domingo, 30 de julho de 2017

FURAHA KUBWA NA KAMILI


Kutafakari kuhusu Mt 13, 44-52


             
           Sura kumi na tatu ya injili ya Mathayo inajulisha mifano mingi ya Yesu ili kuonyesha kwamba hali ya Ufalme wa Mungu siyo mbali na hali zetu bali inatokea miongoni mwetu na ndani yetu. Baada ya mtaguso wa Vaticano wa pili, baba mtakatifu Paulo wa VI aliandika waraka mmoja unaoitwa Evangelii Nuntiandi akiwaimarisha Wakristo kwa kazi ya kueneza injili kwa njia mpya. Kati ya mambo ya waraka, yeye alitaja jambo la ufalme wa Mungu/mbinguni, akisema, “Ufalme ambao injili inatangaza huchukuliwa na watu walio wa utamaduni halisi kwa njia ya ndani. Haiwezekani kujenga ufalme huu kwa kuacha thamani za ustaarabu na tamaduni za kibinadamu” (EN 20). Kwa maneno mengine, hali ya ufalme inachanganyika na hali yetu. Thamani za ufalme zinapaswa kuwa rejeo la maisha yetu. Kwa hivyo Yesu anatujulisha siku ya leo mifano mitatu.

         Katika mfano wa kwanza ufalme wa mbinguni unafanana na hazina iliyofichika na kukutwa shambani; wa pili, unafanana na lulu nzuri kuliko nyingine zote; na tatu, na wavu uliotupwa baharini, ukanasa samaki wa kila aina. Mifano miwili ya kwanza inadhihirisha kwamba Ufalme wa mbinguni ni hali inayopatikana, lakini ni muhimu pia kuitafuta hali hii. Kulingana na utabiri wa nabii Isaya, ndiye Mungu mwenyewe anayepatikana na kwa hivyo tunaalikwa kumtafuta. Anasema Carlo Dellari kwamba, “Sio sisi tuliomfikia Mungu ili kumjua bali ndiye yeye aliyetutangulia katika mkutano na kutuimarisha kutembea ili kukutana naye. Mtakatifu Agustino alikwisha sema uthibitisho huu wakati ulipomfanya Bwana kusema maneno haya, yaani ‘wewe haungenitafuta ikiwa haungalikwisha nikuta mimi’”.

     Basi ufalme sio muundo wa nguvu kama falme za nchi bali ni tendo la Mungu mwenyewe ambaye anapatikana kwa wote. Lakini sio wote ambao wanapatikana kukutana nawe. Ufalme huu una thamani sana na husababisha furaha kubwa katika maisha ya mtu ambaye aliugundua ama aliukuta. lakini kwa ajili ya furaha hii mwanafunzi anaalikwa kujinyima kila kitu, yaani kuacha mahali, mali na “usalama” wa uwongo kwa sababu “bila juhudi za kutafuta na kujinyima, furaha ya mkutano haiwezekani." Uzoefu wa kugundua ufalme kama hazina ni uzoefu wa kukuta maana ya kweli ya maisha. Hali nyingine haina maana tena. Furaha tunayoiona ndiyo matokeo ya chaguo letu.

      Katika mfano wa tatu Yesu alifananisha ufalme na wavu uliotupwa baharini ambao unanasa samaki ya kila aina. Mfano huu unadhihirisha kwamba Mungu ana mpango wa wokovu kwa wote kwa sababu anataka kuwakaribisha wote katika ufalme wake. Lakini ni lazima hukumu iwe kwa sababu makaribisho ya pendekezo lake si sawa kwa wote. Kulingana na maana ya mfano huu, katika mwisho wa nyakati wabaya hawatakuwa na nafasi sawa na wema. Kila mmoja atakuwa na nafasi ambayo alichagua kulingana na maisha aliyoishi. Lakini hakuna sababu ya kukata tamaa kwa maana Mungu anataka kuwaokoa wote na kutuimarisha kutafuta kwanza ufalme wake kama chaguo kamili. 


       Basi, Huu ndio mwendo wa kumfuata Yesu. Yeye ndiye hazina yetu ya kweli. Anatuvutia kwake kwa sababu ya wema, ukweli, uvumilivu na unyenyekevu wake. Yule ambaye anakutana  na Kristo habaki alivyo kwa sababu alikuta lile ambalo linatoa maana kwa kila kitu. Kweli mkutano unaweza kubadilisha maisha yetu kabisa kwa sababu unaleta njia tofauti ya kuona na kutenda. Furaha ndio matokeo ya mkutano naye na kumchagua kama rejeo la pekee la maisha yetu. Yesu alitushirikisha Ufalme wake nasi tunaalikwa kujikabidhi mikononi mwake kwa ajili ya kuchagua vizuri katika kila kitu. Yule ambaye alimchagua Kristo yeye alichagua ufalme ulio hali ya ahadi ya kindugu, ya amani na ya upatanisho. Ndicho kipimo cha furaha kubwa na kamili. 

Fr Ndega
Mapitio ya Kiswahili: Christine Githui

domingo, 23 de julho de 2017

KUIFUATA NJIA YA MUNGU ILI KUONDOA UOVU WA ULIMWENGU


Kutafakari kuhusu Hek 12, 13.16-19; War 8,26-27; Mt 13, 24-43


       Kulingana na tafakari yetu katika wiki iliyopita, kati ya mbegu zilizoanguka kwenye ardhi, moja peke yake ilipatikana kuwa hali nzuri ili kupokea mbegu njema na kuzaa matunda. Mbegu njema ni neno la Mungu ambalo lina nguvu ndani yake ili kuzaa maisha mapya katika mahali linapokaribishwa. Kulingana na andiko la siku ya leo, hata ikiwa ardhi ni sawa, inaweza kupatikana magugu pia. Magugu ni mfano wa ishara za mauti ambazo tunaweza kukuta mahali ambapo ishara za maisha zipo. Hali hii inamaanisha kwamba hata ikiwa moyo fulani ni mwema unaweza kubeba mbegu ya uovu, yaani unaweza kuwa na mwelekeo mbaya. Adui ya Mungu atatenda daima kuwazuia watoto wake waishi kulingana na mapenzi yake.

          Andiko la Hekima ni wimbo unaoongelea wema na uvumilivu wa Mungu kwa watoto wake wote. Enzi na nguvu yake haimzuii kutenda kwa upole na upendo, akiwatunza wote, hasa wale wasio na nguvu. Akitenda hivyo, aliwaelimisha watu wake akiwapa nafasi ya toba na mabadiliko ya maisha ili yawe kulingana na matarajio yake. Mungu ndiye mwenye huruma na mvumilivu kwa sababu anapenda kwa  upendo wa milele, yaani upendo unaotoa tumaini zuri kwa kufungua milango ambayo tumefunga kwa sababu ya makosa yetu. Tunahitaji upendo huu na tunataka sana kupenda kama Mungu alivyo. Hilo ndilo tendo la Roho wake anayekaa ndani yetu ili tujifunze kuomba kwa imani ya watoto, kwa kutamani moyoni mwetu Mungu anayetamani ndani yetu.

         Mfano ambao Yesu anatujulisha unaongelea mwendo wa Ufalme ulio kama mtu mmoja aliyepanda mbegu njema katika konde lake, lakini wakati wa usiku adui yake alikuja na kupanda pia magugu kati ya ngano. Tunataka kutafakari kidogo juu ya tabia mbili, yaani: tabia ya kosa la uvumilivu kwa upande wa watumishi na uvumilivu wa mwenye konde (mbele ya tendo la adui na ya kutokomaa kwa watumishi). Nia ya Yesu ni kuongelea Mungu kama Yule anayepanda mbegu njema katika konde kubwa la ulimwengu wala hawezi kufanya tofauti maana yeye ndiye mwema. Adui yake alipanda magugu, yaani mbegu mbaya. Je, inawezekana kufanya nini kwa magugu haya? Mwenye konde ana mpango mmoja, lakini anapendelea kusubiri na kutenda katika wakati mwafaka, yaani katika wakati wake mwenyewe. Adui aliyepanda magugu alitenda katika usiku, yaani amefichwa. Matendo dhidi ya mapenzi ya Mungu yaonyesha hali za giza maishani mwetu.     

         Ni wazi katika andiko hili kwamba uovu hautoki kwa Mungu; yeye hataki uovu. Yeye mwenyewe anawaimarisha wanafunzi wa Mwanawe waangalie njia yake ya kutenda kwa kuondoa uovu wa ulimwengu na wa maisha yao. Kwa bahati mbaya, binadamu anabeba pia uovu ndani yake pamoja na wema unaotoka kwa Mungu. Haikuwa hivyo tangu mwanzo. Mungu alifanya binadamu kama mtu mwema na mwenye uhuru ili aweze kuchagua, yaani “Mungu alimwambia binadamu, ikiwa unachagua wema na uhai wewe utaishi milele; ikiwa unachagua uovu na mauti wewe utakufa.” Wakati uhuru wa binadamu ‘haufanywi upya na injili’ unaweza kutenda kama adui. Basi, kama matokeo ya uamuzi wa kibinadamu, wema na uovu umekua pamoja ulimwenguni. Mara nyingi uovu unaonekana wenye nguvu kuliko wema kwa sababu tunaulisha zaidi. Tena mara nyingi tumeshangaa tunapoona kwamba mtu fulani anayeonekana mwema ndiye mbaya na yule anayeonekana mbaya ndiye mwema. Kwa matarajio siyo mazuri na kwa haraka tuko na mazoea ya kuwahukumu wengine. Tendo hili siyo kazi yetu.

          Kulingana na mwendo wa mfano huu, ni lazima kuwa na uvumilivu na utambuzi ili kuondoa uovu katika wakati mwafaka na kwa matendo kamili ili yaweze kuimarisha wema pia na sio kupunguza nguvu zake. Ndiyo katika hali hii ya wema na uovu ambayo thamani za Ufalme zilipandwa. Kama Mungu ndiye wa kwanza kwa nia ya kuondoa uovu wa ulimwengu, yeye mwenyewe anatualika kusubiri kwa uvumilivu kwa kujifunza kutoka kwake ambaye anawanyeshea mvua watu wa haki na wasio na haki ama watu wema na wabaya. Kwa uvumilivu wake Mungu ametupa nafasi nyingi za toba na mabadiliko ya maisha. Basi, kuwa na uvumilivu sio kukubali uovu bali kuifuata njia ya Mungu ambaye ana milele mbele yake na kujua jinsi ya kubadilisha uovu kuwa wema kwa sababu anajua jinsi ya kupenda. Kweli huu ndio mwaliko tubadilishe mtazamo wetu kwa kutenda kulingana na moyo wa huruma ya Mungu.


Fr Ndega
Mapitio ya Kiswahili: Christine Githui

sábado, 22 de julho de 2017

SEGUIRE IL MODO DI DIO PER ELIMINARE IL MALE DAL MONDO


Riflessione su Sap 12, 13.16-19; Rom 8,26-27; Mt 13, 24-43


         Come abbiamo riflettuto nella settimana scorsa, tra quattro tipi di terreni, solo uno è trovato nelle condizioni d’accogliere il buon seme e generare frutto. Il buon seme è la parola di Dio che ha la forza in sé per generare nuova vita là dove è accolta. Secondo il testo di oggi, anche se il terreno è buono, può accogliere anche la zizzania. Questa è simbolo dei segni di morte che possiamo trovare anche là dove ci sono i segni di vita. Questo mette in luce che anche se il cuore è buono può portare la semente del male, cioè, può avere cattiva tendenza. Il nemico di Dio agirà sempre per impedire che i suoi figli vivano secondo la sua volontà.

        Il testo della Sapienza è un inno a Dio per la sua bontà e pazienza verso tutti i suoi figli. La sua potenza e grandezza non gli impediscono di agire con mitezza e tenerezza, prendendosi cura di tutti specialmente di coloro che sono più deboli. Con questo suo modo d’agire ha educato il suo popolo offrendo a tutti delle opportunità di cambiare vita perché essa sia secondo il suo desiderio. Dio è indulgente e paziente perché ama con un amore eterno, cioè, un amore che ci dona buona speranza aprendo le porte che abbiamo chiuso con i nostri sbagli. Abbiamo bisogno di questo amore e desideriamo molto amare come Dio. Questa è la azione del suo Spirito che abita dentro di noi affinché sappiamo pregare con fiducia di figli, desiderando nel nostro cuore ciò che Dio desidera per noi.

        La parabola che Gesù ci presenta parla della dinamica del Regno che è come un uomo che ha seminato il buon grano nel suo campo ma durante la notte venne il suo nemico e seminò della zizzania in mezzo al buon grano. Vogliamo soffermarci su due atteggiamenti: il primo è la decisione dei servi, la loro impazienza; il secondo è quello del dono del campo, cioè, la sua pazienza (davanti alla malvagità del suo nemico e alla immaturità dei servi). L’intenzione di Gesù è parlare di Dio come colui che semina il buon grano nel grande campo del mondo e non può fare diversamente perché egli è buono. Il suo nemico ha seminato la zizzania, cioè il grano cattivo. Cosa fare con questa zizzania? Il dono del campo ha già una idea ma preferisce aspettare e agire nel tempo opportuno, vale a dire, nel suo proprio tempo. Il nemico che ha seminato zizzania ha fatto questo di notte, di nascosto. Le azioni contro i desideri di Dio rivelano situazioni di tenebre nella nostra vita.

         È chiaro in questo testo che il male non ha la sua origine in Dio; Egli non vuole il male. Egli proprio motiva i discepoli di Gesù a guardare il suo modo d’agire per rimuovere il male del mondo e della loro vita. Purtroppo l’essere umano porta anche il male dentro di sé insieme al bene che viene da Dio. Non è stato così fin dall’inizio. Dio ha creato l’essere umano come essere buono e libero per potere fare delle scelte, vale a dire, “Se tu scegli il bene, la vita, vivrai; se tu sceglie il male, la morte, tu morirai”. Quando la libertà umana non è ‘evangelizzata’ può agire come nemica. Quindi, come risultato della decisione umana, il bene e il male crescono insieme nel mondo. Alle volte il male sembra più forte perché cerchiamo di alimentarlo di più. Molte volte siamo rimasti sorpresi nel vedere che ciò che sembra buono è cattivo e ciò che sembra cattivo è buono. Con i nostri pregiudizi abbiamo fretta di giudicare gli altri sul loro modo di vivere. Questo non tocca a noi.


         Secondo la dinamica di questa parabola, bisogna avere pazienza e discernimento per eliminare il male nel suo giusto tempo con azioni adeguate che possano anche rafforzare il bene, non indebolirlo. È proprio in mezzo a questa realtà di bene e male che i valori del Regno si trovano seminati. Come Dio è il primo interessato in volere eliminare il male dal mondo, Egli stesso ci invita ad aspettare pazientemente, imparando da lui che fa piovere sui giusti e ingiusti, buoni e cattivi. Tramite la sua pazienza Dio ci ha dato molte opportunità di conversione, di cambiare vita. Allora, avere pazienza non vuol dire accettare il male ma accompagnare il ritmo di Dio che ha l’eternità davanti a sé e sa come trasformare il male in bene perché sa amare. Questo è davvero un invito a cambiare il nostro modo di vedere le cose, agendo secondo il cuore misericordioso di Dio.

Fr Ndega
Revisione dell'italiano: Giusi

domingo, 16 de julho de 2017

MBEGU ZILIANGUKA PENYE UDONGO MZURI NA KUZAA MATUNDA MAZURI


Kutafakari kutoka Mt 13, 1-23



        Tunataka kutafakari juu ya ufanisi wa Neno la Mungu katika maisha yetu na majibu yetu mbalimbali mbele ya tendo la neno hili. Kulingana na maneno ya nabii Isaya, neno la Mungu ni kama mvua na theluji ambazo hazimrudii Mungu bila kuipandishia ardhi na kuifanya kuota (angalia Isaya 55:10). Hivi ndivyo Neno la Mungu katika maisha yetu liko. Mungu anapoongea, yeye huumba na kuumba tena, yaani, anatoa uhai kulingana na mapenzi yake. Picha nyingine ambayo tunataka kutafakari kwa kina ndiyo “mbegu”, ambayo huleta nguvu kubwa ndani yake yenyewe, lakini inahitaji mazingira mazuri ya kuzaa matunda. Lengo la Neno ndilo kuyatimiza mambo yanayompendeza Mungu, yaani, mabadiliko ya maisha yetu.

      Katika mwanzo wa injili, watu walikusanyika ili wasikilize Neno la Mungu kwa kinywa cha Yesu. Tunajua kwamba Katika tangazo la Ufalme wa Mungu, Yesu alipendelea kutumia lugha rahisi ili watu waweze kuyakaribisha mafundisho yake vizuri sana. Yeye aliitumia mifano kuihusu hali ya kimungu na hali ya kibinadamu. Alianza akitumia ishara ambazo watu walizijua na baadaye hatua kwa hatua aliwafunulia upya wa hali ijayo. Hivyo, Yesu aliwafanya watu waone, kwa matarajio, uzima ambao anaahidi, akiongeza matumaini ya wokovu moyoni mwao. Yule ambaye anaongea maneno ya uzima wa milele anataka kusikika, lakini makaribisho hayakuwa sawa kwa upande wa wasikilizaji wake. Kama matokeo, maneno ya Yesu hayakuweza kusababisha mabadiliko aliyotarajia. Haya ndiyo mazingira ambayo mfano wa mpanzi ulizaliwa.

       Kuhusu watu ambao walisikia mifano yake, Yesu alisema, “Mtasikia, lakini hamtaelewa. Mtatazama, lakini hamtaona.” Kwa upande wa wanafunzi wake, Yesu alisema: “Heri yenu nyinyi, maana macho yenu yanaona na masikio yenu yanasikia”. Basi, ikiwa lengo la mifano ni kuwa lugha rahisi ili watu wafahamu siri za Ufalme, kwa nini Yesu alianzisha tofauti kati ya wanafunzi wake na watu wengine? Ndiyo kwa maana wanafunzi wake walikubali mafundisho yake kwa moyo ambao umefunguliwa na kuishi kulingana na mapenzi ya Mungu. Wengine walikuwa na tabia tofauti. Hao walimpinga Yesu tangu mwanzo. Katika Yesu hali ya ufalme imekuwa halisi kupatikana; upinzani dhidi yake ni upinzani kwa mafanikio ya ufalme huu. Tufikirie sasa mfano wa mpanzi.

     Mpanzi alikwenda kupanda mbegu zake nyingi na mbegu zile zilianguka katika mahali mbalimbali. Kama mpanzi huyo, ndivyo Mungu anavyofanya kwa midomo ya Yesu. Yeye ameongea sana na Neno lake lina nguvu ya kuumba na kuzaa maisha mapya. Kwa upande wa Mungu anaona furaha kubwa kuwaambia watu wake kitu. Kila mazungumzo na Yesu ni mwaliko wa kufikiri na kutenda tofauti. Mbegu ni Neno la Mungu. Nia ya Yesu ilikuwa kuongea kuhusu nguvu ya neno lenyewe na kwamba ni lazima kulisikiliza kwa uangalifu ili neno hili liweze kutimiza mapenzi ya Mungu maishani mwa watu. Katika Biblia neno kusikiliza linamaanisha vitendo viwili, yaani, kusikia na kuishi/kushika. Kuhusu mahali pengi, tunafikiria tabia mbalimbali za watu mbele ya Neno la Mungu na tena matokeo mbalimbali katika hali ya kawaida.

     Mbegu zilizoanguka njiani zinaonyesha kwamba mara nyingi tunaposikia Neno la Mungu, bila ahadi kwa Neno hili tunaruhusu ibilisi aliondoe neno lililopandwa mioyoni mwetu. Tendo letu hili linaiondoa maana ya Neno. Mbegu zile zilizoanguka penye mawe zinaonesha kwamba tunaposikia Neno la Mungu tunapokea kwa furaha, lakini kwa sababu ya imani ndogo sisi husadiki kwa muda mfupi tu, na tunapojaribiwa sisi hukata tamaa. Zile zilizoanguka kwenye miti ya miiba ni tunaposikia neno la Mungu, lakini wasiwasi, mali na anasa za maisha zinatuzuia tubadilishe tabia zetu.  Zile zilizoanguka kwenye udongo mzuri ni tunapolisikia Neno la Mungu na kulikaribisha vizuri kwa kuyafananisha maisha yetu kulingana na neno hili. Lakini hali hii ni tendo la Neno lenyewe kwa neema ya Mungu kwa sababu neno la Mungu “ni ufanisi na halimrudii yeye tupu.”


         Kulingana na andiko hilo, kuna tofauti kati ya moyo wa wanaomfuata Yesu na wengine wanaomsikiliza tu. Njia ya kupanda mbegu ni mfano wa ukarimu wa Mungu. Kwa upande wake hakuna mipaka; ni ukarimu tu. Kutoka ukarimu wake tumepokea neema juu ya neema, lakini uwezo wetu wa kuipokea neema yake ni mdogo sana. Hata hivyo, ikiwa tuko tayari kulisikiliza na kulishika neno la Mwanawe, Mungu mwenyewe anazidisha uwezo na ukarimu wetu ili tuweze kusonga mbele kwa matendo mema mengi kulingana na matarajio yake. Tena na tena tunahitaji kufahamu kwamba Mungu anatarajia mafanikio yetu, lakini uamuzi ndio wetu. Tukaribishe pendekezo la Yesu kwa utayarisho wa moyo ili tuweze kupata maisha mapya ambayo Neno lake linatoa.

Fr Ndega
Mapitio ya Kiswahili: Christine Githui

domingo, 9 de julho de 2017

ANAYAPINGA MATARAJIO YA WAKUBWA NA KUYATIMIZA MATUMAINI YA WADOGO


Kutafakari kuhusu Zc 9,9-10; War 8,9.11-13; Mt 11,25-30


       Ni muhimu sana kutafakari tena kuhusu jambo la picha za Mungu kwa sababu mtazamo wetu, mawazo yetu na misimamo yetu mbele ya mambo yote ulimwenguni yategemea picha yetu ya Mungu. Maandiko haya yanatualika kufikiria picha kamili za Mungu ambazo ni muhimu sana katika safari yetu ya imani, yaani Mungu Mnyenyekevu, Mungu wa amani, Mungu Emanueli, Mungu wa Uhai, Mungu Aliyeguswa na hisia, Mungu Baba, Mungu Mpole na Mnyenyekevu wa moyo, Mungu wa wadogo, n.k. Tunaalikwa kumwacha Mungu awe Mungu mwenyewe. 
  
        Ingawa andiko la somo la kwanza liliandikwa baada ya utumwa wa Babeli, nabii Zakaria alitangaza habari ya wakati mpya ujao ambao Watu watafanywa wapya na mfano wa upole wa Mungu. Yeye anatangaza kwamba Mungu anakuja kwao na wakati huo huo yeye anakwisha kuwepo miongoni mwa watu kama Mungu wa amani. Watu ambao wanaweza kumtambua ni wale ambao Yesu atataja katika injili kama “wadogo”. Mfano wa upole wa Mungu unayapinga matarajio ya wale wanaojiona wenye nguvu na kutafuta masuluhisho kwa matatizo kupitia ukatili. Habari njema ambayo tuko nayo ya kutangaza ni kwamba Mungu ni tofauti na zile picha ambazo zinawaogopesha watu. Kulingana na somo la pili, Roho wa Mungu anakaa ndani yetu na kutaka kuongoza matendo yetu ili yamhusu Mungu aliye uhai na kutufanya kuishi kutokana na njia yake.

          Katika injili Yesu anasali kwa shukrani akimwita Mungu kama Baba. Katika injili ya Matayo Yesu anazungumza na Mungu kama Baba kuliko injili nyingine. Akitumia neno hili Yesu anaonyesha kwamba alikuwa na uhusiano wa pekee na Mungu. Ilikuwa kama mtoto mdogo na baba yake. Kwa Kibantu na Kiswahili, neno ambalo Yesu alitumia (Abba) linamaanisha “Tata”. Hakuna Myahudi ambaye aliweza kuwa na uhusiano na Mungu kama hivi kwa sababu hao walimheshimu sana kama mwenye nguvu kuliko kitu kingine chochote. Yesu alijiona kitu kimoja na Baba na kwa hivyo alimtegemea yeye katika mambo yote. Uhusiano wa ndani anaoishi na Baba yake sio umefungwa, bali ni mwaliko ili wanadamu wote washiriki. Ndiyo mapenzi ya Baba jambo hili nayo Mwana peke yake anaweza kulisaidia hilo.

            Uwezo wa maskini wa kuyakaribisha yale ambayo yalifunuliwa na njia ya Mungu ya kutenda inayosababisha sifa na shukrani moyoni mwa Yesu. kweli Mungu “anajifunua kwa wafuasi duni, wasiyo na vyeo vya juu wala sifa kubwa katika jamii. Wao walifanana kama watoto wadogo, katika unyofu na moyo ulio tayari kupokea. Hao ndiyo watakaoweza kutii na kuieneza Injili ulimwenguni kote.” Hivyo, katika kazi yake ya kufunua mpango wa Mungu, Yesu aliyapinga matarajio ya wenye elimu na kuyatimiza matumaini ya maskini. Kweli watu wenye hekima na wenye elimu hawakusadiki kwamba Yesu alikuwa Masiya wala kukaribisha ujumbe wake kama ufunuo wa Mungu kwa watu wake. Kwa upande wa wadogo, Yesu ndiye yule ambaye walimtarajia kwa hamu sana. Watu hawa waliweza kukaribisha mafundisho ya Yesu kama yaliyotoka kwa Mungu kwa sababu mafundisho hayo yaliihusu hali yao ya walio heri wa Mungu.  


           Yesu anatualika kuenda kwake ili tuweze kujifunza na kuishi maisha ya upendo, ya unyenyekevu na upole. Yeye mwenyewe anajijulisha kama rejeo la fadhila hizi kwa sababu alipata kuishi fadhila hizi kabisa. Kama ilivyotokea katika hotuba ya milimani, alipopendekeza heri nane, yeye alipendekeza njia yake mwenyewe ya kuishi kwa sababu ndiye yeye Heri wa pekee. Hivyo, ni rahisi kwa wadogo wajitambulishe naye. Maisha yake ni tangazo ya upole na unyenyekevu wa Mungu. Fadhila hizi ni kipimo ili tuweze kuwa kama wadogo na kuwa na moyo kama yeye alivyo navyo. Yeye peke yake anaweza kutupa fadhila hizi. Yeye anajua kuhusu uzito wetu hasa wakati hatuwezi kuchagua ama kuamua kwa uhuru kabisa hali nzuri kwa maisha yetu ama kwa nchi yetu na kupendelea kutumia ukatili badala ya amani. Masharti ya Yesu hayatufanyi kubeba uzito ulio zaidi kuliko nguvu zetu maana yeye mwenyewe anatusaidia kuchukua hayo. Mfano wake utufaye tayari ya kumkabidhi Mungu maisha yetu badala ya kuutegemea uwezo wetu peke yake.   

Fr Ndega
Mapitio ya kiswahili: Christine Githui

EGLI DELUDE LE ASPETTATIVE DEI POTENTI MA SODDISFA LE SPERANZE DEI PICCOLI


Riflessione su Zc 9,9-10; Rom 8, 9.11-13; Mt 11,25-30


      È molto importante riflettere ancora una volta sull’argomento dell’immagine di Dio, perché il nostro atteggiamento, i nostri pensieri e le nostre posizioni di fronte a tutte le cose del mondo dipendono dalla immagine che abbiamo di Dio. Questi testi ci invitano a considerare alcune immagini giuste di Dio, che sono molto importanti nel nostro cammino di fede, vale a dire, Dio Umile, Dio della pace, Dio Emanuele, Dio della vita, Dio che si lascia coinvolgere dalla realtà umana, Dio Padre, Dio Mite e Umile di cuore, Dio dei piccoli, ecc. Siamo invitati a lasciare che Dio sia Dio.

        Anche se il testo della prima lettura è stato scritto dopo la cattività babilonese, il profeta Zaccaria ha proclamato un tempo nuovo che verrà in cui le persone saranno rinnovate per l’esempio di mitezza di Dio. Egli dichiarò che Dio viene, ma allo stesso tempo è già presente tra la gente come il Dio della pace. Le persone che possono riconoscerlo sono coloro che Gesù menzionerà nel Vangelo come “piccoli”. L’esempio della mitezza di Dio contrasta le aspettative di coloro che si sentono potenti e pensano di trovare soluzioni per i conflitti usando la violenza. La buona notizia che dobbiamo annunciare è che Dio veramente si fa presente nel quotidiano delle persone. In base alla seconda lettura, lo Spirito di Dio abita in noi e vuole guidare le nostre azioni perché possano rivelare la presenza del Dio che è vita e ci fa vivere per causa sua.

          Nel Vangelo Gesù ha pregato in ringraziamento a Dio chiamandolo Padre. Gesù parla di Dio come Padre più in Matteo, che negli altri vangeli. Usando questa parola Abba/Padre Gesù dimostra che aveva un rapporto profondo con Dio. È come un bambino con il suo papà. Nessun Ebreo è riuscito ad avere un rapporto con Dio in questo modo, perché lo rispettavano come più potente di qualsiasi altra cosa. Gesù si sente una cosa sola con il padre e così si fidava di lui in tutte le cose. Il rapporto profondo che egli vive con il padre non è chiuso in se stesso, ma è un invito alla partecipazione di tutti. Questa è la volontà del Padre e solamente il Figlio può assicurare questo.

           L’apertura dei piccoli a ciò che è stato rivelato e il modo d’agire di Dio ha motivato la lode e gratitudine nel cuore di Gesù. Veramente Dio “si rivela ai seguaci umili, che non hanno alti titoli e neanche una grande reputazione nella società. Essi sono come bambini, in sincerità di cuore sempre disposti a ricevere. Essi saranno in grado di obbedire e proclamare il Vangelo in tutto il mondo”. Così, nella sua missione di rivelare il piano di Dio, Gesù si è opposto alla prospettiva dei sapienti e dotti e ha compiuto le speranze dei poveri. Davvero coloro che confidavano in se stessi non hanno creduto che Gesù era il Messia, né hanno accolto il suo messaggio come rivelazione di Dio al suo popolo. Dalla parte dei poveri e piccoli, Gesù era colui che loro aspettavano con passione. Queste persone sono state in grado d’accogliere degnamente gli insegnamenti di Gesù come venuti da Dio stesso, perché tali insegnamenti sono infatti relativi alla loro vita, come beati di Dio.

        Gesù ci invita ad andare da lui in modo che possiamo imparare a vivere una vita d’amore, umiltà e mitezza. Egli stesso si presenta come punto di riferimento di queste virtù, perché per primo egli le ha vissute pienamente. Come è successo nel discorso sul monte, quando egli ha proposto le Beatitudini, ha proposto proprio il suo modo di vivere, perché egli è il Beato per eccellenza. Così è facile per i piccoli identificarsi con lui. La sua vita è l’annuncio della mitezza e umiltà di Dio. Queste virtù sono condizioni perché possiamo essere come i “piccoli” ed avere il cuore come il suo. Solamente lui può assicurarci queste virtù. Lui conosce il peso che portiamo, soprattutto quando non riusciamo a decidere liberamente o scegliere la via migliore per la nostra vita. Le condizione di Gesù per una sequela radicale non sono un peso che non possiamo portare, perché egli stesso vuole portarlo con noi. Che la sua mitezza e umiltà di cuore ci motivi ad essere pronti e disponibili a consegnare a Dio la nostra vita piuttosto che affidarci solo alle nostre capacità.

Fr Ndega
Revisione dell'italiano: Giusi 

domingo, 2 de julho de 2017

KUMFUATA KRISTO KWA UPENDO KAMILI NA WA KIPEKEE


Kutafakari kuhusu 2Waf 4,8-11.14-16a; Mt 10: 37-42


       Mungu anampenda binadamu kwa hiari na bure, yaani halazimishwi kupenda wala anamlazimisha binadamu ampende yeye. Lakini anatarajia tu upendo wa binadamu kwake ufuate njia yake ya kumpenda. Nabii Elisha alitumwa kwenye Shunemu kutembelea wanandoa ambao hawakuwa na mtoto. Mwanamke mwenye nyumba alimkaribisha vizuri akimtambua kama mtu mtakatifu wa Mungu. Pamoja na mumewe walimtendea nabii mema kama mshiriki wa familia yao. Kwa sababu ya ukarimu wake, nabii Elisha alimpatia zawadi ya kumzaa mtoto mmoja. Kujitolea kwake mwanamke kwa ajili ya nabii Elisha ni kwa sababu aliweza kutambua katika mtu huyo maonyesho ya upendo wa Mungu mwenyewe aliyepanga kusababisha hali mpya maishani mwake.

        Katika injili Yesu anaomba upendo kamili na wa kipekee kutoka kwa wanafunzi wake, yaani “Ampendaye baba au mama yake kuliko anipendavyo mimi, hanistahili. Ampendaye mwana au binti kuliko mimi, hanistahili. Mtu asiyechukua msalaba wake na kunifuata, hanistahili.” Kama mwendelezo, yeye aliongeza haja ya kuyasalimisha maisha kwa ajili yake. Inamaanisha kwamba kwa Yesu upendo ni kujisalimisha kwa ajili yake. Wazazi na familia nzima ni zawadi ya Mungu, lakini hawawezi kuchukua nafasi ya Mungu katika maisha ya wanafunzi. Hakuna upinzani kati ya upendo kwa Mungu na kwa wazazi, lakini ni tofauti na tena Yesu anaomba kwamba upendo kwa ajili yake uwe kipaumbele kwa sababu ndio upendo huu unaozaa upendo kwa ajili ya wazazi na ya wengine. 

        Kabla ya andiko hili, Yesu alikwisha sema kwamba hakuja kuleta amani bali kuleta upanga unaowaimarisha watu kuchukua uamuzi katika familia na kumhusu Mungu. Upendo ambao Yesu anaomba kutoka wanafunzi wake unatukumbusha mazungumzo ambayo Yeye alimwuliza Petro kwa mara tatu kuhusu upendo wake, yaani “Simoni, mwana wa Yohane! Je, wanipenda mimi kuliko hawa?” Naye akajibu, “Bwana, wewe wajua yote; wewe wajua kwamba mimi nakupenda.” Ingawa Yesu anajua udhaifu wa wanafunzi wake, anaomba upendo “mara tatu”, yaani “kamili”, maana yeye mwenyewe anawawezesha wanafunzi kupenda hivyo. Yeye anajitambulisha na wanafunzi wake na kwa hivyo anawaalika kuchukua ahadi ya kumpenda hadi mwisho kama yeye alivyo.

        Maneno yake yalikuwa nafasi ya kutafakari kwa kweli maana ya safari yao. Yesu ni wazi sana akiwajulisha masharti ili wawe wanafunzi wa kweli. Hivyo, alizuia kwamba wamfuate kwa njia yoyote. Ikiwa wanataka kupata mafanikio katika safari yao wanapaswa kuchukua matokeo ya uamuzi huu. Hapo tuko na jambo la msalaba ambao ni ishara ya upendo wa Yesu mpaka upeo na tabia ya wanafunzi ambao wanajitambulisha na mwalimu wao. Pendekezo la Yesu linajumuisha kujinyima, kwa sababu yeyote anayekutana na Yesu kwa kweli amekwisha pata hazina ya kweli kwa maisha yake naye hawezi kubaki alivyo, yaani mambo mengine hayana maana tena. Kwa maneno mengine, Yesu anataka kuwa kipaumbele maishani mwa wanaoamua kumfuata. Hakuna jambo lingine ambalo liweze kuitoa maana ya kweli kwa maisha yao ila Yesu mwenyewe.


        Kama wanafunzi wapya wa Yesu sisi tunaalikwa kumtegemea Mungu katika mambo yote na kumpenda juu ya yote kama Yesu alivyo. Yeye anatukabidhi ufalme wake na kutujulisha njia ya msalaba ili tuweze kufanya mapenzi ya Baba yake. Kupitia njia hii, tunatambua kwamba Kumfuata Yesu hakuuleti upendeleo au hadhi, bali nafasi ya kujisalimisha kwa upendo kwa ajili ya ufalme wa Mungu. Basi, yeyote ambaye anataka kuishi shwari na bila ahadi hawezi kumfuata Yesu. Tena yeyote ambaye anatamani kumfuata Kristo bila msalaba hatamfuata Yeye kwa kweli kamwe. Kuchukua msalaba ni ishara ya utayari wetu wa kuyakaribisha mapenzi ya Mungu kwa maisha yetu. Kwa kufikia lengo hili tunapaswa kujikana ili Mungu aweze kujifunua kwa nguvu yote ya upendo wake. Kuacha mahali muhimu ama nafasi ya kuwa rejeo ni njia kamili ili tuweze kuwapa wengine nafasi zaidi. Kwa maneno mengine, tunapaswa kuwafikiria wengine kuwa wa muhimu kuliko sisi wenyewe. Tukifanya hivyo hakika tunaweza kumfuata Yesu kwa upendo kamili na wa kipekee.

Fr Ndega
Mapitio ya kiswahili: Christine Githui

SEGUIRE GESÙ CON UN AMORE TOTALE ED ESCLUSIVO


Riflessione su 2Re 4,8-11.14-16a; Mt 10, 37-42


           Dio ama l’essere umano in modo libero e gratuito, cioè non c’è nulla che lo obblighi a farlo ma allo stesso tempo non esige di essere amato dall’essere umano. Tuttavia aspetta solo che l’amore dell’essere umano segua la via che egli stesso ha percorso nel suo modo d’amare. Il profeta Eliseo è stato inviato a Sunem per visitare una coppia che non aveva figli. La donna lo ha accolto riconoscendolo come un uomo di Dio. Con il marito ha preparato una buona sistemazione per il profeta nella loro casa trattandolo come un membro della loro famiglia. A motivo della generosità di questa donna, il profeta Eliseo la ricompensa con il dono di potere generare un figlio. Lei si è presa cura del profeta Eliseo perché è stata in grado di riconoscere in quest’uomo espressione dell’amore di Dio, che ha pianificato di portare una nuova realtà alla sua vita.

          Nel Vangelo Gesù chiede un amore totale ed esclusivo dai suoi discepoli, vale a dire “Chi ama il padre o la madre più di me non è degno di me; chi ama il figlio o la figlia più di me non è degno di me; chi non prende la sua croce e non mi segue, non è degno di me”. In seguito ha parlato sulla necessità di donare la vita per causa sua. Per Gesù l’amore vuol dire consegna come egli stesso ha fatto. I genitori e tutta la famiglia sono un dono di Dio, ma non possono prendere il posto di Dio nella vita dei discepoli. Non c’è opposizione tra l’amore a Dio e ai genitori ma sono diversi; Gesù chiede che l’amore a Lui/Dio sia priorità perché è questo amore che genera e motiva l’amore ai genitori.

         Nel testo che precede questo brano Gesù ha detto che non è venuto a portare la pace, ma la spada; ha invitato la gente a prendere una decisione portando un modo diverso di vivere il rapporto con Dio e le relazioni nella famiglia. L’amore che Gesù richiede ai suoi ci fa ricordare il dialogo in cui lui ha chiesto a Pietro per tre volte sul suo amore per lui, vale a dire “Simone, figlio di Giona, mi ami più di costoro? “Lui rispose: “Signore, tu sai tutto; Tu sai che ti amo.” Anche se Gesù conosce la debolezza dei suoi discepoli, chiede di amarlo per tre volte, cioè un amore totale, perché egli stesso li rende capaci di amare così. Egli si identifica con i suoi discepoli e proprio per questo li invita a prendere l’impegno di amarlo fino alla fine come egli stesso fa.

          Tramite le parole di Gesù i discepoli hanno avuto la possibilità di riflettere sul vero senso del loro cammino. Gesù è stato molto onesto presentando le condizioni per essere veri discepoli ed evitare una sequela in qualsiasi modo. Per raggiungere un buon risultato nel loro cammino essi devono assumere le conseguenze di questa decisione. Qui si tocca l’argomento della croce come segno dell’amore di Gesù e caratteristica dei discepoli che si identificano con il loro maestro. La proposta di Gesù richiede rinuncia personale, perché chi ha incontrato Gesù ha trovato il vero tesoro della sua vita e non può rimanere come prima; la persona, è chiamata a valutare le altre cose in modo diverso. In altre parole, Gesù vuole essere priorità nella vita di coloro che hanno scelto di seguirlo. Non c'è nulla che possa dare vero senso alla loro vita, se non Gesù stesso.

         Come discepoli nuovi di Gesù, siamo invitati a fidarci di Dio in tutte le cose e ad amarlo soprattutto come Gesù stesso lo fa. Egli ci affidò il suo regno e ci presenta la via della croce in modo che possiamo fare la volontà del Padre suo. In questo modo, ci rendiamo conto che seguire Gesù non porta fama e nemmeno status, ma sacrificio personale e consegna quotidiana per il regno di Dio. Quindi, chi vuole vivere nella tranquillità e senza impegno non può seguire Gesù. E chi vuole seguire Cristo senza croce non lo seguirà mai. Prendere la croce è un segno della nostra disponibilità ad accogliere la volontà di Dio per la nostra vita. Per raggiungere questo obiettivo, dobbiamo lasciare che Dio possa rivelarsi con tutta la potenza del suo amore. Lasciare un posto importante o una opportunità di essere punto di riferimento è una via giusta perché possiamo dare agli altri più opportunità. In altre parole, dobbiamo considerare gli altri più importante di noi e servili con generosità. In questo modo sicuramente possiamo seguire Cristo con un amore totale ed esclusivo.

Fr Ndega
Revisione dell'italiano: Giusi