sábado, 28 de julho de 2018

JUKUMU LA KILA “MTU WA MUNGU”


Kutafakari kutoka 2Waf 4, 42-44; Waef 4, 1-6; Yoh 6, 1-15


       Uwepo na matendo ya Yesu huonyesha ukaribu wa kiamilifu wa Mungu. Moyo wake una hisia kwa hali halisi ya wale wanaohitaji kwa sababu umejaa upole na huruma. Yote anayoishi moyoni mwake, Yesu anashiriki na wanafunzi wake ili wajifunze kutoka kwake jinsi ya kushinda kutojali na wasiangalie tu bali watende pia. Hili ni jukumu la kila “mtu wa Mungu”, kama vile tunaweza kuona katika andiko la kwanza ambalo Elisha anaeleza kwa mtumishi wake kwamba kushiriki zawadi katika jumuiya ni kuweka matendoni kusikiliza ya faida la Neno la Mungu. Hakuna mtu aliye maskini mno asiye na kitu cha kutoa. Kile tulichonacho kinatoka kwa Mungu nasi tunapokishiriki kinazidika kwa sababu hakuna yeyote aliyeweza kushinda ukarimu wa Mungu aliye tayari daima kutupatia zaidi. Katika andiko la pili, Mtakatifu Paulo anawaalika Wakristo waishi kulingana na wito ambao wameitwa. Mwaliko huu unatukumbusha kuhusu hali ya ubatizo wetu kupitia huu tumekuwa mashahidi wa ubaba wa Mungu, ambaye anatenda daima ndani yetu na kupitia kwetu. Basi, Maisha yetu yaweze kuonyesha tendo lake la ukarimu.

      Kwa nguvu yake peke yake, Yesu angeweza kutatua tatizo la umati wenye njaa, lakini alitaka pia wafuasi wake wafanye kitu mbele ya mahitaji ya watu. Hali hii ni kitu cha kuchukua kwa ahadi/sharti. Kwa hili tunapata katika wainjilisti usemi: “Wapeni ninyi chakula” (Mt 14, 16; Mk 6, 37; Lk 9, 13). Katika kifungu cha Yohana, swali kwa Filipi linaonyesha kwamba lile aliloagiza Bwana halimaanishi tendo ambalo wanafunzi watimize peke yao, bali ndio mwaliko wa kushiriki katika mpango ambao Mwalimu alikwisha amua moyoni mwake umejaa upole na huruma. Kila ishara na neno la Mwalimu ni fursa mpya daima ya kujifunza kwa wanafunzi wake. Lakini kwa kuelewa lile Bwana aliamua kutenda ni lazima kufikiri kama vile yeye ambaye hatoi nafasi ya kwanza kwa fedha ilipaswa kutumika lakini kwa haja ya watu. Kipaumbele ni mawazo ya kutoa na sio ya ulaji na ya ubadhirifu. Kwa hivyo, hatimaye mwalimu aliwaomba wakusanye vipande vilivyoachwa.

     Sura ya VI ya injili ya Yohana huanza na hadithi hii nzuri ya kuzidisha mikate na kuendelea na mazungumzo ya Yesu juu ya mkate wa uzima. Kwanza kabisa, baada ya kupita ng’ambo ya ziwa na kupanda mlimani, Yesu aliona umati mkubwa wa watu. Mbele ya mahitaji yao, mtazamo wa Yesu ni wa huruma, yaani: ndio mtazamo wa mtu anayeona hisia sio kwa moyo tu bali anatenda pia kwa hamu ili kubadilisha hali. Watu hawa walimfuata Yesu kwa sababu waliona ishara alizofanya kwa ajili ya wagonjwa. Uhusiano wa Yesu na watu ulikuwa kweli wa ajabu, hasa kwa ajili ya maskini na ya walioteseka. Hali hii ilivutia watu waone katika yeye utimizaji wa ahadi za kimungu. Katika Yesu, Mungu atembelea watu wake na kutembea nao. Watu hawa waliomfuata Yesu walikwisha choka wa kuona kwamba hali yao haikuwa muhimu kwa upande wa viongozi wao. Walikuwa kama kondoo wasio na mchungaji na kwa hivyo, walikuwa wenye njaa na kiu kwa kila maana. 

      Yohana naye ndiye pekee yake ambaye - katika tukio hili la kuzidisha mkate - analitaja jambo la Pasaka: “Pasaka, sikukuu ya Wayahudi, ilikuwa karibu”; na mwishowe, anaongeza kwamba Yesu “alienda tena mlimani yeye peke yake”. Wakati huu hakukubali uwepo wa watu wala wa wanafunzi wake kwa sababu hata hao pia hawakuelewa maana ya ishara. Ndiye Baba tu anaweza kuelewa. Ndiyo muhimu kukumbuka kwamba Mwinjilisti Yohana anapendelea kutumia neno “ishara” badala ya “muujiza”. Ishara zote ambazo Yesu hutimiza katika injili hii ndizo tangazo la kutarajia la “Saa” yake, yaani, Pasaka yake kupitia hii atamtukuza Baba na kuhitimisha kazi yake ya ukombozi. Ndiyo maana inatumika msemi “Pasaka, sikukuu ya Wayahudi” mwanzoni mwa kifungu hiki ili kuonyesha kwamba chakula kilichotolewa na Yesu, yaani, neno lake na mwili wake, kitakuwa Pasaka mpya.


      Jibu la Filipi ni ishara ya kosa la ushirika na moyo wa Yesu anayejua haja yetu kabla ya tumwombe kitu. Mara nyingi, kama Filipi, sisi huchukua muda mrefu tukifikiri kuhusu kile hatunacho na hivyo, hatufanyi mema na kidogo tunacho. Andiko hili inazungumzia pia ushiriki wa Andrea, ndugu wa Petro. Yeye alimtaja mtoto aliyeleta kitu ili kushiriki na kikundi. Ishara ya mtoto ya kutoa kitu ilimpendeza Mungu aliyekitumia kwa ajili ya manufaa ya wote. Tena mara nyingi, kama Andrea, tunatambua kwamba zawadi ziko lakini hatuwezi kuitambua thamani zao. Yesu analaumu tabia ya kutojali lakini anatuambia kwamba ndizo ishara ndogo anazozifanya kwa moyo ambazo zinaweza kufanya tofauti. Yesu anatualika kushiriki na wengine nafsi yetu bora kama zawadi zinazotolewa kwa Mungu. Kwa wema wake, Yesu amekwisha amua kutumia zawadi tuliyo sisi wenyewe ili kulisha dunia kwa sababu katika njia hii maisha yetu yanachukua maana. Kukubali ahadi hii ni changamoto kubwa kwetu nayo ndiyo jukumu la kila mwanamme/mwanamke anayejiona “mtu wa Mungu”.

Fr Ndega

IL COMPITO DI OGNI “UOMO/DONNA DI DIO”



Riflessione a partire di 2Re 4, 42-44; Ef 4, 1-6; Gv 6, 1-15


          La presenza e azione di Gesù rende visibile e attiva la vicinanza di Dio. Il suo cuore è sensibile alla realtà di chi ha bisogno perché è pieno di tenerezza e compassione. Quello che vive nel suo cuore, Gesù lo condivide con i suoi affinché possano imparare da lui a vincere l’indifferenza, passando dal vedere all’agire. Questo è il compito di ogni “uomo di Dio”, come possiamo vedere nel primo testo (2Re 4, 42-44) in cui Eliseo fa capire al suo servo che la condivisione dei doni è una espressione concreta dell’ascolto fecondo della Parola di Dio. Nessuno è così povero da non avere niente da dare. Quello che abbiamo viene da Dio e quando lo condividiamo esso si moltiplica perché Dio non si lascia vincere in generosità, sempre pronto a donarci di più. Nel secondo testo (Ef 4, 1-6), San Paolo invita i cristiani a vivere secondo la vocazione a cui sono stati chiamati. Questo invito ci fa ricordare la realtà del nostro battesimo attraverso il quale siamo diventati testimoni della paternità di Dio, che agisce sempre in noi e per mezzo di noi. Il nostro vivere sia visibilità della sua azione generosa.

        Gesù può risolvere da solo il problema della folla affamata, ma vuole che anche i suoi discepoli facciano qualcosa davanti al bisogno della gente. Questo è un impegno da prendere sul serio. Per questo troviamo nei sinottici l’espressione: “Voi stessi date loro da mangiare” (Mt 14, 16; Mc 6, 37; Lc 9, 13). Nel brano di Giovanni (Gv 6, 1-15), la domanda fatta a Filippo dimostra che l’ordine dato dal maestro non significa una azione da essere compiuta solo dai discepoli ma si tratta di una partecipazione in ciò che il maestro ha già deciso di fare nel suo cuore pieno di bontà e compassione. Ogni gesto e parola del maestro è sempre una nuova opportunità di apprendimento per i discepoli. Ma per capire quello che il maestro sta per fare bisogna ragionare come lui, che non mette al primo posto il denaro da spendere ma il bisogno della gente. La priorità è la logica del dono e non la logica del consumo e dello spreco. Per questo, alla fine devono raccogliere i pezzi avanzati.

       Il capitolo VI del vangelo di Giovanni inizia con questo bel racconto della moltiplicazione dei pani e prosegue con il discorso di Gesù sul pane della vita. Allora, dopo essere passato all’altra riva del mare e salito sul monte, Gesù vide una grande folla. Davanti ai loro bisogni lo sguardo di Gesù è di compassione: è lo sguardo di una persona che non solo si commuove nel cuore ma che si muove e agisce per cambiare la realtà. Erano persone che seguivano Gesù perché vedevano i segni che egli compiva sugli infermi. Era veramente affascinante il rapporto di Gesù con le persone, specialmente con i poveri e sofferenti. Questo attirava la gente a vedere in Lui il compimento delle promesse divine. In Gesù, Dio visita il suo popolo e cammina con esse. Queste persone che seguivano Gesù erano già stanche di vedere che la loro realtà non era presa sul serio da parte dei loro capi. Erano come pecore senza pastore e, quindi, affamati e assettati in ogni sensi. 

     Giovanni, e soltanto lui, in questo evento fa riferimento alla Pasqua: “era vicina la Pasqua, la festa dei Giudei”; e alla fine, aggiunge che Gesù “si ritirò da solo sulla montagna”. Questa volta non ha accettato la compagnia neanche dei suoi discepoli, perché anche loro non hanno capito il segno. Soltanto il Padre lo capisce. È importante ricordare che l’evangelista Giovanni preferisce usare la parola ‘segno’ invece di ‘miracolo’. Tutti i segni che Gesù compie in questo vangelo sono un annuncio in anticipo della sua “Ora”, cioè, la sua Pasqua, attraverso la quale glorificherà il Padre e concluderà la sua Opera redentrice. Per questo viene fatto riferimento alla “Pasqua, la festa dei Giudei”, all’inizio del brano, indicando che il cibo dato da Gesù, cioè, la sua Parola e la sua vita, sarà la nuova Pasqua.

       La risposta di Filippo è segno della mancanza di sintonia con il cuore di Gesù che sa dei nostri bisogni prima che gli chiediamo qualcosa. Molte volte, come Filippo, noi spendiamo molto tempo pensando a ciò che non abbiamo e dimentichiamo di fare del bene con il poco che abbiamo. Questo testo parla anche della partecipazione di Andrea, fratello di Pietro. Lui presenta un ragazzo che ha portato qualcosa da condividere con il gruppo. Quel poco che il giovane ha presentato è stato gradito a Dio che lo ha usato per il bene di tutti. A volte, come Andrea, riconosciamo che i doni ci sono ma non riusciamo a riconoscerne il loro valore. Gesù condanna l’indifferenza e ci dice che sono i piccoli gesti fatti con il cuore che fanno la differenza. Gesù ci invita a condividere con gli altri il meglio di noi stessi come dono offerto a Dio. Nella sua bontà, Gesù ha già deciso di usare questo dono che siamo noi per sfamare il mondo perché è così che la nostra vita prende un senso. Accettare questo impegno è la grande sfida per noi ed è questo il compito di ogni “uomo/donna di Dio”.

Fr Ndega
Revisione dell'italiano: Giusi

sábado, 21 de julho de 2018

MCHUNGAJI MWEMA ANAYAJUA MAHITAJI YA KONDOO



Tafakari kuhusu Mc 6, 30-34


       Andiko hili tunaweza kukuta pia katika injili nyingine (Luka na Mathayo); kila mmoja wao huleta vipengele maalum ambavyo anafanya hadithi hii kuwa nzuri hata zaidi. Kuhusu vipengele vilivyo sehemu zinazokutwa katika injili tatu, tuko na mashua, mkutano wa mwalimu na watu na matumizi ya andiko hili kabla ya kuzidisha ya mikate. Kuhusu tabia zingine, ikiwa tunachukua pia Luka 9, 10-11 na Mathayo 14, 13-14 tunaona kwamba ndiye Marco tu anayetaja kwamba “wanafunzi hakuwa na nafasi hata ya kula chakula”. Luka anaufuata mpango wa Marco, kwa kosa la kipengele kilichotajwa na hata ile huruma ya Bwana, lakini anataja jina la mahali ambapo walikwenda, yaani, Bethsaida. Mathayo, hata hivyo, hataji kushiriki kwa wanafunzi wala wanafunzi mashuani, tena wala jina la mahali, lakini anaongelea huruma ya Bwana mbele ya hali ya watu, kama Marco alivyo.

     Tunaguswa sana tukiona Yesu ambaye hakutumia tu wanafunzi wake kwa kazi bali alipatikana pia ili kusikiliza maelezo ya uzoefu wao. Hakika yeye aliutambua uchovu wao na haja ya kuwafundisha zaidi. Hivyo, aliwaalika kwenda naye kwenye mahali pa faragha. Hapo tunaona maelewano kati ya hamu ya Bwana ya kuwafundisha zaidi na haja ya wanafunzi wake ya kuingiza zaidi pendekezo la Bwana. Watu wengine walioangalia kutoka nje hawakuweza kuelewa uhusiano huu; waliweza kuelewa tu kwamba kupitia mwalimu yule na wanafunzi wake, ndiye Mungu aliye miongoni mwa watu wake, akichukua hali yao kwa upendo. Kweli, wakati walishuka kutoka mashua na kukutana na watu waliwatangulia, mara Yesu moja alielewa sababu ya utafutaji wao na kuwaonea huruma kwa sababu yeye ndiye Mchungaji mwema na kuyajua mahitaji ya kondoo.

     Kupitia kusikiliza kwake kwa macho na mwaliko ili waende peke yao naye kwenye mahali pa faragha, Yesu anaonyesha upendo kwa uhusiano na wanafunzi wake kama mama na watoto wake. Yeye anataka kubaki peke yake na wanafunzi ili kushughulika kwa ajili ya maisha yao na malezi yao. Nafasi hii waliyokuwa pamoja na Bwana itatumika kwa ajili wafanane zaidi maisha yao na yake. Yesu alijua kwamba haikuwezekana kufika mahali huko kulingana na mpango wake kwa sababu ya umati wa watu waliowatangulia kufika. Kisha, yeye alibadilisha mpango wake na nafasi ya pekee alikuwa nayo ili kuwako peke yake na wanafunzi wake ilikuwa ile mashuani. Hakika ilikuwa ni nafasi maalum ya kuimarisha uhusiano na kuanza tena kushiriki kwa wanafunzi na kusikiliza makini kwa Bwana. Yeye alichukua fursa hii ili kusisitiza jambo fulani zaidi ya yale aliyofundisha kabla ya kuwatuma kuinjilisha au kusahihisha baadhi ya mabadiliko kutoka kilichokuwa muhimu kweli. 

      Yesu anatualika kuingia mashuani pamoja naye na kukaa naye. Mashua hii si kusimama katikati ya “bahari ya maisha” lakini yasonga kuelekea umati unao na kiu kwa ajili ya Mungu na ya neno lake. Mashua hii ni mwaliko kwa urafiki na ukaribu. Tunafanya uzoefu wa kubaki pamoja na mwalimu si kwa kujifunza mafundisho fulani bali kutafakari maisha yake na kuingiza pendekezo lake ili tuwe kulingana na matarajio yake na baada ya kuwa wanaamini wa kweli tutaweza kutangaza kwa wengine. Vinginevyo, hatutapata mafanikio kazini. Kulingana na Fr. Raniero Cantalamessa, "Yule anayetangaza Neno hatagusa moyo wa wengine ikiwa Neno halikugusa moyo wake bado.” Neno hili ni Yesu, ambaye anataka kujaza maisha yetu ya maana na kutufungua kwa wengine. Ikiwa tunabaki naye zaidi, tena zaidi tunajiona kuelekezwa kwenye wengine. Ikiwa tunamwangalia yeye zaidi, tena zaidi mtazamo wetu kwenye wengine utakuwa wa upole na wa huruma.

   Pamoja na Yesu mashuani tunakueleza kwenye wengine sio ili kuwahukumu, lakini kuwaangalia tofauti tukijihusisha katika hali yao. Mbele ya hali ngumu ya watu ambao wanaonekana wamepotea na kuwa na kiu ya ndani ya kusikiliza Neno la kweli la Mungu, Yesu anatoa msaada wa kiroho kupitia maneno yake na baadaye anatoa pia msaada wa kimwili kupitia mikate na samaki. Lakini katika andiko hili, kwa muda, Mchungaji Mwema anatoa kuanza chakula kamili kwa sababu anajua haja ya kundi lake. Maudhui ya mazungumzo ya Mchungaji amejaa upole na huruma yangalikuwa nini? Askofu na Shahidi Oscar Romero alisema kwamba Yesu angalizungumza kwao “kwamba wokovu hutoka kwa Mungu peke yake, tena kwamba Mungu anatupenda, tena kwamba Mungu hatuachi, tena kwamba tupendane, tena kwamba tusitawanye.”

     Tuweze kuleta tangazo hili la furaha, kwanza kabisa kupitia maisha yetu yaliyobadilishwa na mkutano na Yesu Mchungaji Mwema na kisha, kwa maneno yetu pia.

Fr Ndega

IL BUON PASTORE CONOSCE I BISOGNI DELLE PECORE



Riflessione su Mc 6, 30-34


      Questo brano è presente anche negli altri sinottici (Luca e Matteo), ciascuno dei quali porta delle particolarità che rende la narrativa ancora più bella. Per quanto riguarda gli aspetti comuni, tutti e tre parlano della barca, dell’incontro del maestro con la gente e mettono questo testo prima della moltiplicazione dei piani. Riguardo alcune particolarità, confrontando Luca 9, 10-11 e Matteo 14, 13-14 vediamo che solo Marco menziona il fatto che i discepoli “non avevano neanche il tempo di mangiare”. Luca segue lo schema di Marco, omettendo oltre l’aspetto menzionato, anche quello della compassione del maestro, ma aggiunge il nome del luogo verso il quale andavano, cioè, Betsaida. Matteo invece, non menziona né la condivisione dei discepoli, né i discepoli sulla barca, né il nome del luogo, ma fa constatare l’aspetto della compassione del maestro nei confronti della gente, come fa Marco.

       Ci colpisce molto vedere che Gesù non solo invia i suoi discepoli in missione ma dedica tempo per ascoltare i dettagli della loro esperienza. Certamente egli si è reso conto della loro stanchezza e il bisogno di un approfondimento. Per questo, li invita ad andare in un luogo in disparte loro soli con lui. Troviamo qui una perfetta sintonia tra il desiderio del maestro di insegnarli di più e il bisogno dei suoi discepoli di assimilare maggiormente la proposta del maestro. Le altre persone che guardano da fuori non capiscono questo rapporto; capiscono soltanto che tramite loro, Dio si fa vicino al suo popolo, prendendo sul serio la loro realtà. Infatti, quando scendono dalla barca e trovano la gente che aspettava, Gesù capisce subito la ragione della loro ricerca e ha compassione perché è il Buon Pastore e conosce i bisogni delle pecore.

     Tramite il suo ascolto attento e l’invito ad andare in disparte da soli con lui, Gesù dimostra tenerezza nei confronti dei suoi discepoli come una mamma con i suoi figli. Gesù vuole stare da solo con i suoi, occupandosi della loro vita e della loro formazione. Il tempo con il maestro servirà per configurare di più la loro vita con la sua. E’ interessante notare che Gesù sapeva che non era possibile raggiungere il luogo in disparte a causa della folla che cercava di arrivare in anticipo. Allora ha cambiato programma e l’unico momento che ha avuto da solo con i suoi discepoli è stato quello sulla barca. Certamente è stato un bel momento di approfondimento con la ripresa della condivisione dei discepoli e l’ascolto attento del maestro. Egli ha approfittato di questa opportunità per sottolineare qualche aspetto in più di ciò che ha insegnato prima di mandarli in missione o correggere qualche deviazione da ciò che era realmente essenziale. 

       Gesù ci invita a salire sulla barca con lui e rimanere con lui. Questa barca non è ferma in mezzo al mare della vita ma si muove verso una folla assetata di Dio e della sua Parola. Questa barca è una chiamata alla intimità e alla vicinanza. Facciamo l’esperienza di stare con il maestro non per imparare una dottrina ma per contemplare la sua vita e incarnare la sua proposta per essere come lui vuole che siamo e soltanto dopo essere veramente convinti, possiamo annunciarlo agli altri. Diversamente non avremo esito nella missione. Secondo don Raniero Cantalamessa: “Colui che annuncia la Parola non arriverà al cuore degli altri se la Parola stessa non è arrivata al suo cuore”. Questa Parola è il proprio Gesù, che vuole riempire la nostra vita di senso e aprirci agli altri. Più rimaniamo con lui, più ci sentiamo orientati verso gli altri; più guardiamo lui, più il nostro sguardo diventa pieno di tenerezza e misericordia verso gli altri.

      Insieme a Gesù sulla barca andiamo verso gli altri non per giudicarli ma per guardarli diversamente coinvolgendoci con la loro realtà. Davanti alla realtà drammatica di quelle persone disorientate e assetate della vera Parola di Dio, Gesù dona un sopporto spirituale tramite le sue parole e subito dopo consegna loro anche il sopporto fisico tramite i pani e i pesci. Ma in questo brano, il Buon Pastore offre per primo il cibo giusto perché conosce il suo gregge. Quale sarebbe stato il contenuto del discorso fatto da questo Pastore pieno di tenerezza e misericordia? Il Monsignore e Martire Oscar Romero, afferma che Gesù avrebbe parlato loro che “l’unica salvezza viene da Dio, che Dio ci ama, che Dio non ci abbandona, che ci amiamo gli uni gli altri, che non ci disperdiamo”.

     Che possiamo portare avanti questo lieto annuncio, prima con la nostra vita trasformata dall’incontro con il Buon Pastore Gesù e poi con le nostre parole.

Fr Ndega
Revisione dell'italiano: Giusi

sábado, 14 de julho de 2018

NJIA KAMILI YA KUWA WANAFUNZI WA YESU


Amosi 7: 12-15; Waefeso 1: 3-14; Mk 6: 7-13



         Nabii Amosi alichaguliwa na Mungu ili kutabiri katika hali ngumu ya watu wa Israeli (Ufalme wa Kaskazini), yaani, kukosekana kwa usawa wa kijamii, udhalimu dhidi ya maskini na matumizi ya dini kulingana na mvuto binafsi wa mfalme. Wakati wa mfalme Yeroboamu wa II, pamoja na hekalu kuu la Yerusalemu (Ufalme Kusini) lilikuwako pia hekalu lingine lililoitwa Betheli (Kaskazini). Amosi alipoanza kazi yake katika mahali huko, alikutana na kuhani wa hekalu la Betheli, aliyeitwa Amazia, ambaye alifanya upinzani dhidi ya unabii wa Amosi. Amazia ni aina ya mtu aliyelipwa ili kudumisha mfumo wa hekalu na kuhalalisha mfumo wa kidhalimu wa mfalme. Ingawa Amosi alitendewa vibaya, tabia yake ni tofauti, yaani alipendelea kumwelezea Amazia maana ya wito wake. Ujumbe wa Amosi kama nabii hautegemei malipo, bali ni maonyesho ya ukarimu na mapenzi ya Mungu anayeruhusu kuguswa na hali ya maskini na ya wanaoteseka.

          Somo la pili ni wimbo wa shukrani kwa Mungu ambaye ametubariki sana katika Kristo tangu mwanzo wa ulimwengu ili tuwe watoto wake. Kwa ujumbe wa Yesu Kristu tumesamehewa dhambi zetu ili tuweze kuishi wito wetu kwa utakatifu. Wito huu ni sehemu ya mpango wa hekima na wema wa Mungu ambaye katika Kristo ametuchagua ili tuwe watu wake mwenyewe. Roho wa Mungu anatusaidia kuishi wito wetu kwa uaminifu na kutupatia utimizaji wa ahadi yake. Kulingana na Baraza ya Vatikano ya II utakatifu ni wito wa wote tangu ubatizo wetu na Mt Yohana Calabria anasema kwamba “hatuhitaji kufanya mambo ya ajabu ili tuwe watakatifu. Tunaweza kuwa watakatifu kupitia hali ya kawaida. Yatosha nia zetu ziwe takatifu katika mambo yote.”    
   
       Baada ya kukataliwa kijijini chake, Yesu aliendelea na ujumbe wake vijijini vingine kandokando huko ambapo alikaribishwa vizuri sana. Aliweza kufanya kazi yake peke yake, bali hakutaka. Kwa hivyo aliwaita Mitume kumi na wawili kama washirika. Kabla ya kuwatuma kwa ujumbe, aliwaita ili kubaki naye, yaani aliwapendekezea uzoefu wa nafsi yake. Uzoefu huu ni wa msingi kwa mafanikio ya kazi. Wakati huu alishiriki nao hisia yake kuhusu hali ya watu walioteseka kwa sababu ya nguvu za maovu na ya magonjwa mengi. Mamlaka ambayo Yesu alishiriki nao yalilenga kuwaimarisha watu ili waweze kushiriki kikamilifu katika jamii. Hatimaye, aliwapa maelekezo hasa kuhusu mahitaji ya njia ya unyenyekevu wa maisha na kuwatuma wawiliwawili. 
   
          Ndiye Yesu aliyechukua nafasi ya kuwaalika wanafunzi. Hakuwatafuta wenye nguvu au wenye umaarufu katika jamii. Aliwachagua watu wanyenyekevu, wafanyakazi na walio makini kwa ufunuo wa Mungu kupitia Mwana wake. Yaliyomo ya maelekezo Yesu aliyowapa yanaufuata mwelekeo tofauti kabisa na matarajio ya binadamu. Kwa mafanikio katika kazi, mitume walipaswa kushinda baadhi ya tabia za binadamu ambazo zipo sana maishani mwetu: dhidi ya tabia ya kutenda kwa njia ya kibinafsi, tunaalikwa kutenda pamoja na kusaidiana katika jumuiya na kwa manufaa ya jumuiya. Kazi ya kuinjilisha sio kazi ambayo mtu anachukua peke yake bali ndiyo kazi ya kijumuiya. Dhidi ya tabia ya kutawala, Yesu anashiriki nasi uwezo wake ili tutumikie watu; dhidi ya tabia ya kuwa na mali, Yesu anatupendekezea kujinyima, unyenyekevu na ukarimu.

        Kama wanafunzi wa kwanza tunapaswa kufahamu kwamba tajiri yetu ndilo ujumbe ambao Mungu anatukabidhi. Siyo mali ambayo inaweza kutuhakikishia usalama, bali ndiye Yule ambaye aliyetualika, akatutuma na kuandamana nasi. Dhidi ya tabia ya kulazimisha, tangazo letu ni pendekezo, pendekezo la toba na la mabadiliko ya maisha. Ikiwa mtu fulani hataki kupokea ujumbe wetu, hatuwezi kumlazimisha bali kuheshimu uhuru wake kwa sababu ni kwa uhuru ambao mtu anaweza kukubali pendekezo la Yesu na kumfuata. Wakati tunapokabiliana na upinzani dhidi ya kazi yetu Yesu anatarajia tuweze kushinda hofu na kufanya upya imani yetu katika Riziki ya Mungu ambaye hawaachi wale wanaotumainia yeye. Njia yetu ya kuishi inaongea zaidi kuliko maneno yetu. Pendekezo la toba ambalo tunawatangazia wengine liwe maonyesho ya mabadiliko ambayo tumeona kwa kupitia uzoefu wetu wa huruma ya Mungu. Mungu anataka kuyapatia maisha mengi kwa watu wake na kuamua kututumia kama washirika wake. Tuko tayari?    

Fr Ndega

sábado, 7 de julho de 2018

VIKWAZO KWA UNABII



Tafakari kuhusu Ez 2, 2-5; 2Kor 12.7-10; Mk 6, 1-6


      Mungu anachukua nafasi daima ya kujifunua naye hahitaji matukio ya ajabu kujionyesha kwa watu. Njia yake ya kutenda inasababisha kushangaza kwetu daima, kwa kushinda matarajio yetu ya kibinadamu. Mantiki na mawazo yake ni tofauti kabisa na yetu. Hii ni mantiki ya unabii katika siku za nyuma na hata leo. Mungu anatumia kama wapatanishi watu wanyenyekevu ambao tunawakutana kwa kila siku na hali ya kawaida ili kuwasiliana nasi. Kwa kuitambua hali hii ni muhimu kujua zaidi ya hali iliyoonekana (binadamu anaangalia hali inayoonekana, lakini Bwana huona ndani ya moyo); ni lazima kuwa na uwezo wa kuona kwa moyo kabla ya kwa macho. Hivyo tu tunaweza kutambua yale ambayo Bwana anafanya katika maisha yetu.

      Watu wa Israeli walifukuzwa katika uhamishoni wa Babeli naye Ezekieli ambaye alikuwa mmoja wa kuhani alienda pamoja nao. Wakati ambapo uharibifu wa Yerusalemu uliyasababisha mashaka kuhusu uaminifu na ahadi ya Mungu, Ezekieli aliitwa kuwa nabii wa Mungu aliye hai kati ya watu ambao waliasi dhidi ya Bwana. Utume wa Nabii Ezekieli ulikuwa kuwasaidia watu kuelewa kwamba uharibifu wa Yerusalemu ambao uliutabiriwa na kuutimiza ulikuwa matokeo ya dhambi zao. Kwa sababu ya hayo nabii Ezekieli alipata upinzani mkubwa lakini alisaidiwa na Roho wa Mungu ili kubaki mwaminifu katika kazi yake. Kwa sababu ya uaminifu wa Mungu kwa ahadi zake, maudhui ya ujumbe wa kinabii pamoja na tangazo la adhabu yatoa pia ahadi ya wokovu. Hivyo kazi ya nabii ndiyo kuwaimarisha watu wawe na imani na tumaini.

      Mtume Paulo alikuwa na nafasi ya kupokea ufunuo kutoka kwa Mungu. Nafasi hii ilitokwa pamoja na upinzani ambao Mtume huyo alikabiliana wakati wa utume wake. Alimwomba Mungu amweke huru toka mwiba huo, na Mungu alimwambia: “Kwako neema yangu yatosha.” Kila mtu anayechaguliwa na kutumwa kwa kazi fulani anapaswa ufahamu kwamba uvumilivu na uaminifu wake wategemea siyo nguvu zake tu bali hasa neema ya Mungu ambaye anamsaidia kubaki imara. Zaidi mtu anapata kuukiri udhaifu wake tena zaidi yeye anajiona mwenye haja ya neema ya Yule ambaye alimwita. Kulingana na Mtakatifu Yohana Calabria, “Mungu hutumia watu wanyenyekevu na wapole ili kutimiza mipango yake mikubwa kwa wanadamu. Yeye hajui kufanya nini na wenye kiburi, kweli huwatoa mbali naye”.
 
      Baada ya uzoefu mzuri kwenye ufuko wa bahari, Yesu alirudi tena kijijini kwake na jumuiya yake, yaani, Nazareti. Huko ndipo mahali ambapo Yesu angekaribishwa vizuri, lakini, haikutokea hivyo. Yesu alipata upinzani kutoka wale waliodhani kwamba maarifa yao kuhusu asili ya kibinadamu ya Yesu yalitosha ili kuwa uhusiano wa kweli na kina naye. Ni vigumu sana kwao kutambua kazi ya Mungu katika mwenzao huyo waliyemwona kukua na kuishi nao hali ya kawaida. Maarifa yao ya Yesu hayakuwa msaada bali kikwazo kwa kufungwa kwao ili kupokea ufunuo Yesu aliowaletea. Kwa hitimisho, Yesu hakutimiza maishani mwao aliyopanga kutenda kama yule aliye na kazi kudhihirisha uso wa huruma ya Baba. Walidanganywa na maarifa yao wenyewe wa Mungu.   

       Ukosoaji mkubwa wa andiko hili ni kuhusu ugumu wa kuamini. Kwa kuyajua mambo mengi ulimwenguni akili yatosha. Lakini hatuwezi kusema sawa kuhusu uzoefu wa Mungu. Tunapaswa kuwa macho kwa sababu mawazo ama mifano ya Mungu ambayo alijifunza kwa akili yetu inaweza kutuzuia kumjua kweli. Hatuwezi kuridhika na kujua mambo juu ya Mungu; ni lazima kumruhusu yeye ajifunue mwenyewe kwetu kwa nguvu zote za upendo wake. Kwa kupata hayo inahitaji imani. Tunataka kupata mabadiliko ulimwenguni na katika maisha yetu, lakini katika chaguzi na tabia zetu sio daima tunaonyesha kwamba tunaamini. Sisi bado tunaishi kama watu ambao somo la kwanza liliongea: “Mataifa wa waasi, walioniasi mimi.” “Kweli ikiwa siku hizi miujiza haitokei siyo kwa sababu haiwezekani bali haitokei kwa sababu ya kosa la imani.”

        Upinzani Yesu aliokabiliana miongoni mwa ndugu zake na wananchi sio kwa maana ya kidini kuhusiana na matarajio ya Masihi lakini pia kwa maana ya mahusiano ya kibinadamu sio tofauti sana na kile kinachotokea mara nyingi katika mahusiano yetu na wengine. “Tuko na ugumu mkubwa wa kuacha mipango yetu na njia yetu ya kuwahukumu wengine na hali kandokando yetu! Mara nyingi tuko na haraka ya kuwahukumu kuhusu njia yao ya maisha, nia yao na utambulisho wao. Hii si jukumu letu. Jukumu letu ni kujifunza daima na kusikiliza kabla ya kuzungumza. Hakuna mtu anayekuwa shahidi ikiwa hafanyi uzoefu na hakuna mtu anayekuwa nabii ikiwa haiwezi kusikiliza. Hata kwa ajili ya chaguzi zetu za msingi uzoefu wa kusikiliza inakuwa rejeo ili tuweze kuwa na utambuzi mzuri  na kuamua kamili.

Fr Ndega


OSTACOLI ALLA PROFEZIA



Riflessione su Ez 2, 2-5; 2Cor 12,7-10; Mc 6, 1-6


       La rivelazione è sempre iniziativa di Dio, egli non ha bisogno di avvenimenti straordinari per rivelarsi alle persone. Egli ci sorprende sempre, superando le nostre aspettative umane. La sua logica è tutta un’altra cosa. Questa è la logica della profezia nel passato e anche di oggi. Dio si serve di persone semplici che incontriamo ogni giorno e di segni semplici e quotidiani della vita per comunicarsi a noi. Per riconoscerlo occorre saper andare oltre le apparenze (l’essere umano guarda le apparenze ma il Signore guarda il cuore); occorre saper vedere col cuore, prima ancora che con gli occhi. Solo così possiamo renderci conto di ciò che il Signore sta facendo nella nostra vita.

      Il popolo di Israele è stato deportato in esilio in Babilonia e con esso è andato anche Ezechiele che era uno dei sacerdote di allora. In un tempo in cui la distruzione di Gerusalemme ha messo in discussione la fedeltà e le promesse di Dio, Ezechiele è stato chiamato ad essere profeta del Dio vivente in mezzo alla sua gente che si è ribellata contro il Signore. La missione del profeta Ezechiele è quella di far capire a tutti che la distruzione di Gerusalemme annunciata e compiuta è stata il risultato dei loro peccati. Il profeta troverà molta resistenza ma è sostenuto dallo Spirito che lo rende fedele nella missione. A causa della fedeltà di Dio alle sue promesse, il contenuto del messaggio profetico oltre all’annuncio di punizione, porta anche la promessa di salvezza. Quindi, la missione del profeta è motivare alla fiducia e alla speranza.

      L’apostolo Paolo ha avuto la grazia di ricevere alcune rivelazioni da parte di Dio. Questa grazia è venuta accompagnata anche dalle resistenze che l’apostolo ha incontrato durante la sua missione. Lui ha chiesto a Dio di liberarlo di tale spina e Dio gli ha risposto: “Per te basta la mia grazia”. Ogni persona scelta e inviata in missione deve essere consapevole che la sua perseveranza e fedeltà sono dovuti non solo alle sue forze ma alla grazie di Dio che la sostiene. Più la persona è consapevole della sua debolezza più si abbandona alla azione della grazia di colui che l’ha chiamata. Secondo San Giovanni Calabria, “Dio si serve di strumenti umili e docili per rivelare i suoi grandi disegni all’umanità. Egli non sa cosa fare con gli orgogliosi, anzi li allontana da sé”.
 
       Dopo la bellissima esperienza vissuta sulla riva del mare, Gesù va nuovamente dal suo popolo, da sua parentela, cioè, a Nazareth. Questo è il posto dove Gesù dovrebbe essere veramente accolto. Invece no. Gesù trova resistenza da parte di coloro che pensano che la loro conoscenza sull’origine umana di Gesù è già abbastanza per avere un vero e profondo rapporto con lui. Per loro è troppo difficile riconoscere l’opera di Dio in questo compaesano che hanno visto crescere, che ha vissuto con loro la normalità della vita. La loro conoscenza su Gesù non è stata un aiuto ma un ostacolo per un’apertura necessaria alla rivelazione che Egli portava loro. Come conclusione, Gesù non ha compiuto nella loro vita ciò che ha voluto fare come il rivelatore del volto misericordioso del Padre. Loro sono stati ingannati proprio dalla loro conoscenza di Dio.   

       La grande critica di questo testo è sulla difficoltà di credere. Per conoscere tante cose nel mondo ci basta l’intelligenza. Però non possiamo dire lo stesso quando si tratta dell’esperienza di Dio. Dobbiamo stare attenti perché le idee o immagini di Dio che acquistiamo con la nostra intelligenza possono impedirci di riconoscerlo veramente. Non possiamo accontentarci solo con la conoscenza di cose su Dio; dobbiamo permettere che egli stesso si riveli a noi con tutta la potenza del suo amore. E per arrivare a questo ci vuole fede. Desideriamo che accadano dei cambiamenti nel mondo e nella nostra vita, ma nelle nostre scelte e atteggiamenti non sempre dimostriamo che siamo persone credenti. Ci comportiamo ancora come quel popolo del quale ci parla la prima lettura: “Una razza di ribelli che si sono rivoltati contro di me”. “Veramente se ai nostri giorni non avvengono miracoli perché sono impossibili, ma non avvengono per la mancanza di fede”.

      La resistenza che Gesù ha trovato tra i suoi parenti e compaesani non solo nel senso religioso per quanto riguarda l’aspettativa messianica ma anche nel senso di rapporto umano non è molto diversa di ciò che accade molto spesso nei nostri rapporti con gli altri. “Quanta fatica facciamo ad uscire dai nostri schemi e dal nostro modo di incasellare le persone e la realtà che ci circonda! Alle volte con i nostri pregiudizi abbiamo fretta di giudicare gli altri sul loro modo di vivere, sulle loro intenzioni ed identità”. Questo non tocca a noi. A noi tocca imparare sempre, sapere ascoltare prima di parlare. Nessuno diventa testimone se non ha fatto l’esperienza e nessuno diventa profeta se non sa ascoltare. Anche per le nostre scelte fondamentali l’esperienza dell’ascolto diventa il punto di riferimento perché possiamo discernere bene e prendere la decisione giusta.

Fr Ndega
Revisione dell'italiano: Giusi