Yesu. Kwa maneno mengine, walipaswa kuyabadilisha maisha yao kabisa. Wale ambao hukutana na Yesu hawakubaki walivyo na hawawezi kumwomba Yesu atende kulingana na mapendekezo yao. Mwendo wapaswa kuwa tofauti. Kwa kumfuata Yesu kweli tunapaswa kupatikana kwa mambo yote kwa ajili ya ufalme wa Mungu kwa kuyaingiza mapendekezo ya Yesu. Tunapaswa kufananisha maisha yetu kulingana na njia ya Yesu ya kuishi  na kuchukua msalaba kama yeye alivyo.


     Injili siku ya leo inatusaidia kutafakari kuhusu njia ambayo tumechagua ili kumfuata Yesu. Je, hii ni njia ya kweli? Tunatambua kwamba Kumfuata Yesu hakuuleti upendeleo au hadhi, bali mateso na kujisalimisha kwa ajili ya injili. Basi, yeyote ambaye anataka kuishi kwa shwari na bila ahadi hawezi kumfuata Yesu. Yeyote ambaye anatamani kumfuata Kristo bila msalaba hatamfuata Kristo kwa kweli kamwe. Kupitia mambo hayo tunaweza kujiuliza maswali: Je, Kristo gani tumemfuata? Mawazo au kitu gani tunahitaji kujinyima bado ili tuweze kumfuata Yesu kikamilifu? Maisha yetu ya kawaida ni ishara ya kwamba tumekuta hazina yetu ya kweli? Tuishi wito wetu wa wanafunzi wa Yesu kwa shauku na furaha kwa sababu Mungu ndiye mwaminifu na kuwa tayari daima kutusaidia hasa wakati tuko na ugumu wa kubeba msalaba wetu. Tumwaminie yeye kwa sababu uaminifu wake ni nguvu yetu.

Fr Ndega

sábado, 8 de setembro de 2018

TUFANYE MAMBO YOTE VEMA



Kutafakari kutoka Isaya 35:4-7; Yak 2:1-5; Mk 7: 31-37


       Katika andiko la kwanza, nabii Isaya anatangaza wakati ujao umejaa tumaini kwa sababu Mungu atatembelea watu wake kama mwokozi na kuwatendea mambo makuu. Hali yote kandokando yao na miongoni mwao itabadilika kuwa ni nzuri, hasa hali ya maskini na wengine walio na shida ya afya. Ahadi hii ya kimasiya, Mungu alitimiza duniani kupitia Mwanawe Yesu Kristo ambaye aliwapa wote uwezo wa kuishi maisha mapya na mazuri.

      Katika andiko la pili Yakobo anawaalika Wakristo kushinda tabia ya ubaguzi katika jumuiya kwa kuthamini uwepo wa kila mtu bila kufikiria msimamo wake katika jamii. Kipaumbele ya jumuiya inapaswa kuwa maskini kwa sababu ndio wenye heri wa Mungu nao watapokea ufalme. Jumuiya za Kikristo haziko ili kufuata mawazo wa jamii bali kutenda kwa njia ya kinabii kulingana na injili. Utabiri wao utaonyeshwa wakati zinapopata kuwakaribisha na kuwanganisha katika uzoefu wake wote hasa wale ambao wanakataliwa.

        Katika injili, matendo ya Yesu yanatambuliwa na watu ambao walitangaza, “amefanya yote vyema: amewajalia viziwi kusikia, na bubu kusema”. Uwepo wa Yesu umeleta wakati mpya ulimwenguni. Katika Yeye ufalme wa Mungu umekuwa hali halisi, ilipatikana kwa wote. Wakati Yesu aliutangaza ujumbe wake katika sinagogi ya Nazareti, mahali alipolelewa, alikataliwa. Lakini alikaribishwa sana katika upande wa ziwa Galilaya, mahali panapoitwa Dekapoli - yaani miji kumi. Kulingana na toleo la Mathayo, Galilaya lilifikiriwa “nchi ya watu wa mataifa”. Uwepo wa Yesu uliwafanya watu waliokaa “gizani” waone mwanga mkubwa.

        Basi, ingawa watu hawa walikuwa na lugha na desturi tofauti na Wayahudi wa Yudea, walimtarajia na kumkaribisha Masiya kwa hamu sana. Injili ya Marko inasisitiza kipengele hiki kwa sababu iliandikwa kwa Wakristu wa huko Roma na lengo la injili hii ni kujibu kwa swali “Yesu ni nani?”. Jibu kwa swali hili tunakuta katika wakati wa mwisho wa maisha ya Yesu msalabani kutoka midomo ya jemadari mmoja wa Roma: “Kweli mtu huyu alikuwa Mwana wa Mungu!”

        Kama Mwana wa Mungu, lengo la Yesu ni kutangaza wokovu wa Mungu si kwa watu fulani tu, bali kwa wote. Yesu alikuwa Myahudi, bali hakuwa mali ya Wayahudi. Ishara zilizotumiwa na Yesu zilidhihirisha kwamba wokovu wa Mungu si mpango kwa wakati ujao tu, bali umekwisha anza katika historia kwa wote. Wakati tunaongea kuhusu “watu waliochaguliwa” tunamaanisha mpango wa hekima ya Mungu ambaye anatumia baadhi ya watu ili kufikia wengine kwa urahisi.

     Hivyo, kutoka Waisraeli Yesu na washirika wake walifikia wasio na Wayahudi pia wakitangaza habari njema ya injili. Mtu yule aliletwa kwa Yesu alikuwa na matatizo mawili, yaani, alikuwa bubu na kiziwi. Aliteseka sana na mara nyingi alikuwa mpweke kwa sababu hakuweza kuwasiliana na wenzake kila alichofikiri au kutamani, na wengine pia hawakuweza kuzungumza naye. Alitamani kukutana na Yesu na kupata maisha mapya ili kuishi uhusiano mwema na wengine. Kabla ya kufanya mwujiza Yesu alimwalika kuenda mahali pa faragha kwa sababu hakutafuta kuwa maarufu wala watafsiri muujiza wake kwa njia siyo kweli. Muujiza wa kwanza Yesu anaotaka kutenda katika maisha ya yeyote ndio kuwa na uhusiano wa ndani nawe. Yesu anatazama juu mbinguni kwa maana ya ushirika wake na Baba aliye wa pekee aliyemwezesha kumponya Bubu kiziwi. Hivyo, mkutano na Yesu kwa uhusiano wa ndani unaleta maisha mapya.

        Kazi ya Yesu ilikuwa kumwalika binadamu kutoka upweke na kutengwa kwa ushirika, yaani ushirika na Mungu na wenzake. Kama wafuasi wa Yesu tunaimarishwa na mfano wake na ishara zake. Ujumbe wetu unapaswa kuwa ni mwendelezo wa ujumbe wake na kama vile yeye tunaalikwa kufanya mambo yote vyema, yaani matendo yetu na mahusiano yetu yapaswa kufanya watu waishi maisha mapya. Yesu anatualika kwa uhusiano naye kwa faragha ili kutuponya kwa maana sisi tu kama mtu bubu na kiziwi, yaani tuna ugumu wa kusikiliza Neno la Mungu vizuri na kulitangaza kwa uaminifu. Matokeo wa uhusiano wetu na Bwana yatakuwa ni matunda mazuri kwa ajili ya utukufu wa Mungu na manufaa ya ndugu zetu. Ndiyo neema ya Mungu inayotenda ndani yetu ili tuweze kutenda kwa jina lake. Kama injili haina mpaka, tunaalikwa kushinda vikwazo ambavyo vinatuzuia kuwakaribisha wengine na kuwa na hisia mbele ya mahitaji yao. Ikiwa ni kweli uhusiano wetu na Bwana, tulime hisia na tabia kama yeye ili wengine wapate maisha mapya na sisi tuwe na furaha kamili.

Fr Ndega