domingo, 27 de setembro de 2015

KUTENDA MEMA KWA JINA LA YESU


Kutafakari kutoka Hes 11:25-29; Mk 9:38-43, 45, 47-48

Mungu hawabagui watu kwa maana anapenda na katika upendo hakuna ubaguzi. Maatarajio yake ni kwamba watu wake wote wangekuwa manabii, wanasikiliza neno lake na kuongea katika jina lake. Kupitia Roho wake Mtakatifu, anawahamasisha watu ili watende mema kulingana na mapenzi yake, akidhibitisha kwamba tendo lake halina mpaka. Mbele ya Mungu hakuna mtu wa heshima zaidi kuliko mwingine. Yeye hakubali umaarufu au ubaguzi, bali anatarajia ahadi kwa njia yake ya kufikiri na kutenda. Maana kwa njia hii ni upendo wake wa bure kwa wote.

Wanafunzi wa kwanza walijaribu kumkataza mtu fulani kufanya mwujiza kwa jina la Yesu kwa sababu hakuwa mmoja wao. Wlifanya hivyo kwa mamlaka gani? Yesu hakubaliani na tabia hii na akawaambia kwamba mtu ambaye anatenda mema kwa jina lake (Yesu) hawezi kumnenea mabaya. Kisha akiendelea kwa mafundisho yake, alisema kwamba watu wanaosaidia wafuasi wake watapokea tuzo kwa sababu ya utambulisho wake na wale waliotumiwa katika jina lake. Yesu anawakumbusha pia kwamba juhudi yote ya wale wanaomfuata lazima kuwa hamasa kwa wale ambao wanaanza kumwamini Kristo au wana ugumu kumwamini. Kashfa ni jambo mahututi sana na ni lazima kuepukwa kwa sababu huivuruga imani.

Tumetafakari kuhusu ugumu wa wanafunzi wa Yesu kuelewa na kuyapokea mafundisho yake. Wanaelewa nusunusu, hasa ile sehemu rahisi, wanaipokea na kuacha yaliyo magumu. Ni hatari mno kuelewa nusu ya ukweli kwa sababu kama hii tunaweza kuleta uzushi. Kujaribu kumkataza mtu fulani ambaye alifanya mema kwa jina la Yesu ni ishara ya ugumu ya kumfahamu Yesu na mapendekezo yake. Maana ya kuwa mfuasi wa kweli wa Yesu si maneno tu, bali ni matendo mema hata kama mtu huyu hayumo kwenye kundi. Badala ya kuwakataa wengine ambao wanatenda mema kwa jina la Yesu, wanafunzi wake wanapaswa kujikataa wenyewe. Kuwa mwanafunzi wa Yesu inamaanisha imani iliyoonyeshwa kwa matendo. Kwani wao wanaokiri na kutenda kama kadiri ya neno” ndiyo mama na ndugu zake na wanafunzi wake. Ikiwa huyo mtu alitenda mema kwa jina la Yesu, tayari alikuwa mwanafunzi wake. Mtazamo wa wanafunzi una upungufu na ubaguzi, lakini mtazamo wa Yesu ni mpana na ni kwa wote wenye mapenzi mema.

Kitu muhimu katika dini au imani ni matendo na siyo maneno. Matendo husema zaidi ya maneno. Mifano halisi ni wakristo wa kwanza, waliweza kuwavuta wengine si kwa maneno, bali njia yao ya maisha. Kuhusu wao watu walisema: “Mwone kama wanavyopendana”! hali hii iliwezekana kwa sababu ya upendo wao ulionyeshwa kupitia ridhaa wao kwa wao, kushiriki pamoja, uvumilivu katika maombi pamoja na unyenyekevu wa moyo. Kuhusu hayo Sinodi ya Afrika imesema: “Sharti muhimu la kuhubiri ni ushuhuda wa maisha”. Mwanafunzi wa kweli wa Yesu hawezi kuwa na ubaguzi na kuamini kuwa watu wa kundi lake pekee, au chama chake cha utume, au kanisa lake ndiyo wanafunzi pekee wa Yesu na wameokolewa. Hatuwezi kufikiri kwamba Yesu ni mali yetu. Ikiwa tunahisi karibu na Yesu, hatuwezi kuishi mbali sana na ndugu zetu, kufungwa kabisa kwa hali kandokando yetu na hata kufikiri kwamba tunakuwa na mamlaka ya kuwazuia wengine watende kwa jina la Yesu. Tuko mbele ya kosa kubwa. Sisi lazima kuwa makini sana kuhusu baadhi ya uzoefu ambao unatufungua kwa Mungu lakini unatufunga kwa wengine. Ikiwa imani yetu haituongozi kukutana na wengine na kutambua mema ambayo wanaweza kufanya imani yetu ni utenganisha. Basi, ili Mungu atufundishe kutambua mwendelezo wa kazi zake mbele ya matendo mema ya wakristo na kusaidiana kwa wema wa wote.

Fr Ndega

Mapitio: Sara

domingo, 20 de setembro de 2015

UFUNDISHAJI NA TABIA YA AJABU


Wis 2:12.17; Jas 3: 16-4:3; Mk 9,30-37


       Kifungu hiki kutokana na kitabu cha Hekima ya Sulemani kinaongea kuhusu ushuhuda muhimu wa mtu mwenye haki na upinzani wa wale ambao hawaukubali ushuhuda wake na wanamtendea vibaya, kupanga mauti yake. Hali hii inatokea kwa sababu ya njia ya maisha yake kulingana na mapenzi ya Mungu. Njia hii inawasikitisha wale wanaopendelea kuishi vibaya, mbali na Mungu. Hata hivyo, mtu huyo mwenye haki ni mwana wa Mungu, na Mungu mwenyewe atamtegemeza na kumwokoa mikononi mwa adui zake. Hii ni ishara ya Kristo, aliye Mwana wa Mungu kwa namna ya pekee kabisa. Yeye, katika uaminifu wake kwa mpango wa Mungu, alipata wokovu hata kwa wale waliwakandamiza wengine. Somo la pili linasema kuwa hekima ambayo inasababisha kujua kamili inatoka kwa juu kwa sababu ni Mungu mwenyewe chanzo cha hekima ya kweli. Mtu anayeongozwa na hekima hii anaweza kuwa mwenye moyo safi, tena ni mtu wa amani, ya upole, tayari kusikiliza maneno ya watu na kutenda mema kwa ajili yao.

         Injili ni mwendelezo wa tangazo la Petro kuhusu utambulisho wa Yesu na mwaliko wa Yesu mwenyewe kwa wafuasi wake wamfuate katika kujisalimisha kwake ili wapate uzima. Yesu alitambua kwamba wakahitaji kujua zaidi kuhusu maana ya umasiha wake na kuyafahamu vizuri mapendekezo yake. Kwa hivyo alitumia kipindi maalum kuwafundisha peke yao kuhusu maana kamili ya umasiha aliochagua na uanafunzi. Hakutaka watu wafahamu alipo. Yesu alijaribu tena kuongea na wanafunzi kuhusu mateso, kifo na ufufuko wake, lakini walionekana mbali sana na mwalimu. Hawakuelewa tena kwa sababu walishughulika sana kwa mawazo na nia tofauti. Hata hivyo Yesu anatumia mifano ili waweze kufahamu ufunuo wake. Vipengele vya msingi vya ufunuo huu ni, maana ya kuwa wa kwanza katika ufalme wa Mungu, jinsi ya kumpokea na hatimaye kuwa watumishi katika ufalme wake.
  
         Yesu anadhihirisha utambulisho wake kama Mwana wa Adamu (mtu). Katika Agano la Kale tunakuta maneno haya katika kitabu cha nabii Danieli na Ezekieli. Kulingana na Daniel Mwana huyu ni hali ya utukufu wa yule ambaye atakuja siku ya mwisho (Dan 7:13). Kulingana na toleo la Ezekieli maneno Mwana wa Mtu yanatumika kueleza ubinadamu na kifu chake (Ezk 2:1,3:1, 25, 17:2). Hii ni maana iliyotumiwa na Yesu ili kuongea kuhusu utambulisho wake kwa uhusiano na hali ya binadamu na fumbo la mateso, kifo na ufufuko wake kwa ajili ya wenye dhambi. Kulingana na injili ya Marko Yesu ni mwenye unyeti mbele ya hali ya ujinga na udhaifu wa wanafunzi wa kwanza; aliwafundisha polepole na kwa uvumilivu, akitumia mifano kadiri ya mazingira na akili zao na kufungua ufahamu wao ili waelewe mpango wa Mungu. Mtoto alijulishwa na Yesu ni tena sehemu ya ufundishaji na tabia yake ya ajabu.

         Watoto wadogo wana mahali maalum moyoni mwa Yesu. Alisema kwamba Ufalme wa Mungu ni wa watoto na mtu ambaye anataka kuingia katika Ufalme huu anapaswa kuwa kama wao. Siku hizi Yesu anatuongelea kwamba ni lazima mabadiliko ya mawazo na tabia ili tuweze kumfuata kwa kweli. Tena rejea kwa njia hii ni watoto wadogo ambao wana tabia kamili katika uhusiano wao na Mungu na wengine. Wanatusaidia kutafuta muhimu zaidi ya maisha yaani ukweli, unyenyekevu wa moyo, ufukara na imani kama mtoto mchanga kwa uhusiano na wazazi wake. Kama wanafunzi wa kwanza sisi pia hatupati kufahamu kila kitu kumhusu Yesu na mapendekezo yake, lakini ikiwa turuhusu, yeye anaweza kufungua akili zetu na kubadilisha mioyo yetu ilingane na matarajio yake. Ili mfano wa watoto wadogo utusaidie kufahamu nia za Yesu kuhusu maisha yetu na kukubali mapendekezo yake ili tupate uzima.

Fr Ndega

Mapitio: Sara

quinta-feira, 17 de setembro de 2015

KUJIKANA KUUCHUKUA MSALABA NA KUMFUATA YESU


Kutafakari kutoka Is 50:5-9; Mk 8:27-35

      Yesu alikuwa anatembea pamoja na wanafunzi wake na karibu na Kaisarea Filipi anawauliza maswali kuhusu utambulisho wake kulingana na mtazamo wa watu. Majibu yalikuwa ishara ya kwamba wazo kuhusu Yesu halikuwa wazi sana kwa upande wa watu. Ingawa halikuwa wazi kwa watu, kwa wafuasi wa Yesu lazima kuwe tofauti, kwa sababu kwa Yesu si muhimu sana yale ambayo watu wanafikiri, bali kukiri kwa wafuasi wake. Petro anadhihirisha yale ambayo wanafunzi wengine kumi na mmoja wanajua pia: Yesu ni masiya wa Mungu. Lakini hawawezi kutangaza habari hii kwa sababu ya kutokuwa na maana kamili. Yesu alitambua kwamba wafuasi wake walihitaji ufunuo zaidi na kujifunza vizuri maana ya umasiha wake na masharti kwa uanafunzi wa kweli.

         Mawazo ya wafuasi wa Yesu kuhusu masiya yalifuata matarajio ya wayahudi wengine, yaani, masiya wa kisiasa atakayetumia nguvu zake za kimungu ili kuwakomboa Wayahudi toka ukoloni wa Warumi. Bila shaka kwamba yesu anayakanusha mawazo hayo kwa kuonyesha njia tofauti ya kutimiza ujumbe wake wa masiya, ni kwamba, kupitia mateso, kifo na kufufuka. Umasiha ulichaguliwa na Yesu ni umasiha wa mtumishi mwema kulingana na Somo la kwanza. Utambulisho wa Mtumishi huyo ni kuwa makini kwa sauti ya Mungu ili aweze kufanya mapenzi yake kutumikia kabisa. Kwa kufanya mapenzi ya Mungu mtumishi huyo anapaswa kuteseka na kufa, lakini alisimama upande wa Mungu ambaye alimsaidia akimfanya mshindi. Pamoja na wazo wa wongo kuhusu umasiha wa Kristo, itikio la Petro lilidhihirisha pia baadhi ya upinzani dhidi ya njia ya maisha ambayo Yesu alichagua ili atimize mapenzi ya Mungu. Uamuzi wa Yesu ulikuwa katika ushirika na Baba yake na upinzani dhidi ya njia hii ni upinzani dhidi ya mapenzi ya Mungu.

    Wanafunzi wa kwanza walihitaji mwendo mrefu ili kujifunza kumhusu Yesu na kuyafahamu mapendekezo yake sawasawa. Wakati Yesu alimkemea Petro na kumwalika afuate mtazamo wa Mungu, alihitajika rejea za nguvu kwa uanafunzi wa kweli. Kidogo kidogo walitambua kwamba kwa kujitoa kama Yesu alivyo, walipaswa kuzifuata hatua tatu, yaani, kujikana wenyewe, kuichukwa misalaba yao na kumfuata Yesu. Kwa maneno mengine, walipaswa kuyabadilisha maisha yao kwa jumla. Kama hii ni lazima kuwa kwa sisi sote. Wale ambao hukutana na Yesu hawakubaki walivyo na hawawezi kumdai Yesu atende kulingana na mapendekezo yao. Mwendo lazima kuwa tofauti. Kwa kumfuata Yesu kweli tunapaswa kupatikana kwa kila kitu na kuweka ndani ya maisha yetu mapendekezo ya Yesu. Tunapaswa kufanya maisha yetu kulingana na njia ya Yesu ya kuishi  na kuchukua msalaba kama yeye alivyo.


      Injili ya Marko katika kifungu hiki inatusaidia kutafakari kuhusu njia ambayo tumechagua ili kumfuata Yesu. Je, hii ni njia ya kweli? Tunatambua kwamba Kumfuata Yesu hakuuleti upendeleo au hadhi, bali mateso na kujisalimisha kwa ajili ya injili. Basi, yeyote ambaye anataka kuishi shwari na bila ahadi hawezi kumfuata Yesu. Yeyote ambaye anatamani kumfuata Kristu bila msalaba hatamfuata Kristo kweli kamwe. Kupitia mambo hayo tunaweza kujiuliza maswali: Je, Kristu gani tumemfuata? Mawazo au kitu gani tunahitaji kujinyima bado ili tuweze kumfuata Yesu kikamilifu? Maisha yetu ya kawaida ni ishara ya kwamba tumekuta hazina yetu ya kweli? Ili Ekaristi hii takatifu itusaidie kuishi wito wetu wa wanafunzi wa Yesu kwa shauku na furaha. Ili ujumbe wa liturujia ya siku ya leo uiimarishe imani yetu na kutuhamasishe kumfuata Yesu kwa uaminifu na tayari kwa kila kitu kwa ajili ya injili, kwa ajili ya ufalme wa Mungu.

Fr Ndega
Mapitio: Sarah

domingo, 6 de setembro de 2015

HE HAS DONE WELL EVERYTHING


Reflection from Isaiah 35:4-7; Jas 2:1-5; Mk 7: 31-37

     According to the First reading, the People of Israel were exiled in Babylon and the prophet Isaiah announced new time, a time of liberation and joy.  According to the prophet that People was like blind person whom lived in the darkness of Babylon and didn’t get to see the way to go back home; they were like paralysed person whom is not able to use the own legs to leave the place where he didn’t feel well; and they were like deaf and dumb person because closed the ear to the Word of God. However God will come to save them because these people belong to God and he loves them. This marvellous action which God will perform to the people of Israel will be assumed later by Jesus for all humanity because he is the salvation of God for all. In the Second reading James invites the Christians to overcome the tendency of discrimination in the community and to value the presence of each one more than his/her economic condition or capacities. The person values for what he/she is.
      
       In the Gospel the good actions of Jesus are recognized by the people, whom exclaimed with enthusiasm, “He has done well everything!” he even causes the deaf to hear and the dumb to speak!” The presence of Jesus brings new time to the world. In him the Kingdom of God became a concrete reality, inviting all to participate. When he announced his mission in the synagogue of Nazareth, place where he was brought up, he was rejected. But he was most welcomed in the side of Galilee, place called Ten Towns. According to Mathew’s version, Galilee is considered Land of Gentiles (non-Jews). The presence of Jesus made the people, whom were in the “darkness”, to see a great light. Although these people had different tongue and customs in relating to Jews of the Judea, they also expected the Messiah anxiously. We get to understand this reality because the Gospel of Mark was written for the Christians of Roma and the objective of this gospel is to answer to the question “Who is Jesus?”. The answer to this question we find in the last moment of the human life of Jesus on the cross from the mouth of the roman army officer: “This man was really the Son of God!” 
       
      As Son of God, the objective of Jesus is to announce the salvation of God not only for some people, but for all. Jesus was a Jews, but not property of the Jews. The signs used by Jesus revealed that the salvation of God is not a plan for the future time only, but it starts in the history and exists for all. When we speak about the “chosen people” we want to mean the plan of wisdom of God whom uses some people in order to reach others more easily. Like this, from the people of Israel, Jesus and his collaborators reached also the ones whom aren’t Jews, proclaiming the good news of the Gospel. That man brought to Jesus had two problems: he was deaf and dumb. He suffered a lot and many times lived isolated because wasn’t able to communicate himself with his neighbours what he thought and desired, and others couldn’t dialogue with him. He desired to meet Jesus and to experience new life in order to perform good relationship with others. Before performing the miracle, Jesus looks at heaven because it is God only whom makes possible to heal the deaf-mute person. 
       

      As followers of Jesus, we are motivated by his decision and gestures. Our mission is continuity of his mission and like him, we are invited to do well everything. The deaf and dumb person is sign of our difficulty to listen to the Word of God and to proclaim it with fidelity. But through us, even with our weaknesses, Jesus continues doing wonders in the life of many people. The gospel doesn’t have borders; in the same way must be the good actions of the Christians. We are invited to overcome obstacles which prevent us to welcome others and to be sensible to their needs. After the people sow the miracle of Jesus and proclaimed it without ceasing, in the same way we must proclaim the wonders of God in order the people experience new life.

Fr Ndega

AMEFANYA MAMBO YOTE VEMA


Kutafakari kutoka Isaya 35:4-7; Yak 2:1-5; Mk 7: 31-37

       Kulingana na somo la kwanza, Watu wa Israeli walikuwa wafungwa katika Babiloni na nabii Isaya aliwatangaza wakati mpya, wakati wa ukombozi na furaha. Kulingana na nabii Watu hawa ni kama vipofu ambao wanaishi gizani mwa Babiloni na hawapati kuona njia ya kurudi nyumbani; tena wao ni kama walemavu ambao hawawezi kutumia miguu yenyewe ili kuacha mahali ambapo walikuwapo; pia wao ni kama viziwi na bubu kwa sababu waliyafunga masikio kwa Neno la Mungu. Hata hivyo Mungu atakuja kuwaokoa kwa sababu watu hawa ni mali yake na awapenda. Tendo hili la ajabu ambayo Mungu atatenda kwa ajili wa Watu wa Israeli yatachukuliwa na Yesu kwa watu wote kwa sababu yeye ni wokovu wa Mungu kwa wote. Katika somo la pili Yakobu anawaalika wakristo kushinda tabia ya ubaguzi katika jumuiya na kuthamini uwepo wa kila mtu zaidi kuliko hali au uwezo wake.

       Katika injili, matendo ya Yesu yanatambuliwa na watu ambao walitangaza, “amefanya yote vyema: amewajalia viziwi kusikia, na bubu kusema”. Uwepo wa Yesu umeleta wakati mpya ulimwenguni. Katika Yeye ufalme wa Mungu umekuwa hali halisi, ukiwaalika wote washiriki. Wakati aliutangaza ujumbe wake katika sunagogi ya Nazareti, mahali alipolelewa, alikataliwa. Lakini alikaribishwa sana katika upande wa ziwa Galilaya, mahali panapoitwa Dekapoli - yaani miji kumi. Kulingana na toleo la Mathayo, Galilaya ilifikiriwa “nchi ya watu wa mataifa”. Uwepo wa Yesu unawafanya watu waliokaa “gizani” waone mwanga mkubwa. Basi, ingawa watu hawa walikuwa na lugha na desturi tofauti kwa ushusiano na wayahudi wa Yudea, walimtarajia Masiya kwa hamu sana. Tunapata kufahamu hali hii kwa sababu Injili ya Marko iliandikwa kwa wakristu wa huko Roma na lengo la injili hii yote ni kujibu kwa swali “Yesu ni nani?”. Jibu kwa swali hili tunakuta katika wakati wa mwisho wa maisha ya Yesu kutoka midomo ya jemadari mmoja wa Roma: “Kweli mtu huyu alikuwa Mwana wa Mungu!”

      Kama Mwana wa Mungu, lengo la Yesu ni kutangaza wokovu wa Mungu si kwa watu fulani tu, bali kwa wote. Yesu alikuwa myahudi, bali hakawa mali ya Wayahudi. Ishara zilizotumiwa na Yesu zilidhihirisha kwamba wokovu wa Mungu si mpango kwa wakati ujao tu, bali unaanza katika historia na upo kwa wote. Wakati tunaongea kuhusu “watu waliochaguliwa” tunamaanisha mpango wa hekma ya Mungu ambaye anatumia baadhi ya watu ili kufikia wengine kwa urahisi. Kama hii, kutoka Waisraeli Yesu na washirika wake walifikia wasio na Wayahudi pia wakitangaza habari njema ya injili. Mtu yule aliletewa kwa Yesu alikuwa na matatizo mawili, yaani, alikuwa bubu na kiziwi. Aliteseka sana na mara nyingi alikuwa mpweke kwa sababu hakuweza kuwasiliana na wenzake kila alichofikiri au kutamani, na wao pia hawakueza kuzungumza naye. Alitamani kukutana na Yesu na kupitia maisha mapya ili kufanya uhusiano mwema na wengine. Kabla ya kufanya mwujiza Yesu anatazama juu mbinguni kwa maana ni Mungu peke aliyemwezesha kumponya Bubu kiziwi.


       Kama wafuasi wa Yesu tunahamasishwa na uamuzi na ishara zake. Ujumbe wetu ni mwendelezo wa ujumbe wake na kama yeye tunaalikwa kufanya mambo yote vema. Mtu bubu na kiziwi ni ishara ya ugumu wetu wa kusikiliza Neno la Mungu na kulitangaza kwa uaminifu. Lakini kupitia sisi hata kwa udhaifu wetu Yesu anaendelea kufanya mambo makuu maishani mwa watu wengi. Injili haina mpaka; vivyo hivyo ni matendo mema ya wakristo. Tunaalikwa kushinda vikwazo ambazo vinatuzuia kuwakaribisha wengine na kuwa na unyeti mbele ya mahitaji yao. Kama watu waliona mwujiza wa Yesu na kutangaza bila kuchoka, vivyo hivyo tunapaswa kutangaza makuu ya Mungu ili watu wengine wapate  maisha mapya.

Fr Ndega
Mapitio: Sara