sábado, 28 de maio de 2016

ANATUFUNDISHA KUSHIRIKI KILE TULICHONACHO

Kutafakari kuhusu Lk 9, 11b-17


Tunaadhimisha sikukuu ya Mwili na Damu takatifu ya Bwana wetu Yesu Kristo. Sikukuu hii ni ukumbusho wa karamu ya mwisho tunayosherehekea katika Alhamisi kuu. Lakini, katika siku ile hatuwezi kusherehekea kwa shangwe kubwa kwa sababu ya kukumbuka mateso ya Bwana. Siku hii ya leo tunaalikwa kusherehekea kwa shangwe na shukrani pamoja na kanisa zima, hasa kwa maandamano, kwa sababu ya zawadi hii kubwa ambayo tunakumbuka kufa na kufufuka kwa Yesu na kujitolea kwake kama chakula chetu cha kiroho. Hiki ni chakula kinachodumu milele nacho kilishuka mbinguni kuutoa uhai kwa ulimwengu.

Neno Ekaristi linatokana na neno la kigiriki na kumaanisha shukrani. Huu pia ni mwaliko wa kumshukuru Mungu kwa zawadi nyingi ambazo tumepokea kutoka kwake na hasa kwa zawadi hii kubwa ya Ekaristi takatifu. Maandamano ni sehemu ya maonyesho ya shukrani hii. Tunaposhukuru tunaonyesha kwamba tunathamini zawadi tuliyopewa. Ili tuweze kushukuru tunahitaji kukumbuka. Kukumbuka katika Ekaristi ni kuishi na kushiriki, kwa sababu Yesu aliwaambia wanafunzi wake maneno haya, yaani, “Fanyeni hivi kwa kunikumbuka mimi.” Kwa maneno mengine, tunapokumbuka Yesu tunashiriki katika tukio ambalo tunaadhimisha. Basi kusherehekea Ekaristi takatifu ni kuishi pamoja na Yesu, uzoefu wa kujisalimisha kwake kwa ajili ya wokovu wa ulimwengu. Ndiye anatushirikisha katika sadaka yake yenye uzima na utakatifu.

Injili inaongea kuhusu kuzidishwa kwa mikate na samaki. Kupitia uzoefu huu Yesu aliwalisha chakula umati wa watu na kutangaza wakati mpya. Andiko hili linakuja baada ya mitume watumwe na Yesu kwa nguvu ya kuponya wagonjwa na kuondoa pepo wabaya. Waliporudi wakampasha Yesu habari kuhusu mafanikio ya kazi yao naye Yesu aliwaalika waende pamoja naye kwenye mahali pa faragha. Mwaliko huu wa Yesu haukumaanisha kujifunga ama kutofautiana kuhusu hali ya watu. Kisha, watu waliwatafuta; nao ingawa waliivuruga nia ya Yesu na wanafunzi wake, walikaribishwa vizuri na Yesu ambaye aliwahubiria habari ya ufalme. Hapo tuko na mwanzo wa uzoefu wa muujiza, kwa maana Yesu alitambua kuwa watu waliomfuata walikuwa na njaa mbili, yaani, njaa ya chakula cha kimwili na pia njaa ya kusikiliza neno la Mungu. Kama waliyatafuta maisha mapya, Yesu akawazungumzia juu ya ufalme na kuwaponya wagonjwa.

Wanafunzi wa Yesu walikuwa wametumwa kuwatumikia watu, lakini uamuzi wa kumwomba Yesu aufukuze umati unadhihirisha kwamba uzoefu ule haukutosha kwa kubadilisha mawazo yao. Kwa kutaka kuwaaga watu bila kufikiria hali yao ya njaa na ya mateso ni kutofautiana, yaani, hili ni kosa la ahadi. Yesu alishiriki na wanafunzi wake mamlaka yake na pia unyeti wake kuhusu hali ya watu. Kushiriki hata kile kidogo walichonacho kwa ajili ya watu wenye njaa ni sehemu ya utambulisho wao kama wafuasi wa Yesu. Kile ambacho walikidhania kuwa kitu kidogo sana kiweze kuwalisha watu, kwa upande wa Yesu kina thamani kubwa. Yesu angeweza kufanya muujiza peke yake lakini alipendelea kuwashirikisha Mitume, akiwasaidia kufahamu kwamba uzoefu wa kumfuata unadai mawazo mapya na tabia mpya. Shauri ya Kristo alibadilisha tabia ya wanafunzi na kuziweka kupatikana zawadi za Mungu kwa wote. Kama matokeo ya uzoefu huu, watu walishiba, wakishinda ukusanyaji na kuepuka ubadhirifu wa chakula. 


Kupitia Ekaristi takatifu iliyowekwa na Yesu, Mungu anatulisha kama alivyofanya na Waisraeli kupitia chakula cha mana. Katika kila Ekaristi tunayoadhimisha tunaishi tena matendo na maneno ya Yesu akiwahakikishia wote chakula na kutualika kushinda mwelekeo wa kijamii wa ukusanyaji  na ubadhirifu wa chakula ambao unauzuia uzoefu wa ndugu wa kweli ulio matokeo ya adhimisho la Ekaristi. Ikiwa uzoefu wetu wa Ekaristi ni wa kweli, tunapaswa kujifunza kushiriki kile tulichonacho na kufanya kwa ukarimu kile tunachoweza, tukiamini kuwa Yesu yupo nasi na kutunganisha naye ili matendo yetu yawe ushiriki katika kujitolea kwake kwa uhai wa ulimwengu. 

Fr Ndega
Mapitio na marekebisho: Sarah


CINCUENTA Y CINCO AÑOS DEL INICIO DEL CONCILIO VATICANO II

Perspectivas evangelizadoras para una Iglesia Sierva y Kenótica

El Concilio Vaticano II sucedió entre los años 1962 y 1965. La Iglesia cargaba una fama de que cuando se reunía en concilio era para formular y declarar algún dogma o para condenar anatemas. Inclusive había sido electo un papa de edad avanzada, pues sorprendió, convocando a toda la Iglesia, el día 25 de enero de 1959, al abrir las ventanas, para que los nuevos aires sacasen el moho que se había acumulado. Él estaba hablando de lo Nuevo, del Soplo del Espíritu que, encontrando espacio, actuó de forma más profunda en todos los miembros de esta Gran Asamblea. En el próximo año estaremos celebrando cincuenta y cinco años del comienzo de este acontecimiento. Delante de las muchas interpelaciones que trajo a la vida cristiana, de un modo general, es necesario preguntarse: ¿qué perspectivas evangelizadoras tenemos?

Sin lugar a dudas, el Concilio Vaticano II dio una nueva dirección para la Iglesia, en cuanto continuadora de la Obra de Cristo a favor de la humanidad. Más allá de adecuarla a las nuevas situaciones vividas por los hombres y mujeres de nuestro tiempo, le trajo un nuevo vigor interno, haciéndola redescubrir toda su riqueza mistérica. Como el Vaticano II fue un concilio de cuño pastoral, favoreció un agiornamiento de la Iglesia y esta actitud trajo a la conciencia la necesidad de una constante actualización a la luz del Espíritu de Dios. Atenta a las señales de los tiempos, es así que la Iglesia es llamada a conducir su pastoral, en el amor de Cristo Buen Pastor, abrazando al mundo entero. La Iglesia continúa siendo invitada a abrirse a todos los pueblos y culturas, en un diálogo verdadero y revelador de la bondad y misericordia de Dios.

La realidad es siempre más desafiante y la Iglesia se muestra atenta a eso. Delante de los males que amenazan la dignidad humana y ocultan los verdaderos valores, la iglesia se siente en el deber de anunciar la buena nueva de la vida, siendo testimonio de la verdad y de la paz. Estamos, por lo tanto, delante de una Iglesia Sierva, que se proyecta hacia delante, en medio de tantas señales de muerte, con una propuesta kenótica, como procedió su Fundador, diciendo que es necesario vaciarse de sí mismo para que el otro pueda vivir. El Concilio la hizo percibir que su misión consiste en estar siempre próximo a las personas, principalmente de los más pobres y sufridores. La Iglesia es consciente de su papel de ser “LUZ” para tantas personas en busca de la Verdad de Dios.

Aproximándonos a la celebración de los cincuenta y cinco años del acontecimiento que transformó la vida de la Iglesia – Nuevo Pentecostés – estamos invitados siempre de nuevo a testimoniar las maravillas de Dios de modo accesible a todos y todas. El Concilio nos hizo mirar la realidad y la historia no de manera trágica o pesimista, sino con una mirada de esperanza, mostrando el rostro de una Iglesia que busca comprender la historia en que está inserta, no para condenar, sino para evangelizar más eficazmente. Una Iglesia que se pone en búsqueda del dialogo con el mundo es una Iglesia abierta y renovada. El horizonte que se abre para la Iglesia la provoca siempre más a ser Sacramento de salvación de Dios, pues es su deseo que todas las personas se salven y lleguen al conocimiento de la verdad. La vida cristiana se renueva y revigora: vino nuevo en odres nuevos, comunidades siempre más vivas y participativas, señal del Reino que viene, semilla del Reino que ya está presente.

Fr Ndega

Traducion: Nomade de Dios

domingo, 22 de maio de 2016

TUMEHUSISHWA KATIKA USHIRIKA WA UTATU MTAKATIFU


Mit 8: 22-31; Rum 5: 1-5; Yoh 16,12-15

          Tunaadhimisha sikukuu ya Utatu Mtakatifu. Utatu Mtakatifu ni fumbo la Mungu aliye ushirika wa Baba, Mwana na Roho Mtakatifu. Hii ni Jumuiya ya umungu na ukamilifu. Utatu Mtakatifu ni ushirika wa upendo kwa maana Mungu ni upendo. Upendo ni asili ya Mungu. Hivyo, “Mungu ni Utatu kwa sababu ndiye upendo”. Mungu alitaka kuwa familia ili ashiriki upendo na uhai wake. Yeye ni Mungu wa kipekee lakini haishi peke yake kwa sababu alitaka kuwa na kuishi katika familia. Uumbaji wote ni uenezi wa nafsi yake na fumbo lake. Viumbe vyote vinaitwa kuingia katika mwendo huu wa upendo na kuwa maonyesho ya wema wake. Tumsifu Mungu kwa ushirika wake wa upendo, atukuzwe Baba na Mwana na Roho Mtakatifu... 

          Tunaposema ishara ya msalaba, yaani, “Kwa jina la Baba na la Mwana na la Roho Mtakatifu”, tunaongea kuhusu Mungu wa ukweli, ambaye yupo hapa na katika kila mahali. Yeye yu upendo aliye juu ya vyote na ndani ya vyote. Hadithi fulani inatusaidia kulikaribisha viizuri mwendo huu, yaani “Siku moja Mtakatifu Agostino, aliye mchungaji na mwalimu wa kanisa, alikuwa akitembea katika pwani ya bahari, akijiuliza swali kuhusu fumbo la Utatu Mtakatifu, akisema, “inawezekanaje Mungu kuwako kama Mmoja na Utatu wakati huo huo? Ghafla, alimwona mtoto mdogo aliyefanya shimo katika mchanga na kukimbia kuenye bahari, akichukua maji kidogo na kuyaweka shimoni. Baada ya kuangalia mchezo huu wa mtoto mdogo kwa mara nyingi, Agostino aliamua kumwuliza maana ya mchezo huo. Mtoto mdogo akamjibu akisema: “Najaribu kuweka maji yale yote ndani ya shimo hii”. Ameshangaa sana, Agostino akasema: “Hutapata kufanya hivyo kamwe!” Kisha, mtoto mdogo akamwambia akisema: “ni rahisi kwangu kuyaweka maji yale yote shimoni kuliko wewe upate kufahamu fumbo la Utatu Mtakatifu kwa akili yako. Mwishowe, mtoto mdogo alitoweka na Mtakatifu Agostino akajiambia: “Labda mtoto huyo angekuwa malaika!”

     Hadithi hii inatufundisha hali muhimu sana, yaani, fumbo la Utatu mtakatifu si fumbo la kufahamiwa bali la kukaribishwa. Ikiwa tunajifungua zaidi kwa fumbo hili tunaweza kuhisi zaidi fumbo hili ndani yetu. Ujumbe wa masomo ya siku ya leo unatusaidia katika mwendo huu. Katika somo la kwanza hekima alijidhihirisha kama nafsi ya Mungu. Hekima hii yu Yesu Kristo ambaye alikuwako na yuko pamoja na Mungu milele na kufanya kazi naye kabla ya kuumbwa chochote. Yeye ni nafsi ya pili ya Mungu na viumbe vyote vilivyokuwako viliumbwa kwa njia yake, pamoja naye na ndani yake. Yeye ni ukamilifu wa viumbe vyote. Bwana wetu Yesu Kristo alitushirikisha katika utukufu wa Mungu. Kupitia yeye tulipewa Roho Mtakatifu ili tuishi kama watoto. Tendo la Roho huyu limemimina mioyoni mwetu pendo la Mungu kuthibitisha kwamba sisi ni watoto wake na tunaweza kumwita Baba yetu kwa uhuru kabisa. Ikiwa sisi ni watoto sisi pia ni warithi pamoja na Yesu kuhusu zawadi sawa, yaani, ushiriki katika uhai wa Mungu pia. Ushiriki huu unawezekana kupitia ubatizo. Tulipobatizwa tulikuwa hekalu hai la Mungu, makao ya Utatu Mtakatifu.     


          Umuhimu wa ujumbe ambao Yesu ametukabidhi ni kwamba yeye ndiye ukweli wa Baba katika Roho Mtakatifu. Hao ni Utatu na hutenda pamoja kwa ushiriano kamili. Yesu, aliyetumwa na Mungu Baba, alitangaza ukweli akiwahusisha watu katika ushirika mmoja ambao anaishi na Baba na Roho Mtakatifu. Utimizaji wa ahadi kuhusu ujio wa Roho huyo unatuhakikishia umoja wetu, kutunganisha kama wana wa familia moja. Kupitia Roho huyo tunaangazika ili tuweze kukumbuka mafundisho ya Yesu na kuyatangaza kwa uaminifu. Wakati sisi hupendana tunaonyesha ukweli wa uhusiano wetu na Mungu aliye Utatu Mtakatifu. Tunapoishi uhusiano wa kweli na Yesu vivyo hivyo tunahisi ndani yetu tendo la Baba na Roho wake. Uzoefu wetu wa Yesu katika Ekarist ni uzoefu wa Utatu Mtakatifu. Mungu anatumikia, yeye yu kati yetu na ndani yetu; anatuunganisha naye na miongoni mwetu. Hili ni fumbo la ushirika ambao Mungu ametuhusisha kwa maana anataka tuwe washiriki katika uhai wake mwenyewe. Kwa hivyo tuombe, atukuzwe Baba na Mw...

Fr Ndega
Mapitio na marekebisho: Sarah

segunda-feira, 16 de maio de 2016

TUMEPOKEA NGUVU KUTOKA JUU


Mdo 2: 1-11; 1Wak 12: 3b-7, 12-13; Yo 20: 19-23

    Tunaadhimisha sikukuu ya Pentekoste, iliyo ukamilifu wa wakati wa Paska. “Neno Pentekoste linatokana na neno la Kigiriki linalomaanisha “–a hamsini”, yaani siku hamsini. Jina lingine la Pentekoste ni “Sikukuu ya Majuma.” Iliitwa sikukuu ya Majuma kwa sababu sikukuu ya Pentekoste iliangukia siku ya hamsini, juma la majuma saba baada ya Sikukuu ya Paska (Tobiti 2,1). Katika Agano Jipya sikukuu ya majuma imepewa maana mpya. Sikukuu ya Pentekoste ni sikukuu ya kushuka kwa Roho Mtakatifu.” Sikukuu hii inasherehekea ujio wa Roho Mtakatifu juu ya wanafunzi wa kwanza na mwanzo wa utume wa Kanisa, lililo Jumuiya ya Agano Jipya. Katika sikukuu hii tunasherehekea uhakika wa uwepo wa Roho Mtakatifu kanisani na ndani yetu. Huyo ndiye Roho wa Yesu na Baba; aliye Roho wa faraja kwa wale wanaohisi kutokuwako kwa Yesu; huyo ndiye Roho wa nguvu kwa wale wanaohitaji ujasiri ili wawe mashahidi wa Yesu kwa wote; yu Roho wa umoja ili ushuhuda kuhusu Yesu uwe kuaminika.

      Masomo mawili, yaani, somo la kwanza na somo la tatu, yanaongea kuhusu mahali ambapo wafuasi walikuwa wamekusanyika, kushiriki pamoja matarajio yao kuhusu ahadi ya Yesu, lakini bila shauku kwa sababu ya upinzani wa jamii ya Wayahudi dhidi ya mafundisho ya Yesu na wafuasi wake. Yesu aliahidi kuwepo pamoja nao siku zote na aliwashauri kusubiri nguvu kutoka juu, ambaye atakuja juu yao hivi karibuni. Hivyo imani yao iliimarishwa katika neno la Yesu na waliweza kusubiri kwa uvumilivu, wakimwomba Mungu ili wapate nguvu hii. Ghafla, kulingana na mapenzi ya Mungu, Roho aliwashukia akiwajaza wote na mahali pote. Kulingana na Injili ya Yohane zawadi hii ya Roho Mtakatifu ilitolewa katika siku moja ya Ufufuko kama alama ya maisha mapya ya Yesu kwa wote. Kutokana na uzoefu huu Sikukuu ya Pentekoste ya Wayahudi ikawa Sikukuu ya uumbaji mpya kupitia tendo la Roho wa Yesu. Wote walibadilika na kuumbwa tena. Kama hii, kanisa, jumuiya ya wafuasi wa Yesu, lilianza safari yake ya umoja kwa nguvu ambayo ikalifungua kwa dunia nzima.

      Kuingia kwa Yesu katika mahali ambapo wanafunzi walikusanyika kuliwasaidia kushinda hofu na kugundua tena shauku katika safari yao. Yesu alimvuvia Roho Mtakatifu juu yao, kutimiza ahadi yake na kuwapa maana ili wawe mashahidi. Kupitia tendo la Roho wanafunzi walipokea zawadi ya amani na furaha ili watangaze matendo ya ajabu ya Mungu, wakiusaidia upatanisho kati ya watu. Zawadi ya lugha tofauti inaonyesha kwamba Kanisa linaitwa kuwepo katika hali ya watu na kuongea nao kwa lugha rahisi, ambayo inajenga ufahamu na ushirika. Kupitia tendo la Roho Mtakatifu watu wote wameitwa kwa ushirika na ndugu, yaani, kutokana na uzoefu wa lugha nyingi kuwa lugha ya kipekee, yaani lugha ya upendo. Lugha za binadamu ni ishara ya tamaduni zote, zinazofikiwa na upendo wa Mungu na kualikwa kujenga familia moja ya kipekee, yaani familia ya watoto wa Mungu, kutangaza maajabu yake kwa njia tofauti.


      Liturujia hii ni mwaliko wa kuishi katika umoja na upendo wa Kristo. Kama wakristo sisi tu sehemu za mwili wake. Mwili huu unahitaji kutenda vizuri ili weze kufikia lengo lake. watu wanahitaji si tu kusikiliza mambo mema kuhusu Yesu, bali wanahitaji pia kuona ukweli wa tangazo hili kupitia  ushuhuda wa ushirika wa Wakristu. Mtakatifu Yohane Paulo wa II aliandika katika waraka wake, yaani, Ut Unum Sint, kwamba kutafuta umoja na ushirika kamili miongoni mwa Wakristo sio shughuli huria, lakini ni sehemu ya ahadi ya Kanisa kama mtumishi wa Kristo (UUS, 20). Ingawa siku za nyuma zilikuwa chungu kwa Ukristo na kuendelea kusababisha majeraha mengi miongoni mwa Wakristo, tunasukumwa na upendo wa Roho Mt. tusameheane na kuishi kama ndugu. Upatanisho ni zawadi tumepokea kama kipimo ili tuweze kuishi umoja, uliotarajiwa na Kristu, “ili wao wawe kitu kimoja”. Roho Mtakatifu atusaidie katika lengo hili.

Fr Ndega

quinta-feira, 12 de maio de 2016

ALIINUA MIKONO YAKE NA AKAWABARIKI


Kutafakari kutoka Mdo 1, 1-11; Waef 1, 17-23; Lk 24, 46-53

           Tunasherehekea kupaa kwa Bwana wetu Yesu Kristo. Yeye alifanya kazi miongoni mwa wanadamu kwa miaka mitatu. Kupaa ni hitimisho ya kazi yake, lakini anaendelea kwepo ulimwenguni kupitia Roho wake. Basi, sikukuu hii inatufafanulia fumbo la kuaga na uwepo wa Yesu kwa sababu yeye hakumwacha Baba alipokuja kwetu na hakutuacha alipomrudia Baba. Kupaa kwake kunaongea kuhusu njia mpya ya uwepo wake miongoni mwetu, kutangaza hatua mpya ya kazi yake. Huu ni wakati wa Kanisa, jumuiya ya wanafunzi wa Yesu. Ujumbe muhimu kuhusu hali hii ni wazi sana katika maandiko mawili ya Luka, yaani, Injili na kitabu cha Matendo ya Mitume. Katika Injili anajulisha vitendo vya Yesu, na katika Matendo ya Mitume anajulisha vitendo vya wanafunzi wake waliosaidiwa na Roho wake Mtakatifu.    

          Kuonekana kwa Yesu kwa muda fulani kuwaimarisha wanafunzi wake kugundua tena maana ya uanafunzi, wakishinda hofu na mashaka kuhusu hali ya ufufuko wake. Uzoefu huo ulikuwa mpya sana kwao naye Yesu alifahamu kwamba alipaswa kuwa na utulivu kwa sababu ya imani yao ndogo. Mwendo ulikuwa wa muda mrefu, lakini wenye ufanisi sana, ukisababisha mabadiliko makubwa maishani mwa wanafunzi, yaani, kutokana na uzoefu wa wanaume wenye hofu kuwa mashahidi wenye ujasiri. Katika maneno ya mwisho kwao, Yesu aliwasaidia kufahamu uhusiano kati ya yale aliyoyatenda na kufundisha na yale yaliyoandikwa na manabii wa zamani. Habari ya toba na ondoleo la dhambi linapaswa kuwa umuhimu wa ujumbe wa waliotumwa kwa jina la Yesu aliye uso wa huruma ya Mungu Asiyeonekana. Uzoefu wao pamoja na Yesu uliwawezesha kuwa wanafunzi wa kweli, lakini walipaswa kuingojea nguvu kutoka juu ili waweze kuwa mashahidi wa Bwana Yesu tangu Yerusalemu mpaka mwisho wa nchi. Roho mmoja aliyekwepo katika mwanzo wa uumbaji na wakati wa utume wa Yesu, anapaswa kuiongoza kazi ya wanafunzi wake.

       Yesu aliyashiriki mamlaka yake na wanafunzi wake ili wawatumikie watu, wakiwatendea mema. Kutokana na mfano wa kujisalimisha kwake Kristo ushuhuda wao wa kwanza ni kujitolea kwao bila kipimo. Wanafunzi  walitumwa kama wajumbe wa habari njema kwa mataifa yote kwa sababu injili haina mpaka. Yesu alikuwa amewaahidia kuandamana na safari yao mpaka upeo. Ingawa uwepo wake wa kimwili/fizikia hauwezi kuonekana tena, Roho wake yu dhamana ya kwamba hawatendi peke yao katika kazi yao. Uwepo wa Roho wa Yesu daima katika safari ya mitume yake umeyafanya maneno yao ufanisi kupitia ishara nyingi na matendo mazuri. Kulingana na Mtakatifu Paulo, Roho ambaye aliwapewa kwa jumuiya ya kwanza ni Roho wa umoja. Kupitia Roho huyo tunaweza kumjua Mungu vizuri na kuishi katika umoja miongoni mwetu kama anavyotarajia Bwana wetu. Kila mtu anaitwa kuchukua ahadi hii ya umoja kama maana ya utambulisho. Katika jumuiya ya kikristo tumezipokea zawadi nyingi kutoka kwa Mungu ili tuwe zawadi sisi kwa sisi, na kusaidia kujenga kwa mwili mmoja, ambao ni takatifu na hai kwa sababu ni Roho mmoja anayetenda ndani yake. Hili ni fumbo la uwepo wa Yesu katika kanisa lake ambalo ni mwili wake mwenywe naye yu kichwa cha mwili huu.


    Malaika waliwaambia wanafunzi wa kwanza na wanatuambia siku ya leo: “mbona mmesimama mkitazama mbinguni?” Hakika kama Wakristo tunahitaji kurudisha mtazamo wetu kwa Yesu, aliye mfano wetu na kichwa chetu ili tuendeleze kazi yake kwa uaminifu, lakini hatuezi Kubaki wamesimama kutazama mbinguni kama ishara ya uvivu, utazamaji na upoozaji. Bwana anatutaka tuwe waangalifu na wenye ufanisi. “Wabarikiwa watumishi wale ambao watakuwa wakitumikia Bwana wao atakaporudi”. Maisha ya Kikristu ni kutafakari na kitendo, imani na matendo. Ishara za uwepo ufanisi wa Yesu zinaonyeshwa kupitia mapendo ya wale wanaomwamini na wanazifuata nyayo zake. Roho Mtakatifu afanye uwepo wa Yesu uwe ufanisi katika maisha yetu na kazi zetu ili tuendelee utume wake kwa uaminifu.  

Fr Ndega 
Mapitio na marekebisho: Sarah

terça-feira, 10 de maio de 2016

ACOGIDA Y HOSPITALIDAD EN EL SEGUIMIENTO DE JESÚS: UNA REFLEXIÓN EN LA ÓPTICA DEL PUEBLO NEGRO



La acogida y la hospitalidad son virtudes que no pueden faltar en la convivencia humana, pues son reveladoras de lo divino en nosotros. Ellas son fuente de vida y de bendición, pues quien ve o viene en nombre de Dios es portador de su bendición. Al gesto del despojamiento y simplicidad de la persona de Dios, sigue el gesto de generosidad y gratitud de las personas de la casa – como en el caso de Eliseo y de la familia que lo recibe. Una situación provoca a la otra. El bien que se hace a alguien vuelve en doble, pues Dios no se deja vencer en generosidad. Lo que se hace a un enviado suyo es a él mismo a quien se lo hace.

El seguimiento de Jesús tiene mucho de eso. El llamado que Dios hace a alguien es expresión de su bondad y generosidad, pero Jesús dice que es necesario radicalidad para corresponder, principalmente en el modo de amar y servir. Él dice que es necesario amar a las personas, así como citó el ejemplo del buen samaritano y dejó como testamento el amarnos los unos a los otros, como identidad de sus discípulos y discípulas. La manera como la gente ama comprueba se estamos aptos para seguirlo. Para comenzar, el compromiso que asumimos con él está sobre todo. Aquí está la medida de nuestro amor por Jesús: sobre todo, hasta de los compromisos familiares. Debemos amar a la familia y a todas las personas, pero no al mismo nivel de Dios. Pero Jesús recuerda todavía a sus discípulo que el amor de Dios, del cual él habla, no puede ser abstracto, espiritual apenas. Pasa por la cruz de la contradicción, que es la lógica del Reino: perder para ganar, morir para vivir, ser el último para ser el primero. Cargar la cruz como Cristo es reconocer que esta cruz ha sido pesada en los hombros de tantos hermanos y hermanas que, por clamar por justicia, respeto y dignidad son literalmente crucificados. Pensemos en el drama del racismo, de la discriminación, del pre concepto y de la intolerancia religiosa… son verdaderas cruces en las cuales están prendidos muchos afrodescendientes o es peso que la sociedad cree que deben cargar por el resto de sus vidas. La dinámica del seguimiento de Jesús, dice que es necesario “bajarlos de la cruz”, o, al menos, no aumentar el peso en sus hombros.

“Existe un principio en el judaísmo en que el mensajero es encarnación de aquel que lo envió”. Jesús se identifica con aquellos y aquellas que son enviados en su nombre y recuerda que todo gesto de amor y acogida en relación a ellos no quedará sin recompensa. Por lo tanto, recibir bien a las personas nos lleva a hacer experiencia del Jesús peregrino, de pies y manos callosos y rostro curtido. Jesús cuando se encarnó, asumió nuestra humanidad y tomó en serio esta opción. Él dignificó lo humano, divinizándonos, de manera que no necesitamos dejar los humano para encontrarlo. Él se hace encontrar en las experiencias humanas, o sea, el ser humano se volvió espacio de encuentro con lo divino en Jesús. A través de él nuestra humanidad alcanza el grado más alto de dignidad. Cuando esta humanidad es herida, dañada la persona de los pobres y víctimas de racismo, y sus vertientes, seguramente Jesús es afectado. Para el pueblo negro, el ser humano es sagrado por haber sido creado por Dios y por ser parte integrante del universo, Santuario de Dios, en el cual la tierra es el altar de su ofrenda, en la oferta y en la acogida de la vida, de la riqueza y compartir de dones, en fin, en la fraternidad.

Los males que todavía existen en nuestra sociedad que agreden la dignidad de las personas, revelan nuestra resistencia en relación a la vida nueva que Jesús nos trajo y que el bautismo nos hace experimentar de una manera sin igual. Tratar mal a las personas es una opción, pero es una opción indigna del ser humano salvado por Jesús. Jesús también experimentó en la propia piel lo que es ser discriminado, despreciado: “¿0puede venir algo bueno de Nazaret?”. “¿Quién es este que dice estas cosas?” “¿No es el hijo del carpintero?”. Por lo tanto, Jesús sigue su camino, libertando a quien está oprimido e invitando a la conversión a los opresores. Es así que debe actuar el afrodescendiente y todo el que se dice discípulo de Jesús: seguir su camino, haciendo historia, aún sin reconocimiento, pero consciente de su papel de agente de transformación.

Más allá de identificarse con quien va, Jesús quiere que recibamos bien a quien llega. En África, la acogida va más allá de un simple gesto. Cuando las personas entran en la amistad de la familia, pasa a ser parte de aquella familia. En Brasil, en épocas de esclavitud, el pueblo negro, en los quilombos, recibían a los indígenas que estaban siendo diezmados y a los de otras razas que, por no estar de acuerdo con el sistema esclavista opresor, eran perseguidos. Estas personas eran incorporadas a la familia quilombola, protegidas y tratadas dignamente. Esta cultura de la acogida está muy arraigada en el pueblo brasilero, especialmente entre los más pobres, que “hacen de tripa corazón” para recibir bien a alguien. Son capaces de quedarse hasta sin alimentos para que la visita pueda comer.

De un modo general, para recibir bien no basta tener buena voluntad, es necesario espíritu de fe, en caso contrario seremos dominados por el interés y segundas intenciones. Nosotros, enviados en nombre de Jesús, somos comparados a los profetas de la Antigua Alianza: somos personas de Dios, cuando tomamos conciencia de ser portadores de su mensaje de salvación para un mundo que se olvidó de amor. Carguemos la cruz que Jesús nos concedió, la cruz del despojamiento, de la fidelidad al proyecto de Dios, de la vida y de la salvación, por más que estemos en medio de situaciones de muerte. Jesús se identifica con nosotros y sufre con nosotros los rechazos. Al mismo tiempo, pide que multipliquemos los gestos de acogida y hospitalidad, para humanizar el mundo y las relaciones. Recibamos a las personas como “personas de Dios que necesitan de un lugar en nuestra vida, en nuestra amistad, en nuestro corazón”.

Padre Degaaxé

Traducción Nómade de Dios.

LA TRINIDAD, LA JUVENTUD Y LA ECONOMÍA



Me gustaría iniciar esta corta reflexión invitando a todos a darle las gracias al Padre, por el Hijo, en el Espíritu Santo, por la vida de la juventud y por una oportunidad más de experimentar la maravilla de su amor, como sus hijos e hijas.

Aprendemos en la catequesis que nuestro Dios es Uno y Trino, y no pocas veces nos preguntamos cómo es posible esto. Cuando se piensa en Dios como Uno, recordamos su unidad, así como Jesús reza: yo y el Padre somos uno, quien me ve, ve al Padre; que sean uno así como el Padre y tú, Padre, somos uno.

Cuando pensamos en Trino, recordamos que son personas distintas, cada una con su misión específica, más presente y actuante en la misión de la otra, de manera que donde una de las personas está, están las otras dos y cada una contiene las otras dos. Son personas que se aman eternamente y tan intensamente que evitan el aislamiento e impiden la exclusión, promoviendo la vida y la comunión. Este es, por lo tanto nuestro Dios, Santísima Trinidad: unidad en la diversidad, la mejor comunidad. Él es el único, pero no está solo; es relación. Por ser comunidad de amor, es permanente novedad, envolviendo el universo entero en una dinámica constante de recreación, comprometiendo al ser humano a orientar todo su vivir según este misterio.

Así, cuando hablamos en economía, nuestra reflexión necesita volverse para la intención de Dios Trinidad respecto de la vida y del ser humano. En teología, hablamos de Economía de la salvación, designando los planes de la  vida que Dios tiene para nosotros, que nos proporciona abundancia de dones y de bienes.

Esa reflexión nos lleva a cuestionar el modelo económico injusto, adoptando en nuestro país, que privilegia algunos y marginaliza tantos hermanos y hermanas. Esta economía que usa los jóvenes y los descarta según sus intereses, con certeza, no es querida por Dios; al contrario, es un atentado a la imagen presente en cada joven. Cuestionamos el acumular y el consumismo desenfrenado que aísla siempre más a las personas y las vuelve indiferentes frente a la realidad de sus semejantes.

La economía necesita estar al servicio de la vida y no la vida al servicio de la economía. Cuando se coloca al servicio de la vida, ella nos abre perspectivas más amplias. Se vuelve una realidad promotora de la solidaridad, de la justicia, del cuidado de la naturaleza, de atención a las necesidades básicas de todos y todas. La abundancia de la mesa nos hace pensar en la abundancia de la vida que el Dios Trinidad nos quiere proporcionar, invitándonos a ser parte de su ministerio.

En la medida en que traemos de vuelta la economía para sus verdaderos objetivos, nos damos cuenta de la dimensión transcendente de la existencia humana, llamada a participar de la abundancia de los bienes divinos, que ya comienzan a ser compartidos en este mundo, por los valores que la fe cristiana nos presenta.

Que el misterio del Dios Uno y Trino nos inspire actitudes más proféticas, para cultivar una nueva economía pautada por la justicia y la solidaridad, promoviendo la vida y la dignidad para todos y todas. Este es el espíritu que debe animar el caminar de nuestra juventud como expresión de compromiso y cuidados para con nuestra “Casa Común”, gran don del Dios comunión.

Padre Degaaxé.

Traducción: Nómade de Dios.

terça-feira, 3 de maio de 2016

KUISHI KAMA MAKAO YA UTATU MTAKATIFU


Kutafakari kutoka Mdo 15,1-2.22-29; Ufu 21, 10-14.22-23; Yoh 14, 23-29

     Ujumbe muhimu wa liturjia ya siku ya leo ni kuhusu hali ya makao ya Mungu ulimwenguni na ndani ya kila mtu kupitia upendo. Hali hii inatualika kufanya upya ahadi zetu za waliobatizwa na kuboresha uhusiano wa kweli na yule ambaye anapendezwa kukaa ndani yetu. Hali ya somo la kwanza inaongea kwamba mwanzoni mwa uinjilishaji wanafunzi wa Yesu walihitaji utambuzi sana watangaze habari njema ya Yesu bila kipimo na masharti. Baadhi ya desturi za binadamu ni kama mzigo katika uhusiano wa watu na Mungu. Mazungumzo ya Pulo na Barnaba pamoja na mitume wengine wameongozwa na Roho Mtakatifu ni mfano wazi kuhusu njia ya Kanisa ya kutenda ili liweze kutatua shida na ugumu miongoni mwa wana wake kwa sababu ya tofauti ya tamaduni, ya mawazo na kadhalika. Kulingana na mtazamo wa Yohana, Mungu alifanya makao duniani na kupitia Yesu, aliye hekalu la kipekee tunaweza kukutana na Mungu kwa kweli. Mwelekeo wa safari yetu kama watu wa Mungu ni kushiriki katika utukufu wake na kutiwa nuru kupitia Mwana wake ambaye ni mwanga wa ulimwengu.

      Katika injili tuko na hotuba ya kuaga ya Yesu anayewashauri wafuasi wake walishike neno lake kama alama ya upendo wao kwake. Wanafunzi wana maana nzuri ya kufanya hivyo kwa maana hiyo ni njia maalum ya kuwa makao ambapo Utatu Mtakatifu wanaweza kuja na kukaa. Uhusiano wa ushirika kati ya Mwana na Baba na Roho Mtakatifu ni mwaliko wa ushiriki wa wale watakaoendeleza kazi ya Yesu ulimwenguni. Kipimo cha mwendo huu ni neno lake linalo asili katika Baba na linapatikana katika nyakati zote kupitia tendo la Roho Mtakatifu. Roho huyo ni msaadizi anayeweza kubadilisha maisha ya yeyote anayejifungua kwa tendo la neema ya Mungu. Wanafunzi wanaalikwa kuishi hatua mpya katika safari yao na maneno haya ya Yesu ni faraja inayoijaza mioyo yao kwa  matumaini. Yesu anawafundisha kwa uvumilivu jinsi ya kuishi utambulisho wa wanafunzi na kumkaribisha nyakati zote. Ingawa tangu mwanzo wa kazi yake Yesu alijifunua kupitia hali ya kawaida, mpaka hapo wanafunzi wake walikuwa na mazoea ya kumtambua Yesu kupitia mambo makuu. Kutoka hapo, wanapaswa kumtambua Yesu na kumdhihirisha kwa njia tofauti kabisa.

     Yesu atatoweka kimwili lakini ataendelea kwepo ndani ya wanafunzi wake kupitia upendo. Mahali ambapo Yesu yupo vivyo hivyo Baba na Roho Mtakatifu wapo. Ikiwa mara iliyopita (Yoh 13, 31-35) tulitafakari kuhusu haja ya kupendana kama Yesu alivyopenda, yaani, amri ya kupendana kama kipimo ili watu watambue nani ni kweli wanafunzi wa Yesu, sasa umuhimu wa kutafakari kwetu ni upendo kati ya Yesu na wanafunzi wake ambayo ni njia ya kweli ya kumfanya Mungu atambuliwe kwa wote baada ya kifo cha Yesu. Yesu hakuwaacha wanafunzi wake kama walio yatima bali ataendelea miongoni mwao kwa njia tofauti. Yeye, pamoja na Baba na Roho Mtakatifu wanakuja daima kwetu na kutarajia kukaribishwa vizuri. Ujio wao ni ufanisi sana, kulingana na Baba wa Kanisa Gregori, yaani, “wanakuja kwetu twende kwao; wanakuja kusaidia wakati wa dhiki; tunakwenda kwao kwa kutii; wanakuja kwa kutuelimisha, tunawaendea kwa kutafakari; wanakuja kwa kutujaza, tunawaendea kwa kushikilia; ufunuo wao si wa nje bali wa ndani; makao yao kwetu si ya muda bali ya milele. Imesemwa tutakuja kwake na kufanya makao kwake.”  


       Yesu anaongea kuhusu Baba kwa hamu na kutambua sana msaada wa Roho Mtakatifu katika kazi yake. Huu ni mwaliko wa tuishi uhusiano mpya miongoni mwetu hata tufikirie wengine muhimu kuliko sisi wenyewe na kutambua kazi yao muhimu zaidi kuliko zetu. Ufunuo wa Yesu unaleta changamoto kwetu tulioalikwa kuendeleza kazi yake. Alitaka kwamba kupitia maneno na matendo yetu dunia itamjue. Bila shaka kwamba tunapaswa kuwa waaminifu na mwendo huu ni matokeo ya kulisikia na kulishika neno lake ambalo ni kipimo cha upendo wetu kwake. Wakati tunalishika neno lake Yesu tunaruhusu kuingia kwa Utatu Mtakatifu ndani yetu. Hali hii tumeona tangu ubatizo wetu, lakini tumekosa ahadi ya kuishi kulingana na uwepo huu. Kuhusu hayo Mt. Paulo anatukumbusha haja ya heshima kwa miili yetu kwa sababu hii ni hekalu la Roho wa Mungu. 

Fr Ndega

KUPITIA KUPENDANA TUNAKUWA WAJUMBE WA HABARI NJEMA KWA WOTE


Kutafakari kuhusu Yoh 13, 31-35

          Umuhimu wa liturjia ya siku ya leo ni amri ya upendo kama Yesu alivyofundisha. Kila kitu ambacho tunatenda kinapaswa kuwa alama ya upendo. Tendo bila upendo halina maana. Mtume Paulo aliliweka wazi jambo hilo: “Pia nikiwa na unabii, na kujua mafumbo yote na maarifa yote, na kuwa na imani yote hata kuhamisha milima, nikikosa upendo, sina maana” (1 Wakorintho 13:2).

          Mazingira ya andiko la siku ya leo ni ya karamu ya mwisho ambayo Yesu alianzisha Ekaristi iliyo sakramenti ya upendo na utumishi. Yesu alijua wazi kwamba Saa yake ilikuwa imefika. Katika injili ya Yohane, kila ishara ambayo Yesu anatenda ni tangazo kuhusu Saa hii ambayo inajumuisha mateso, kifo na kufufuka kwake. Kupitia Saa hii atamtukuza Baba na kutimiza utume wake. Kwa upande wa wanafunzi wa Yesu, Saa hii ni kipindi cha uamuzi, yaani, wanapaswa kuamua ikiwa wanataka kuendelea kazi ya mwalimu au la. Mwinjilisti Yohane alitaja wakati kamili ambao Yuda alitoka mahali pa mkutano na wakati wa kumtukuzwa kwa Yesu na Baba yake. Yuda alitoka kwa sababu mbele ya ishara ya kujisalimisha kwa Yesu haiwezekani kutofautiana. Yesu alimsaidia Yuda kuamua kwa sababu, ingawa Yuda alikuwa mmojawapo wa kikundi, yeye ndiye alimpinga Yesu. Naye Yesu mwenyewe alikuwa amekwisha tangaza kwamba yeyote asiyetenda pamoja naye anagawa. Basi, kupatikana na hatia kwa Yesu kulikuwa msaada kwa uamuzi wa Yuda. Yeyote anayekubali pendekezo la Yesu ndiye anabadilishwa na upendo wake na kualikwa kufanya vivyo hivyo. Yeyote anayekataa hili anapaswa kuondoka mahali na kukiacha kikundi.

           Mazungunzo ya Yesu na Yuda na kuondoka kwake kulikwa maandalizi kwa kipindi kifuatacho cha zawadi kubwa ya amri mpya kama urithi wa Yesu kwa watoto wadogo wake. Yesu alikuwa akizungumza nao kama vile mama na baba wanavyofanya na watoto wao. Yeye alishiriki nao hisia zake na kitu muhimu sana, yaani, amri mpya ya upendo. Kwa upande wa wanafunzi amri hii siyo amri mpya kwa sababu imekwepo tangu Agano la Kale. Lakini wanapaswa kuishi kwa njia mpya, kulingana na hayo aliyowafundisha Yesu. Basi, pamoja na zawadi kubwa ya amri hiyo Yesu aliwaonyesha jinsi ya kuishi zawadi hii. Kipimo cha upendo wao kinapaswa kuwa upendo wa Bwana wao. Nayo njia yao ya kupendana inapaswa kuwa njia ya kupenda aliyochagua Yesu.

           Yesu anawapenda wanafunzi wake mpaka upeo, kwa sababu hajui kupenda kwa njia nyingine. Ilikuwa kwa upendo kwamba Mungu alimtoa Mwanawe pekee kwa wokovu wa ulimwengu. Upendo tu uliimarisha kazi yake katika nyakati zote. Ilikuwa kwa upendo kwamba Mwana wa Mungu aliutoa uhai wake. Umuhimu wa mafundisho yake ni upendo kama amri mpya na maana ya utambulisho wa wanafunzi wake. kupitia kupendana wao kwa wao kama Yesu alivyowapenda watu wote watawatambua kama wafuasi wa Yesu. Upendo wa Yesu ni alama ya furaha yake, yaani, furaha ya ushirika wake na Baba, furaha ya kuishi miongoni mwa binadamu, furaha ya kuwachagua baadhi ya wanadamu kama washirika katika kazi yake na furaha ya kuutoa uhai kwa ajili yao. Akiushiriki upendo na wafuasi wake, Yesu aliyajaa maisha yao kwa furaha kubwa, maana kati ya upendo na furaha uhusiano uko. Mtu anayependa kwa kweli yu mwenye furaha ya kweli.


        Ilikuwa kutokana na mfano wa unyenyekevu na utumishi kwamba Yesu aliwapa wafuasi wake amri yake mpya. Huu ni ushuhuda wetu wa kwanza kulingana na uzoefu wa wakristo wa kwanza, yaani, “Mwone kama wanavyopendana!” Upendo wao ulionyeshwa kupitia ridhaa wao kwa wao, kushiriki pamoja, mshikamano, uvumilivu katika maombi pamoja na unyenyekevu wa moyo. Tunaalikwa kuchukua hayo kama mpango wa maisha. Upendo unapaswa kuwa umuhimu kati yetu na maana ya kazi zetu. Kupitia kupendana tunaalikwa kujitolea kama vile Kristo na kuwafanya wanafunzi wapya kwake. Kupitia kupendana tunakuwa wajumbe wa habari njema kwa wote. Kupitia upendo twatambua kwamba hatutendi peke yetu bali kwamba sisi tu vyombo mikononi mwa Bwana ambaye ana nguvu kwa kubadilisha kila kitu tena na tena kupitia upendo.

Fr Ndega
Mapitio na marekebisho: Sarah