domingo, 27 de dezembro de 2015

FAMILIA TAKATIFU, YESU, MARIA NA YUSUFU


Kutafakari kutoka YbS. 3,2-6, 12-14; Wak 3, 12-21; Lk 2: 41-52


   Tunasherehekea Jumapili ya Familia Takatifu Yesu, Maria na Yosefu. Sikukuu hii inatukumbusha kwanza kuhusu mkutano wa wachungaji na Maria Yusufu, na Mtoto mchanga amelala horini. Hakika kutembelea huku kulisababisha kutafakari kubwa mioyoni mwa Maria. Sikukuu hii inataja pia ushiriki wa familia takatifu katika hekalu ya Yerusalemu. Tukio hili liliwasaidia wazazi wa mtoto Yesu kujua kidogo zaidi kuhusu hazina kubwa ambayo aliwakabidhi Mungu. Hasa kwa upande wa Mama Maria hii ilikuwa nafasi maalum ya kutafakari kuhusu mpango wa Mungu. Hii ni nafasi pia ya kutafakari kusuhu maana ya familia za binadamu na mahitaji ya kuishi thamani nyingi za Familia takatifu ambazo zinampendeza Mungu na kuisaidia jamii.       
        Ushiriki wa Familia takatifu (Yesu, Maria na Yosefu) katika jumuiya yake ni kielelezo/hamasa kwa Ushiriki wetu katika jumuiya/kanisa. Kulingana na andiko hili la Luka ushiriki wa familia hii ulikuwa desturi. Miongoni mwa Wayahudi kila Myahudi anapaswa kwenda Yerusalemu angalau mara moja kwa mwaka kwa sababu ya sherehe ya pasaka pamoja na wengine. Yesu alikuwa kijana wa umri wa miaka kumi na miwili, na ilionekana alipotea hekaluni, lakini kwa kweli yeye alijikuta mwenyewe kwa sababu inampendeza kuhusishwa na kushughulika kuhusu hali ya Baba yake. Hali hii ilikuwa ngumu sana kwa Maria na Yosufu wafahamu. Hasa Mariamu, ingawa hakufahamu hali hii, alikuwa na tabia nzuri ya kuweka moyoni mwake matukio muhimu, akitafakari na kutafsiri ili atende mapenzi ya Mungu. Maria alikuwa makini sana kwa matendo ya Mungu katika historia ya watu wake. Moyo wake ulikuwa makao ya Mungu, mahali pa kwanza, ambapo Yesu alizaliwa. Kwa hivyo haikuwa ngumu sana kwa yeye kuishi ushirika wa ndani na moyo wa mwana wake Yesu.
       Sehemu ya mwisho ya injili hii inasema kwamba Yesu alirudi Nazareti pamoja na wazazi wake na alikuwa akiwatii. Hii ilikuwa njia yake ya kuishi ambayo inampendeza Mungu na ni mfano kwa wanadamu wote. Kuhusu hayo somo la kwanza pia linathibitisha umuhimu wa uhusiano wa ndani kati ya wana wa familia, kufikiria watoto kama baraka kwa wazazi. kuwatii na kuwaheshimu wazazi kunayahusu mapenzi ya Mungu na kunazivutia baraka nyingi kwa familia. Kulingana na Mt Paulo mifano ya Kristo ya utii na upendo lazima kuwa kipimo cha uhusiano kati ya wanandoa kwa sababu thamani hizi zinampendeza Mungu na zinawahamasisha watoto katika safari yao. Familia inampedeza Mungu ambaye, tangu mwanzo, alimpanga binadamu kwa mfano wake, akisema: “Si vizuri huyu mwanamume kuwa peke yake. Nitamfanyia msaidizi wa kumfaa”. Basi Uumbaji wa wanadamu ulikuwa mwaliko kwa kuishi katika familia. Ni mapenzi ya Mungu waweze kuwa pamoja, kupendana na kusaidiana. Kwa nini familia ni muhimu sana? Kwa sababu familia ni msingi wa uzoefu wa binadamu; Kwa sababu pasipo familia uimara wa jamii hauwezekani. Kwa sababu bila familia mawasiliano ya thamani ya jamii kizazi kwa kizazi hayawezekani. Kwa maana uhusiano kati ya wazazi na watoto unawafanya kuwajibika na kukomaa zaidi. Kwa sababu bora kuliko chochote, familia inayaridhisha mahitaji ya hisia na fizikia/mwili, kuwapa watoto utoto salama na imara.
      Yesu anapenda sana kushiriki katika maisha ya familia. Yeye alizaliwa katika familia moja na kutokana na makao ya Nazareti alibariki familia zote za ulimwengu. Uwepo wake ni ufanisi ili familia  zetu zifikie lengo lao kulingana na utambulisho asili. Kumheshimu Maria, mama yake, kunatusaidia kutambua uwepo na matendo ya Mwanawe katika familia ili ishinde hofu, changamoto taabu na majaribio mengi, hasa majaribio ya uzinzi na talaka. Jukumu la Yosefu pia ni chanzo cha msukumo kwa akina baba wote ili wawe ishara za ulinzi na utunzaji wa Mungu, kuzaa hali ya usalama na utulivu katika familia. Uwepo wa Yesu, Maria na Yusufu unaiweka wakfu familia ukiifanya takatifu. Familia ni mahali pa kumcha Mungu; basi, ni mahali patakatifu. Baba Mt Yohane Paulo II alisema kwamba ni lazima kuiokoa familia. Nasi tunaweza kufanya hivyo hasa kwa kuziheshimu na kuzisaidia thamani ambazo zinaishiwa katika familia na zinatufanya binadamu wa kweli.
Fr Ndega

Mapitio: Sara 

SIKUKUU YA KUZALIWA KWAKE BWANA


Kutafakari kuhusu Luka 2, 1-14

Kulingana na liturujia ya siku hii takatifu, ujumbe kuhusu kuzaliwa kwa Yesu ni ujumbe wa furaha kubwa kwa wote, kwa sababu Mwokozi amezaliwa kwa wote. Tufurahi kwa sababu Mungu anatupenda, yeye yupo kati yetu na analeta wokovu kwetu. Wokovu ni kazi ya Mungu, lakini unatendeka duniani na ushiriki wa binadamu. Basi tuchukue Mariamu na Yusufu kama mifano. Katika tukio hilo la ajabu na unyenyekevu wa watu waliohusishwa, Mungu alidhihirisha njia yake yenyewe ya kutenda. Hali hii inathibitisha msemo wa Afrika ambao husema, “watu wanyenyekevu, kufanya vitu rahisi na katika mahali rahisi wana uwezo wa kubadilisha ulimwengu.” Mabadiliko makubwa ambayo jamii yetu inahitaji lazima kutokea ndani ya mwanadamu. Jamii mpya itatokea wakati kila mtu atatambua mahitaji ya kujibadilisha mwenyewe zaidi kuliko ajaribu kubadilisha wengine. Kulingana na Baba Mtakatifu Francisco, “Dunia itabadilika ikiwa tuanze kubadilisha matendo yetu kupitia tabia zetu na chaguzi zetu.” Kwa hiyo, Krismasi ni wakati wa kubadilisha tabia na chaguzi zetu.
Katika Yesu, Mungu amekuwa mmoja wetu, kuchukua hali halisi yetu ya binadamu na kulitoa pendekezo mpya la maisha. Kwa hivyo haitoshi kukiri katika Yesu wokovu wa Mungu; ni muhimu turuhusu kuongozwa na ujumbe wake wa amani na upendo. Kuzaliwa kwa Yesu kuliwabadilisha binadamu wote katika familia kwa njia ya kipekee, kujaza mioyo ya watu kwa furaha na matumaini. Kwa kweli, Mungu anajifunua kama jirani, maskini na anayekataliwa, kualika tutambue thamani ya ishara ndogo na miradi midogo. Bila shaka chaguo hili la Mungu linatuaibisha, kutualika kufikiri na kutenda tofauti. Kupitia udogo Mungu hufanya makuu. Hivyo, Krismasi ni wakati wa kubadilisha mawazo wetu.
Kipengele kingine cha kutafakari kwetu katika usiku huu ni kuhusu wachungaji, waliokuwa watu wa kawaida wadharauliwa katika jamii. Wachungaji walikuwa watu waangalifu ambao walichunga wanyama wao karibu na Bethlehem wakati wa usiku. Walikuwa kweli waangalifu kwa sababu ndani yao hisia kuhusu Mungu na ukaribu wake ulikuwa hai sana. Wachungaji walikuwa watu wa kwanza kuupokea ujumbe mkubwa wa furaha kwa sababu mioyo yao ilikuwa macho. Yeyote tu aliye na moyo makini ana uwezo wa kuamini katika habari njema na kutarajia hali nzuri katika kila alfajiri mpya. Mtu tu aliye na moyo makini ana ujasiri wa kuanza safari kwa kukutana na Mungu katika mahali pasipotarajiwa, yaani katika hali ya mtoto mdogo na mahali maskini sana. Hivyo, Krismasi ni wakati wa kuangalia tofauti ili kuona zaidi na kufanya tofauti katika maisha ya watu wengi.
Mungu Mwenyezi anakubali hali ya mtoto mdogo, katika utegemezi kabisa na utunzaji na upendo wa binadamu. Imani inatuongoza kumtambua mtoto huyu mdogo wa Bethlehemu katika kila mtoto ambaye sisi hukutana katika safari yetu ya kila siku. Kila mtoto anaomba upendo wetu. Tufikiri leo, kwa njia maalum, kuhusu baadhi ya watoto ambao hawana uzoefu wa upendo wa wazazi wao; kuhusu pia watoto wa mitaani ambao hawana mahali pa kuishi; kuhusu watoto ambao wanatumika kama askari, wanaobadilishwa katika vyombo vya vurugu, badala ya kuwa vyombo ya upatanisho na amani; tena kuhusu watoto ambao ni waathirika wa unyanyasaji wa kijinsia, na kuhusu watoto maskini waliolazimishwa kuziacha ndoto zao kwa sababu ya hali mbaya ya kiuchumi. Mtoto mdogo wa Bethlehemu ni mapitio mapya ili tuweze kujitoa ili dhiki ya watoto hawa ikomeshwe. Mwanga wa Bethlehemu uguse mioyo yetu, kuifanya yenye unyeti kwa hali hii. Hivyo, Krismasi ni wakati wa utunzaji na upendo kwa walio na mahitaji mengi.
Ingawa sisi huishi katika jamii ya ulaji ambayo inatuzuia kushughulika kwa thamani muhimu sana, tunapaswa kuwa macho. Krismasi si ulaji. Ni sikukuu ya ufunuo wa Fumbo la upendo wa Mungu unaobadilisha moyo wa binadamu na kuufanya wenye unyeti kwa mapitio ya Mungu. Mungu anatupenda bure na kwa ukarimu, bila astahili kwa upande wetu. Uzoefu huu lazima kutuongoza tufanye vile vile anavyofanya. Kama hii, Krismasi itakuwa zaidi kuliko kipindi kimoja kwa mwaka. Itakuwa Krismasi daima ikiwa tujifunze kupenda kweli na kuweka juhudi zaidi kwa kujenga jamii ya ndugu na haki kwa wema wa wote.

Fr Ndega

Mapitio: Sara

domingo, 20 de dezembro de 2015

UTUMISHI NA UKARIMU WA BIKIRA MARIA


Kutafakari kuhusu 5,2-4; Waebrania 10, 5-10; Luka 1:39-45

      Liturujia ya jumapili hii inatujulisha mtu muhimu sana kama kielelezo cha matayarisho na makaribisho kwa Yule atakayekuja, yaani Bikira Maria. Mkutano wake na dada yake Elizabeti ni alama ya mambo makuu ya Mungu ambaye ana mtazamo maalum kwa hali ya wanyenyekevu na maskini. Kutokana na hali hii alidhihirisha fumbo la mapenzi yake. Anawatumia waliopatikana ili mipango yake yatimize. Katika somo la kwanza nabii Mika anatangaza kuzaliwa kwa mkombozi mmoja kwa Waisraeli atakayetawala milele kwa nguvu za Bwana. Yeye ni mfano wa mwokozi wetu Yesu Kristo aliyekuja kwa ajili ya ulimwengu wote akifanya mapenzi ya Mungu, kulingana na ujumbe wa Waraka kwa Waebrania. Kupitia kujisalimisha kwake mara moja tu tumepata utakaso na wokovu. 
    
     Alipoelewa mpango wa Mungu katika maisha yake Maria alijibu: “Mimi ni mjakazi wa Bwana, nitendewe kulingana na neno lako”. Hili lilikuwa jibu la ajabu la Bikira Maria mbele ya tangazo la Malaika Gabrieli. Wito wa Maria ni maonyesho ya ukarimu wa Mungu. Ukarimu wa Bwana ulihamasisha ukarimu wa mtumishi wake aliyeenda kwa haraka kutembelea dada yake Elisabeti ambaye pia alikuwa amepata mimba na alikaribia kuzaa kwani ilibaki miezi mitatu. Mkutano wa wanawake wawili ni mkutano wa agano, yaani Agano la Kale linalikaribisha Agano Jipya. Kuna pia mkutano wa vizazi, yaani mzee anamkaribisha kijana na kijana anamtumikia mzee. Mpango wa Mungu unajumuisha vizazi vyote na kila kizazi kinaalikwa kuchukua ujumbe wake kulingana na mwendo wake wenyewe. Tukio hili la wanawake hawa wawili linaonyesha njia maalum ya Mungu ya kutenda, dhidi ya matarajio ya binadamu, ni kwamba, mwanamke asiyezaa anakuwa mwenye rutuba na mwanamke bikira anapata mimba kwa njia ya ajabu.

    Maria alitaka kushiriki furaha ya Elizabeti kwa kuwa Mungu alikuwa ameingia katika maisha yake. Elizabeti na Yohana Mbatizaji ambaye alikuwa bado hajazaliwa wanashiriki pia furaha ya Maria na Yesu ambaye hajazaliwa. Wanawake wawili kukutana, watoto wao pia wanakutana. Maria anatukumbusha kwamba ni lazima kuondoka na kuenda kukutana na wengine na kuyatambua matendo ya Mungu maishani mwao. Maria anatusaidia kuamini kwamba matendo makuu ya Mungu katika historia ni ishara ya uaminifu wake. Tunaalikwa kuchukua ahadi ya kuondoka na kuenda kwa wengine kuona walivyobarikiwa na Mungu. Wengi wanangojea kutembelea kwetu na mshikamano wetu. Kwa kufanya hivyo tunahitaji kushinda baadhi ya vikwazo vinavyotuzuia kushirikiana na baadhi ya watu katika jamii au kabila jingine.


      Basi, ni mwenye furaha aliyeamini katika ahadi ya Mungu, kwa maana Yule anayeahidi ni mwaminifu. Imani inakuwa kigezo/kipimo cha msingi wa furaha. Maria anakuwa ishara ya ubinadamu mpya, uliobadilishwa na kuokolewa na Mwanae. Maria ni mmoja wetu ambaye alijihisi aliyeangaliwa kwa huruma na akaishi kwa shukrani. Aliyeangaliwa kwa huruma kwa sababu Mungu alitenda makuu maishani mwake. Yeye aliishi kwa shukrani kwa sababu aliyapatikana maisha yake ili, kupitia jibu lake, Mungu atende makuu maishani mwa watu hasa maskini. Kwa kiwangu kidogo sisi pia tunapitia tabia hizi, ni kwamba, tumeangaliwa kwa huruma kupitia zawadi kubwa ya wito. Tabia ya shukrani ndani yetu inaonyeshwa nje kupitia utumishi kwa furaha na ukarimu. Hali ya kuwa walioangaliwa kwa huruma haitutegemei sisi, bali inamtegemea Mungu ambaye anatujalia baraka nyingi; hali ya kuwa kama walio na shukrani inatutegemea sisi peke yetu. Mbele ya majaribio ya kufa moyo au kukata tamaa Maria ni kielelezo kwetu kwa upatikanaji kabisa kwa mipango ya Mungu. Kama yeye tunaalikwa pia kuishi kama wamebarikiwa na kumchukwa Yesu kwa wengine katika mahali po pote tuendako.   

Fr Ndega
Mapitio: Sara

quinta-feira, 17 de dezembro de 2015

MUNGU ALICHUKUA BINAFSI HISTORIA YA WATU WAKE


Kutafakari kutoka Mt 1, 1-17

Kutokana na siku hii ya leo tunalianza juma maalum katika maandalizi yetu ya Krismasi. Kwa hivyo injili inatuletea ukoo wa Yesu. Majina haya mengi yaliyojulishwa na Mathayo yanatusaidia kufahamu mwelekeo wa binadamu wa Mwana wa Mungu. Ni ushahidi kwamba Yesu hakuonekana ghafla wala ni mgeni katika historia ya binadamu, bali tukio lake lilitokea polepole, hatua kwa hatua na kwa muda mrefu. Mungu aliwaandaa watu wake kwa uvumilivu kupitia Mwana wake ili historia hii ilikuwe na uwezo wa kumpokea katika wakati muafaka. Yesu Kristo anakamilisha ahadi aliyoitoa Mungu katika Agano la Kale. Kwa sababu hii, Yesu anatambulishwa kuwa ni mwana wa Mfalme Daudi na pia mzao wa Abrahamu. Mathayo anatumia mifano mingi kutoka katika unabii uliotolewa na manabii wa Agano la Kale, kueleza maisha ya Yesu ambaye alikuja kuwa Mwokozi wa Wayahudi (huu ni ufahamu wa kwanza kuhusu utume wake). Lakini mpango na lengo la Maandiko Matakatifu ni kuwasaidia watu kufahamu ufundishaji wa Mungu mwenyewe ambaye anatumia watu fulani kwa kufikia wote. Kama hii Mwanao hakutumiwa ili awe mali ya Wayahudi, bali Mwokozi wa ulimwengu wote.
Kwa nini yeye ni Mwokozi wa ulimwengu wote? Ni muhimu sana kujipatia nia ya Mungu kuhusu ubinadamu tangu uumbaji. Kwanza kabisa ulikuwa uamuzi wa Mungu kumwumba binadamu kushiriki naye uzima wake mwenyewe. Upinzani asili kupitia dhambi haukumzuia Mungu kuendelea mpango wake. Na, halafu aliamua kumwokoa binadamu mpotevu. Mungu mwenyewe aliwaandaa watu wake kwa muda mrefu akiifanya historia yao kuwa historia ya wokovu. Kwa sababu ya nia na matendo ya Mungu hatuwezi kuongelea historia mbili, bali historia ya Mungu na binadamu, yaani Historia ya wokovu. Mungu anamtafuta binadamu kumpa uzima wa milele ambao ni uhai wake mwenyewe. Historia hii inatokea polepole kati ya mwanga na vivuli. Kizazi cha Daudi kinaitwa kizazi cha mwanga kwa sababu ya mwelekeo wake kuelekea kwa Yesu. Kizazi cha utumwa wa Babeli kinafikiriwa kizazi cha vivuli kwa sababu upinzani wa watu dhidi ya mwongozo wa Mungu uliwazuia kuishi kama Watu wa Mungu. 

Tunaweza kuongelea njia maalum ya kuingia katika historia ya binadamu. Mungu anaingia katika maisha ya watu kwa wakati halisi. Yeye aliongea kwa namna mbalimbali kupitia manabii na mababu zetu ya zamani na siku hizi anaongea kupitia Mwanae mwenyewe. Yeye huongea kila wakati, lakini  haongei hewani bali hupitia katika matukio mazuri au mabaya  katika historia ya watu. Mungu alijifanya mmoja wetu na bado yuko nasi kwa namna mbali mbali. Kwa kivyo hakuna tukio lolote la historia lisilokuwa na maana. Angeweza kufanya kila kitu peke yake bali hakutaka. Alichagua Maria, Yosefu, Yohane na viongozi wengi kama washirika, akiingia katika historia kwa namna ya pekee na inabidi watu watayarishwe kumkaribisha Masiya wake kwa wakati wote. Sisi ni sehemu ya mwendo huu na kualikwa kumsaidia Mungu kwa mafanikio ya mipango yake kwa ubinadamu wote. Tumshukuru Mungu kwa matendo yake makuu katika historia yetu na kwa wito wetu kama washirika wake.

Fr Ndega
Mapitio: Sara

MAANA YA UWEZO WA YOHANA WA KUWATHIBITISHIA WASIKILIZAJI WAKE


Kutafakari kuhusu Sef 3, 14-18; Wap 4, 4-7; Lk 3, 10-18

       Liturujia ya jumapili hii tatu inaleta mwaliko kwa furaha kwa sababu ya ukaribu wa ujio wa Bwana wetu. Hali hii tunaweza kutambua kupitia ujumbe wa nabii Sefania ambaye waliwahamasisha waisraeli wafurahi na kumshangilia Mungu mfalme wao. Maana ya furaha kubwa ni kwa sababu uwepo wa Mungu katikati yao ulileta ukombozi ukidhamini usalama na ulinzi dhidi ya maadui yao. Ujumbe wa furaha unaendelea pia kupitia waraka wa Paulo kwa Wafilipi kwa sababu Mungu yu karibu na neno lake ni alama ya ukaribu wake. Ukaribu wa Mungu ni uwepo wake kwa wakati sawa na uwepo wake ni ufanisi, yaani ni nafasi ya wokovu.
        Kuhusu injili tuna vipengele vingi kwa kutafakari kwetu. Andiko hili ni mwendelezo wa injili ya jumapili iliyopita. Luka anaendelea kueleza kuhusu kazi ya Yohane Mbatizaji na kipengele cha kwanza ni kuhusu uwezo wa Yohana wa kuwathibitishia wasikilizaji wake. Kama ilitokea na manabii wa zamani, tunaamini kwamba uwezo huu unatokana na uzoefu wa kweli wa Neno la Mungu. Yohane alifikiwa na Neno la Mungu jangwani. Yeye aliishi katika upweke wa jangwa, aliyefunguliwa kabisa kwa msukumo wa Mungu. Alijifunza kutokana na Neno la Mungu jinsi ya kuwa shahidi wa habari njema ya wokovu. Miongoni mwa wasikilijazi wa Yohane, Luka anawataja watoza ushuru na askari ambao walitaka kubatizwa. Hasa watoza ushuru walichukiwa na Wayahudi wenzao kwa sababu walikuwa washirika wa Roma. Wakati wa Yesu, watoza ushuru waliwekwa katika kundi maalum la wenye dhambi. Kuchanganyika nao kulimfanya mtu apate dhambi yao pia. Yesu alichanganyika nao, akivuka mipaka iliyowekwa na watu. Kikundi hiki pamoja na askari walitambua ukweli wa hali yao na hivyo wakaomba msamaha. Lakini nia njema pekee haitoshi. Yohane anawataka watende haki.  Kwa hivyo aliwaalika washiriki mali yao.
       Ukuu wa Yohane Mbatizaji ulikuwa kutambua ukuu wa Bwana, akijifikiria mwenyewe kama sauti tu na asiyestahili kuulegeza ukanda wa viatu vyake. Yesu mwenyewe alitambua ukuu wa Yohane akiweka unyenyekevu wake kama rejea. Hatuhitaji kumlinganisha Yesu na Yohane Mbatizaji ili tugundue ni nani kati yao ni mtu mkuu. Bila shaka Yesu ni mkubwa zaidi kuliko Yohane. Lakini ni vizuri sana kutambua uhusiano huu wa ajabu kati ya wote wawili. Ikiwa Yohane anaongea kuhusu Yesu anamsifu; ikiwa Yesu anaongea kuhusu Yohana anafanya vivyo hivyo. Tunahitaji kujifunza sana kutokana na uhusiano huu, kwa manufaa ya Kanisa na kwa wema wa uhusiano wetu kama wakristo, watumishi wa mwili wa Bwana.
         Basi, ni kazi ya Yohane kutangaza mwisho wa wakati wa kumgojea Masiya na mwanzo wa historia mpya, ambayo ilifanywa na watu wapya waliofanywa upya katika Roho wa Kristo. Kama huu ni uzoefu wa ubatizo. Lakini ni lazima kukumbuka baadhi ya tofauti kati ya ubatizo uliotolewa na Yohane na ule atakaotoa Masiya. Yohana aliwabatiza watu kwa maji kama kielelezo cha kugeuka kwao. Uzoefu huu ulikuwa hatua muhimu, bali haikufikia mabadiliko kamili ya ndani. Ubatizo wa Roho Mtakatifu na moto una nguvu ya kufanya mabadiliko kwa sababu unamfanya mtu kuzaliwa katika familia ya Mungu. Alama yetu kama watoto wa Mungu haiwezi kufutika. Hii ni chapa ya ubatizo wetu. Ipo daima!

        Wakati wa Yohane Mbatizaji unaomhusu Kristo ni mwendelezo, lakini unaushinda wakati wa maandalizi wa zamani. Huu ni wakati wa kutangaza kuhusu mahitaji ya kumkaribisha Bwana aliyetaka kukutana na binadamu. Basi kwa upande wa Mungu, mwendo wa mkutano uko tayari. Kwa upande wa binadamu ni lazima imani na kukubalika kwa uhuru na binafsi. Ikiwa ukuu wa Yohana ulikuwa kutambua ukuu wa Bwana, ukuu wa kila mtu katika ufalme wa Mungu ni kuyakubali mapendekezo ya Yesu na kuzifuata nyayo zake. Kielelezo cha Yohane kiwe daima rejea kwa safari yetu ya kukubalika kwa mipango ya Mungu na kuutangaza wakati wa kutembelea kwake kwetu daima. 

Fr Ndega

terça-feira, 8 de dezembro de 2015

RESULT OF THE TRUE EXPERIENCE OF THE WORD OF GOD


Reflection from Bar 5, 1-9; Phil 1: 3-6, 8-11; Lk 3, 1-6


     The liturgy of this Sunday continues inviting us to welcome the Lord who is coming to bring salvation to us. It is necessary to prepare ourselves in order we can receive the Messiah in any time. The Advent season helps us to recognise that the right preparation needs transformation total of the heart. The words of the prophet Baruch motivated the people in the Babylon’s exile, proclaiming the nearness of their liberation. After all that sufferings they could go back home Jerusalem with great joy because God remembered them and guided them in his light and glory. Paul recognises that the faith and communion of the Philippians are extension of the gospel which they received with enthusiasm and willingness. Through Jesus Christ and his gospel they can bear good fruits for the glory and honour of God.     
      The gospel speaks about John the Baptist whom was reached by the Word of God in the desert. In the bible, the desert is special place for the experience of the Word of God’s. In that place many people were transformed in strong leaders in order to lead the People of God according to his guidelines. John the Baptist is considered the last and the greatest of all prophets. The Luke’s version mentions priests and politics leaders in order to show that through his messenger, God enters in the concrete life of the people in a specific time. God doesn’t speak in the ear, but through good and bad events in the history of the people. God made himself one of us and continues with us in different ways. For that there is no event in the history without meaning. In order to show the vocation of John in the events of his time, Luke shows that the greatest event was very near. God enters in the history with very particular way and requests that the people should be prepared to welcome the Messiah whom was expected for long time.
The coming of John the Baptist has a great meaning and follows the plan of God who has right time for everything. His Word transforms the life of John in instrument of salvation. As John is link between the Old and the New Testaments, his mission announces that the time of the Messiah is near to start. He is only the voice which prepares the ways of the Lord. John prepared the people to receive the Messiah using the baptism. Through this sign he proclaimed the mercy of God available for each person because it is plan of God that his salvation should reach all. So, the gesture of John was condition to pass from life of sin and dearth to grace and the new life of God. Important aspect in this action of John is that he baptized those who were in need of the mercy of God and repented their sins. John and that people believed that it is God whom forgives their sins.   
The Baptism of John is different of ours, but both are opportunity to live new life. For us Christians the new life is gift of Christ and result of his mission. The Christian baptism, besides the forgiveness of sins, guarantees participation in the life of the own God. The baptism is the first of the three sacraments of initiation followed by Chrism and Eucharist. Our baptism is external sign of the death to life of sins and sign also of the resurrection in Christ who is victorious against the sin and the dearth. He is the true light which enlightens each person. Through this process we become sons and daughters of the light in order to walk in the light of God each day of our life.

The Advent season helps us to prepare ourselves to celebrate the birth of Jesus. While the world of business advice the people to prepare themselves to Father Christmas buying something, Advent season proposes inner spiritual preparation and the effort for reconciliation with God and others. There are obstacles to remove with the help of the forgiveness of God. For that let us assume this good time to celebrate the sacrament of Reconciliation and to live in new way the relationship with God and others. 

Fr Ndega

MATOKEO YA UZOEFU WA KWELI WA NENO LA MUNGU


Kutafakari kuhusu Bar 5, 1-9; Wafil 1: 3-6, 8-11; Lk 3, 1-6

      Liturujia ya jumapili hii inaendelea kutumwalika kumkaribisha Bwana anayekuja kutuletea wokovu. Tunapaswa kujiandaa vizuri ili tuweze kumpokee Masiya wakati wowote. Wakati wa Majilio unatusaidia kutambua kwamba kwa matayarisho kamili ni lazima mabadiliko ya moyo, kwa njia mpya kabisa.  Maneno ya nabii Baruku yalihamasisha watu utumwani Babeli yakitangaza ukombozi karibu. Baada ya mateso hayo yote wataweza kurudi nyumbani Yerusalemu kwa furaha kubwa kwa sababu Mungu aliwakumbuka na kuwaongoza katika mwangaza na utukufu wake. Huu ni mfano wa wokovu wetu katika Kristo. Paulo anatambua kwamba imani na ushirika wa Wafilipi ni uenezi wa injili waliyochukua kwa shauku na utayari. Kwa njia ya Kristo na injili yake wanaweza kuzaa mazao mazuri kwa utukufu na sifa ya Mungu.  

       Injili inaongelea Yohane Mbatizaji anayefikiwa na Neno la Mungu jangwani. Katika biblia jangwa ni mahali maalum kwa uzoefu wa Neno la Mungu. Katika mahali huko watu wengi walijibadilisha kuwa viongozi wenye nguvu kwa kuwaongoza Watu wa Mungu kulingana na mwongozo wake. Yohane Mbatizaji anafikiriwa kuwa nabii wa mwisho na mkuu wa manabii wote. Toleo la Luka linataja makuhani na viongozi wa kisiasa ili kuonyesha kwamba kupitia mjumbe wake, Mungu huingia katika maisha halisi ya watu kwa wakati fulani. Mungu haongei hewani bali hupitia katika matukio mazuri au mabaya  katika historia ya watu. Mungu alijifanya mmoja wetu na bado yuko nasi kwa namna mbali mbali. Kwa kiyo hakuna tukio lolote la historia lisilokuwa na maana. Kwa kuonyesha wito wa Yohane katika matukio ya wakati wake, Luka anaonyesha kwamba tukio kubwa liko karibu. Mungu anaingia katika historia kwa namna ya pekee na inabidi watu watayarishwe kumkaribisha Masiya aliyetarajiwa kwa muda mrefu.

Kuja kwake Yohane Mbatizaji kuna maana na kuufuata mpango wa Mungu ambaye ana wakati kamili kwa kila kitu. Neno lake linayabadilisha maisha ya Yohane katika chombo cha wokovu. Kama Yohane ni kiungo kati ya Agano la kale na Jipya, kazi yake inatangaza kwamba nyakati za Masiya ziko karibu kuanza. Yeye ni sauti tu ambayo inatayarisha njia za Bwana. Yohane aliwatayarisha watu kumpokea Masiya kwa ubatizo. Kupitia ishara hii alitangaza huruma ya Mungu iliyopatikana kwa kila mtu kwa sababu ni mpango wa Mungu kwamba wokovu wake ufikie wote. Basi ishara ya Yohane ilikuwa kielelezo cha kupita kutoka katika dhambi na mauti kwenda katika neema na maisha mapya ya Mungu. Kipengele muhimu katika tendo hili la Yohana ni kwamba aliwabatiza wale waliomhitaji Mungu na kutubu dhambi zao. Yohane na watu hao waliamini kwamba ni Mungu anayesamehe dhambi zao.

Ubatizo wa yohane ni tofauti na ubatizo wetu, lakini yote mbili ni nafasi ya kuishi maisha mapya. Kwa upande wetu maisha mapya ni zawadi ya Kristo na matokeo ya utume wake. Ubatizo wa kikristo, pamoja na maondoleo ya dhambi, unadhamini ushiriki katika uzima wa Mungu mwenyewe. Ubatizo ni wa kwanza katika sakramenti tatu za mwanzo ukifuatiwa na Kipaimara na Ekaristi. Ubatizo wetu ni alama ya nje ya kufa katika dhambi, na pia ni ishara ya ufufuko wa maisha mapya katika Kristo aliye mshindi dhidi ya dhambi na mauti. Yeye ni mwanga wa kweli ambao unamtia nuru kila mtu. Kupitia mwendo huu tumekuwa wana wa nuru ili tutembee katika nuru ya Mungu kila siku ya maisha yetu.


Kipindi cha Majilio kinatusaidia kujiandaa kusherehekea kuzaliwa kwa Yesu. Wakati ulimwengu wa biashara unashauri watu wajiandae kwa Noeli kwa kununua vitu, kipindi cha Majilio kinatupendekezea matayarisho ya ndani kiroho, na hamu ya kutaka kutupatanishwa na Mungu na wenzetu. Kuna vikwazo vya kuondoa katika maisha yetu kwa msaada wa neema ya msamaha wa Mungu. Kwa hivyo tuchukue wakati mzuri huu kuadhimisha msamaha wa Mungu kwa sacramenti ya Upatanisho na kuishi kwa njia mpya uhusiano wetu na Mungu na wengine.


Fr Ndega
Mapitio: Sara