domingo, 20 de setembro de 2015

UFUNDISHAJI NA TABIA YA AJABU


Wis 2:12.17; Jas 3: 16-4:3; Mk 9,30-37


       Kifungu hiki kutokana na kitabu cha Hekima ya Sulemani kinaongea kuhusu ushuhuda muhimu wa mtu mwenye haki na upinzani wa wale ambao hawaukubali ushuhuda wake na wanamtendea vibaya, kupanga mauti yake. Hali hii inatokea kwa sababu ya njia ya maisha yake kulingana na mapenzi ya Mungu. Njia hii inawasikitisha wale wanaopendelea kuishi vibaya, mbali na Mungu. Hata hivyo, mtu huyo mwenye haki ni mwana wa Mungu, na Mungu mwenyewe atamtegemeza na kumwokoa mikononi mwa adui zake. Hii ni ishara ya Kristo, aliye Mwana wa Mungu kwa namna ya pekee kabisa. Yeye, katika uaminifu wake kwa mpango wa Mungu, alipata wokovu hata kwa wale waliwakandamiza wengine. Somo la pili linasema kuwa hekima ambayo inasababisha kujua kamili inatoka kwa juu kwa sababu ni Mungu mwenyewe chanzo cha hekima ya kweli. Mtu anayeongozwa na hekima hii anaweza kuwa mwenye moyo safi, tena ni mtu wa amani, ya upole, tayari kusikiliza maneno ya watu na kutenda mema kwa ajili yao.

         Injili ni mwendelezo wa tangazo la Petro kuhusu utambulisho wa Yesu na mwaliko wa Yesu mwenyewe kwa wafuasi wake wamfuate katika kujisalimisha kwake ili wapate uzima. Yesu alitambua kwamba wakahitaji kujua zaidi kuhusu maana ya umasiha wake na kuyafahamu vizuri mapendekezo yake. Kwa hivyo alitumia kipindi maalum kuwafundisha peke yao kuhusu maana kamili ya umasiha aliochagua na uanafunzi. Hakutaka watu wafahamu alipo. Yesu alijaribu tena kuongea na wanafunzi kuhusu mateso, kifo na ufufuko wake, lakini walionekana mbali sana na mwalimu. Hawakuelewa tena kwa sababu walishughulika sana kwa mawazo na nia tofauti. Hata hivyo Yesu anatumia mifano ili waweze kufahamu ufunuo wake. Vipengele vya msingi vya ufunuo huu ni, maana ya kuwa wa kwanza katika ufalme wa Mungu, jinsi ya kumpokea na hatimaye kuwa watumishi katika ufalme wake.
  
         Yesu anadhihirisha utambulisho wake kama Mwana wa Adamu (mtu). Katika Agano la Kale tunakuta maneno haya katika kitabu cha nabii Danieli na Ezekieli. Kulingana na Daniel Mwana huyu ni hali ya utukufu wa yule ambaye atakuja siku ya mwisho (Dan 7:13). Kulingana na toleo la Ezekieli maneno Mwana wa Mtu yanatumika kueleza ubinadamu na kifu chake (Ezk 2:1,3:1, 25, 17:2). Hii ni maana iliyotumiwa na Yesu ili kuongea kuhusu utambulisho wake kwa uhusiano na hali ya binadamu na fumbo la mateso, kifo na ufufuko wake kwa ajili ya wenye dhambi. Kulingana na injili ya Marko Yesu ni mwenye unyeti mbele ya hali ya ujinga na udhaifu wa wanafunzi wa kwanza; aliwafundisha polepole na kwa uvumilivu, akitumia mifano kadiri ya mazingira na akili zao na kufungua ufahamu wao ili waelewe mpango wa Mungu. Mtoto alijulishwa na Yesu ni tena sehemu ya ufundishaji na tabia yake ya ajabu.

         Watoto wadogo wana mahali maalum moyoni mwa Yesu. Alisema kwamba Ufalme wa Mungu ni wa watoto na mtu ambaye anataka kuingia katika Ufalme huu anapaswa kuwa kama wao. Siku hizi Yesu anatuongelea kwamba ni lazima mabadiliko ya mawazo na tabia ili tuweze kumfuata kwa kweli. Tena rejea kwa njia hii ni watoto wadogo ambao wana tabia kamili katika uhusiano wao na Mungu na wengine. Wanatusaidia kutafuta muhimu zaidi ya maisha yaani ukweli, unyenyekevu wa moyo, ufukara na imani kama mtoto mchanga kwa uhusiano na wazazi wake. Kama wanafunzi wa kwanza sisi pia hatupati kufahamu kila kitu kumhusu Yesu na mapendekezo yake, lakini ikiwa turuhusu, yeye anaweza kufungua akili zetu na kubadilisha mioyo yetu ilingane na matarajio yake. Ili mfano wa watoto wadogo utusaidie kufahamu nia za Yesu kuhusu maisha yetu na kukubali mapendekezo yake ili tupate uzima.

Fr Ndega

Mapitio: Sara

Nenhum comentário: