domingo, 30 de agosto de 2015

UHUSIANO WA KIROHO NA MUNGU


Kutafakari kutoka Kum 4:1-2.6-8; Mk 7:1-8.14-15.21-23

     Mungu aliwapa watu wake Amri zake na akawafundisha njia ya kuzishika. Haziwezi kubadilishwa kulingana na mapenzi ya kibinadamu. Kama maonyesho makuu ya upendo na utunzaji wa Mungu, Yesu anatukumbusha muhimu zaidi ya sheria na anatufundisha kuishi na uhusiano wa kiroho na Mungu. Uhusiano huu uko juu ya sheria zote.  

       Kulingana na somo la kwanza, kupitia utumishi wa Musa, Mungu anawaalika watu wa Israeli washike amri zake kama miongozo kwa uzima. Baada ya kuwaweka uhuru kutoka Misri, Mungu alianzisha agano na watu hawa huko Sinai na Amri zilikuwa miongozo kama maonyesho ya matarajio yake kuhusu maisha ya watu wake. Kuishi kulingana na Amri kumekuwa umuhimu katika safari ya Watu wa Israeli ambao Sheria ni Neno la Mungu na Neno la Mungu ni Sheria. Wakati wao husema “Sheria ya Mungu ni kamilifu, faraja kwa roho”, wanamaanisha Neno la Mungu. Kuna uhusiano wa ndani kati ya Sheria na Neno, kwa sababu amri za Sheria zinaonyesha utunzaji na upendo wa Mungu anayeongea kuonyesha njia za ukombozi. Na tena zinadhihirisha utambulisho na hekima ya Watu ambao wanamtii Mungu wao. Utii kwa amri ni chanzo cha baraka kinachoelekeza kwa uhai, wakati uasi kwa hizo unaelekeza kwa mauti.      

       Katika Sheria kuu, Wayahudi waliweka maagizo mengi ya kibinadamu na kidogo kidogo walibadilisha mwelekeo kutoka zile zilizokuwa muhimu zaidi. Hata kwa wao wenyewe ni ngumu kuishi maagizo yote yaliyoongezwa. Hii ni maana ya mapambano kati ya Yesu na Waandishi na Mafarisayo ambao walikuwa wakuu kwa mabadiliko ya maana ya Sheria. Kabla ya Yesu manabii wengi walikwisha pinga kuhusu tabia hii. Miongoni mwao wapo Isaya, Hosea na Amosi. Hasa kulingana na nabii Isaya, tunakuta tangazo muhimu kutoka kwa Mungu: “Watu hawa huniheshimu kwa maneno tu, lakini mioyoni mwao ni mbali nami; nao waniabudu bure. Wanayafundisha maagizo ya kibinadamu tu.”

    Yesu anawakosoa walimu wa sheria na mafarisayo kwa sababu walitafsiri sheria kulingana na mawazo yao na walikuwa vielelezo vibaya kwa watu wote hasa kwa wanafunzi wake. Mara nyingi Yesu alipokutana nao hafikii mafanikio kuhusu mapendekezo yake ya maisha mapya kwa sababu wao ni wanafiki na wanapendelea kumjaribu Yesu kuliko kujiruhusu kubadilishwa kulingana na matarajio yake. Kwa hivyo mkutano wa Yesu nao ni maana ya mapambano daima. Wao ni wenye upayukaji kwa sababu hawatendi yale wanayosema. Waliyaondoa maana ya unabii wa sheria na wanafundisha maagizo ya kibinadamu tu. Wanajifikiria watu wema na wanajijulisha vizuri nje mbele ya wengine, lakini ndani yao ni tofauti, ni hali mbaya. Wanatumia dini kwa uradhi wa binafsi yao na wanawazuia wengine kuishi kwa uhuru na furaha. Kutokuwa na uhalisi na ukweli kuifanya imani yao ishara ya kutafuta heshima  na sifa kwa wao wenyewe, mbali sana na Mungu.   

      Upinzani wa Yesu dhidi ya tabia ya vikundi hivi viwili ni mwaliko kwa mabadiliko ya mawazo yetu kuhusu dini, kuhusu uhusiano wetu na Mungu. Utambulisho wetu wa dini hauwezi kuwa ishara ya nje tu, yaani, kwenda kanisani na ushiriki katika sakramenti, kutii amri za kanisa. Yesu alithamini zaidi maisha ya watu kuliko sheria. Yesu anajali zaidi uhusiano wa kiroho na Mungu, anatualika zaidi kubadilika kiroho. kushiriki kanisani kunatupasa kuwa watu wapya na tofauti nyumbani kwa wema wa familia. Maneno au matendo mabaya ni ishara ya kutokuwa na uzoefu wa ndani na Mungu. Utambulisho wetu kama wafuasi wa Yesu unatuongoza kuheshimu uhuru wa watu na kupendelea mazungumzo kuliko kulazimisha. Kama watoto wa Mungu sheria yetu ni udugu, kuwafikiria wengine kuwa muhimu zaidi kutuliko sisi wenyewe. Yesu anatarajia tuwe na uhusiano wa kiroho na Mungu.

Fr Ndega

Mapitio: Sara

segunda-feira, 24 de agosto de 2015

MANENO YA UHAI WA MILELE


Kutafakari kuhusu Yohana 6: 60-69

     Katika injili, tuko mbele ya maneno ya mwisho ya Yesu katika sura hii ya sita ya Yohane, baada ya mwujiza wa mikate na samaki. Kile Yesu alichoongea mpaka sehemu hii ya mwisho kilikuwa kigumu sana kwa wasikilizaji wake kufahamu na kukubali. Tumetafakari kwamba Yesu alijaribu kuwathibitishia kuhusu utambulisho wake kama mkate unaoshuka kutoka mbinguni na mkate ambao ni mwili wake wenyewe,  lakini hakupata mafanikio maana ya mawazo yao yaliyofungwa. Ishara zilizotumiwa na Yesu zilikuwa ngumu sana kwa wale ambao walikuwa na kujua awali kuhusu mwelekeo wa binadamu wake. Walijua Yusufu baba yake, Maria, mama yake na walishiriki pamoja shule moja. Hakika hawakuweza kukubali kwamba mwenzao huyu alishuka mbinguni. Lakini ugumu huu wao haukumzuia Yesu awadhihirishie njia tofauti na iliyojaa ya maana kwa maisha yao.

       Yesu alipoongea na watu akaongea kuhusu hali ya milele, ambayo ni mwisho wa safari ya maisha yetu. Anataka kusikika kwa sababu Neno lake lenye nguvu, linachoma mioyo na kusababisha uamuzi. Hakuna hata mmoja asikilize neno hili na kubaki alivyo. Miongoni mwa wale waliosikiliza Yesu walikuwapo wanafunzi kumi na wawili. Ingawa maneno haya yalikuwa magumu pia kwa wao, wanatambua kitu ambacho hakikutambuliwa na wengine. Hali hii ilionyeshwa kupitia tangazo la Petro: “Bwana, tutakwenda kwa nani? Wewe unayo maneno ya uhai wa milele. Sisi tunaamini na tunajua kwamba wewe ndiwe yule Mtakatifu wa Mungu.” Tunajua kwamba ingawa wanafunzi kumi na wawili walikuwapo pamoja na Yesu tangu mwanzo wa huduma yake kwa umma, hawakuweza kuingiza jumla maana ya utambulisho na ujumbe wa Mwalimu, lakini maneno haya ya Petro yanaonyesha ridhaa ya ndani kwa mtu na mpango wa Yesu. Maneno ya Yesu yaliyapigia chapa maishani mwao njia maalum kwamba hawawezi kupata maana mbali na Mwalimu.

     Kama hii lazima kuwa utambulisho wetu na mtu wa Yesu. Baba Mtakatifu Francisco amesisitiza sana kuhusu mahitaji ya “mkutano wa binafsi na Yesu” ili aliyemfuata aweze kumshuhudia kwa uaminifu. Yesu ni Neno lililofanyika mwili na Neno hili linayatoa maana kwa maisha yetu. Kwa hivyo tunaalikwa kuchukua tangazo la Petro kama rejea ili tuwe na tabia kamili mbele ya Neno la Mungu. Kuhusu mambo hayo Mtakatifu Yohana Calabria alisema: sisi ni makini sana kwa maneno ya binadamu na kuhusu hiyo ni sawa. Lakini sisi lazima kuwa na uangalifu zaidi kwa Neno la Mungu ambalo ni – consecratory – linafanya wakfu, ni kwamba, linalifanya lile linalosema.” Mtakatifu Yohane Calabria alikuwa anasema hasa kuhusu injili ambayo ni sheria kwetu - Poor Servants of Divine Providence. Katika sehemu nyingine ya maandiko yake alisema: “Ikiwa sisi huamini katika maneno ya kuapishwa kwa – consecration – katika misa: “twaeni mle wote, twaeni mnywe wote”, sisi lazima kuamini pia wakati Yesu asema: “Msiwe na wasiwasi” au “Baba yeno wa mbinguni anajua kwamba mnahitaji vitu hivyo vyote” au mtafuteni kwanza juu ya ufalme wa Mungu na matakwa yake, na hayo yote mtapewa kwa ziada.” katika maneno mengine, kutokana na Maneno ya Yesu tunaalikuwa kuwa “Injili hai.” Hili ni lengo la Maneno ya uhai wa milele.


      Kupitia adhimisho la Ekaristi tunalishwa na mkate wa Neno na mkate wa Ekaristi. Katika uzoefu huu Yesu anajitoa jumla kwetu, kuchoma mioyo yetu na kutushibisha ili tuwe na hamasa na shauku katika kazi zetu. Eukaristi hii itusaidie kufikia lengo hili.

Fr Ndega
Mapitio: Sara

segunda-feira, 17 de agosto de 2015

LA OTRA ORILLA EN EL SEGUIMIENTO DE JESÚS


Reflexión a partir de 1Rey 19, 9-13 y Mt 14, 22-33

El texto del libro de los Reyes, destacando la figura de Elías, nos invita a reflexionar sobre la manera particular en la que Dios se revela. Aunque la perspectiva de Elías sea que Dios se revelase en el viento, en la tempestad o en el terremoto, en fin, en los fenómenos extraordinarios, Dios, por el contrario, se revela en la brisa suave.

Elías está huyendo de una situación violenta que él mismo había causado al proponer el desafío sobre el verdadero Dios que debían seguir, y mandar a matar a los profetas de Baal. La reina Jesabel lo persigue, queriendo matarlo. Caminando para el monte Horeb, frustrado y desilusionado, Dios viene a su encuentro de una forma simple, discreta, diferente de lo que él había hecho pensar a los demás. Esta situación nos desafía a cultivar momentos de serenidad, de silencio, de escuchar y dejar que Dios se deje descubrir a su manera y no como lo entendemos.

Muy diferente es la situación presentada en el Evangelio, donde en medio de las tempestades y vientos Dios se manifiesta. Descubramos, en un primer momento, que Jesús invita a pasar para la otra orilla, mientras él despide a las multitudes. Para ser verdadero discípulo de Jesús, es necesario cambiar de orilla, dejar las seguridades, las estructuras, ciertas mentalidades, lanzarse en una aventura, aventura de fe. Cambiar de orilla tiene mucho que ver con la desinstalación, con la conversión y ahí va a suceder la ruptura, una de las marcas registradas del seguimiento de Jesús. No se puede seguir a Jesús y permanecer de la misma forma que antes. Se fuese para dejar todo de la misma manera, no habría necesidad de Jesús ni de su mensaje. Encontrarse con Cristo es una experiencia que provoca decisión.

Jesús da un gran testimonio respecto de la vida de oración. Revela ser fundamental la intimidad con Dios, de una manera profunda y constante. Esta actitud la encontraremos durante todo el Evangelio: ya estaba con el pueblo, ya con el Padre. Jesús puede realizar la síntesis más perfecta entre ser todo del pueblo y todo de Dios.

Sus discípulos enfrentan la noche, amenazados por las ondas y por los vientos. Ellos están preocupados, con miedo y angustiados. La noche siempre está ligada a este tipo de sensación. La confusión es de tal tamaño que les impide reconocer a aquel que viene al encuentro, pues no abandona a quien lo sigue. La dificultad de reconocer a Jesús también puede estar ligada a la resistencia de romper ciertas estructuras y seguridades a las cuales todavía estamos apegados. Jesús siempre viene a nuestro encuentro porque es un Dios peregrino. Nos pone a prueba  para ver nuestra fe y llevarnos a seguirlo con mayor convicción.

Muchas veces prestamos más atención a aquello que nos causa miedo y temor que a la certeza de que Jesús está siempre con nosotros. No reconocerlo quiere decir que no lo amamos verdaderamente, pues “sólo se ama a quien se conoce”. Donde hay amor no hay miedo, pues el amor saca todo miedo e inseguridad. El amor nos abre a la fe. Cuando nos falta una verdadera intimidad con Dios, fácilmente nos asustamos con su forma de intervenir en nuestra vida. Él será siempre un extraño y jamás descubriremos su verdadera intensión respecto de nosotros. ¿Él será un fantasma? Jesús enseguida gritó: soy yo, ¡no tengan miedo!

El miedo hace hundir. La confianza en la ayuda divina sustenta y hace caminar. En el ejercicio de la misión no puedo contar apenas con mis fuerzas y buena voluntad. Necesitamos convencernos de que es la gracia de Dios y la plena confianza en su providencia que nos pueden sostener en el caminar.  Que la lección de la barca nos lleve a asumir con coraje la misión que nos es confiada, dejando que Jesús sea parte de la barca de nuestra vida para vencer todos los miedos y adversidades. Nuestro testimonio debe llevar a las personas a creer que Dios no abandona a quien se confía a Él.

Fr Ndega
Traducion: Nomade di Dios

domingo, 16 de agosto de 2015

CHANZO CHA UZIMA WA KWELI NA FURAHA MILELE

Kutafakari kutoka Mithali 9, 1-6; Waefeso 5: 15-20; Yoh 6, 51-58

     Kulingana na Somo la kwanza, Hekima ni nafsi ya Mungu ambaye anawaalika watu wote kwa sikukuu yake. Kwa watu, Kukubali kushiriki katika karamu hii, ambayo Mungu mwenyewe alitengeneza ilikuwa mwaliko ili kuacha ujinga na kupata kuishi, wakifuata njia ya akili. Mwaliko huu ni ishara ya Ekaristi takatifu ambayo ni Yesu mwenyewe. Yeye anatualika kwenye karamu, kushiriki furaha yake kubwa na uzima wa milele. Mt Paulo anatualika kuishi kama wenye hekima, kutumia kwa njia ya hekima kila nafasi inayotokea. Kulingana naye njia ya hekima ni kugundua na kufanya mapenzi ya Mungu. Roho Mt. ndani ya kila mtu anazaa upatikanaji kwa sauti ya Mungu na uhusiano wema na wengine. 
     
   Kristu aliwaalika wasikilizaji wake kwa uzoefu wa ndani ambao ni ufunuo kuhusu utambulisho wake kama chakula kilichoshuka kutoka mbinguni si kwa binadamu tu bali kwa ajili ya uhai wa ulimwengu wote. “Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu hata alimtoa Mwana wake wa pekee, ili kila amwaminiye asipotee, bali awe na uhai wa milele (Jo 3, 16)”. Mwana anajitoa kama chakula kinachodumu hadi uzima wa milele kwa sababu ya mapenzi ya Baba ambaye ni uhai na anasababisha uzima ndani ya kila mtu anayempokea Mwanawe. Maneno haya ni awali ya mafundisho ya Yesu kuhusu ujumbe wake kama mwokozi na mkombozi wa ulimwengu. Yesu alijaribu kuwathibitishia wasikilizaji wake kuhusu hali hii, lakini hapati mafanikio maana ya mawazo yao yaliyofungwa. Ishara zilizotumiwa na Yesu – “kama mkate unaoshuka kutoka mbinguni” na “mkate huu ni mwili wangu wenyewe” -  zilikuwa ngumu sana kwa wale ambao walikuwa na kujua kwa awali kuhusu mwelekeo wa binadamu wa Yesu. Walijua Yusufu baba yake, Maria, mama yake na walishiriki pamoja shuleni moja. Hakika hawaweza kukubali kwamba mwenzao huyu alishuka mbinguni. Lakini ugumu huu haukumzuia Yesu awadhihirishie njia tofauti na iliyojaa ya maana kwa maisha yao.

    Yesu anaongea kuhusu uzima bila mwisho na kwamba uko kwa wote ambao ni yeye mwenyewe. Inawezekana kuupokea uzima huu kwa kuula mwili wake na kuinywa damu yake, kwa sababu yeye ni hai – hawezi kufa - na anaishi ndani ya wale ambao wanampokea. Yesu halazimishwi kufanya hivyo. Haya ni maonyesho ya kujisalimisha kwake kwa bure, kuendeleza uwepo wake miongoni mwa wanadamu na kufundisha njia ya utimizaji uliojaa. Hiyo ni Ekaristi kama zawadi kubwa ya Mungu ambaye hataki kuwapo mbali ya binadamu. Ekaristi ni hazina ya kanisa, uwepo maalum ya mume wake na awali ya uzoefu wa kiroho yake kama mke wa mume Kristu. Linaishi kwa sababu ya Kristu. Vivyo hivyo ni kwa wote ambao wanashiriki mkate mmoja na kikombe kimoja. Uzoefu huu ni ukamilifu wa ushirika wetu na Mungu, chanzo cha uzima wa kweli na furaha milele.


      Tunapokula chakula cha kawaida miili yetu huweza kuingiza chakula hiki ili uwe na afya nzuri. Kama hii, chakula kinaingizwa na miili yetu. Kuhusu Ekaristi, chakula cha uzima, matokeo ni tofauti: wakati tunampokea Yesu, ni sisi tunaoingizwa naye. Katika maneno mengine, Yesu anatuingiza, anatuchukua kwake ili tuishi naye. Yeye anakaa ndani yetu nasi ndani yake. Anatuunganisha naye, kutuhusisha katika ushirika sawa kati ya yeye na Baba. Bila shaka kwamba matokeo ni pia udugu wenye nguvu na mwafaka miongoni mwetu. Tumwombe Mungu, kupitia sacrament hii takatifu, neema ya kuishi kwa ndani uzoefu wetu na Mwanawe ili tufikie ushirika sawa upo katika Utatu Mtakatifu.

Fr Ndega 
Mapitio: Sara

terça-feira, 11 de agosto de 2015

KUFUFUKA KWETU KATIKA KRISTU

Kutafakari kutoka Yoh 11: 11-27

        Tunaposherehekea uzima, tunasherehekea fumbo kuu ambalo ni zawadi yenye thamani itokayo kwa Mungu. Katika Kristu zawadi hii inapata ukamilifu na vilevile tunapata kuelewa kwamba maisha hayafikii mwisho hapa. Urithi wa maisha ya wale waliotuacha ina thamani kuu kwetu tunaoitwa kuendelea katika imani  kuishi maisha yenye maana. Ikiwa hatuwezi kuona tena wale ambao walitutangulia, yale maadili waliyoishi na kutuachia ndiyo ushuhuda wa kwamba kuwepo kwao kati yetu hayakuambulia patupu. Mtakatifu John Calabria alikuwa na mazoea ya kusema, “Ikiwa tuna Mungu ndani yetu, tutafanya yale mazuri hata kwa kupita kwetu tu”. Kusherehekea wafu, kwa mfano, ni alama kuu ya kwamba tunafahamu vile wanavyoendelea kuwa muhimu kwetu sote, kwa vile kifo sio mwisho wa maisha haya: kinadhihirisha tu mwisho wa sehemu moja ya maisha. Katika nyakati za sorrow na huzuni, tujiruhusu kusaidiwa na maombi ya marafiki na kuhamasishwa na neno la Mungu linalotuimarisha katika imani na kujitolea maishani.
           Kama Wakristo, tabia yetu kuu ni tumaini. Kwa hivyo, Mt. Paulo akasema: “Na kama Kristo hakufufuka, imani yenu ni bure”. Mungu ambaye tunaamini ni Mungu wa uhai na anapotupa uzima, yeye hujiunganisha nasi na kutufanya wanawe wapendwa. Kwa kuwa mateso katika maisha haya, hakuna kinacholinganishwa na furaha tutakayohisi na utukufu utakaotufunuliwa. Vilevile, tujifunze kutoka kwa Yesu ambaye hata katika wakati wa huzuni na mateso aliyopitia kwa njia ya msalaba, alisimamia imani yake katika tendo la riziki ya Mungu: “Ee Baba, mikononi mwako naiweka roho yangu”. Hili lazima kuwa ujasiri na kilio cha roho zetu ili kutuhakikishia kwamba Mungu hawezi kutuacha wala kunyamaza mbele ya kinachotufanyikia. Jibu kutoka kwa Mungu mbele ya kufa kwa Yesu inaandamana moja kwa moja na ufufuko wake. Hilo linatupa matarajio ya kufufuka kwetu na hivyo, yatuhakikishia maisha kamili kwani yeye si Mungu wa wafu bali wa wanaoishi. Hivyo ni kusema kwamba Mungu hataki kifo. Katika Yesu anajifunua kama ufufuko na uhai.
            Kwa nini watu  hufa? Yesu alitufundisha kukuza imani yetu katika Mungu Baba, ambaye anatuangazia kwa nguvu na sifa yake yote ya pendo lake lenye huruma na ukombozi. Yeye hutuvuta kwake kwa dhamana za huruma na anatamani kuwa mmoja nasi. Kwa wakati huo huo, yeye huja kwa mwelekeo kwetu na hutarajia kukaribishwa. Maisha yetu humu duniani hupita tu sehemu moja. Lazima kuendelea safari yake katika sehemu nyingine, kwa sababu twaitwa kwa ukamilifu. Katika maana hii, Agostino asema: “Ee Mungu ulituumba tuwe wako na moyo wetu unahangaika hadi tunapopumzika kwako”. Kwa Yule mwenye imani, kifo ni pumziko katika Mungu ambako sisi sote lazima kupitia ili kuwa wakamilifu. Wakati muhimu sana maishani mwetu  utakuja na tutakutana na Mungu kwa njia ya kipekee. Tutakapokuwa mbele yake hatutaulizwa iwapo tulishiriki katika dini yoyote wala mara ngapi tulienda kanisani bali kiasi cha tulivyoweza kupenda. Chaguo tunayochagua katika mkondo wa safari yetu itadhihirisha mwelekeo ambao maisha yetu yatachukua. Kulingana na mapenzi ya Mungu, maisha yetu yanafaa kupata ukamilifu uanzao na uangalifu wa kila siku katika ishara za upendo nyumbani na kujitolea kwa jumuiya. Kwa hivyo tunapata kuungana na Mungu aliye mwanzo na chanzo cha uzima na asiyepungukiwa kamwe.

Fr Ndega

Mapitio: Sara

domingo, 2 de agosto de 2015

MUNGU ANAENDELEA KUONYESHA UPENDO NA UTUNZAJI WAKE


Kutafakari toka Kutoka 16: 2-4, 12-15; Efe. 4: 17, 20-24; Yn. 6: 24-35

         Mungu anawapatia watu wake chakula ishara ya uzima wa milele ambao tunaupokea katika kila Ekaristi takatifu tunayoadhimisha.
       
        Ingawa wana wa Israeli walikuwa watumwa katika Misri, wakawa na vyakula vingi ili wale hata kushiba. Walipoacha Misri na nguvu ya Mungu, wakapata utambulisho mpya kama Watu wenye uhuru.  Utambulisho huu mpya ulileta baadhi ya changamoto kama kuishi jangwani, kuwa na chakula kidogo au kutokuwa na chakula, kutokuwa na maji, uvamizi/utekaji na watu wengine, na kadhalika. Hali hii ya kutokuwa na chakula iliwafanya kulalamika dhidi ya Musa na Mungu. Mungu Aliyasikiliza malalamiko yao, kupitia upatanishi wa Musa na akionyesha upendo na utunzaji kwao, akawapa mkate kwa kila siku, yaani, mana. Wakala wakashiba.

       Mt. Paulo anafanya tofauti wazi kati ya maisha ya mtu kabla ya ubatizo na kutoka ubatizo. Kabla ya ubatizo mtu huishi maisha ya dhambi na bila ahadi. Kupitia ubatizo mtu anabadilishwa kabisa na kualikwa kuishi maisha mapya, yaliyojaa na maana. Mbele ya majaribio ya kuishi kama kabla ya utambulisho huu mpya, Mt Paulo anatuonya tuishi kama wautu wapya, yaani tuishi kitakatifu. Hii ni hali ya mtu aliyepokewa kuzaliwa kupya katika kristo.

       Yesu alitenda ishara kuu, kupitia kushirikiana kwa mikate na samaki kwa umati wa watu, akiwaonyesha unyeti mbele ya mahitaji yao na uamuzi kuhusu hali ya wenye njaa. Baada ya kula hata kushiba watu walitaka kumfanya Yesu mfalme wao. Yeye akijua mpango wao alitoroka akienda mlimani peke yake. Lakini watu walimtafuta na walimkuta na wanafunzi wake katika kapernaumu. Kulingana na Yesu hawakufahamu ishara na hawakuwa na maana kamili ili kumtafuta. Kwa hitimisho aliwaalika kumkubali kama mkate wa kweli kutoka kwa Mungu ambao unaupa ulimwengu uzima. Yeyote ambaye anakuja kwake na kumwamini hataona njaa na kiu kamwe.

        Yesu alikuwa na unyeti mbele ya mahitaji ya watu na alijaribu kuutoa mwelekeo upya kwa maisha yao kupitia uzoefu wa huruma na kushirikiana, lakini maana ya tumbo lao, wakawa vipofu na wasio na imani. Hawakufikia mafanikio katika kumtafuta Yesu kwao kwa sababu ya Kutokuwa na maana kamili. Kwa kweli nia ya Yesu akiwalisha watu ilikuwa kuwaandaa kwa mafundisho yake kuhusu mkate tofauti na kweli. Yeye anatutolea chakula kinachodumu mpaka uzima wa milele ambacho ni yeye mwenyewe. Anadhihirisha pia kwamba siyo Musa ambaye aliwapa watu mana, lakini ni Mungu. Mana ni mfano wa zawadi kuu ambayo Mungu aliitoa kwa uzima wa ulimwengu, ambaye ni  Mwanawe wa pekee. Kupitia Neno lake na kujitoa kwake Mwanao katika Ekaristi, Mungu anaendelea kuwalisha watu wake na kuwaonyesha upendo na utunzaji wake.

        Basi, Ekaristi ni ishara kubwa ya upendo wa Mungu na maonyesho ya kujitoa kwake Kristo kwa bure. Ekaristi ina maana tu ikiwa ni maonyesho ya upendo na udugu. wale tu wanaopenda kwa kweli wanaweza kwenda mpaka matokeo ya mwisho kama Kristo alivyo. Upendo tu unazaa ushirika na “vitu tu vinavyofanywa kwa upendo vina ushupavu”. Kupitia Ekaristi tunabadilishwa kamili katika Yule tunayeadhimisha, kukubali ahadi ya kuishi maisha mapya yanayozaliwa kutokana na mkutano naye. Hivyo Baada ya kila adhimisho ya Ekaristi sisi hukubali changamoto ya kurudia shughuli za kila siku kama mashahidi wa Kristo ambaye anayatoa maisha yake kwa upendo ili watu wote wawe na uzima wa milele.

Fr Ndega

Mapitio: Sara