sábado, 22 de junho de 2019

DATEGLI VOI STESSI DA MANGIARE



Riflessione a partire di Lc 9,11b-17



   Celebriamo oggi la festa del Corpo e Sangue di Cristo, la festa popolare dell’Eucaristia. Diversamente dal Giovedì Santo in cui abbiamo un clima più di raccoglimento e riflessione, oggi è un giorno di festa e di intensa gioia in cui esprimiamo pubblicamente la nostra fede nell’eucaristia, presenza reale di Gesù tra noi. Il Concilio Vaticano II definisce l’Eucaristia “Sorgente e finalità di tutta la vita e missione della Chiesa”. Le letture parlano della relazione che esiste tra Eucaristia e Vita, tra il Pane che è Cristo e il pane che alimenta il corpo. Non è possibile entrare in comunione con il Corpo del Signore senza vivere la fraternità, la solidarietà e la condivisione. 

     Il primo brano ci presenta la figura del re e sacerdote Melchisedek, che offre ad Abramo pane e vino, dopo averlo benedetto nel nome del Signore. Questo sacerdote è considerato figura di Cristo sommo ed eterno sacerdote. Anche se appartiene a un popolo diverso da quello di Abramo, ha saputo condividere, sentirsi fratello. Questa è la esperienza che ogni Eucaristia ci fa vivere.

     Nel secondo brano Paolo racconta l’Istituzione dell’Eucaristia, facendo memoria del grande dono fatto dal Signore mentre mangiava con i suoi in un clima di famiglia, di intimità, di confidenza e di accoglienza. Tutti questi valori erano incompatibili con le discordie e divisioni che la comunità di Corinto stava affrontando. Dobbiamo stare attenti perché il nostro modo di comportarci nel quotidiano non sia una negazione del Cristo che celebriamo e riceviamo nell’eucaristia.

       Nel Vangelo ci viene presentata la moltiplicazione dei pani secondo Luca. Con il suo racconto, l’evangelista ci spiega cosa significa ‘spezzare il pane’ nel giorno del Signore. Quello che richiama la nostra attenzione all’inizio del brano è che Gesù accoglie le folle e annuncia loro il Regno di Dio con parole e gesti. Le parole di Gesù sono “la risposta di Dio al bisogno di pienezza che ognuno si porta dentro”; e i suoi gesti agiscono per sanare, per guarire per donare vita nuova.

     Gesù condanna l’indifferenza dei discepoli che gli consigliano di congedare la gente affinché provveda per proprio conto a procurarsi il cibo. La risposta di Gesù: ‘Voi stessi date loro da mangiare’ non indica soltanto dare qualcosa perché il popolo possa mangiare ma anche un darsi in alimento come Gesù fa. Così ogni persona che mangia Gesù diventa a sua volta eucaristia, cioè, dono per gli altri coltivando gli stessi sentimenti di Gesù. Con Gesù non si impara a moltiplicare pani ma a condividere con i fratelli quello che si ha e quello che si è.

      Celebrare veramente l’Eucaristia è accogliere Gesù e essere trasformati in colui che riceviamo. Questo ci fa superare ogni indifferenza riguardo gli altri. Colpiti dall’amore del Sacro Cuore, dopo ogni Eucaristia celebrata, siamo inviati ad essere moltiplicatori di quest’amore, attenti a chi soffre. “Attraverso la condivisione del pane si risolve il problema della fame. Finché le persone trattengono i doni per sé, c’è l’ingiustizia e c’è la fame; quando quello che si ha non si considera esclusivamente proprio ma lo si condivide per moltiplicare l’azione creatrice del Padre si crea la sazietà si crea la abbondanza”. Che la celebrazione del Corpo e il Sangue del Signore ci motivi ad essere quello che siamo chiamati a vivere: un solo corpo veramente unito nel quale tutte le divisioni siano superate.

Fr Ndega
Revisione dell'italiano: Giusi

sábado, 15 de junho de 2019

UMOJA WA UTATU MTAKATIFU NI CHEMCHEMI YA UMOJA WETU



Mit 8: 22-31; Rum 5: 1-5; Yoh 16,12-15



      Utatu Mtakatifu ni fumbo la Mungu aliye ushirika wa Baba na Mwana na Roho Mtakatifu, yaani fumbo la upendo. Upendo ni utambulisho wa Mungu. Hivyo, “Mungu ni Utatu kwa sababu ndiye upendo”. Yeye ni Mungu wa kipekee lakini haishi peke yake kwa sababu alitaka kuwa ushirika wa upendo. Uumbaji wote ni uenezi wa nafsi yake na fumbo lake. Viumbe vyote vinaitwa kuingia katika ushirika huu wa upendo na kuwa maonyesho ya wema wake. Tunaposema ishara ya msalaba, yaani, “Kwa jina la Baba na la Mwana na la Roho Mtakatifu”, tunakiri kwamba nafsi yetu ndiyo makao ya uwepo maalum tangu ubatizo wetu. Ndio uwepo wa upendo na kutuomba uhusiano wa upendo nawe. Inawezekaje Mungu Mkubwa mno akae ndani yetu wadogo mno?

    Hilo ndilo fumbo kubwa kuliko yote ya imani yetu. Kutoka ufunuo wa Yesu tunapata kujifunza mengi na kuendelea kwa msaada wa Roho Mtakatifu ili tujihisi kuhusishwa katika fumbo hili hata bila kufahamu kamili. Kuna hadithi fulani inayoongea zaidi kuhusu hali hii: “Siku moja Mtakatifu Agostino alikuwa akitembea katika pwani ya bahari, akijiuliza swali kuhusu fumbo la Utatu Mtakatifu, akisema, “inawezekanaje Mungu kuwako kama Mmoja na Utatu wakati huo huo? Ghafla, alimwona mtoto mdogo aliyefanya shimo katika mchanga na kukimbia kwenye bahari, akichukua maji kidogo na kuyaweka shimoni. Baada ya kuangalia mchezo huu wa mtoto mdogo kwa mara nyingi, Agostino aliamua kumwuliza maana ya mchezo huo. Mtoto mdogo akamjibu akisema: “Najaribu kuweka maji yale yote ndani ya shimo hii”. Ameshangaa sana, Agostino akasema: “Hutapata kufanya hivyo kamwe!” Kisha, mtoto mdogo akamwambia akisema: “ni rahisi kwangu kuyaweka maji yale yote shimoni kuliko wewe ukapate kufahamu fumbo la Utatu Mtakatifu kwa akili yako. Mwishowe, mtoto mdogo alitoweka na Mtakatifu Agostino akajiambia mwenyewe: “Labda mtoto huyo alikuwa malaika fulani!”

      Hadithi hii inatufundisha hali muhimu sana, yaani, fumbo la Utatu Mtakatifu sio fumbo la kufahamika bali la kukaribishwa. Ikiwa tunajifungua zaidi kwa fumbo hili tunaweza kuhisi zaidi fumbo hili ndani yetu. Ujumbe wa masomo ya leo unatusaidia katika mwendo huu. Katika somo la kwanza hekima anajifunua kama nafsi ya Mungu. Hekima hii ni Mwana wa Mungu ambaye yuko pamoja na Mungu milele na kutenda naye kabla ya kuumbwa ulimwengu. Yeye ni Akili ya Mungu na viumbe vyote vilivyokuwako viliumbwa kwa njia yake, pamoja naye na ndani yake. Yeye ni ukamilifu wa viumbe vyote. Somo la pili linatuambia kwamba Mwana alitushirikisha katika utukufu wake na Baba. Kupitia yeye tulipewa Roho Mtakatifu ili tuishi kama watoto. Tendo la Roho huyu limemimina mioyoni mwetu pendo la Mungu likithibitisha kwamba sisi ni watoto wake na hivyo tunaweza kumwita Baba yetu kwa uhuru kabisa. Ikiwa sisi ni watoto sisi pia ni warithi pamoja na Yesu kwa kupokea uhai wake wa kimungu. Ndiyo hali hii ambayo ubatizo wetu unatufanya kuishi.
    
      Umuhimu wa ujumbe ambao Yesu ametukabidhi ni kwamba yeye ndiye ukweli wa Baba na kutenda kwa Roho Mtakatifu. Mungu ndiye Utatu na hutenda pamoja kwa ushirikiano kamili. Yesu, aliyetumwa na Mungu Baba, alitangaza ukweli akiwahusisha watu katika ushirika sawasawa anaoishi Baba na Roho Mtakatifu. Utimizaji wa ahadi kuhusu ujio wa Roho huyo unatuhakikishia umoja wetu, kutuunganisha kama wana wa familia moja. Kupitia Roho huyo tunaangazika ili tuweze kukumbuka mafundisho ya Yesu na kuyatangaza kwa uaminifu. Wakati sisi hupendana tunaonyesha ukweli wa uhusiano wetu na Mungu na hali ya Mungu mwenyewe kama Utatu Mtakatifu. Tunapoishi uhusiano wa kweli na Yesu vivyo hivyo tunahisi ndani yetu tendo la Baba na Roho wake. Uzoefu wetu wa Yesu katika Ekaristi ni uzoefu wa Utatu Mtakatifu. Mungu anatumikia anakaa kati yetu na ndani yetu. Yeye anatuunganisha naye na miongoni mwetu. Hili ni fumbo la ushirika ambao Mungu ametuhusisha kwa maana anataka tuwe washiriki katika uhai wake mwenyewe. Kwa hivyo, tuombe atukuzwe Mungu Baba na Mwana na Roho Mtakatifu...

Fr Ndega

domingo, 2 de junho de 2019

YESU ANATENDA PAMOJA NA WANAFUNZI WAKE KUPITIA ROHO WAKE



Kutafakari kuhusu Mdo 1, 1-11; Waef 1, 17-23; Lk 24, 46-53



     Siku ya leo tunasherehekea kupaa kwa Bwana wetu Yesu Kristo. Yeye alifanya kazi miongoni mwa wanadamu kwa miaka mitatu. Kupaa ni hitimisho ya kazi yake, lakini anaendelea kuwepo ulimwenguni kupitia Roho wake. Basi, sikukuu hii inatufafanulia fumbo la kuaga na uwepo wa Yesu kwa sababu yeye hakumwacha Baba alipokuja kwetu wala hakutuacha alipomrudia Baba. Kupaa kwake kunaongea kuhusu njia mpya ya uwepo wake miongoni mwetu kwa kutangaza hatua mpya ya kazi yake. Huu ni wakati wa Kanisa lililo jumuiya ya wanafunzi wa Yesu. Ujumbe muhimu kuhusu hali hii ni wazi sana hasa katika maandiko mawili ya Luka, yaani, Injili na kitabu cha Matendo ya Mitume. Katika Injili yeye anajulisha vitendo vya Yesu, na katika Matendo ya Mitume anajulisha vitendo vya wanafunzi wake waliosaidiwa na Roho wake Mtakatifu.    

     Kuonekana kwa Yesu kwa muda fulani kuwaimarisha wanafunzi wake kugundua tena maana ya uanafunzi, wakishinda hofu na mashaka kuhusu hali ya ufufuko wake. Uzoefu huo ulikuwa mpya sana kwao naye Yesu alifahamu kwamba alipaswa kuwa na utulivu kwa sababu ya imani yao ndogo. Mwendo ulikuwa wa muda mrefu, lakini wenye ufanisi sana, ukisababisha mabadiliko makubwa maishani mwa wanafunzi, yaani, kutokana na uzoefu wa wanaume wenye hofu kuwa mashahidi wenye ujasiri.

    Katika maneno yake ya mwisho, Yesu aliwasaidia kufahamu uhusiano kati ya yale aliyoyatenda na kufundisha na yale yaliyoandikwa na manabii wa zamani. Habari ya toba na ondoleo la dhambi linapaswa kuwa umuhimu wa ujumbe wa waliotumwa kwa jina la Yesu aliye uso wa huruma ya Mungu Asiyeonekana. Uzoefu wao na Yesu uliwawezesha kuwa wanafunzi wa kweli, lakini walipaswa kuingoja nguvu kutoka juu ili waweze kuwa mashahidi wa Bwana Yesu tangu Yerusalemu mpaka mwisho wa nchi. Roho mmoja aliyekuwepo katika mwanzo wa uumbaji na wakati wa utume wa Yesu ataiongoza kazi ya wanafunzi wake.

       Yesu aliyashiriki mamlaka yake na wanafunzi wake ili wawatumikie watu, wakiwatendea mema. Kutokana na mfano wa kujisalimisha kwa Kristo ushuhuda wao wa kwanza ni kujitolea bila kipimo. Wanafunzi  walitumwa kama wajumbe wa habari njema kwa mataifa yote kwa sababu injili haina mpaka. Yesu alikuwa amewaahidia kuandamana nao mpaka upeo. Ingawa uwepo wake wa kimwili hauwezi kuonekana tena, Roho wake anawahakikishia kwamba hawatendi peke yao katika kazi. Uwepo wa Roho wa Yesu ulifanya maneno yao yawe ufanisi kupitia ishara nyingi na matendo mazuri.

      Kulingana na Mtakatifu Paulo, Roho ambaye aliwapewa kwa jumuiya ya kwanza ni Roho wa umoja. Kupitia Roho huyo tunaweza kumjua Mungu vizuri na kuishi katika umoja miongoni mwetu kama anavyotarajia Bwana wetu. Kila mtu anaitwa kuchukua ahadi hii ya umoja kama maana ya utambulisho. Katika jumuiya ya Kikristo tumezipokea zawadi nyingi kutoka kwa Mungu ili tuwe zawadi sisi kwa sisi, na kusaidia kujenga mwili mmoja, ambao ni takatifu na hai kwa sababu ni Roho mmoja anayetenda ndani yake. Hili ni fumbo la uwepo wa Yesu katika kanisa lake ambalo ni mwili wake mwenyewe naye yu kichwa cha mwili huu.

    Malaika waliwaambia wanafunzi wa kwanza na kutuambia pia siku ya leo: “mbona mmesimama mkitazama mbinguni?” Hakika kama Wakristo tunahitaji kurudisha mtazamo wetu kwa Yesu aliye mfano wetu na kichwa chetu ili tuendelee kazi yake kwa uaminifu, lakini hatuwezi Kubaki wamesimama kutazama mbinguni kama ishara ya uvivu na utazamaji na kipooza. Bwana anatutaka tuwe waangalifu na wenye ufanisi kama ilivyoandikwa: “Wabarikiwa watumishi wale ambao watakuwa wakitumikia Bwana wao atakaporudi”. Maisha ya Kikristu ni kutafakari na kitendo, imani na matendo. Ishara za uwepo ufanisi wa Yesu zinaonyeshwa kupitia mapendo ya wale wanaomwamini na kuzifuata nyayo zake. Roho Mtakatifu afanye uwepo wa Yesu uwe ufanisi katika maisha yetu na kazi zetu ili tuendelee utume wake kwa uaminifu.  

Fr Ndega