quinta-feira, 17 de setembro de 2015

KUJIKANA KUUCHUKUA MSALABA NA KUMFUATA YESU


Kutafakari kutoka Is 50:5-9; Mk 8:27-35

      Yesu alikuwa anatembea pamoja na wanafunzi wake na karibu na Kaisarea Filipi anawauliza maswali kuhusu utambulisho wake kulingana na mtazamo wa watu. Majibu yalikuwa ishara ya kwamba wazo kuhusu Yesu halikuwa wazi sana kwa upande wa watu. Ingawa halikuwa wazi kwa watu, kwa wafuasi wa Yesu lazima kuwe tofauti, kwa sababu kwa Yesu si muhimu sana yale ambayo watu wanafikiri, bali kukiri kwa wafuasi wake. Petro anadhihirisha yale ambayo wanafunzi wengine kumi na mmoja wanajua pia: Yesu ni masiya wa Mungu. Lakini hawawezi kutangaza habari hii kwa sababu ya kutokuwa na maana kamili. Yesu alitambua kwamba wafuasi wake walihitaji ufunuo zaidi na kujifunza vizuri maana ya umasiha wake na masharti kwa uanafunzi wa kweli.

         Mawazo ya wafuasi wa Yesu kuhusu masiya yalifuata matarajio ya wayahudi wengine, yaani, masiya wa kisiasa atakayetumia nguvu zake za kimungu ili kuwakomboa Wayahudi toka ukoloni wa Warumi. Bila shaka kwamba yesu anayakanusha mawazo hayo kwa kuonyesha njia tofauti ya kutimiza ujumbe wake wa masiya, ni kwamba, kupitia mateso, kifo na kufufuka. Umasiha ulichaguliwa na Yesu ni umasiha wa mtumishi mwema kulingana na Somo la kwanza. Utambulisho wa Mtumishi huyo ni kuwa makini kwa sauti ya Mungu ili aweze kufanya mapenzi yake kutumikia kabisa. Kwa kufanya mapenzi ya Mungu mtumishi huyo anapaswa kuteseka na kufa, lakini alisimama upande wa Mungu ambaye alimsaidia akimfanya mshindi. Pamoja na wazo wa wongo kuhusu umasiha wa Kristo, itikio la Petro lilidhihirisha pia baadhi ya upinzani dhidi ya njia ya maisha ambayo Yesu alichagua ili atimize mapenzi ya Mungu. Uamuzi wa Yesu ulikuwa katika ushirika na Baba yake na upinzani dhidi ya njia hii ni upinzani dhidi ya mapenzi ya Mungu.

    Wanafunzi wa kwanza walihitaji mwendo mrefu ili kujifunza kumhusu Yesu na kuyafahamu mapendekezo yake sawasawa. Wakati Yesu alimkemea Petro na kumwalika afuate mtazamo wa Mungu, alihitajika rejea za nguvu kwa uanafunzi wa kweli. Kidogo kidogo walitambua kwamba kwa kujitoa kama Yesu alivyo, walipaswa kuzifuata hatua tatu, yaani, kujikana wenyewe, kuichukwa misalaba yao na kumfuata Yesu. Kwa maneno mengine, walipaswa kuyabadilisha maisha yao kwa jumla. Kama hii ni lazima kuwa kwa sisi sote. Wale ambao hukutana na Yesu hawakubaki walivyo na hawawezi kumdai Yesu atende kulingana na mapendekezo yao. Mwendo lazima kuwa tofauti. Kwa kumfuata Yesu kweli tunapaswa kupatikana kwa kila kitu na kuweka ndani ya maisha yetu mapendekezo ya Yesu. Tunapaswa kufanya maisha yetu kulingana na njia ya Yesu ya kuishi  na kuchukua msalaba kama yeye alivyo.


      Injili ya Marko katika kifungu hiki inatusaidia kutafakari kuhusu njia ambayo tumechagua ili kumfuata Yesu. Je, hii ni njia ya kweli? Tunatambua kwamba Kumfuata Yesu hakuuleti upendeleo au hadhi, bali mateso na kujisalimisha kwa ajili ya injili. Basi, yeyote ambaye anataka kuishi shwari na bila ahadi hawezi kumfuata Yesu. Yeyote ambaye anatamani kumfuata Kristu bila msalaba hatamfuata Kristo kweli kamwe. Kupitia mambo hayo tunaweza kujiuliza maswali: Je, Kristu gani tumemfuata? Mawazo au kitu gani tunahitaji kujinyima bado ili tuweze kumfuata Yesu kikamilifu? Maisha yetu ya kawaida ni ishara ya kwamba tumekuta hazina yetu ya kweli? Ili Ekaristi hii takatifu itusaidie kuishi wito wetu wa wanafunzi wa Yesu kwa shauku na furaha. Ili ujumbe wa liturujia ya siku ya leo uiimarishe imani yetu na kutuhamasishe kumfuata Yesu kwa uaminifu na tayari kwa kila kitu kwa ajili ya injili, kwa ajili ya ufalme wa Mungu.

Fr Ndega
Mapitio: Sarah

Nenhum comentário: