domingo, 27 de dezembro de 2015

SIKUKUU YA KUZALIWA KWAKE BWANA


Kutafakari kuhusu Luka 2, 1-14

Kulingana na liturujia ya siku hii takatifu, ujumbe kuhusu kuzaliwa kwa Yesu ni ujumbe wa furaha kubwa kwa wote, kwa sababu Mwokozi amezaliwa kwa wote. Tufurahi kwa sababu Mungu anatupenda, yeye yupo kati yetu na analeta wokovu kwetu. Wokovu ni kazi ya Mungu, lakini unatendeka duniani na ushiriki wa binadamu. Basi tuchukue Mariamu na Yusufu kama mifano. Katika tukio hilo la ajabu na unyenyekevu wa watu waliohusishwa, Mungu alidhihirisha njia yake yenyewe ya kutenda. Hali hii inathibitisha msemo wa Afrika ambao husema, “watu wanyenyekevu, kufanya vitu rahisi na katika mahali rahisi wana uwezo wa kubadilisha ulimwengu.” Mabadiliko makubwa ambayo jamii yetu inahitaji lazima kutokea ndani ya mwanadamu. Jamii mpya itatokea wakati kila mtu atatambua mahitaji ya kujibadilisha mwenyewe zaidi kuliko ajaribu kubadilisha wengine. Kulingana na Baba Mtakatifu Francisco, “Dunia itabadilika ikiwa tuanze kubadilisha matendo yetu kupitia tabia zetu na chaguzi zetu.” Kwa hiyo, Krismasi ni wakati wa kubadilisha tabia na chaguzi zetu.
Katika Yesu, Mungu amekuwa mmoja wetu, kuchukua hali halisi yetu ya binadamu na kulitoa pendekezo mpya la maisha. Kwa hivyo haitoshi kukiri katika Yesu wokovu wa Mungu; ni muhimu turuhusu kuongozwa na ujumbe wake wa amani na upendo. Kuzaliwa kwa Yesu kuliwabadilisha binadamu wote katika familia kwa njia ya kipekee, kujaza mioyo ya watu kwa furaha na matumaini. Kwa kweli, Mungu anajifunua kama jirani, maskini na anayekataliwa, kualika tutambue thamani ya ishara ndogo na miradi midogo. Bila shaka chaguo hili la Mungu linatuaibisha, kutualika kufikiri na kutenda tofauti. Kupitia udogo Mungu hufanya makuu. Hivyo, Krismasi ni wakati wa kubadilisha mawazo wetu.
Kipengele kingine cha kutafakari kwetu katika usiku huu ni kuhusu wachungaji, waliokuwa watu wa kawaida wadharauliwa katika jamii. Wachungaji walikuwa watu waangalifu ambao walichunga wanyama wao karibu na Bethlehem wakati wa usiku. Walikuwa kweli waangalifu kwa sababu ndani yao hisia kuhusu Mungu na ukaribu wake ulikuwa hai sana. Wachungaji walikuwa watu wa kwanza kuupokea ujumbe mkubwa wa furaha kwa sababu mioyo yao ilikuwa macho. Yeyote tu aliye na moyo makini ana uwezo wa kuamini katika habari njema na kutarajia hali nzuri katika kila alfajiri mpya. Mtu tu aliye na moyo makini ana ujasiri wa kuanza safari kwa kukutana na Mungu katika mahali pasipotarajiwa, yaani katika hali ya mtoto mdogo na mahali maskini sana. Hivyo, Krismasi ni wakati wa kuangalia tofauti ili kuona zaidi na kufanya tofauti katika maisha ya watu wengi.
Mungu Mwenyezi anakubali hali ya mtoto mdogo, katika utegemezi kabisa na utunzaji na upendo wa binadamu. Imani inatuongoza kumtambua mtoto huyu mdogo wa Bethlehemu katika kila mtoto ambaye sisi hukutana katika safari yetu ya kila siku. Kila mtoto anaomba upendo wetu. Tufikiri leo, kwa njia maalum, kuhusu baadhi ya watoto ambao hawana uzoefu wa upendo wa wazazi wao; kuhusu pia watoto wa mitaani ambao hawana mahali pa kuishi; kuhusu watoto ambao wanatumika kama askari, wanaobadilishwa katika vyombo vya vurugu, badala ya kuwa vyombo ya upatanisho na amani; tena kuhusu watoto ambao ni waathirika wa unyanyasaji wa kijinsia, na kuhusu watoto maskini waliolazimishwa kuziacha ndoto zao kwa sababu ya hali mbaya ya kiuchumi. Mtoto mdogo wa Bethlehemu ni mapitio mapya ili tuweze kujitoa ili dhiki ya watoto hawa ikomeshwe. Mwanga wa Bethlehemu uguse mioyo yetu, kuifanya yenye unyeti kwa hali hii. Hivyo, Krismasi ni wakati wa utunzaji na upendo kwa walio na mahitaji mengi.
Ingawa sisi huishi katika jamii ya ulaji ambayo inatuzuia kushughulika kwa thamani muhimu sana, tunapaswa kuwa macho. Krismasi si ulaji. Ni sikukuu ya ufunuo wa Fumbo la upendo wa Mungu unaobadilisha moyo wa binadamu na kuufanya wenye unyeti kwa mapitio ya Mungu. Mungu anatupenda bure na kwa ukarimu, bila astahili kwa upande wetu. Uzoefu huu lazima kutuongoza tufanye vile vile anavyofanya. Kama hii, Krismasi itakuwa zaidi kuliko kipindi kimoja kwa mwaka. Itakuwa Krismasi daima ikiwa tujifunze kupenda kweli na kuweka juhudi zaidi kwa kujenga jamii ya ndugu na haki kwa wema wa wote.

Fr Ndega

Mapitio: Sara

Nenhum comentário: