sábado, 17 de novembro de 2018

KUNA TUMAINI KWA WAKATI UJAO WETU



Kutafakari kuhusu Dan 12: 1-3; Waeb 10: 11-14; Mk 13: 24-32


Tuanze tafakari hii tukijiuliza swali moja: “Je, Wakristo wanapaswa kuwa na tabia gani wakati wa mazingira magumu na mbele ya kosa la uhakika lililo tabia ya wakati huu? Sisi tu watu wa tumaini kwa sababu maisha ya mtu anayemfuata Yesu yamejaa maana. Basi, ujumbe wa liturgia hii ni msukumo kwetu tulioalikwa kutoa maana za tumaini letu kupitia imani yetu katika Kristo. Uhakika wa ukaribu wake ndio nguvu yetu. Tukikumbuka kwamba leo ndiyo Siku ya Kidunia ya Maskini, tunataka kuwa manabii wa tumaini dhidi ya utabiri wa kukata tamaa ambao unatuzuia kupanga wakati mwema kwa maskini wa jamii yetu. Jambo hili lina uhusiano gani nasi? Baba Mtakatifu Francisco anatuambia kwamba: “Manabii wako upande wa maskini kwa sababu wanajua ndipo katika upande huu kwamba Mungu ako”.  
   
Somo la kwanza linalotokana na kitabu cha nabii Danieli ni ufunuo kuhusu hukumu na ufufuko. Hilo ndilo mojawapo kati ya maandiko ya Agano la Kale yanayoongelea imani katika ufufuko (angalia pia 2 Mac 7, 9). Watu wa Israeli walitumwa na Wagiriki na kuteseka sana. Wengi miongoni mwao waliacha kumwamini Mungu, lakini wengine ambao waliendelea kumwamini walihitaji ujumbe wa tumaini na kutia moyo ili kuendelea safari yao kwa uvumilivu. Mungu ndipo daima kati ya watu wake na kuwasaidia mbele ya mazingira magumu ambayo wanakabiliana. Tendo lake kupitia malaika yake linahakikishia ukombozi na tena uzima kwa wale ambao walikufa kwa sababu ya kumwamini Bwana na kutenda mema hadi upeo.

Kulingana na somo la pili toleo la Kristo lilishinda dhabihu zote za makuhani wa Agano la Kale. Dhabihu zao zilitendeka mara nyingi wala hazikuwa na nguvu ya kuondoa dhambi za watu, yaani zilikosa ufanisi. Kwa upande wa Kristo, hali ni tofauti. Toleo lake lilitendeka mara moja tu nayo ilitosha kwa kuwatakasa watu wengi katika nyakati zote kwa sababu alijitolea mwenyewe. Katika kila misa takatifu tunasherehekea fumbo la toleo hii. Ndiye Kristo mwenyewe ambaye anatuhusisha katika mwendo huu kwa ajili ya wokovu wetu na wa wengine.

       Mwanzoni mwa sura ya kumi na tatu ya injili hii ya Marko Yesu aliongea kuhusu uharibifu wa Yerusalemu. Ufunuo huu uliwaimarisha baadhi ya wanafunzi wake wamwulize kuhusu ishara gani na siku gani na saa gani ya uharibifu huu. Kisha, Yesu alitumia nafasi hii ili kuongelea mambo mengi yatakayotokea na haja ya ushuhuda ili kukutana naye tena na kushiriki katika furaha yake. Aliporudi tena atawakusanya wateule wake kutoka dunia nzima. Alitabiri kwamba “nguvu za mbingu zitatikiswa” akimaanisha kwamba miungu ya uongo, yaani jua, mwezi, itapoteza mwanga wao. Hata wale waliojiona watu wa kimungu (nyota za angani) ambao wanawatesesha watu wa mataifa hasa walio maskini, hao (miungo ya uongo) wataanguka na mtazamo wa wote utamwelekezea Mwana wa Mtu akija amejaa nguvu na utukufu kama mshindi. Hakuna mtu anayejua wakati kamili ambao mambo yote yatatokea ila Baba peke yake. Kwa hivyo ni lazima kumwamini yeye.

         Ingawa uharibifu wa mji wa Yerusalemu ulitokea katika mwaka wa 70 B.K., nia ya Yesu haikuwa kuwajulisha kuhusu tukio hili, bali kuhusu matokeo ya tukio hili maishani mwa wafuasi wake. Ni lazima kutafakari injili hii kulingana na mazingira ambayo jumuiya ya Marko ilikuwa inaishi, yaani wanafunzi wa Yesu waliishi kipindi cha machafuko na kujaribiwa kukata tamaa kuhusu utambulisho wao wa wafuasi kwa maana ya majaribio na mateso mengi. Hao walijiuliza: “hayo yatokeayo yamaanisha nini?”. Mbele ya hali hii mwinjilisti aliwakumbusha mafundisho ya Yesu yasemayo kwamba baada ya mambo yote wanafunzi watakuwa washindi kama mwalimu kwa sababu ya uvumilivu wao mpaka upeo. Bwana wa Mtu ndiye msingi na lengo la historia. Kwa hivyo historia haiendi kwa mwisho bali kwa lengo kamili: Yesu Kristo mwenyewe.

        Andiko hili linatuambia kwamba Kristo ni mshindi na atafanya kuwa washindi wale ambao wanamfuata. Ujio wake mara ya pili utaanzisha historia mpya na ubinadamu mpya. Yeye anataka kushiriki na wanafunzi wote watakaobaki wamesimama kupitia imani na ushuhuda kwa uaminifu. Maneno yake yatuambia kuwa mazingira magumu ni sehemu ya safari ya wale ambao wanamfuata katika nyakati zote, lakini tena yatuhakikishia kwamba ikiwa tunabaki tumesimama kwa uvumilivu mpaka upeo tutaokolewa. Kuhusu wakati huu, hakuna mtu anayejua. Hii ni sehemu ya mpango wa hekima na wema wa Baba. Kwa hivyo ni lazima kumwamini yeye ambaye anaiongoza historia ya kibinadamu kwa lengo kamili. Tuko mikononi mwake; kwa hivyo tuko katika mikono mizuri”. Ujumbe huu unatoa tumaini kwa maisha yetu. Sisi tulioalikwa kuendelea utume wa Mwana wake Yesu, tunapaswa kuwa macho kwa ishara za uwepo wake ambazo zimetokea kati yetu. Ili hali mpya ikatokee maishani mwetu, miungu mingi ya uongo yapaswa kuanguka na kupoteza thamani yao. Kwa maneno mengine, tunapaswa kuacha picha za uongo za Mungu, mawazo na tabia ambayo inayapinga mafundisho ya injili. Tuishi wito wetu kwa shauku na furaha kwa sababu kuna tumaini kwa wakati ujao wetu.

Fr Ndega

HA UNA SPERANZA PER IL NOSTRO FUTURO



Riflessione a partire Dan 12, 1-3; Eb 10, 11-14; Mc 13, 24-32


        All’inizio di questa riflessione vogliamo porci una domanda: “Come devono comportarsi i cristiani nei momenti difficili e davanti alle incertezze di questo nostro tempo? Siamo un popolo di speranza, perché la vita di chi segue Gesù Cristo è piena di senso. Il messaggio di questa liturgia è un buon motivo perché possiamo vivere la nostra vocazione con gioia, dando ragione della nostra speranza tramite la fede in Cristo. La certezza della sua vicinanza è la nostra forza. Ricordando la Giornata Mondiale per i Poveri, cerchiamo di essere profeti di speranza contro le profezie di sventura che non permettono di pensare una migliore situazione per i più poveri dalla nostra società. Cosa ha a che fare questo con noi? Ci dice papa Francesco, “I profeti sono dalla parte dei poveri perché sanno che è da questa parte che Dio sta”.  

      Il brano del profeta Daniele ci parla di giudizio e risurrezione. Questo è uno dei testi dell’Antico Testamento che parlano di fede nella Resurrezione (vedi anche 2 Mac 7, 9). Questa profezia è sorta in un periodo in cui il popolo di Israele era sotto il dominio greco e soffriva molto. Molti di loro avevano smesso di credere nel Dio dei padri e coloro che cercavano di mantenere la fede avevano bisogno di un messaggio di speranza per continuare il loro cammino. Dio è sempre presente in mezzo al suo popolo, lo motiva quando deve affrontare delle situazioni difficili ed è pronto a ricompensare con vita piena coloro che perseverano fino in fondo nella causa della sua giustizia.

       La lettera agli Ebrei sottolinea che il sacrificio di Cristo ha superato tutti i sacrifici che i sacerdoti compivano nell’Antico Testamento. I sacrifici che offrivano non avevano la forza per rimuovere i peccati della gente, cioè erano inefficaci. Riguardo Cristo, Egli ha offerto se stesso una volta per tutte e proprio per questo la sua offerta è stata in grado di purificare tutti dai loro peccati e fare sorgere una umanità nuova. In ogni messa celebriamo il mistero di questo unico sacrificio rinnovando la nostra adesione alla vita che esso offre, per la nostra salvezza e per tutti.  

       All’inizio del capitolo tredicesimo del vangelo di Marco Gesù annuncia la distruzione di Gerusalemme. Questa rivelazione ha motivato alcuni dei suoi discepoli a chiedere riguardo i segni, il giorno e l’ora di questo drammatico avvenimento. Gesù ha usato questa opportunità per rivelare loro altre cose che devono accadere riguardo la storia e la missione della comunità da lui fondata. Lui deve tornare una seconda volta per portare la creazione alla pienezza radunando tutti i popoli intorno a sé. Così “si compie il disegno del Padre: fare di Cristo il cuore del mondo”.

        Davanti alla manifestazione gloriosa del Cristo risorto, Figlio dell’uomo, “i poteri dei cieli saranno sconvolti”, cioè, il sole, la luna, riconosciuti come dei dalle culture antiche, perderanno i loro splendore. I potenti di questo mondo che attribuiscono a sé onori divini (per questo “stelle del cielo”) assoggettando i popoli e che con i loro sistemi condannano i poveri alla marginalità, anche loro cadranno. Lo sguardo di tutti si volgerà al Figlio dell’uomo vincitore, centro e giudice della storia. Egli porta con sé la nascita di una nuova umanità e quindi l’inizio di una nuova storia. Riguardo il giorno e l’ora di tutto questo capovolgimento, nessuno lo sa; soltanto il Padre.

     Anche se la distruzione della città di Gerusalemme è avvenuta nell’anno 70 D.C., l’intenzione di Gesù non era dare informazioni su questo evento ma sulle conseguenze di esso e di altri, per la vita dei suoi seguaci. Dobbiamo considerare che quando Marco ha scritto il suo vangelo, la comunità cristiana viveva un periodo di crisi a motivo delle ininterrotte persecuzioni, che causavano la morte di alcuni di suoi membri (i martiri) e che portavano altri a rinunciare alla loro identità di seguaci di Gesù. Davvero sembrava la fine del mondo. Coloro che perseveravano si domandavano: “Cosa vuol dire tutto questo?”. Il ricordo degli insegnamenti di Gesù è stato fondamentale per una ripresa di quello che dava vero senso alla loro vita, consapevoli che se Gesù è il punto di riferimento di tutto, allora, la vita e la storia non camminano per una fine ma per un vero fine: Gesù stesso.

      Gesù è vincitore del peccato e della morte e farà vincitori tutti coloro che lo seguono. Alla sua venuta alla fine dei tempi (adempimento dei tempi) vuol trovarci “pazienti e vigilanti”, fedeli ai suoi insegnamenti per condividere con lui la sua stessa gioia. La sua Parola ci dice che le prove e difficoltà accompagnano la nostra condizione di cristiani, però ci assicura anche che “è per la nostra perseveranza che saremo salvi”. Questo è un messaggio che ci riempie di speranza. Siccome non sempre riusciamo a capire gli avvenimenti attorno a noi, dobbiamo avere fiducia nel Padre, consapevoli che “siamo nelle sue mani e, quindi, in buone mani. Nulla sfugge dal suo sguardo. Tutto guidato da un piano suo di saggezza e bontà” (S. G. Calabria). Quindi, dalla nostra parte, fiducia in colui che sta conducendo la storia. Siamo stati invitati a continuare la missione di suo Figlio Gesù e dobbiamo essere attenti ai segni della sua presenza accanto a noi. Perché lui sia davvero Sovrano nella nostra vita, molte falsi idoli devono perdere il loro splendore, ad esempio, i falsi valori e le false immagini di Dio che coltiviamo, la mentalità e i comportamenti contrari agli insegnamenti del Vangelo, ecc. Basta ipocrisia! Basta mediocrità! Hai una speranza per il tuo futuro! Vivi questo, proclama questo! Viviamo con gioia ed entusiasmo la nostra vocazione e tutto sarà bello per noi e per gli altri!

Fr Ndega
Revisione dell'italiano: Giusi

sábado, 10 de novembro de 2018

IL GESTO GRANDIOSO NON PUÒ CHE SCATURIRE DA UN CUORE GENEROSO



Riflessione su 1 Re 17,10-16; Eb 9, 24-28; Mc 12, 38-44


      Dio non si lascia vincere in generosità. Chi è generoso verso di Lui riceverà in sovrappiù. Questo è ciò che la figura delle due vedove della liturgia di oggi ci insegnano. Nel primo brano, Elia è inviato a una vedova a Sarepta. Questo incontro cambia completamente la prospettiva di vita di quella donna e di suo figlio i quali vivono una situazione drammatica, vale a dire: “mangeremo e dopo moriremo”. La risposta generosa alla richiesta del profeta esprime un atteggiamento di abbandono fiducioso all’azione provvidente di Dio per cui nulla risulta impossibile. È a questo atteggiamento che siamo chiamati perché l’azione della grazia di Dio sia efficace nella nostra vita.

Il brano della Lettera agli Ebrei sottolinea che Cristo ha annullato il peccato mediante la consegna totale di sé sulla croce. Questo è il mistero che ci ha salvato e che riviviamo in ogni Eucaristia che celebriamo. Tramite esso pregustiamo la generosità abbondante di Dio che tanto ci ha amato da dare suo Figlio per la nostra salvezza. Quindi, non è solo la memoria di un avvenimento storico ma l’opportunità di partecipazione alla vita stessa di Cristo, che ci motiva a portare avanti la sua opera tramite la donazione della nostra vita come lui stesso ha fatto.

         Nella prima parte del Vangelo Gesù richiama l’attenzione dei suoi discepoli riguardo gli atteggiamenti degli scribi come un comportamento da evitare nella sua sequela. Loro gradiscono innalzarsi ed essere lodati dalla gente. Pregano per molto tempo ma senza la giusta intenzione. Si sentono superiori agli altri e sfruttano le vedove. Davanti a questo Gesù manifesta preoccupazione perché questo modo di vivere fa opposizione a quello che lui propone ai suoi discepoli.

     La gente capisce che c’è una grande differenza e soprattutto discordanza tra gli insegnamenti di Gesù e quelli degli scribi. Gesù insegna alla gente con l’autorità ricevuta dal Padre. Riguardo l’autorità degli scribi, è stata una convenzione post esilio babilonese in quanto dopo che gli israeliti sono tornati da questa esperienza, gli scribi assunsero un compito molto importante nella gestione della vita sociale e religiosa. “Durante l’esilio sono stati loro a scrivere i primi cinque libri della bibbia, la Torà. Soltanto loro erano in grado di giudicare e dare delle sentenze secondo la Legge” (cf F. Armellini). Loro esortano la gente ad essere fedeli all’Alleanza e a custodire la Legge come fondamento della loro vita. Ma anche se insegnavano alla gente a vivere la Legge il loro modo di vivere era lontano dal loro insegnamento.

         Siamo tutti d’accordo che l’abuso di autorità, la vanagloria e l’ipocrisia sono tentazioni costanti nella vita di chi ha la responsabilità di guidare le persone nelle nostre comunità cristiane e anche nella società. Però non soltanto loro sono colpiti da questi mali. Sono vizi che accompagnano la nostra debole condizione umana di cui nessuno è esente. Abbiamo molte volte la tentazione di fare le cose per essere apprezzati, di sfruttare gli altri sentendoci superiori a loro, volendo essere serviti piuttosto che servire. Per combattere questa tendenza, dobbiamo sempre fissare lo sguardo su Gesù che aveva una logica diversa e una via infallibile per superare tutte le tentazione, vale a dire la logica e la via dell’amore senza riserve. E’ solo per questa via che possiamo piacere a Dio.

       È questa la via che ha scelto la vedova di cui parla la seconda parte del Vangelo. “Lei non conosceva Gesù, non era battezzata” ma ha manifestato il modo giusto di essere discepoli di Gesù. E’ andata al tempio per fare un’offerta. Giusto in quel momento Gesù era seduto vicino al tesoro del tempio insieme ai suoi discepoli. Mentre la gente metteva i soldi nel tesoro richiamando l’attenzione di tutti per la quantità, è arrivata questa madre vedova che ha messo soltanto due monete. Questo gesto semplice e quasi nascosto, pieno di generosità, ha richiamato l’attenzione di Gesù che subito lo presenta ai suoi discepoli come modello da seguire.

         Gesù è in grado di vedere quello che gli altri non vedono perché è attento ai dettagli, a ciò che è nascosto, vale a dire: “l’essere umano guarda l’apparenza ma Dio guarda il cuore”. Quindi, guardando il suo cuore, Gesù conclude che nella sua offerta, la vedova ha gettato tutto quello che aveva per vivere, cioè, ha messo la sua vita in gioco, ha donato tutta se stessa. Questa è l’offerta che piace a Dio. Lui non gradisce la quantità di cose che qualcuno è in grado di offrire o di fare nel suo nome ma la generosità del cuore. Troviamo il vero senso della vita quando siamo in grado di imitare Dio che nella sua generosità, non ci offre qualcosa, ma se stesso.

      Il valore della nostra offerta è misurato secondo la generosità del nostro cuore. La grandezza del cuore di una persona non è misurata dalla grandiosità del regalo che offre ma dalla bellezza del suo gesto. Infatti, sono i piccoli gesti che fanno la differenza. Il grande bene che possiamo fare agli altri è essere per loro quello che siamo chiamati ad essere. Dove non c’è questo c’è l’ipocrisia che ci impedisce di coltivare rapporti veri con gli altri. Combattiamo questo cattivo atteggiamento imparando dalle persone umili che attorno a noi costruiscono fraternità e sono espressione della bontà e generosità di Dio.

Fr Ndega
Revisione dell'italiano: Giusi

ISHARA KUU INATOKANA NA MOYO WA UKARIMU



Kutafakari kutoka 1 Waf 17, 10-16; Waeb 9, 24-28; Mk 12: 38-44


       Mungu hawezi kushindwa katika ukarimu. Yeyote anayetenda kwa ukarimu atapokea ukarimu mwingi zaidi kutoka kwake. Hilo ndilo ambalo wajane wa Liturjia ya leo wanatufundisha. Katika andiko la kwanza, Eliya alitumwa kwa mjane katika Sarepta. Kukutana na mtu huyo wa Mungu matarajio ya maisha ya mama mjane na mtoto wake yalibadilisha kabisa. Hao walikuwa wanaishi mazingira magumu sana, yaani: “tuweze kula na kufa”. Jibu lake la ukarimu kwa ombi la nabii linaonyesha tabia ya kuamini katika riziki ya Mungu ambaye hakuna kisichowezekana. Mwishoni muujiza ulitokea kwa njia ya ajabu. Sisi twalikwa kuwa na tabia hii ili tendo la neema ya Mungu maishani mwetu liwe ufanisi.

     Kifungu cha waraka wa Waebrania kinaongea kwamba Kristo alikatisha dhambi zake kwa kujisalimisha mwenyewe msalabani. Hili ndilo fumbo ambalo ametuokoa nasi tunaguswa kwa njia mpya daima katika kila Ekaristi ambayo tunasherehekea. Hili silo tukio la kihistoria tu bali nafasi ya kushiriki katika maisha ya Kristo mwenyewe ambayo inatuimarisha kuendelea kazi yake kwa kuyatoa maisha yetu kama yeye alivyo.

     Sehemu ya kwanza ya Injili inajulisha upinzani wa Yesu dhidi ya njia ya waalimu wa sheria ya kuishi. Hao wanapenda sana kujiinua na kupendezwa. Wanasali kwa muda mrefu lakini bila kusudi kamili. Wanajihisi bora kuliko wengine na kudhulumu wajane. Yesu ana wasiwasi kuhusu njia hii ya unafiki kwa sababu inalipinga pendekezo lake kwa wanafunzi wake.

      Watu walijua kwamba kuna tofauti hasa mfarakano kati ya mafundisho ya Yesu na ya waalimu wa sheria. Yesu aliwafundisha watu kwa mamlaka aliyopokea kutoka kwa Baba. Kuhusu mamlaka ya walimu wa sheria, yakosa ukweli. Baada ya uhuru kutoka utumwani Babeli walimu walikuwa viongozi muhimu kwa ajili ya Wayahudi kwa sababu waliandika Vitabu Vitano via mwanzo wa biblia vinavyojulikana kama Vitabu vya Musa, yaani Toraa na hao peke yao waliweza kuhukumu na kujulisha sentensi kulingana na sheria. Hao waliwasisitiza Wayahudi kuzingatia agano kwa kuzishika sheria za Mungu kama msingi wa taifa lao jipya. Lakini ingawa waliwafundisha watu waishi sheria, tabia yao ilikuwa mbali sana na mafundisho yao.

     Utumiaji mbaya wa mamlaka ni majaribu daima katika maisha ya walio na jukumu la kuwaongoza watu katika jumuiya zetu za Kikristu na pia katika jamii. Lakini sio hao tu ambao wanaguswa na majaribu haya. Hata sisi pia tuko na mwelekeo huu. Majaribu ya kawaida ni yaani kujiona bora kuliko wengine, kutaka kutumikiwa badala ya kutumikia, kuwanyonya wengine na kadhalika. Yeyote ambaye anataka kuwaongoza wengine anapaswa kuiga mfano wa Yesu aliyekuwa na mawazo tofauti na kujua njia kamili ya kushinda majaribio yote. Hatuwezi kumpendeza Mungu wala kuwa wenye furaha ikiwa hatuishi majukumu yetu kama utumishi.  

     Lakini katika sehemu ya pili ya injili hii tuko na njia kamili ya kuwa mwanafunzi wa Yesu, yaani mfano wa mama mmoja mjane maskini aliyeenda hekaluni kutoa sadaka yake. Yesu alikuwa ameketi karibu na sanduku la hazina pamoja na wanafunzi wake. Alitazama jinsi watu walivyoweka pesa sandukuni. Yeye aliweza kuona moyo na kusudi kwa kila mmoja alipotoa sadaka. Alipotazama mjane akiweka fedha sandukuni yeye alitambua kwamba mama huyo alitoa zaidi kuliko wengine kwa sababu sadaka zao zilikuwa ziada ya matajiri bila kusudi kamili kwa moyo. Sadaka ya mjane ilimpendeza Mungu kwa sababu alitoa kila alicho nacho cha kuishi, yaani alitoa maisha yake kama zawadi, kama sadaka. 

     Mama mjane maskini hakumjua Yesu, lakini alimpendeza kwa sababu alitenda kulingana na pendekezo la binadamu mpya.  Mtu anakuta maana ya kweli ya maisha wakati anapoweza kutenda kama Mungu katika ukarimu wake, yaani zaidi kuliko kutoa kitu, mtu anaweza kujitoa mwenyewe kama sadaka yote kwa kuonyesha kwamba maisha yake ya kila siku yanamtegemea Mungu. Tuko na tabia ambayo inadhihirisha ukuu wa moyo wa mtu fulani.

    Tunaalikwa kwa macho kwa ishara halisi ndogo zinazotoka kwa watu unyenyekevu tunaowakutana kwa kawaida na kujifunza kutoka kwao tabia kamili mbele ya Mungu. Yeye hupendezwa sio na wingi wa vitu ambavyo tunatoa bali na ukarimu wa moyo wetu. Thamani ya sadaka yetu hupimwa kulingana na ukarimu wetu. Ukuu wa mtu hautokana na kipimo cha zawadi ambayo anatoa bali na uzuri wa ishara yake na upendo wake. Kweli, ndizo ishara ndogo zinazofanya tofauti. Msaada mkubwa ambao ninaweza kumpa wengine ndimi ninayealikwa nilivyo. Zaidi ya hilo ndio unafiki ambao unanizuia kuwa na uhusiano mwema na wengine. Tunaweza kushinda hali mbaya hii kwa msaada wa watu wanyenyekevu ambao wanajenga undugu kandokando yetu na kuwa maonyesho ya ukarimu wa Mungu.

Fr Nega

sexta-feira, 2 de novembro de 2018

MPENDENI MUNGU NA JIRANI KAMA NILIVYOWAPENDA NINYI


Kutafakari kutoka Kum 6:2-6; Waeb 7:23-28; Marko 12,28-34


      Kulingana na Maandiko Matakatifu Mungu ana uhusiano maalum na Watu wa Israeli. Alianzisha agano na watu hawa, akiwapa baadhi ya mwongozo ili watembee salama na kuwa maisha mengi. Katika mazingira haya tunaweza kukiri kuzaliwa kwa Amri kumi. Kuishi Amri kulikuwa muhimu kwa Waisraeli ambao wanafikiria Neno la Mungu kuwa ni Sheria na Sheria kuwa ni Neno la Mungu. Wanaposema kwamba “Sheria ya Bwana ni kamili, faraja ya roho”, wanaongea kuhusu Neno la Mungu. Kuna uhusiano wa ndani kati ya Sheria na Neno, kwa sababu Amri za Sheria zinaonyesha utunzaji wa upendo wa Mungu ambaye anapoongea anaongoza njia kamili ya ukombozi na uzima. Kutii kwa Amri ni chanzo cha baraka maana huongoza kwa uzima, wakati kutotii kwa Amri kunaongoza kwa mauti.

      Basi, chanzo cha Amri ndio upendo wa Mungu. Yeye ni upendo na kupenda kwa hiari. Anafikia wote kwa uhusiano huu. Yeye anatarajia tuweze kumpenda pia kwa sababu aliweka moyoni mwa kila mtu uwezo huu tangu mwanzo mwa uumbaji. Upendo ni sheria yake ya kipekee. Sheria hii hailazimishi bali ndiyo zawadi na kuonyesha njia ya uhuru wa kweli. Hii ndiyo maana ya hotuba ya Musa kwa Watu wa Israeli katika somo la kwanza. Kupitia Musa, Mungu anaongea na Watu kutoka moyo kwa moyo, sababu Mungu anataka kuandika sheria yake mioyoni mwa wote. Yeyote anaishi sheria ya Mungu kwa kweli ikiwa anaweza kupenda. Kumpenda Mungu kunamaanisha kuishi kulingana na mapenzi yake. Katika somo la pili Kristo ni kuhani mkubwa kuliko makuhani wa Agano la Kale kwa maana alijitoa nafsi yake kwa upendo kwa ajili ya wenye dhambi wote, akitufundisha njia halisi ya kumpenda Mungu kwa kweli.

     Kando ya sheria kuu Wayahudi waliweka sheria nyingi ambazo polepole zilibadilisha makini kutoka muhimu sana. Jibu la Yesu ni kugundua tena jambo hili yaani, “Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa akili zako zote, na kwa nguvu zako zote... Mpende jirani yako kama nafsi yako”. Kumpenda Mungu ni kwanza wa Amri zote, lakini Yesu aliiunganisha na upendo kwa jirani, akionyesha kwamba haiwezekani kumpenda Mungu kwa kweli bila kumpenda jirani. Kutokana na Amri ya kumpenda Mungu inaububujika upendo kwa jirani kama matokeo. Chanzo ni Mungu daima, kwa sababu alitupenda kwanza na kwa hiari. Ndio kutokana na njia ya Mungu ya kutupenda kwamba tunapaswa kuwapenda wengine. Hii ni changamoto kwa tamaduni yote hasa mahali ambapo uaminifu kwa familia na desturi kwa kawaida umekuwa kama amri ya kwanza.


     Hivyo, baadaye Yesu alitaka kufanya rahisi zaidi akijionyesha kama mfano. Kwa hivyo alibadilisha Amri mbili hizi ziwe moja peke yake, yaani tupendane kama yeye alivyotupenda. Kama Mungu alivyotupenda katika Kristo tunaalikwa kupendana kutoka kwa Kristo. Mtu ambaye anapenda kulingana na njia hii alifahamu umuhimu wa sheria naye sio mbali na Ufalme wa Mungu. Kwa kweli, mtu ambaye anamfuata Yesu hafuati sheria au mafundisho bali anamfuata Mtu aliyetupenda mpaka upeo. Tunajua kwamba katika jamii kuna sheria nyingi. Watu wenye hekima na upevu wanatii sheria lakini hawakuwa watumwa kwa sababu wanafahamu kwamba muhimu siyo sheria yenyewe bali ndiyo roho inayosukuma sheria na tabia mtu anayochukua mbele ya sheria. Lengo la sheria yote ni kuwafanya watu waishi vizuri, yaani kwa maelewano. Sheria inakuwa bila maana ikiwa lengo lake ni kuonea ama kusaidia marupurupu kwa baadhi ya watu kwa kubagua wengine. Hali hii ni pendekezo sio kwa jamii tu, bali pia kwa Kanisa, kwa jumuiya na kwa familia zetu. Changamoto kwetu leo ni kuweka juhudi ili sheria yote iwe chombo cha ndugu kama maonyesho ya upendo kwa Mungu na kwa jirani.    

Fr Ndega

AMATE DIO E AMATE IL PROSSIMO COME IO HO AMATO VOI



Riflessione a partire di Dt 6:2-6; Eb 7:23-28; Mc 12,28-34


       La Scrittura, particolarmente nell’Antico Testamento parla di un rapporto speciale tra Dio e il popolo di Israele. Egli ha stabilito un patto con gli israeliti, indicando loro le vie giuste per camminare alla sua presenza e avere una vita lunga sulla terra. È in questo contesto che nascono i Dieci comandamenti. Vivere i comandamenti è esperienza centrale nella vita di questo popolo per cui la Parola di Dio è la Legge e la Legge è Parola di Dio. Quando dicono che “la legge del Signore è perfetta, conforto per l’anima”, parlano della Parola di Dio. C'è quindi un legame stretto tra la Legge e la Parola, perché i comandamenti della Legge indicano la cura affettuosa di Dio che quando parla indica la via giusta per la giustizia e la liberazione. L’obbedienza ai comandamenti è la fonte di ogni benedizione che porta alla vita, mentre la disobbedienza ad essi porta alla morte.  

    Pertanto, la sorgente dei comandamenti è l’amore di Dio. Egli è amore e ama gratuitamente facendosi vicino a tutti. Aspetta che siamo in grado di amarlo, perché ha messo questa capacità nel cuore di ogni persona fin dall'inizio della creazione. La sua legge è l’amore. Questa legge non costringe, ma è un dono che porta alla vera libertà. Questo è il senso del discorso di Mosè al popolo d’Israele nella prima lettura. Attraverso Mosè, Dio parla al popolo da cuore a cuore, perché la sua intenzione è fissare la sua Legge nel cuore di tutti. Vive veramente la Legge di Dio chi è in grado di amare. Amare Dio vuol dire impostare tutta la vita secondo la sua volontà. La seconda lettura ci parla della superiorità del sacerdozio di Cristo riguardo a quello del Vecchio Testamento. Diversamente da quei sacerdoti, Cristo non ha bisogno di offrire sacrifici per i peccatori; egli ha offerto se stesso per amore e quindi, l’offerta perfetta, assicurando la salvezza per tutti.

       Normalmente gli incontri di Gesù con gli scribi (e anche con i farisei) sono conflittosi ma questa volta questo capo scriba che si avvicina a Gesù sembra amichevole. La prova di questo è che alla fine il dialogo finisce con un scambio di elogi e di apprezzamenti dalle due parti. Lui ha chiesto a Gesù quale sia il primo dei comandamenti di Dio. Gesù non risponde direttamente alla sua domanda ma fa una mirabile sintesi di tutti i comandamenti contenuti nella Torà ebraica, vale a dire: amare Dio e amare il prossimo. Custodire questa realtà nel cuore è più importante che memorizzare tutti i “comandamenti” (erano 613), che loro hanno messo attorno a quello che è stato ispirato da Dio, deviando l’attenzione da ciò che è veramente essenziale da custodire.   

     Secondo il primo comandamento, non si ama Dio in qualsiasi modo ma con tutte le potenze della vita, vale a dire: con cuore, anima, intelligenza e forza. E non sarà ancora un vero amore se non si ama anche il prossimo. In altre parole, la corrispondenza all’amore che ci ha amato si dà in due direzione: Dio e il prossimo. Non si può vivere uno senza l’altro. San Giacomo parla duramente su questa realtà: “Chi dice di amare Dio che non vede e non ama il prossimo che vede è un bugiardo”. L’amore verso i fratelli e le sorelle è il vero sacrificio che giunge gradito a Dio. Nella sua risposta Gesù non fa riferimento a un decreto da obbedire ma a un rapporto da coltivare. Dobbiamo riconoscere che non è un compito molto facile da portare avanti. Più noi procediamo nella vita, più sperimentiamo come sia difficile amare veramente Dio e il prossimo.

      Gesù era consapevole di questa difficoltà quando era ancora con i suoi discepoli. Per questo ha offerto se stesso come modello. A partire da lui diventa più facile amare. Allora, non sono più due comandamenti ma quello di Cristo, il comandamento nuovo, che è il centro e la sintesi del Vangelo, il programma della nostra vita. La persona che sa mettere l’amore per primo e sopra ogni cosa non è lontano dal Regno perché agisce secondo la volontà divina. “Possiamo imparare ad amare se ci lasciamo amare da Dio, poiché non si può amare se non essendo amati, e non c’è nient’altro che Dio, che possa amarci veramente, perché egli è Amore”. Rispondere all’amore si può! Allora, rispondiamo all’amore amando come Lui stesso ci ha amati per primo.  

Fr Ndega
Revisione dell'italiano: Giusi