domingo, 25 de junho de 2017

MAANA YA KUISHI KWA TUMAINI


Kutafakari kutoka Yer 20,10-13; War 5, 12-15; Mt 10: 24-33


       Mazingira magumu ni sehemu ya maisha yetu ya binadamu. Katika safari tunakabiliana na changamoto nyingi. Mara nyingi tunaogopa kwa sababu tunafikiri kwamba tunaweza kushinda magumu kwa nguvu zetu peke yake nasi tunashindwa. Hapa ni muhimu kugundua tena kiini cha ujumbe wa Kikristo, yaani ubaba na utunzaji wa Mungu kwa watoto wake. Ujumbe huu ni habari njema inayotupa maana ya kuishi kwa tumaini na kusadiki kwamba mambo yote ulimwenguni ni sehemu ya mpango wa hekima ya wema wa Mungu ambaye anatenda makuu hata mbele ya udhaifu na maovu ya kibinadamu. Mazingira ni magumu lakini tuko na Mungu aliye Baba.

       Nabii Yeremia ni mfano wa hali hii. Yeye alikabiliana na mazingira magumu na kuteseka kwa sababu ya uaminifu wake kwa Mungu aliyemwita kuwa nabii tangu tumbo la mama yake. Uhakika kuhusu ulinzi na utunzaji wa Mungu ulimwimarisha wakati wote wa safari yake. Katika maneno ya Yeremia tunaweza kutambua kwamba alikuwa na uhusiano wa ndani na Mungu. Uhusiano huu ndio maana ya uvumilivu wake na kuwaaibisha maadui yake. Yule anayemtumainia Mungu hakati tamaa kwa sababu Mungu hawaachi waliomtumainia yeye. Kulingana na somo la pili, tuko na maana za kuamini kuliko kukata tamaa kwa sababu, ingawa wanadamu wote waliguswa na dhambi ya Adamu nao walitenda dhambi, neema ya msamaha ambayo ilikuja kwetu kwa Yesu ilishinda mno hali ya dhambi. “Mbele ya ukubwa wa dhambi, Mungu anajibu kwa msamaha kamili. Huruma itakuwa daima kubwa kuliko dhambi yoyote, na hakuna awezaye kuuwekea mipaka upendo wa Mungu anayesamehe daima” (Papa Francisco).

      Katika injili, Yesu aliwaambia wanafunzi wake “Msiogope." Je, kwa nini alisema hivyo kwa mara tatu? Alisisitiza kwa neno “Msiogope" kwa sababu alitaka wawe mashahidi jasiri wa uzoefu ambao ulibadilisha ulimwengu ukishinda giza na kuzifukuza hofu zote. Yesu alijua kwamba wataonja mateso kama yeye na kwamba imani yao ni haba kwa kubaki imara. Kwa hivyo, aliwahakikishia uwepo wake maishani mwao na kuongea kuhusu utunzaji wa Mungu kwao. Kwa Mungu maisha yao yanathamani sana. Mungu anaweza kubadilisha hali mbaya kuwa hali nzuri. Anafanya hivyo kwa sababu anawapenda na kuwatunza wale ambao aliwachagua. Maneno haya ya Yesu yaliwaimarisha ili waiendeleze kazi ambayo yeye aliwakabidhi.

      Wakati Yesu alishiriki mamlaka yake na wanafunzi wake alilenga waweze kutangaza kwa wote. Hii ni maana ya habari inayopaswa kutangazika hadharani. Kiini cha ujumbe wao ni utunzaji wa Mungu anayeshughulika hata kwa mambo madogo ya maisha. Kwa kutangaza ujumbe huu wanafunzi wanapaswa kushinda hofu kwa sababu hali ya hofu inaonekana kukana ukweli wa ujumbe huu. Tunajua kwamba ukatili dhidi ya wajumbe wa Mungu ulikuwepo zamani na unaendelea siku hizi. Lakini wameutendea mbaya mwili tu. Shida inaanza wakati wanaochaguliwa sio waaminifu na kusababisha kashfa, wakivuruga wale wanaotaka kusadiki. Hali  hii ni kifo cha mwili na roho pamoja.

      Tunataka kukumbuka Waathirika wa ukatili kwa sababu ya Imani katika nyakati zote. Kama mwalimu wao, walibaki imara katika ahadi yake. Njia yao ya kuishi mbele ya ukatili imewaaibisha maadui zao na kuwasaidia kutafakari. Siku moja Yesu aliwaambia wanafunzi wake, “Mtu akikupigia kofi shavu la kulia, mgeuzie pia la pili”, yaani njia tofauti iliyo njia kamili ya kutenda. Ukatili hauwezi kushinda ukatili bali ndio wema wa moyo unaoweza kufanya hivyo.


       Hata sisi tunapoona hali mbaya tunajaribiwa kuwa na hofu, kukata tamaa, kufa moyo na kuacha ahadi yetu. Lakini uhakika wa uwepo wa Yesu na utunzaji wa Mungu unatuimarisha kuendelea na safari. Kwa hivyo maneno haya ya Yesu ni faraja pia kwetu: “Msiogope”! Mwe na imani tu! Mungu anajua jinsi ya kubadilisha hali mbaya kuwa hali nzuri. Yeye anajua analofanya. Matarajio yake, kulingana na mafundisho ya Yesu, ni kwamba tujione watoto wake na kwa hivyo, tumruhusu kutenda maishani mwetu kulingana na mapenzi yake. Tusiogope kwa maana tuna thamani kuliko shomoro wengi na Mungu hawaachi wanaomwamini na kumtumainia yeye.

Fr Ndega
Mapitio ya Kiswahili: Christine Ghitui

LA RAGIONE PER VIVERE CON SPERANZA


Riflessione su Ger 20,10-13; Rom 5, 12-15; Mt 10, 24-33


       La realtà difficile fa parte della nostra vita umana. Dobbiamo affrontare molte sfide lungo il cammino. Spesso abbiamo paura perché crediamo di essere capaci di superare le sfide solo con le nostre forze e non riusciamo. Qui è importante ricordare l’essenza del messaggio cristiano, cioè la paternità e la cura di Dio per tutti i suoi figli. Questo messaggio è una buona notizia che ci fa vivere con gioia e speranza e credere che tutto ciò che accade nel mondo non sta fuori a un piano di saggezza e di bontà di Dio che riesce a fare meraviglie anche in mezzo a debolezze e malvagità umane. La realtà è difficile, ma abbiamo un Dio che è Padre.

         La vita del profeta Geremia è un esempio di questa situazione. Egli soffre a causa della sua fedeltà a Dio che lo ha chiamato fin dal seno di sua madre. La certezza circa la cura e la protezione di Dio lo ha motivato durante tutto il suo lavoro come profeta. Nelle parole dello stesso Geremia, percepiamo che aveva un rapporto profondo con Dio. Questo rapporto è la ragione della sua perseveranza e della confusione dei suoi nemici. Colui che ha fiducia in Dio non dispera, perché Dio non abbandona mai coloro che confidano in Lui. In base alla seconda lettura, abbiamo ragione più per credere che per la disperazione, perché anche se l’essere umano ha peccato, la grazia del perdono che Gesù ci ha portato ha superato molto di più la realtà di peccato. “Dinanzi alla grandezza del peccato, Dio risponde con il giusto perdono. La misericordia sarà sempre più grande di ogni peccato, e nessuno può limitare l’amore di Dio che perdona sempre” (Papa Francesco).

         Nel Vangelo, Gesù dice ai suoi discepoli: “Non abbiate paura”. Perché ha detto questo per tre volte? Egli ha sottolineato questo perché ha voluto che i suoi discepoli fossero coraggiosi testimoni dell’esperienza che ha cambiato il mondo vincendo il buio e superando tutte le paure. Egli, sapendo che avranno molto da soffrire a causa del suo nome e conoscendo la debolezza della loro fede, ha assicurato la sua presenza nella loro vita e ha parlato della cura di Dio per loro vite. Per Dio la loro vita ha un valore inestimabile. Egli può fare di ogni una brutta situazione una opportunità buona. Lo fa perché ama e si prende cura di chi egli sceglie. Queste parole di Gesù hanno motivato i discepoli a continuare la missione che egli aveva loro consegnato.

          Quando Gesù ha condiviso la sua missione con i suoi discepoli voleva proprio questo, che fossero capaci di diffondere a tutti il suo messaggio. Questo è il senso della notizia che deve essere annunciata dalle terrazze: la cura di Dio che è Padre e si occupa anche delle piccole cose della vita. Per proclamare questo messaggio i discepoli devono superare la paura, perché lo stato di paura sembra negare l’autenticità di questo messaggio. Sappiamo che, a causa della fede, le persone erano uccise ieri e continuano a essere uccise in questi giorni. Ma coloro che uccidono fanno male soltanto al corpo. I problemi cominciano quando gli eletti non sono fedeli al messaggio e provocano scandalo, lasciando in confusione coloro che vogliono credere. Questa situazione uccide il corpo e l’anima insieme.

        Vogliamo ricordare le vittime della violenza a causa della fede di tutte le generazioni. Come il loro maestro, anche loro sono rimasti perseveranti nell’impegno che hanno assunto. La loro risposta davanti alla violenza ha lasciato i loro nemici sconcertati e ha portato loro alla riflessione. Un giorno Gesù disse ai suoi discepoli: “Se qualcuno ti dà un schiaffo sulla guancia destra, porgigli anche l’altra”, cioè mostrare un modo diverso e giusto da agire. La violenza non può superare la violenza, ma è la bontà del cuore che può farlo.

        Anche noi davanti alle difficoltà siamo tentati dalla paura e dalla disperazione a lasciare il nostro impegno. Ma la certezza della presenza di Gesù e la cura di Dio deve motivarci a proseguire il cammino. Così le parole di Gesù sono anche la nostra consolazione: “Non temere!” Dio sa come trasformare brutte situazioni in buone. Le sue prospettive, secondo gli insegnamenti di Gesù, è che viviamo come suoi figli e permettiamo che la sua volontà sia fatta nella nostra vita. Non abbiate paura perché valiamo di più di molti passeri e Dio non abbandona coloro che credono e sperano in lui.

Fr Ndega
Revisione dell'italiano: Giusi 

domingo, 18 de junho de 2017

CIBO CHE CI FA DIVENTARE UN SOLO CORPO IN CRISTO


Riflessione su Deut 8,2-3.14b-16a; 1Cor 10,16-17; Giovanni 6, 51-58


        Celebriamo la festa del cibo che Dio ci ha dato e che dura per sempre, cioè l'Eucaristia. Questo è sacramento della presenza di Gesù vivo in mezzo a noi. L’origine di questa festa è l’Ultima Cena nel Giovedì santo, ma il clima di silenzio e riflessione del vespro del Venerdì Santo ci impedisce di celebrare con grande gioia. Per questo il papa Urbano IV, nel 13° secolo ha istituito questa celebrazione del Corpo e del Sangue di Cristo. Tramite questa solennità e processione, noi possiamo proclamare pubblicamente la nostra fede e il nostro amore per l’Eucaristia e sentire Cristo rinnovando il suo gesto d’amore per la nostra salvezza. Egli stesso ci invita al banchetto della vita in modo da poter condividere la sua grande gioia e la vita eterna.

           Queste letture evidenziano che è Dio stesso che nutre il suo popolo. Ancora dal tempo nel deserto, il popolo di Israele ha avuto la possibilità di conoscere Dio come Provvidente, colui che dà un cibo diverso da quello d’Egitto. Gli israeliti hanno ricevuto la Manna grazie alla generosità divina per rinnovare la loro forza fisica e motivare il ringraziamento a Dio, che è sempre stato presente in mezzo a loro. Secondo San Paolo il vero cibo che Dio dà al suo popolo nuovo è il suo Figlio Gesù. Egli stesso invita tutti a vivere in comunione con lui tramite la celebrazione del suo corpo e sangue. Anche se siamo in tanti, siamo diventati un solo corpo a causa dell’unico Pane che è Cristo stesso.

             Nel Vangelo Gesù invita il suoi ascoltatori ad accogliere la rivelazione circa la sua identità come il pane disceso dal cielo, non solo per gli esseri umani, ma per la vita dell’universo, vale a dire: “Dio ha tanto amato il mondo che ha dato il suo unigenito Figlio, affinché chiunque crede in lui non muoia, ma abbia la vita eterna (Gv 3, 16)”. Il Figlio si dona come cibo che dura per la vita eterna per fare la volontà del Padre che è la sorgente della vita. È lui che fa sgorgare la vita all’interno di ogni persona che riceve il suo Figlio. Siamo qui dinanzi all’essenza degli insegnamenti di Gesù come Salvatore e Redentore del mondo. Ma i suoi contemporanei non riuscivano a capire perché conoscevano la condizione umana di Gesù. Conoscevano i suoi genitori cioè Giuseppe e Maria e probabilmente hanno frequentato insieme la stessa scuola. Di certo non potevano accettare che questo loro collega fosse disceso del cielo. Tuttavia queste difficoltà non hanno impedito a Gesù di rivelare il senso pieno alla loro vita.

            Gesù parla di vita senza fine che è disponibile per tutti. La condizione per ricevere questa vita è mangiare la sua carne e bere il suo sangue, perché egli è la vita e vivrà in coloro che lo ricevono. Questo è un gesto d’amore che Gesù fa liberamente perché il suo desiderio è rimanere tra gli uomini e in ogni persona. Questo è il mistero dell’Eucaristia. Questo è il grande dono del Dio che non vuole vivere lontano dagli esseri umani. L’Eucaristia è il tesoro della Chiesa, cioè il centro della sua esperienza. L’ Eucaristia fa la Chiesa e la Chiesa vive dell’Eucaristia. Nella visione del Vaticano II, “tutta l’attività della Chiesa scaturisce dall’ Eucaristia e trova in essa la sua finalità”. È così per tutti noi che mangiamo lo stesso pane e beviamo lo stesso calice. Questa esperienza è la pienezza del nostro rapporto con Dio e fonte di ispirazione per il nostro impegno per la fraternità.

           "Quando mangiamo il cibo ordinario il nostro corpo assimila questo cibo per avere buona salute. Così, il cibo è assimilato da nostro corpo. Per quanto riguarda l’Eucaristia, il pane della vita, il risultato è diverso: quando riceviamo Gesù, siamo noi che siamo assimilati da lui. In altre parole, Gesù ci assume, ci porta con sè perché viviamo di lui e per lui. Egli dimora in noi e noi in lui. Egli ci unisce a sè, facendoci partecipare della stessa comunione che egli vive con il Padre. In questa esperienza, siamo diventati colui che celebriamo a causa della crescita del corpo stesso. Così, quando celebriamo l’Eucaristia con profondità le nostre relazioni cambiano e diventiamo strumenti di unità, di riconciliazione e di pace secondo gli stessi sentimenti di Cristo.

Fr Ndega
Revisione dell'italiano: Giusi 

sábado, 17 de junho de 2017

CHAKULA KINACHOTUFANYA KUWA NI WAMOJA NA KRISTO


Kutafakari kutoka Kum 8,2-3.14b-16a; 1Wak 10,16-17; Yoh 6, 51-58


          Tunasherehekea sikukuu ya chakula kinachodumu milele, yaani Ekaristi takatifu. Hii ni sakramenti ya uwepo hai wa Yesu kati yetu. Asili ya sherehe hii ni Karamu ya mwisho katika Alhamisi Takatifu lakini hali ya ukimya na tafakari kwa sababu ya Ijumaa Kuu inatuzuia  kusherehekea kwa furaha kubwa. Kwa hivyo Baba Mtakatifu Urbano wa IV katika karne ya 13 alianzisha sherehe hii ya Mwili na Damu ya Kristo. Katika sikukuu hii tunaweza kutangaza hadharani imani na upendo wetu kwa Ekaristi Takatifu na kujiona kuungana na Kristo anayefanya upya ishara yake ya upendo kwa ajili ya wokovu wetu na kutualika kwenye karamu ili tuweze kushiriki furaha yake kubwa na uzima wa milele.

        Masomo haya ni uthibitisho kwamba ndiye Mungu mwenyewe anayewalisha watu wake. Muda ambao Watu wa Israeli waliishi jangwani ulikuwa nafasi ya kumjua Mungu kama Mtoaji ambaye aliwapatia chakula tofauti na kile cha Misri. Walipokea Mana kutokana na ukarimu wa Mungu kwa ajili ya kufanya upya nguvu zao za kimwili na kuwaimarisha kumshukuru Mungu aliyekuwepo miongoni mwao daima. Kulingana na Mtakatifu Paulo, chakula ambacho Mungu anawapatia watu wake wapya ndiye Mwanawe. Yeye anawaalika wote wale mwili na damu yake ili tuwe wamoja naye. Ingawa sisi ni wengi tumefanyika mwili mmoja kwa sababu ya Mkate mmoja tunaoumega ulio Kristo mwenyewe. 

           Katika injili Kristo aliwaalika wasikilizaji wake kuukaribisha ufunuo juu ya utambulisho wake kama chakula kilichoshuka kutoka mbinguni si kwa binadamu tu bali kwa ajili ya uhai wa ulimwengu wote. “Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu hata alimtoa Mwana wake wa pekee, ili kila amwaminiye asipotee, bali awe na uhai wa milele (Jo 3, 16)”. Mwana anajitoa kama chakula kinachodumu hadi uzima wa milele kwa sababu ya mapenzi ya Baba aliye chemchemi ya uzima. Yeye ndiye anayesababisha uzima ndani ya kila mtu anayempokea Mwanawe. Tunaongea hapa kuhusu kiini cha mafundisho ya Yesu kama mwokozi na mkombozi wa ulimwengu, lakini wasikilizaji wa Yesu hawakuweza kuelewa kwa sababu walijua hali ya Yesu ya kibinadamu. Waliwajua wazazi wake, yaani Yusufu na Maria na kushiriki pamoja naye katika shule moja. Hakika hawakuweza kukubali kwamba mwenzao huyu alishuka mbinguni. Lakini ugumu wao haukumzuia Yesu kufunua njia iliyojaa maana kwa maisha yao.

        Yesu anaongea kuhusu uzima bila mwisho unaopatikana kwa wote. Inawezekana kuupokea uzima huu kwa kuula mwili wake na kuinywa damu yake, kwa sababu yeye ndiye uhai na huishi ndani ya wale wanaompokea. Yesu anatenda ishara hii ya upendo kwa uhuru kabisa na kulenga kukaa miongoni mwa wanadamu na ndani ya kila mtu. Hiki ndicho kipimo cha kupata uzima. Hilo ndilo fumbo la Ekaristi takatifu. Ndiyo zawadi kutoka kwa Mungu ambaye hataki kuishi mbali na binadamu. Ekaristi ni hazina ya kanisa na kiini cha uzoefu wake. Ekaristi inalifanya Kanisa na Kanisa linaishi kwa Ekaristi. Kulingana na Mtaguso Mkuu wa Vatikano wa pili, “matendo yote ya Kanisa yatoka kwa Ekaristi na kulenga Ekaristi”. Ndivyo hivyo kwa sote tunaoumega mkate mmoja na kunywa kikombe kimoja. Uzoefu huu ni ukamilifu wa ushirika wetu na Mungu na msukumo kwa ahadi yetu ya kindugu.


          “Tunapokula chakula cha kawaida mwili wetu unaingiza chakula hiki ili uwe na afya nzuri. Hivyo, chakula kinaingizwa na mwili wetu. Kuhusu Ekaristi, chakula cha uzima, matokeo ni tofauti: wakati tunampokea Yesu, ni sisi tunaoingizwa naye”. Kwa maneno mengine, Yesu anatuingiza, anatuchukua kwake ili tuishi naye na kwa sababu yake. Yeye anakaa ndani yetu nasi ndani yake. Yeye anatuunganisha naye, kutuhusisha katika ushirika sawa anaoishi na Baba. Katika uzoefu huu tunabadilika kuwa yule tunayempokea kwa ajili ya ukuaji wa mwili mmoja. Hivyo, wakati tunaposherehekea Ekaristi kwa kina mahusiano kati yetu yabadilika na sisi tunakuwa vyombo vya umoja, upatanisho na amani kulingana na hisia za Kristo. 

Fr Ndega
Mapitio ya Kiswahili: Christine Githui

domingo, 11 de junho de 2017

DIO È COMUNITÀ D’AMORE


Es 34, 4b-6.8-9; 2Cor 11, 11-13; Gv 3,16-18


          Siamo invitati a riflettere sul mistero della Santissima Trinità. Trattasi della relazione di comunione del Dio che è Padre, Figlio e Spirito Santo. È una comunione d’amore perché Dio è amore. L’amore è l’identità di Dio. Così, “Dio è Trinità, perché è amore” (L. C. Susin). Dio è unico ma non vive da solo perché ha voluto vivere in comunione. Tutta la creazione scaturisce dal suo essere e dal suo mistero. Tutte le creature sono chiamate a entrare in questa dinamica d’amore che è la Trinità, ed essere manifestazione della sua bontà. Lodiamo Dio per la sua comunione d’amore, dicendo Gloria al Padre e del Figlio e dello Spirito Santo ...

         Quando facciamo il segno della croce, cioè, “Nel nome del Padre e del Figlio e dello Spirito Santo”, parliamo dell’identità di Dio ed esprimiamo il nostro senso di appartenenza a questo Dio che è presente in noi e in ogni luogo. Egli è amore che è sopra tutti e in tutti. Egli si rivela a tutti e si fa incontrare da tutti, ma continua ad essere un mistero perché non c'è nulla che possa imporre limiti al suo essere. Secondo S. Agostino, “Dio è tanto inesauribile che quando è trovato è ancora tutto da trovare”. Esiste un racconto su Sant’Agostino che ci aiuta a riflettere sulla Santissima Trinità come un mistero, non da essere capito ma accolto. Se ci consegniamo sempre più a questo mistero ancora di più possiamo sentire la sua azione in noi.

 “Un giorno Sant’Agostino – vescovo dottore della Chiesa - stava camminando sulla riva del mare, interrogandosi sul mistero della Santissima Trinità. Si domandava: “come può esistere Dio, Uno e Trino, allo stesso tempo?” Improvvisamente, vide un bambino piccolo che faceva un buco nella sabbia e correva verso il mare, prendeva un po’ d’acqua e la metteva nel buco. Dopo aver osservato questo movimento del bambino per un po’ di tempo, Agostino decise di chiedere al bambino il significato di questo gioco. Questi rispose dicendo: “Io cerco di mettere tutta quell’acqua in questo piccolo buco”. Molto stupito, Agostino disse: “Questo è impossibile!”. Allora il bambino gli disse: “E’ più facile per me mettere tutta quell’acqua in questo buco che tu possa capire il mistero della Santissima Trinità con la tua mente”. Alla fine, il bambino scomparve e S. Agostino disse a se stesso: ‘Questo bambino non era forse un angelo?!’”

       Il messaggio delle letture d’oggi ci conduce verso una apertura sempre maggiore di questo mistero. Questi testi parlano di un Dio che si è rivelato come il Signore della storia, ma che è allo stesso tempo un Dio “misericordioso e pietoso, lento all’ira e ricco di amore e di fedeltà”. L’Antica Alleanza testimonia che egli dona il suo perdono. Nella Nuova ed eterna Alleanza, tramite il suo Figlio, Egli dona se stesso. Per questo suo gesto supremo d’amore il mondo ha trovato salvezza essendo coinvolto nella stessa comunione del Dio che non sa fare altra cosa eccetto amare.

      Quindi, la salvezza del mondo è un’azione amorosa della Santissima Trinità, cioè il Figlio è stato inviato dal Padre sotto la potenza dello Spirito Santo. Similarmente, lo Spirito Santo viene dal Padre e ci porta a comprendere pienamente gli insegnamenti del Filho. Noi crediamo che mediante il battesimo, siamo diventati tempio vivente di Dio e dimora della Santissima Trinità. Quest’azione propria dello Spirito Santo porta ai nostri cuori l’amore di Dio perché viviamo come figli del Padre, fratelli di Gesù e tra noi. È per mezzo di questo Spirito che possiamo chiamare Dio nostro Papà con totale libertà e fiducia.

        Il messaggio sulla comunione trinitaria è un grande aiuto che il cristianesimo offre per la nostra società che si lascia condurre dall’ individualismo e dalla competizione. Gesù ci ha affidato il messaggio d’amore come ragione di tutte le cose. Noi siamo capaci di mostrare la verità di questo messaggio se rimaniamo uniti a lui (alla Trinità). Un giorno egli disse, pregando per i suoi: “Che loro siano una cosa sola; come tu, Padre, sei in me e io in te; siano anch’essi in noi, affinché il mondo creda”. Nell’intimità della nostra relazione con il Figlio, sentiamo anche in noi l’azione del Padre e dello Spirito. La nostra esperienza di Gesù nell’Eucaristia è un’esperienza della Santissima Trinità; Egli è tra noi e dentro di noi. Egli stesso ci unisce a se’ e ci unisce tra di noi. Lo fa perché vuole che siamo partecipi della sua stessa vita. Pertanto, preghiamo: “Gloria al Padre e al Figlio e allo Spirito Santo”...

Fr Ndega
Revisione dell'italiano: Giusi   

MUNGU NDIYE USHIRIKA WA UPENDO


Mit 8: 22-31; Rum 5: 1-5; Yoh 16,12-15


        Tunaalikwa kutafakari kuhusu fumbo la Utatu Mtakatifu. Utatu Mtakatifu ni fumbo la Mungu aliye ushirika wa Baba na Mwana na Roho Mtakatifu. Yeye yu ushirika wa upendo kwa maana Mungu ni upendo. Upendo ni tabia ya Mungu. Hivyo, “Mungu ni Utatu kwa sababu ndiye upendo” (L. C. Susin). Mungu yu wa kipekee lakini haishi peke yake kwa sababu alitaka kuwa na kuishi kwa ushirika. Uumbaji wote ni uenezi wa nafsi na wa fumbo lake. Viumbe vyote vinaitwa kuingia katika mwendo huu wa upendo na kuwa maonyesho ya wema wake. Tumsifu Mungu kwa ushirika wake wa upendo, atukuzwe Baba na Mwana na Roho Mtakatifu... 

          Tunapofanya ishara ya msalaba, yaani, “Kwa jina la Baba na la Mwana na la Roho Mtakatifu”, tunaonyesha hisia yetu ya kuwa miliki ya Mungu na tena tunaongea kuhusu ukweli wa Mungu, ambaye yupo hapa na katika kila mahali. Yeye yu upendo aliye juu ya vyote na ndani ya vyote. Hivyo, anapatikana kwa wote lakini yeye ni fumbo daima kwa sababu hakuna lolote ambalo laweza kuweka mipaka kwako. Kulingana na Mtakatifu Agustino, “Mungu ni wa milele mno hata wakati yeye anapopatikana kuna yote ya kupatikana bado.” Kuna hadithi fulani ya Mtakatifu huyo ambayo inatusaidia kutafakari fumbo la Utatu Mtakatifu kama fumbo si la kufahamiwa bali la kukaribishwa. Ikiwa tunajifungua zaidi kwa fumbo hili tunaweza kuhisi zaidi tendo lake ndani yetu.

        “Siku moja Mtakatifu Agustino, aliye mchungaji na mwalimu wa kanisa, alikuwa akitembea katika pwani ya bahari, akijiuliza swali kuhusu fumbo la Utatu Mtakatifu, akisema, “inawezekanaje Mungu kuwako kama Mmoja na Utatu wakati huo huo?” Ghafla, alimwona mtoto mdogo aliyefanya shimo katika mchanga na kukimbia kwenye bahari, akachukua maji kidogo na kuyaweka shimoni. Baada ya kuangalia mchezo huu wa mtoto mdogo kwa mara nyingi, Agustino aliamua kumwuliza maana ya mchezo huo. Mtoto mdogo akamjibu akisema: “Najaribu kuweka maji yale yote ndani ya shimo hii”. Ameshangaa sana, Agustino akasema: “Hutapata kufanya hivyo kamwe!” Kisha, mtoto mdogo akamwambia akisema: “ni rahisi kwangu kuyaweka maji yale yote shimoni kuliko wewe upate kufahamu fumbo la Utatu Mtakatifu kwa akili yako. Mwishowe, mtoto mdogo alitoweka na Mtakatifu Agustino akajiambia: “Labda mtoto huyo angeweza kuwa ni malaika!”

          Ujumbe wa masomo ya siku ya leo unatusaidia kujifungua kwa fumbo hili, yaani fumbo la Mungu ambaye anajifunua kama Bwana wa historia na pia kama Mungu wa huruma kabisa. Ndivyo hivyo anaonyesha upendo wake. Kwa upendo huu anatoa Mwana wake kwa ajili ya kuokoa ulimwengu. Basi, wokovu wa ulimwengu ndio tendo la Utatu Mtakatifu, yaani Mwana alitumwa na Baba na kutenda kwa nguvu ya Roho Mtakatifu. Vile vile, Roho Mtakatifu alitoka kwa Baba kutuongoza kuelewa kamili mafundisho ya Mwana. Tunasadiki kwamba, kwa njia ya ubatizo, tumekuwa hekalu hai la Mungu na makao ya Utatu Mtakatifu. Roho Mtakatifu anaweka mioyoni mwetu pendo la Mungu akitufanya kuwa ni watoto wake na ndugu wa Yesu na kati yetu. Kwa kifupi, kwa njia ya Roho Mtakatifu tunaweza kumwita Mungu kama Baba yetu kwa uhuru kabisa.    


         Ujumbe wa uhusiano wa Utatu Mtakatifu ni msaada mkubwa ambao Ukristu unatoa kwa jamii yetu ambayo inaongozwa kwa njia ya ubinafsi na mashindano. Yesu alitukabidhi ujumbe wa upendo kama maana ya mambo yote. Tunaweza kuonyesha ukweli wa ujumbe huu ikiwa tunaishi kuungana naye (na  Utatu). Siku moja alisema “wote wawe na umoja; kama wewe Baba, ulivyo ndani yangu, nami ndani yako; hao nao wawe ndani yetu ili ulimwengu upate kusadiki.” Tunapoishi kwa uhusiano wa ndani na Yesu vivyo hivyo tunahisi ndani yetu tendo la Baba na Roho wake. Uzoefu wetu wa Yesu katika Ekaristi ni tena uzoefu wa Utatu Mtakatifu. Kulingana na fumbo hili, Mungu anatumikia, yeye yupo kati yetu na tena ndani yetu. Ndiye yeye mwenyewe anayetuunganisha naye na miongoni mwetu. Anafanya hivyo kwa sababu anataka tuwe washiriki katika uhai wake mwenyewe. Kwa hivyo, tuombe “Atukuzwe Baba na Mwana na Roho Mt... 

Fr Ndega
Mapitio ya Kiswahili: Christine Githui 

domingo, 4 de junho de 2017

WATU WENGI KWA LUGHA MOJA PEKE YAKE


Kutafakari kuhusu Mdo. 2,1-11; 1Kor. 12,3b-7.12-13; Yoh 20,19-23


          Siku ya leo tunasherehekea ujio wa Roho Mtakatifu juu ya wanafunzi wa kwanza na mwanzo wa utume wa Kanisa, lililo Jumuiya ya Agano Jipya. Sherehe hii inatuhakikishia kwamba Roho Mtakatifu ndiye kuwepo kanisani na ndani ya kila mmoja wetu. Huyo ndiye Roho wa Yesu na Baba aliye Roho wa faraja kwa wale wanaohisi kutokuwepo kwa Yesu kwa kimwili. Huyo ndiye Roho wa nguvu kwa wale wanaohitaji ujasiri ili wawe mashahidi wa makuu ya Mungu kwa wote. Huyo ndiye Roho wa umoja ili ushahidi wetu kwa Yesu uwe wa kuaminika.

      Kulingana na somo la kwanza, wafuasi walikusanyika kusali wakishiriki pamoja matarajio yao kuhusu ahadi ya Yesu pamoja na mama yake na wanawake wengine, lakini walikuwa wamejawa na hofu kwa sababu ya upinzani wa jamii ya Wayahudi dhidi ya mafundisho ya Yesu na wafuasi wake. Yesu aliahidi kuandamana nao siku zote, lakini walikuwa hawajafahamu bado maana ya uwepo huu. Walihitaji nguvu kutoka juu kwa uelewa kabisa kuhusu maneno ya Yesu. Hao walisubiri wakimwomba Mungu kwa uvumilivu na imani ili wapate nguvu hii. Ghafla, Roho aliwashukia wote kama ndimi za moto uliowakalia kila mmoja wao. Ndimi hizi za moto zilizo mfano wa zawadi za Roho Mtakatifu, zilichoma hofu ambayo iliwazuia kuongea na kuwafanya kuwa mashahidi jasiri.

        Mwinjilisti Luka anasema kwamba Roho Mtakatifu alikuja katika Sikukuu ya Pentekoste ambayo Wayahudi walisherehekea Sikukuu ya Majuma ama ya mavuno. Tena walikumbuka utoaji wa Amri kumi Mlimani Sinai. Kwa wanafunzi wa Yesu hii imekuwa Sikukuu ya uumbaji mpya kwa tendo la Roho wa Yesu. Mungu alifanya Agano jipya na watu wapya. Kwa hivyo ishara nyingi za ajabu zilionyeshwa kama zilitokea katika Agano la kwanza, yaani moto, tetemeko la ardhi, upepo wa nguvu na kadhalika. Hivyo, Kanisa lililo jumuiya ya Agano Jipya, lilianza safari yake kwa nguvu ambayo ikalifungua kwa dunia nzima. Zawadi ya lugha mbalimbali inaonyesha kwamba Kanisa linatumwa kwa wote na kuongea nao kwa lugha rahisi ili iwafanye watu wote wawe familia moja.

            Kwa upande wa injili ya Yohane, Roho Mtakatifu ndiye zawadi iliyotolewa katika siku ile ya Ufufuko kama alama ya maisha mapya ya Yesu Mfufuka kwa wote. Yeye aliingia katika mahali ambapo wanafunzi walikusanyika ili kuwasaidia kushinda hofu na kugundua tena msukumo katika safari yao. Yesu aliwavuvia akiwapa Roho Mtakatifu. Lakini kabla ya kuwapa zawadi hii kubwa Yesu alisimama katikati yao na kuwahakikishia hali nzuri kama maandalizi ya kupokea Roho yake Mtakatifu. 

           Kwanza kabisa, aliwapa zawadi ya amani nao walifurahia uwepo wa Bwana Mfufuka. Yesu aliwashirikisha katika kazi yake akiwatuma kama mashahidi wa furaha ili watangaze mambo makuu ya Mungu. Watapaswa kutangaza huruma ya Mungu na upatanisho kati ya watu. Kazi hii muhimu haiwezekani kufanya bila msaada wa Roho Mtakatifu. Kwa hivyo, Yesu aliwapa Roho yake kwa hiari.  ‘Roho waliyempokea kutoka kwa Yesu anawafanya wapya na kuwapa nguvu ya kufanya maajabu kwa jina la Yesu.’


          Hili ndilo tendo la Roho Mtakatifu maishani mwetu tulio wanafunzi wapya wa Yesu. Ikiwa katika tukio la pentekoste Roho Mtakatifu aliwakalia kila mmoja wa wanafunzi wa kwanza, yeye anaendelea kufanya kazi kwa ajili ya wanaomfuata Yesu kwa vizazi vyote. Sisi tumepokea Roho Mtakatifu huyo tangu ubatizo wetu. Makaribisho ni ya kibinafsi lakini uzoefu huu tunaishi katika jumuiya na kwa ajili ya jumuiya ya wanafunzi wa Yesu. Kwa kifupi, “kila mmoja hupewa ufunuo wa Roho Mtakatifu kwa kufaidiana.” 

          Ingawa hatutambui, sisi tumeongozwa na Roho Mtakatifu kila wakati. Hivyo, hatuwezi kusema Yesu ni Bwana isipokuwa katika Roho Mtakatifu. Tena hatuwezi kutenda mema ama kumwomba Mungu kama ipasavyo isipokuwa katika Roho huyo. Ingawa sisi ni wa tamaduni mbalimbali na kuongea lugha nyingi, tunaweza kupanga pamoja kwa ajili ya wote kwa sababu ya Roho huyo ambaye anaongea lugha moja peke yake, yaani lugha ya upendo iliyo lugha ya msamaha na ya amani. Roho Mtakatifu atupatie lugha hii.

Fr Ndega
Kiswahili review: Christine Githui

MOLTI POPOLI CON UN UNICO LINGUAGIO


Riflessione su Atti. 2,1-11; 1 Cor. 12,3b-7,12-13; Gv 20,19-23


       Oggi celebriamo la venuta dello Spirito Santo sui primi discepoli e l’inizio della missione della Chiesa, la comunità della Nuova Alleanza. Questa solennità conferma che lo Spirito Santo non solo è presente nella chiesa ma anche dimora in ciascuno di noi. Egli è lo Spirito di Gesù e del Padre; è lo Spirito di consolazione per coloro che sentono l’assenza fisica di Gesù. Egli è lo Spirito di forza per chi ha bisogno di coraggio per essere testimoni degli grandi meraviglie di Dio. Questo è lo spirito di unità affinché tramite l’unità la nostra testimonianza su Gesù sia credibile.

     Secondo la prima lettura, i discepoli si sono riuniti in preghiera condividendo le loro aspettative circa la promessa di Gesù insieme con la sua madre e le altre donne, ma erano pieni di paura a causa dell’opposizione della società giudaica contro gli insegnamenti di Gesù e contro i suoi seguaci. Gesù ha promesso loro di accompagnarli sempre, ma essi non avevano ancora capito il significato di questa presenza. Avevano bisogno della Forza dall’alto per una comprensione piena circa le parole di Gesù. Hanno aspettato con pazienza e fiducia chiedendo Dio questa Forza. All’improvviso, lo Spirito cadde in forma di lingue di fuoco che si posarono su ciascuno di loro. Queste lingue sono simboli dei doni dello Spirito Santo che hanno bruciato la paura che li impediva di parlare. Essi si sono diventati testimoni coraggiosi delle meraviglie di Dio.

       L’evangelista Luca dice che lo Spirito Santo è venuto nel giorno della Pentecoste nel quale i Giudei celebrano la festa delle Settimane, chiamata anche del Raccolto. Loro ricordano anche in questo giorno la consegna dei Dieci Comandamenti sul Monte Sinai. Per i discepoli di Gesù è stata una nuova creazione causata dall’azione dello Spirito di Gesù. Dio ha fatto un nuovo patto con il nuovo popolo. Questa è anche la ragione che Luka mete nel racconto tanti segni come è avvenuto nel primo patto, cioè fuoco, terremoto, vento forte e così via. Così, la Chiesa che è la comunità della Nuova Alleanza, ha iniziato il suo cammino motivata per la forza che l’apre a tutto il mondo. I doni delle lingue diverse dimostra che la Chiesa è inviata a tutti popoli e a parlare con loro in un linguaggio semplice e accessibile, che possa fare di tutte le persone una unica famiglia.

        Per quanto riguarda il Vangelo di Giovanni, lo Spirito Santo è un dono dato nel giorno della risurrezione, come dono della nuova vita che Gesù Risorto offre a tutti. Egli entrò nel luogo dove i discepoli si sono riuniti per aiutarli a superare le paure e ricuperare la bellezza e la gioia di essere discepoli. Soffiò su di loro dando loro lo Spirito Santo. Ma prima di dare questo grande dono, Gesù si mete in mezzo a loro e garantisce un clima proprio come preparazione perché loro possano ricevere il suo Spirito. 

       Prima di tutto, ha dato il dono della pace e come conseguenza la gioia li viene al cuore a causa della presenza del Signore risorto. E poi egli condivide con loro la sua missione inviandoli a proclamare le meraviglie di Dio. Essi devono annunciare il perdono di Dio e il bisogno di riconciliazione tra le gente. Questo compito così importante non è possibile farlo senza l’aiuto dello Spirito Santo. Per questo Gesù ha dato loro gratuitamente il suo Spirito. “Lo spirito che hanno ricevuto da Gesù li fa rinascere li dà forza di compiere meraviglie nel nome di Gesù”.


     Questa è l’azione dello Spirito Santo nella nostra vita che siamo i nuovi discepoli di Gesù. Se nel avvenimento di Pentecoste lo Spirito Santo scese su di ogni uno dei primi discepoli, egli ha continuato il suo lavoro nella vita di coloro che hanno seguito e seguono Gesù per tutte le generazioni. Abbiamo ricevuto questo Spirito fin dal nostro battesimo. L’accoglienza è personale, ma questa esperienza è vivida in comunità e per la causa della comunità dei discepoli di Gesù. In poche parole, “a ciascuno è data una manifestazione particolare dello Spirito per il bene comune”. 

       Anche se non lo percepiamo, siamo guidati dallo Spirito Santo in ogni momento. Quindi, non possiamo dire Gesù è Signore se non sotto l’azione dello Spirito Santo. E non possiamo fare del bene o chiedere a Dio qualsiasi cosa nel modo giusto se non nello Spirito. Anche se noi siamo di culture diverse e parliamo molte lingue, siamo in grado di pianificare alcun progetto comune, a causa dell’aiuto da questo Spirito che parla un unico linguaggio, vale a dire il linguaggio dell'amore, che è allo stesso tempo il linguaggio del perdono e della pace. Per questo, diciamo, Spirito Santo daci questo linguaggio.

Fr Ndega