sexta-feira, 29 de dezembro de 2017

IL PIENO COMPIMENTO DELLA NOSTRA ATTESA


Riflessione su Gn 15,1-6; 17,5; 21,1-3; Eb 11, 8.11-12. 17-19; Lc 2, 22-40

        Quando lo Spirito di Dio trova apertura nel nostro cuore, ci fa sperimentare la vicinanza divina in modo sorprendente. Il brano del libro della Genesi ci parla dell’esperienza di Abramo che ha creduto alle promesse di Dio e ha potuto sperimentare grande gioia a causa della fedeltà divina. La sua testimonianza di fede è un grande aiuto perché possiamo coltivare un abbandono fiducioso in Dio che non abbandona mai coloro che confidano in lui. La lettera agli ebrei riprende l’esperienza di fede di Abramo e la mette nella logica del dono. Quando Abramo è stato messo alla prova, non ha esitato a offrire a Dio il dono più prezioso che Dio stesso gli aveva dato. La certezza dell’azione provvidente di Dio era molto viva nella sua memoria e nel suo cuore. La consapevolezza di avere ricevuto molti doni da parte di Dio ci porta ad essere generosi nelle nostre risposte a lui. Egli che non si lascia vincere in generosità, ci donerà sempre di più.

        Il vangelo narra la presentazione del bambino Gesù nel tempio, secondo la legge del Signore. Richiama molto la nostra attenzione la partecipazione semplice e umile di Maria, Giuseppe e il bambino alla vita della loro comunità, in mezzo alla gente che va al tempio ogni giorno, specialmente per compiere il rituale dell’offerta dei doni seguendo la legge del Signore. Quindi, dovrebbe essere una situazione normale di una partecipazione comunitaria, ma l’azione dello Spirito, protagonista del racconto, fa che questa “situazione normale” diventi opportunità rivelatrice: il profeta Simeone e la profetessa Anna riconoscono in quel bambino presentato nel tempio, la salvezza che Dio ha promesso al suo popolo e lo stesso Spirito che li guida a questa riconoscenza, li motiva anche a parlarne a tutti quelli che come loro vivevano questa esperienza di attesa: “Ora, Signore… è compiuta”. 

      La santa famiglia si sottomette alla legge del suo popolo perché la considera di ispirazione divina e ha fatto anche l’offerta al Signore come famiglia povera, vale a dire, una coppia di tortore o due giovani colombi, perché per Dio non importa la misura o la quantità dell’offerta ma l’intenzione del cuore. Durante la sua missione pubblica, Gesù insisterà su questo. Basta ricordare il semplice e significativo gesto della vedova in mezzo a tanti che offrivano grandi quantità dal loro superfluo. Solo Gesù ha percepito perché sa guardare oltre il gesto. Nel momento che Maria e Giuseppe presentano il bambino nel tempio, Dio lo presenta al mondo. Questa è la vera e maggiore offerta ormai fatta da Dio stesso, che non solo sostituisce tutte le altre offerte ma garantisce la salvezza.

      In mezzo a tanta gente presente nel tempio, quando Gesù è stato presentato, solamente Simeone e Anna hanno percepito la particolarità di questo bambino. Loro sono i ‘giusti’ che hanno saputo attendere la promessa di un nuovo tempo e che adesso lodano Dio per questa opportunità di avere potuto riconoscere Cristo, la salvezza di Dio. Specialmente Simeone, secondo il testo, va al tempio mosso dallo Spirito. È proprio questa la ragione della capacità di Simeone. Lo Spirito Santo viene menzionato per tre volte come segno di totalità e pienezza. Vuol dire che davvero il vecchio Simeone aveva intimità con lo Spirito. Sappiamo che l’opera di Luca parla molto dell’azione di questa Persona divina come punto di riferimento di tutta la novità che Gesù ha portato. Dal ‘Sì’ di Maria nell’annunciazione all’azione delle Comunità dei discepoli la presenza dello Spirito è costante.

          Allora, questo Spirito che guida Simeone a ‘riconoscere il Cristo’, è molto presente in noi e ci guida a una esperienza vera di Dio dal nostro battesimo. Lo Spirito è colui che motiva la profezia. Egli ci rende nuovi e ci dà la forza per vivere e realizzare i disegni di Dio. Questo Spirito rende Maria solidale con la missione del Figlio con una fede umile e adesione piena al progetto di Dio. Infatti, la sua fedeltà come Madre e discepola la porterà a condividere il dolore del Figlio accompagnandolo fino alla fine. L’esempio di fedeltà di Maria ci rende forti per portare avanti la nostra decisione di essere discepoli di suo Figlio fino in fondo. Siamo invitati ad “accogliere Gesù con la stessa gioia di Simeone, con la stessa perseveranza nell’attesa, con la medesima docilità all’azione dello Spirito”.


Fr Ndega
Revisione dell'italiano: Giusi

domingo, 24 de dezembro de 2017

MWOKOZI WETU NDIYE MUNGU PAMOJA NASI


Kutafakari kuhusu Luka 2, 1-14

Tangazo la kuzaliwa kwake Yesu ndio ujumbe wa furaha kubwa kwa wote, kwa sababu Mwokozi amezaliwa kwa wote. Tufurahi kwa sababu Mungu anatupenda, yeye yupo kati yetu na kuleta wokovu kwetu. Mungu aliweza kufanya mambo yote peke yake lakini alipendelea kuuomba msaada wa Bikira Maria, wa Yusufu na wengine wengi. Katika mpango wake wa wokovu watu wanaalikwa kufania kitu kulingana na uwezo kibinafsi wa kila mtu. Katika tukio la kuzaliwa kwa Yesu, Mungu alionyesha njia yake mwenyewe ya kutenda, yaani, tukio rahisi na mahali padogo na watu wanyenyekevu. Hali hii inathibitisha msemo wa Afrika ambao husema, “watu wanyenyekevu, wakifanya vitu rahisi na katika mahali padogo wanaweza kubadilisha ulimwengu.” Mabadiliko makubwa ambayo jamii yetu inahitaji yapaswa kutokea ndani ya binadamu. Jamii mpya itatokea wakati kila mtu atambue haja ya kujibadilisha mwenyewe badala ya kujaribu kuwabadilisha wengine. Kulingana na Baba Mtakatifu Francisco, “Dunia itabadilika ikiwa tuanze kuyabadilisha matendo yetu kupitia tabia zetu na chaguzi zetu.”
Katika Yesu, Mungu amekuwa mmoja wetu, akichukua hali yetu ya kibinadamu na kulitoa pendekezo mpya la maisha. Kwa hivyo haitoshi kumkiri Yesu kama wokovu wa Mungu; ndiyo muhimu turuhusu kuongozwa na ujumbe wake wa amani na upendo. Kwa kuzaliwa kwake, Yesu aliwafanya binadamu wote kuwa ni familia moja na kujaza mioyo ya watu kwa furaha na matumaini. Kweli, Mungu anajifunua kama jirani, maskini na anayekataliwa, kutualika kutambua thamani ya ishara ndogo na miradi midogo. Katika ufalme, wake wadogo na waliokataliwa wanakuwa ni wakuu.
Wachungaji pia wanatufundisha sana. Hao walikuwa watu waangalifu ambao walichunga wanyama wao karibu na Bethlehemu wakati wa usiku. Walikuwa kweli waangalifu kwa sababu ndani yao hamu ya Mungu na uhakika wa ukaribu wake ulikuwa hai sana. Hivyo, hao walikuwa watu wa kwanza wa kuipokea habari ya kuzaliwa kwa Yesu kwa sababu mioyo yao ilikuwa macho. Mtu aliye na moyo makini anaweza kuamini katika habari njema na kutarajia hali nzuri katika kilaalfajiri mpya”. Mtu aliye na moyo makini ana ujasiri wa kuanza safari kwenye mkutano na Mungu katika mahali pasipotarajiwa, yaani katika hali ya mtoto mdogo na mahali maskini sana.
Mungu Mwenyezi alikubali kuwa ni mtoto mdogo, akiutegemea utunzaji na upendo wa binadamu. Akifanya hivyo, anatufundisha tuwe na unyenyekevu na kukubali udhaifu wetu wa kibinadamu ulio muhimu katika uhusiano wetu nawe. Imani inatuongoza kumtambua mtoto huyu mdogo wa Bethlehemu katika kila mtoto ambaye hukutana na sisi katika safari yetu ya kila siku. Kila mtoto anaomba upendo wetu. Tufikiri leo, kwa njia maalum, kuhusu baadhi ya watoto ambao hawana uzoefu wa upendo wa wazazi wao wala hawana mahali pa kuishi; kuhusu watoto ambao wanatumika kama askari, wanaobadilishwa katika vyombo vya vurugu, badala ya kuwa vyombo ya upatanisho na amani; tena kuhusu watoto walio waathirika wa unyanyasaji wa kijinsia, na kuhusu watoto maskini waliolazimishwa kuziacha ndoto zao kwa sababu ya hali yao mbaya ya kiuchumi. Mwanga wa Bethlehemu uguse mioyo yetu ili tuwe na utunzaji na upendo kwa walio na mahitaji mengi.

Ingawa sisi huishi katika jamii ya ulaji ambayo inatuzuia kushughulika kwa thamani muhimu sana, tunapaswa kuwa macho. Krismasi si ulaji. Ni sikukuu ya ufunuo wa Fumbo la upendo wa Mungu unaoweza kubadilisha moyo wa kibinadamu. Upendo wa Mungu kwetu haitegemei astahili yetu bali wema na ukarimu wa Mungu mwenyewe. Uzoefu huu unatuimarisha tufanye vivyo hivyo ili kushinda hali ya vurugu na chuki katika hali yetu. Hivyo, Krismasi itakuwa sio kipindi kimoja kwa mwaka bali kila wakati. Itakuwa Krismasi daima ikiwa tujifunze kupenda kwa njia ya kweli na kuweka juhudi zaidi ili kujenga jamii ya undugu na haki kwa wema wa wote

Fr Ndega

BIKIRA MARIA NDIYE JIBU LETU KWA MWALIKO WA MUNGU


Kutafakari kutoka Luka 1, 26-38


Sisi tuko karibu sana kwa kusherehekea tukio kuu ambalo linaleta mafanikio ya mpango wa Mungu kwa dunia, yaani, Kuzaliwa kwa Mwana wake. Ndio wakati maalum wa kufungua moyo ili kukaribisha na kuinua mikono ili kushukuru, kwa sababu Mungu anaonyesha upendo wake mkuu kwetu, kwa kufanya makao kati yetu na kuleta wokovu kwetu. Wokovu ni kazi ya Mungu, lakini yeye hakutaka kuifanya peke yake; alipendelea kuuomba ushiriki wa binadamu. Bikira Maria ndiye mmoja wetu aliyejibu kwa mwaliko wa Mungu kwa upatikanaji kabisa. Uamuzi wa Mungu wa kumchagua mwanamke huyo mdogo unaonyesha kwamba njia yake ya kutenda ni tofauti na yetu.

            Katika andiko la kwanza, tuko na andiko la kitabiri nje ya maandiko ya manabii. Bwana Mungu anaonyesha hamu yake ya kukaa miongoni mwa watu wake lakini ana njia yake mwenyewe wa kufanya hivyo. Kupitia ukoo wa Daudi, atamtuma mfalme mpya ambaye ataanzisha ufalme imara na milele. Utabiri huu ulitimiza katika Kristo ambaye tangu mwanzo wa maisha yake ya kidunia, alichukua ahadi na historia yetu na kujitambulisha na hali yetu. Yeye ndiye Mungu pamoja nasi. Paulo anajiona mjumbe mwaminifu wa injili ya Yesu Kristo ambaye alitabiriwa na manabii wote. Yeye ndiye ufunuo mkuu wa upendo wa Mungu na kupitia yeye watu wote wanaalikwa kumwamini Mungu na kukubali mipango yake katika maisha yao.  

Andiko la Luka hili linajulikana kama andiko la “Kupasha habari”. Ndilo tangazo la kuzaliwa kwa Yesu Kristo aliye utimizaji wa ahadi za Mungu za Agano la Kale. Ndiye Masihi aliyetarajiwa kwa muda mrefu na alikuwa hali halisi duniani kupitia Bikira Maria. Makaribisho yako yalikuwa maalum kwa sababu aliishi matarajio ya ujio wa Masihi kulingana na mapenzi ya Mungu na kabla ya kuzaa Yesu katika tumbo lake, yeye alimzaa moyoni mwake. Kama mwanamke mwangalifu, alikuwa makini sana kwa hali ya dunia na mahitaji ya wanadamu. Aliikataa mipango yake ya kibinafsi kama kijana ili aishi mpango wa wokovu wa Mungu. Mariamu alipata kuishi wito wake kupitia kusikiliza Neno la Mungu na kutenda kulingana na neno hili kama tabia yake ya kawaida. Mwinjilisti Luka anaongea kuhusu tabia hii akisema, “Mama yake aliyaweka maneno hayo yote, akiyafikiri moyoni mwake”.

 Hivyo, neno la kwanza la malaika ndio mwaliko wa furaha kwa sababu maisha ya Bikira Maria yalimpendeza Mungu. Mariamu alishangaza maana ya habari hii kwako kwa sababu ya unyenyekevu wake lakini yeye aliandaliwa na Mungu na kusaidiwa na neema yake kwa ajili ya kuwa Mama ya Mwokozi. Tangazo la Malaika Gabrieli lilimwomba Mariamu uthibitisho wa “ndiyo” ambayo yeye alikwisha ishi kama tabia ya kawaida. Hivyo, ingawa Mungu aliomba jibu la ukarimu na Bikira Maria alijibu kwa njia kamili. Katika udogo na unyenyekevu wake tunaweza kuona ukuu wake, kulingana na maneno yake mwenyewe: “Mungu anamwangalia mtumishi wake katika unyenyekevu wake... watu wote wataniita amebarikiwa (Lk 1,48).” Maisha na chaguzi za Mariamu ni tangazo kuu la maajabu ya Mungu. Kulingana na maisha yake, mtu ambaye huamini katika ahadi ya Mungu ni mwenye furaha, kwa sababu Mungu anayeahidi ni mwaminifu.


Maisha ya Bikira Maria yanashuhudia kwamba Mungu hahitaji matukio makubwa kwa kujifunua mwenyewe. Anakuja kututembea katika maisha yetu ya kawaida naye ana mpango wa upendo kwa kila mtu. Anachukua nafasi ya kutualika kama washirika katika kazi zake na kutupa uwezo kwa kumjibu kwa upatikanaji kabisa kama Bikira Maria. Mungu ndiye mwaminifu kwetu kama alivyokuwa kwa Bikira Maria. Furaha yetu ilianzishwa na uaminifu wake. Tunamshukuru Mungu kwa tendo lake katika maisha yetu kwa njia ya Bikira Maria. Ukarimu na upatikanaji wake kwa mapenzi ya Mungu unatuimarisha katika jibu letu la kila siku kwa mwaliko wake na kutualika tuwatumikie wengine kwa furaha na shukrani kama maonyesho halisi ya jibu letu la ukarimu. 

Fr Ndega

domingo, 17 de dezembro de 2017

ANNUNCIARE DIO SENZA PRENDERE IL POSTO DI DIO


Riflessione su Gv 1, 6-8.19-28


      Giovanni è un uomo mandato da Dio. Da questo mandato dipende tutta la sua esistenza. Egli era consapevole della sua missione perché ha ricevuto un mandato di Dio per questo. Così sono i profeti: loro non inventano la loro “missione”, semplicemente la accolgono. È una iniziativa divina a partire da un rapporto intimo con la persona scelta e con una finalità ben concreta – come nel caso di Giovanni - per dare testimonianza alla luce. Lui è un tramite, un mediatore, un precursore. Tramite lui la gente è stata attirata alla luce. Più il testimone si nasconde, più la luce brilla.

          Giovanni è interrogato sulla sua identità, vale a dire, ‘tu, che dici di te stesso?’ La sua risposta è una grande lezione di umiltà, contrariando tutte le aspettative umane. Normalmente noi approfittiamo dell’occasione opportuna per presentare i nostri titoli e le cose che facciamo. In altre parole, normalmente parliamo di noi stessi. Giovanni invece no. La sua testimonianza è una negazione di se stesso per affermare l’identità di un altro. La sua vera identità era quella di annunciare l’identità di un altro. La testimonianza di Giovanni è già annuncio di come dovrà essere la vita dei futuri discepoli di Gesù.

       Giovanni dichiara di essere soltanto una voce che grida nel e dal deserto: ‘rendete diritta la via del Signore’, diceva. I profeti sono ‘portavoce di Dio’, cioè parlano in nome di Dio. E questo è dovuto a una intensa esperienza di lui. Il deserto è l’ambiente proprio per essa. I grandi personaggi biblici hanno trovato in questa esperienza la ragione della loro identità, la forza e l’entusiasmo necessario per la missione che Dio ha affidato loro.  Giovanni è una persona che è stata cambiata dalla Parola in una esperienza vissuta nel deserto e ‘dal deserto’ - in quanto esperienza vera di trasformazione - annunzia i cambiamenti necessari per la gente. Il suo compito è preparare le persone per l’incontro con Colui che era già in mezzo a loro ma che essi non conoscevano.

        La testimonianza di Giovanni è vera perché parte da una esperienza che ha vissuto con Gesù fin dall’inizio quando era ancora nel grembo di Elisabetta. Ci sono delle persone che trovano senso per la loro vita cercando riconoscimento dagli altri. Giovanni invece incontra senso nell’essere soltanto la voce che annuncia una presenza, che prepara l’incontro e, al suo tempo, si assenta per non disturbare il rapporto che ognuno è chiamato a fare con colui che deve venire. La sua mediazione non dà fastidio ma facilita. L’esempio di Giovanni ci fa capire che bisogna essere consapevoli della propria identità per non occupare il posto che appartiene a un altro. E Giovanni non ha nessuna pretesa in questo senso perché sa che il punto di riferimento non è se stesso ma un altro.  
  
        Il gesto di Giovanni di battezzare la gente parlava della condizione umana peccatrice e della accessibilità della misericordia di Dio. Ma era solo una preparazione. Il suo gesto è stato significativo in quel momento e poi si è fermato perché annunciava un altro battesimo che rimarrà per sempre trasformando interiormente il cuore di ogni persona. Questo gesto che la chiesa ripete fin dall’inizio della sua fondazione configura la gente con Cristo. È un gesto che annuncia Cristo perché parla della nuova condizione di coloro che rinascono da Cristo. Nella nostra vita cristiana, è Cristo il punto di riferimento e così deve continuare perché sia una vita cristiana vera. Quando mettiamo noi stessi al centro, noi annunciamo un altro e non il vero Cristo. Dobbiamo pensare come diceva Madre Teresa, “Signore, quando penso solo a me stesso, attira la mia attenzione su un’altra persona”.

        L’esperienza intensa vissuta nel deserto ha dato a Giovanni Battista la consapevolezza della sua vera identità. Forse ci manca un rapporto più profondo con colui che ci ha chiamato ad essere suoi messaggeri. La mancanza di intimità con il Signore può portarci ad occupare nella vita delle persone un posto sbagliato. Non possiamo dimenticare che siamo soltanto “la voce e non la parola”. Una volta che abbiamo facilitato l’incontro, dobbiamo farci da parte come ha fatto molto bene il Battista. La nostra missione è “raccontare la bellezza di essere innamorati di Dio” con la vita più delle parole. Se leghiamo le persone a noi stessi, siamo noi i protagonisti e non Dio. Penso che il nostro impegno a partire da questa riflessione è quello di annunciare Dio senza prendere il posto di Dio.

Fr Ndega
Revisione dell'italiano: Giusi 

sábado, 9 de dezembro de 2017

MTINDO KAMILI WA KUANDAA NJIA YA BWANA


Kutafakari kutoka Is 40, 1-5, 9-11; 2Pt 3, 8-14, Mk 1, 1-8

 

Maandiko haya yanatualika kuandaa njia ya Bwana kupitia safari ya kutubu, kwa kukubali mapendekezo ya Neno la Mungu na kutangaza habari njema kutoka uzoefu wa Neno hili. Wale ambao waliongea kwa jina la Mungu walikuwa watu waliobadilishwa na Neno hili kwa njia ya ndani na kwa hivyo, walikuwa mashahidi wa kweli. Mtu yeyote ambaye anaongea kwa jina la Bwana, anaweza kusaidia wengine watembee katika njia ya Bwana.
Nabii Isaya alitabiri kuhusu wakati mpya kwa watu waliokuwa wakiteseka uhamishoni mwa Babeli na kuutarajia ukombozi. Mungu hakuwasahau watu wake na kutaka waonje hali mpya. Hata hivyo ni lazima kuandaa njia ya Bwana, yaani, maisha yao wenyewe. Kama kosa la uaminifu kwa Mungu lilisababisha uhamisho, hakuna njia nyingine ya kuona maisha mapya ila uzoefu wa huruma ya Mungu kwa kupitia kutubu. Mungu anaonyesha enzi yake hasa anapoonea huruma. Hivyo, utukufu wake unadhihirishwa zaidi wakati tabia yetu yabadilika kwa sababu ya mkutano na huruma hii. Hii ndiyo habari nzuri ambayo yapaswa kutangazika. Katika somo la pili, maneno ya Petro ndiyo ushauri ili watu wasubiri ujio wa Bwana wakiwa macho na kujitolea kwa manufaa ya jumuiya. Kulingana na Petro, Mungu ni mvumilivu na mwenye huruma. Hivyo, yeye hataki kuwaadhibu watu, bali atarajia waweze kutubu na kuokolewe.
Miongoni mwa wainjilisti ndiye Marko peke yake ambaye anaingiza injili yake kwa kutumia maneno Habari njema wakati anapoongea kuhusu Yesu. Maneno haya habari njema yalijulikana wakati wa Yesu, lakini hayakutumia katika maana ya kidini; yalitumia ili kutangaza habari ya furaha, mfano, kuzaliwa kwa mfalme ama kutembelea kwa mfalme katika sehemu fulani ya ufalme wake. Tangazo la habari hii lilileta matarajio ya mabadiliko ya hali, lakini baadaye mambo yote yakaendelea kama kawaida. Nia ya Marko ndiyo kujibu swali kuhusu utambulisho wa Yesu, yaani, Yesu ni nani? Kweli katika mwanzo na mwisho wa injili hii tunakuta maneno ‘Mwana wa Mungu’ kumhusu Yesu na mambo yote ambayo Yesu anatenda katika injili hii yaonyesha kwamba Yesu anatoka kwa Mungu kweli. Basi, kulingana na Marko, habari inayoleta furaha ya kweli kwa dunia hii ndiye Yesu aliye Mwana wa Mungu.
 Habari njema ya Yesu inaanza kupitia kazi ya Yohana Mbatizaji, ndiye nabii mkuu, kulingana na Yesu mwenyewe. Yohana anajulishwa kama mfano kwa wote kwa sababu alitumia nguvu zake zote ili kuwaandaa watu wakaribishe Mwana wa Mungu, ndiye Yesu Kristo. Yohana aliishi katika upweke wa jangwa na kufunguliwa kabisa kwa msukumo wa Mungu. Katika mahali hapo alijifunza kutokana na Neno la Mungu, jinsi ya kushuhudia habari njema za wokovu. Ndilo jambo la ajabu tabia yake ya unyenyekevu hasa kuhusu mavazi na chakula. Ukuu wa Yohana ulionyeshwa katika uwezo wake wa kutambua ukuu wa Bwana, akijifikiria mwenyewe kama sauti tu ambaye huandaa njia ya yule atakayekuja. Katika ujumbe wake, Yohana alitangaza huruma ya Mungu akisema: “Mmrudie Bwana! Mungu atawasamehe dhambi zenu.” Pamoja na maneno haya, Yohana aliwabatiza watu kama ishara halisi ya kutubu na makaribisho ya huruma ya Mungu.

Sababu ya uaminifu wa ujumbe wa Yohana ilikuwa sio maneno yake tu, bali pia unyenyekevu wake na njia ya kweli ya kuishi. Hata bila maneno, maisha yake yalikuwa tangazo la kweli la hali mpya ambayo Yesu alikuja kuleta duniani. Maisha ya Yohane yatuambia kwamba tunaweza kufanya tofauti maishani mwa watu, lakini ahadi haiwezekani bila uzoefu wa jangwa, yaani, uzoefu wa ndani wa Mungu na wa Neno lake. Ndio kutoka jangwa kwamba pendekezo la mabadiliko linakuja kwetu. Tukiishi uzoefu wa mabadiliko tunaweza kuwa mashahidi wa habari njema kwa uaminifu kwa sababu ushuhuda wa maisha ndio ufanisi kuliko maneno. Uvumilivu na huruma ya Mungu ndiyo nafasi tunayohitaji ili tuweze kumrudia yeye. 

Fr Ndega

IL MODO GIUSTO DI PREPARARE LE VIE DEL SIGNORE


Riflessione su Is 40, 1-5, 9-11; 2Pt 3, 8-14, Mc 1, 1-8

 

Questi testi ci invitano a preparare le vie del Signore tramite un cammino di conversione, accogliendo le proposte della Parola di Dio e proclamando un lieto annuncio a partire dell’esperienza di questa Parola. Coloro che parlavano nel nome di Dio erano persone che sono state cambiate dalla sua Parola in modo profondo e proprio per questo sono diventate testimoni veri. Colui che parla nel nome del Signore può aiutare gli altri a camminare nelle vie del Signore.
Il profeta Isaia parla di una nuova realtà per il popolo che stava soffrendo nell’esilio della Babilonia e desiderava la liberazione. Dio non ha dimenticato il suo popolo e vuole che esso abbia una nuova vita. Tuttavia, bisogna preparare le vie del Signore, cioè, la loro propria vita. Come la mancanza di fedeltà ha causato l’esilio, non c’è un altro modo per avere una vita nuova eccetto l’esperienza della misericordia di Dio tramite un processo sincero di conversione. Dio mostra la sua potenza salvatrice specialmente tramite la misericordia. Allora, quando cambiamo i nostri atteggiamenti la sua gloria diventa più visibile. Questo è un lieto annuncio che deve essere proclamato. Nella seconda lettura, le parole di Pietro sono un consiglio perché la gente attenda la venuta del Signore in modo vigilante tramite una vita impegnata per la comunità.
Tra gli evangelisti c'è solo Marco che introduce il suo vangelo con l’espressione ‘Buona Novella’ quando parla di Gesù. Questa espressione ‘Buona novella’ era conosciuta al tempo di Gesù, ma non era usata in senso religioso. Era usata per proclamare una grande gioia, un lieto annuncio, per esempio, la nascita di un re o la visita del sovrano ad alcuna parte del suo regno. Questa proclamazione portava aspettativa di cambiamento della realtà, ma alla fine tutto continuava come prima. L’intenzione di Marco è di rispondere alla domanda su “Chi è Gesù?” Infatti all’inizio e alla fine di questo Vangelo troviamo l’espressione “Figlio di Dio” per quanto riguarda Gesù e tutto ciò che Gesù fa lungo questo vangelo mostra che davvero Egli viene da Dio e che davvero ci sono già i cambiamenti. Quindi, secondo Marco, la notizia che porta la vera gioia a questo mondo è Gesù il Figlio di Dio.
La buona notizia di Gesù inizia con l’attività di Giovanni Battista, il maggiore dei profeti, secondo Gesù. Giovanni è presentato come modello per tutti perché ha impiegato tutte le sue energie per preparare la gente ad accogliere il messia Figlio di Dio. Giovanni ha vissuto nella solitudine del deserto ed era totalmente aperto all’ispirazione di Dio. In quel luogo ha imparato dalla Parola di Dio come testimoniare la buona notizia della salvezza. Veramente ci colpisce il suo stile di vita semplice specialmente per quanto riguarda il vestito e il cibo. La grandezza di Giovanni era dimostrata nel riconoscere la grandezza del Signore, considerando se stesso come soltanto una voce che grida “dal” deserto preparando la strada a colui che deve venire. Nel suo messaggio, Giovanni ha proclamato la misericordia di Dio, dicendo: “Ritornate al Signore! Dio perdonerà i vostri peccati”. Oltre le parole, Giovanni battezzava la gente come un segno concreto di conversione e apertura alla misericordia di Dio. Il suo gesto era anche annuncio del nuovo e vero battesimo.
La ragione della credibilità del messaggio di Giovanni non erano solamente le sue parole, ma anche la sua umiltà e il suo stile semplice di vivere. Anche se le parole non ci fossero, la sua vita era già un vero annuncio della nuova realtà che Gesù ha portato sulla terra. La vita di Giovanni ci dice che possiamo fare la differenza nella vita di molte persone, ma non c’è profezia senza ‘esperienza di deserto’, cioè, esperienza profonda di Dio e della sua Parola. È, quindi, dal ‘deserto’ che ci viene la proposta di ritornare, di cambiare le vie, la mentalità, insomma, di cambiare qualcosa. Se la nostra vita è cambiata dalla Parola saremo davvero testimoni di una buona notizia perché la testimonianza di vita è più efficace delle parole. La pazienza e misericordia di Dio sono l’opportunità di cui abbiamo bisogno per ritornare a lui e rimanere sempre in comunione con Lui.

Fr Ndega
Revisione dell'italiano: Giusi

domingo, 3 de dezembro de 2017

BWANA WETU ANAKUJA KUTUPA FURAHA NA WOKOVU


Kutafakari kuhusu Isaya 63: 16-17; 64: 1, 4-8; 1Wak 1, 3-9; Mk 13: 33-37


Kulingana na liturjia ya Kanisa Katoliki, tunaanza wakati mpya uitwao Majilio. Wakati huu unatukumbusha Ujio wa kwanza wa Bwana Yesu na kutuandaa ili tusherehekee sikukuu ya kuzaliwa kwake katika Krismasi. Tena Majilio yaimarisha matumaini yetu juu ya kuja kwake mara ya pili katika mwisho wa umri. Ujio wake kama Bwana wa maisha yetu na wa historia hauleti hofu bali furaha. Masomo haya ndio mwaliko wa kukesha ili tutambue na kuzikaribisha ishara za uwepo wa Bwana katika hali yetu ya kila siku. Ndio mwaliko pia wa shukrani maana Bwana anakuja kukutana nasi daima, ili kutupa wokovu wake. Matukio yote makuu yahitaji maandalizi mema na ndani ili kusherehekewa mema. Hivyo ndivyo Majilio kama maandalizi ya tukio kuu la Krismasi.
Katika somo la kwanza, nabii Isaya alimwelekea Mungu maombi ya imani na upendo, akimtambua kama Baba. Nabii huyo anaongelea uaminifu wa Mungu anayewaokoa watu wake, na tena kosa la uaminifu wa watu kwa ajili ya Agano. Upinzani dhidi ya maongozi ya waliotumwa na Mungu uliwafanya watu wajione mbali na Mungu. Maombi ya nabii ni faraja na msaada ili kufufua matumaini katika Bwana ambaye yuko tayari kutoa nafasi mpya kwa yeyote anayetaka kumrudia yeye. Katika somo la pili, Paulo anamshukuru Mungu, kwa sababu ya tendo la neema yake katika jumuiya ya Wakorintho, ambayo imezaa matunda mazuri kama jibu la tendo hili. Jumuiya hii inatarajia ujio wa Bwana sio kwa njia yoyote bali kwa imani halisi iliyo maonyesho ya ahadi yao kwa karama ilizopokea. Matakwa ya Mtakatifu Paulo ni kwamba jumuiya hii iendelee kwa imara katika ujumbe uliotolewa kuhusu Yesu na kukua katika imani kwake anayeaminika.
Katika Injili, Yesu anazungumza kuhusu fumbo la Kuja kwake. Ni sehemu ya mpango wa hekima na wema wa Baba. Ikiwa tunachukua mwanzo wa  sura ya kumi na tatu ya Marko, tunatambua kwamba Yesu anaongea kuhusu uharibifu wa hekalu la Yerusalemu na kuendelea kwa kuongelea dhiki ya mti huu. Tena anajali kuhusu nabii wa uongo na haja ya uvumilivu katika ushuhuda mpaka upeo ili kupokea wokovu. Wokovu ndio zawadi ya ujio wa Bwana ambao, kulingana na andiko hili hakuna yeyote ambaye anajua wakati kamili wa tukio lake. Wote wanaalikwa kukesha. Baadhi ya mifano inatusaidia kuingia vizuri katika mwendo wa ujio huu:
Kipengele cha kwanza ni wazo wa wakati. Tuko na maneno mawili ya Kigiriki ili kuongea kuhusu wakati, yaani Kronos na Kairos. Neno ambalo andiko hili linatumia ndilo Kairos linalomaanisha wakati mwafaka, nafasi ambayo Bwana anatupa. Bwana haji ili kuadhibu bali kuleta furaha: tuwe macho ili kuchukua nafasi ya kuwa wenye furaha! Kipengele cha pili ni mtu mwenye kusafiri. Huyo ndiye Yesu aliye Mwenye nyumba na Bwana wa historia. Cha tatu ni watumishi. Katika biblia, watumishi ni wale ambao walitoa maisha yao kwa ajili ya mpango wa Mungu. Cha nne ni nyumba: ndiyo jumuiya ya wanafunzi ambao waliingia katika ufalme kwa sababu walikubali pendekezo la nane heri. Bwana alimkabidhi kila mtu mpango wake na kutaka kuwazawadisha watumishi ambao wanakesha ili kushiriki naye furaha yake.
Cha tano ni Bawabu. Huyo ndiyo dhamiri ya kila mtu ambayo inapaswa kukesha ili kuepuka ingizo ya mtu mgeni yeyote ambaye anataka kuwa mwenye nyumba. Tunaalikwa kuwa macho ili tutambue Bwana anapokuja na kuufungua mlango kwake peke yake. Yeye anataka kukutana nasi na kutaka tena tubaki katika ushirika naye. Anatarajia kukaribishwa vizuri, kulingana na maneno yake mwenyewe: "Mimi nasimama mlangoni na kubisha hodi. Mtu akisikia sauti yangu na kufungua mlango, nitaingia nyumbani kwake na kula chakula pamoja naye, naye atakula pamoja nami” (Apocalypse 3, 20). Kipengele sita ni usiku. Usiku ni ishara ya giza na dhambi. Wakati tunaposema kwamba Bwana anakuja usiku inamaanisha kwamba anakuja kama mwanga ili kufukuza giza, chambi, huzuni na kuanzisha hali mpya kabisa.  
Basi, Kuja kwake Bwana badala ya kuwaogopesha watu, kunayaimarisha matumaini katika wokovu wake, kwa sababu yeye ni Mwokozi na kuja ili kuokoa. Safari ya Kikristo ni safari ya furaha ili kukutana naye kwa sababu yeye huja daima kukutana na sisi. Uwepo wake ni dhamana ya ulinzi, kulingana na maneno yake mwenyewe: “Nitakutegemeza salama wakati ule wa dhiki inayoujia ulimwengu mzima... Naja kwako upesi (Apoc. 3, 10b-11a). Kutoka upande wetu ni muhimu kuwa macho kwa kuja kwake ili kumkaribisha kwa upatikanaji na uaminifu. Maonyesho halisi ya makaribisho huu ndio utumishi wetu katika jumuiya kwa ukarimu na furaha.

Hivyo, Majilio ni wakati wa kufanya upya ahadi yetu na Bwana, katika mwendo wa mabadiliko daima. Kuhusu hili, Bwana anatuambia tena: "Wewe unayo saburi, umestahimili taabu nyingi kwa ajili ya jina langu, wala hukuvunjika moyo. Lakini ninalo jambo moja dhidi yako: wewe hunipendi tena sasa kama pale awali. Basi, pakumbuke pale ulipokuwa kabla ya kuanguka, ukatubu na kufanya kama ulivyofanya pale awali” (Ufu 2, 3-5a). Kusali zaidi na kupatikana ni tabia za mwanafunzi wa kweli anayejua Bwana wake naye uko tayari daima ili kumkaribisha. Kukesha kwa uaminifu na ukarimu ni ishara halisi ya matarajio yetu kwa ujio wa Bwana.

Fr Ndega