sábado, 28 de setembro de 2019

HALI MPYA KATIKA MAISHA YA MILELE



Kutafakari kuhusu Am 6, 1a. 4-7; 1Tm 6, 11-16; Lk 16, 19-31


       Mungu analaumu kila kutojali na unafiki kati ya watu wake. Kama anatamani wawe na furaha kamili na maisha mengi, yeye anapendekeza njia kamili ya kuishi.

       Kulingana na somo la kwanza, nabii Amosi anatusaidia kufahamu kwamba hali mbaya ya utumwa katika safari ya Waisraeli haikuwa adhabu ya Mungu bali matokeo ya uamuzi ya kuishi mbali sana naye. Nabii huyo anashutumu njia ya kianasa ya wakubwa ambayo inajaa udhalimu na kosa la undugu kati ya watu. Hali hii mbaya ya kuishi ilivutia utumwa kwa maisha yao. Wakati mwafaka Mungu ataonyesha upendo wake hasa kwa ajili ya wadogo na ya maskini. Maisha ya kianasa na ya wingi mtu anayoishi yaweza kuwa kikwazo ili awe na macho mbele ya hali ya walio na shida. Kipimo cha uhusiano mwema na Mungu na kupata furaha kamili ni hisia ya kindugu.

      Somo la pili linaonyesha shauri ya Mtakatifu Paulo kwa Timotheo na kwa kila Mkristo. Andiko linaanzwa hivyo: “Bali wewe, mtu wa Mungu, uyakimbie mambo hayo”. Ni kuhusu mambo gani? Ndiyo mambo ya kila namna ya kupenda fedha ambayo anaharibu imani na kuvutia kila namna ya maovu.  Haitoshi kuwa na jina la Kikristo ili kuwa mwanafunzi wa kweli wa Yesu. Mtakatifu Paulo anatualika kufuata njia ya haki, utauwa, imani, upendo, uvumilivu na upole.   

     Yesu anasimulia mfano wa mtu tajiri na Lazaro maskini anawaonya wasikilizaji wake kuhusu hali ijayo iliyo matokeo ya chaguzi za watu katika wakati huu. Kwanza kabisa ni lazima tufahamu kwamba kuzimu iko bali kuna pia peponi. Sio wote wa matajiri wataenda kuzimuni na sio wote wa maskini wataenda peponi. Mwelekeo wa maisha ya mtu utakuwa kulingana na njia ambayo alichagua kuishi na tabia mbele ya vitu vya dunia. Yesu anafundisha tabia kamili.

       Basi, palikuwa na mtu mmoja tajiri na Lazaro maskini. Mtu wa kwanza ni ishara ya walio na mazoea ya kuitumainia mali bila kuguswa na hisia kuhusu kile kinachotokea kandokando yao. Hao walichagua kwa nafsi yao njia ambayo itawaongozea mauti. Lazaro ni ishara ya walio maskini ambao wameachwa bila ulinzi na utunzaji; wanapiga kelele ili wapate nafasi ya kuishi kwa heshima. Tena Lazaro ni pendekezo la kuishi tofauti, kuyalenga maisha katika thamani za kweli. Huyo ni ishara ya uvumilivu, ya mapigano na mwaliko wa kumtumainia Mungu ambaye katika riziki yake hawaachi wale ambao wanamwamini.

     Kupitia mfano huu Yesu anatukumbusha kuhusu hali mbaya ambayo ipo katika jamii yetu, yaani kosa la usawa kati ya watu. Katika mafundisho yake, Kanisa limeshutumu hali hii mara nyingi kwa kusema, “Hali mbaya ya kijeuri imezaa matajiri mno daima na tena kwa upande mwingine imezaa maskini mno daima.” Hali hii ni dhidi ya mipango ya Mungu anayefanya mvua inyeshe kwa wenye haki na wasio na haki, tena kwa walio wema na kwa wabaya ili vitu vyote alivyoumba kwa wote tena vipatikane kwa wote.

      Mfano mzuri kuhusu hayo tunapata katika Wimbo wa Bikira Maria ambao unaishuhudia njia ya ajabu ya Mungu ya kutenda, yaani yeye huwashusha wakuu na kuwapandisha wadogo ili waweze kuishi pamoja kama ndugu na kwa usawa wa haki na wa heshima. Mungu anajitambulisha na hali ngumu ya wasio na nguvu na ya maskini. Udhalimu wote unaofanyika kwao unamgusa Mungu ambaye anasimama katika upande wao.

      Katika wakati ujao, baada ya hali ya dunia, hali itakuwa tofauti kabisa, yaani waliopokea mambo mema katika maisha yao bila ahadi na hisia kuhusu hali ya walio na shida hawatakuwa na hali nzuri kwa maisha yao. Kwa upande wa wale waliopata mabaya kama Lazaro alivyo, watafarijiwa. Yeyote ambaye anatumia mali yake ili kuwadharau wengine anatupa maisha yake takatakani kwa sababu maisha ya kweli hayamaanishi kuwa na mali mengi bali kuwa na uwezo wa kutenda mema. Mtakatifu Yohane Calabria asema: “Maskini wako ili matajiri waokolewe”. 

       Hali ya maskini inatuhusu sote, kwa sababu “dhambi ya kijamii ni matokeo ya kiasi cha dhambi za kibinafsi”. Basi, ni lazima mabadiliko sio tu kuhusu dhambi za kibinafsi, bali pia kuhusu dhambi ya kijamii. Mwendo huu unaweza kwanza kupitia tabia ya kuacha njia ya ukusanyaji ambayo kwa kawaida inatuongoza kuwa na kutojali kuhusu hali ya wengine. Vitu tulivyo navyo ni zawadi za Mungu. Tunaalikwa kuchukua njia ya unyenyekevu kwa kuepuka matumizi ya vitu vya bure na kuwa na hisia kuhusu wale wasio navyo. Mungu anatuokoa maana ya upendo wake, lakini anathamini sana juhudi zetu kama alivyosema Baba Mtakatifu Benedito wa kumi na sita: “kwa kweli, wokovu ni zawadi iliyo neema ya Mungu, lakini ili uwe ufanisi katika maisha yangu unadai ridhaa yangu, ambayo inaonyeshwa kupitia matendo, yaani kupitia utayari wa kuishi kama Yesu alivyo kwa kuufuata mfano wake.”

Fr Ndega

IL ROVESCIO NELL’ALDILÀ DELL’ESISTENZA



Riflessione a partire da Am 6, 1a. 4-7; 1Tm 6, 11-16; Lc 16, 19-31


      Dio condanna ogni indifferenza e ipocrisia in mezzo al suo popolo. Siccome desidera per i suoi figli piena gioia e tutto provvede per il loro maggior bene, propone un modo giusto di vivere.

        Nella prima lettura, il profeta Amos ci aiuta a capire che la terribile esperienza dell’esilio non è stata una punizione di Dio per il popolo di Israele, ma il risultato della loro decisione di vivere lontano da Lui. Il profeta denuncia lo stile di vita lussuoso e abbondante da parte dei potenti del popolo che genera grande ingiustizia nei confronti dei piccoli. Questa situazione attirerà l’esilio, la rovina per tutto il popolo. Al momento giusto Dio farà sentire il suo amore specialmente per i più piccoli e poveri. Una vita lussuosa e abbondante può essere un ostacolo per vedere i bisognosi che ci stanno attorno. La condizione per un buon rapporto con Dio e per una piena gioia è l’impegno fraterno.

       La seconda lettura ci porta i consigli di San Paolo a Timoteo e ad ogni cristiano. Il testo comincia così: “Ma tu, uomo di Dio, evita queste cose”. Quali cose? Trattasi dell’avidità del denaro, che rovina la fede e attrae ogni tipo di male. Non basta avere il nome cristiano per essere un vero discepolo di Gesù. L’apostolo Paolo ci invita a seguire la via della giustizia, della pietà, della fede, della carità, della pazienza e della mitezza.

    Volendo coinvolgere la gente nella sua proposta di salvezza, Gesù racconta una parabola. C’era un uomo ricco ma egoista, che ha vissuto per sé stesso e che non ha ascoltato Mosè e i profeti; e c’era anche un uomo povero e disprezzato, sofferente, chiamato Lazzaro. Questo nome viene da Eliezer, che vuole dire Dio è il mio aiuto. Come era il rapporto fra di loro? Il ricco era indifferente al povero. Quando muoiono, cosa succede? Vediamo che quel Lazzaro morente se ne va nel seno di Abramo, di cui ha condiviso la fede, cioè nella gioia e nel riposo, mentre l’uomo ricco si avvia verso l’inferno. In altre parole, avviene un capovolgimento nell’aldilà dell’esistenza.

      Raccontando questa parabola, Gesù “si propone di cambiare le idee sbagliate e le pretese di alcuni Giudei e soprattutto dei farisei. Essi stimavano che le ricchezze fossero una prova evidente del favore di Dio. È vero che nell’economia giudaica i giusti avevano la promessa delle benedizioni terrestri. Ma i Giudei erano stati mancanti in ciò che Dio aveva affidato loro, come il fattore infedele (inizio del capitolo 16 di Luca con la parabola dell’amministratore disonesto) e i farisei che pretendevano di aver diritto al favore di Dio erano attaccati al denaro (v.14) ed egoisti, e godevano ingiustamente delle loro ricchezze (v.9) disprezzando i poveri”. Dio non è indifferente a quello che accade ai poveri. È sempre pronto ad agire in vista di una vita dignitosa per tutti i suoi figli. 
  
   La prima parte di questa parabola ci fa riflettere sulla grave situazione della disuguaglianza sociale, che è un grande problema a livello mondiale, vale a dire: coloro che sono ricchi diventano sempre più ricchi e chi è povero diventa sempre più povero. Questo va contro la volontà di Dio e Gesù lo ricorda molto bene quando presenta il capovolgimento di questa situazione nell’aldilà della esistenza. Secondo lui “i figli del regno increduli (coloro che offrono resistenza al suo messaggio) vengono gettati fuori, mentre i credenti delle nazioni (coloro che lo accolgono) vengono introdotti nel regno con Abramo, Isacco e Giacobbe (Matteo 8,11-12; 15,21-28). Gesù stesso, povero, disprezzato e rifiutato, entra nella gloria”.

       Ma attenzione: dobbiamo innanzitutto evitare il pensiero sbagliato che uno va all’inferno perché è ricco e che l’altro, Lazzaro, si trova nel seno d’Abramo perché è povero. Non tutti i ricchi andranno all’inferno e non tutti i poveri andranno in paradiso. Il problema di fondo non sono le ricchezze in sé che uno ha, ma l’indifferenza e il disprezzo per quanto riguarda la fraternità. La parabola orienta al buon uso delle ricchezze e della attenzione verso i bisognosi. È certo che avremo un giudizio universale con la seconda venuta di Cristo alla fine dei tempi, ma secondo questa parabola, prima di quello universale, con la morte c’è il giudizio individuale, che non sarà più modificato. Così dice il brano che abbiamo sentito: “è stato fissato un grande abisso: coloro che di qui vogliono passare da voi, non possono, né di lì possono giungere fino a noi”.

      Ma ciò che è importante custodire ora è che Dio ci ha preparato un bel posto nel seno di Abramo e ci attira a sé con legami di misericordia e tenerezza. Ha pensato per la nostra vita una eternità felice come quella di Lazaro, ma rispetta molto la nostra libertà.  La salvezza o la perdizione non dipendono dalla posizione sociale terrestre, ma da quanto valorizziamo le opportunità che Dio ci dà per la nostra conversione. Dio non vuol condannare nessuno. Egli ci offre la sua misericordia e spera torniamo da lui finché vi è tempo. Le cose materiali, per cui abbiamo tanto lottato, non possiamo portarle con noi. Il vero bene della vita è il tempo. Ecco perché non dobbiamo sprecarlo ma impegnarlo per prepararci alla vita eterna, accumulando l'unico tesoro che ha valore nel Regno: i nostri gesti d’amore. Il resto non conta nulla. Ci prepariamo a ricevere l’abbraccio della misericordia e cominciare una vita nuova.

Fr Ndega
Revisione dell'italiano: Giusi

sexta-feira, 20 de setembro de 2019

WASIMAMIZI WAMINIFU WA ZAWADI ZA MUNGU



Kutafakari kuhusu Am 8, 4-7; 1Tm 2, 1-8; Lk 16, 1-13



       Mungu anatarajia kwa watu wake maisha marefu na ya heshima. Mambo yote ambayo hayaisaidii hali hii yanakataliwa na Mungu. Hivyo, kupitia nabii Amos, katika somo la kwanza, yeye (Mungu) anashutumu aina yote ya ukandamizaji ambao uliwazuia watu waishi kama watu wa Mungu hasa hali ya udhalimu dhidi ya maskini na wenye njaa. Mateso yao yadhihirisha kwamba tuko na jamii ya kijeuri ambapo wako baadhi ya watu wenye nguvu ambao wanamiliki mali na pesa nyingi wakati wengine wengi hawana kilicho cha kutosha kwa kuishi.

      Kama dhambi ya kijamii ni matokeo ya kiasi cha dhambi za kibinafsi, hivyo, hata sisi tuko na jukumu katika hali hii ya udhalimu. Kuhusu hayo Baba Mtakatifu Francisco asema: “Ulaji umetuongoza kutumia vitu chepesi pamoja na ubadhirifu wa chakula cha kila siku... Tunapaswa kukumbuka kwamba chakula ambacho sisi hutupa takatakani ni kama ikiwa tulikuwa tumeiba kutoka meza ya walio maskini na wenye njaa.” Hali ya watu hawa ilikuwa kipaumbele katika kazi ya Yesu ambaye alichukua ahadi ya kuwa maskini ili kuwatajirisha wote kwa umaskini wake.    

     Katika somo la pili, Mt. Paulo anatushauri kuwaombea watu wote hasa wale ambao wako na mamlaka ya kuongoza na kutawala, yaani Viongozi wa Kanisa, Serikali na kadhalika. Hao wanapaswa kufanya kazi yao vizuri ili tuweze kuishi maisha ya utulivu na amani. Sisi ni wa Mungu na kwa hivyo, kazi ya viongozi wote kwa ajili ya maisha yetu ni ushiriki katika utawala wa Mungu mwenyewe ambaye hutaka watu wote waokolewe, na kupata kujua yaliyo kweli ama Aliye ukweli.  Ni jukumu letu ili watawale vizuri nalo linampendeza Mungu.

     Tukiendelea kutafakari kwetu, tuko na mfano ambao Yesu alisimulia kuongea kuhusu mahitaji ya kuwa mwaminifu kuhusu jukumu ambalo tumepokea kutoka kwa Mungu. Kile kilicho nacho kinatoka kwa Mungu kwa sababu vyote vizuri vyatoka kwake. Anatukabidhi utunzaji wa vyote na kutarajia tupate kusimamia zawadi zake kulingana na mapenzi yake. Sisi sio walio na mali bali ndio wasimamizi tu wa zawadi za Mungu. Hivyo, tunapaswa kuitumia pesa sio kama lengo la maisha, bali kama chombo cha kuizaa hali nzuri kwa wote.

     Tunaishi katika jamii ambapo pesa ni kipimo cha kila kitu na pia inaonekana kwamba pesa inatutawala. Kila kitu ambacho tunahitaji hakiwezekani kupata bila pesa. Hii ni nguvu na maana ya kuishi kwa watu wengi. Je, Wakristo wanapaswa kuwa na tabia gani mbele ya utajiri? Wale wanaofuata Kristo wanapaswa kuwa waaminifu katika mambo yote na kutumia tabia kamili kuihusu pesa. Kutokuwa na tabia kamili kuhusu jambo hili kunatuongoza kusahau haja ya uangalifu kwa ajili ya familia, utunzaji kwa afya yenyewe, uhusiano wa kweli na Mungu n.k.

      Mara nyingi uhusiano wetu na Mungu unasumbuliwa kwa sababu ya hamu ya kuwa na pesa na mali nyingi. Yesu hasemi kwamba pesa si muhimu, lakini asema kwamba haiwezi kutushika na kutumiliki. Yesu anataka tufahamu kwamba pesa haijengi thamani za kweli ambazo zinazaa uzima na furaha. Tunaweza kuitumia pesa ili kumtumikia Mungu, bali hatuwezi kumtumia Mungu ili tupate pesa. Tunapaswa kuwa macho kwa sababu hali hii inaweza kutokea na mara nyingi bila tutambue hiyo. Pesa ni kitu ambacho kinaweza kututumia na kutubadilisha kuwa wasio na hisia kwa ajili ya Mungu na kwa mahitaji ya wengine. 
    
      Pesa inatusaidia kuishi lakini imewaweka watu mbali sana wao kwa wao. Pesa inaijenga nyumba lakini inaweza kuharibu familia. Kupitia pesa tunaweza kuinunua nguo, chakula na kadhalika, lakini pia inaweza kuzaa upendeleo, ubaguzi na utoaji rushwa. Hatuwezi kuruhusu kwamba pesa iwe chombo cha tofauti kati yetu kwa kutuongoza kuwabagua wengine. Kati yetu tunajua jinsi vile pesa imekuwa muhimu, hasa kuhusu sadaka ya ukarimu kwa ajili ya kulijenga kanisa-hekalu na kwa ajili ya mahitaji mengi katika kazi zetu za kuinjilisha. Tunamshukuru Mungu kwa matumizi ya pesa kama maonyesho ya ukarimu kwa manufaa ya jumuiya zetu kwa kulijenga Kanisa la Bwana. Tena tumwombe neema ya kuwa na tabia kamili mbele ya pesa kwa kutumia ishara hii si kama chombo cha ubaguzi, bali kama chombo cha undugu.   

Fr Ndega

AMMINISTRATORI FEDELI DEI DONI DI DIO



Riflessione su Am 8, 4-7; 1Tm 2, 1-8; Lc 16, 1-13



      Dio desidera per il suo popolo lunga vita e dignità. Tutte le cose che non vanno in questa direzione vengono da lui rifiutate. Così, tramite il profeta Amos, nella prima lettura, Dio ha condannato tutte le forme di oppressione che impediscono di vivere come popolo di Dio, soprattutto la situazione di violenza contro i poveri e gli affamati. La loro sofferenza è una dimostrazione che abbiamo una società ingiusta dove esistono persone potenti, che hanno proprietà e ricchezze, mentre altre non hanno il sufficiente per vivere.

      Come il peccato della società il risultato di un accumulo di peccati personali, bisogna che siamo attenti per non contribuire ancora di più con questa ingiustizia sociale. A proposito di questo, Papa Francesco dice: “Il consumismo ci ha indotti ad abituarci al superfluo e allo spreco quotidiano di cibo... Ricordiamo bene, però, che il cibo che si butta via è come se venisse rubato dalla mensa di chi è povero, di chi ha fame!” La situazione di queste persone era una priorità nella missione di Gesù che ha preso l’impegno di essere povero per arricchire tutti con la sua povertà.

      Nella seconda lettura, San Paolo ci consiglia di pregare per tutti gli uomini specie per coloro che hanno la responsabilità di condurre e di governare: ministri della Chiesa, capi di governo e così via, affinché possano fare il loro lavoro bene, così che tutti possiamo vivere una vita di serenità e di pace. Noi siamo di Dio, e pertanto, l’autorità che i capi hanno sulle nostre vite è solo una partecipazione nella missione di Dio stesso che vuole che tutti gli uomini siano salvati e che conoscano la verità. È anche nostra responsabilità che facciano un buon lavoro e questo è gradito a Dio.

    Continuando la nostra riflessione, abbiamo una parabola in cui Gesù ci parla della necessità di essere fedeli nel compito che abbiamo ricevuto da Dio. Ciò che abbiamo appartiene a Dio, per cui ogni bene viene da lui. Lui ci affida la custodia di tutto e aspetta che noi agiamo secondo la sua volontà. Non siamo i proprietari, ma gli amministratori dei doni di Dio, per questo dovremmo usare i soldi non come fine nella vita, ma come strumento per produrre buone condizioni per tutti.

      Viviamo in una società dove il denaro è la misura di tutto e tutto dipende dal denaro. Si tratta di un potente mezzo di vita per molte persone. I cristiani, che comportamenti devono avere di fronte alla ricchezza? Coloro che seguono Cristo dovrebbero essere onesti in tutte le cose e avere il giusto comportamento in relazione alla ricchezza. La mancanza di un giusto rapporto con questa ci conduce a dimenticare la cura per la famiglia, l’attenzione alla propria salute, una vera relazione con Dio e con gli altri.

      Spesso nel rapporto con Dio c’è qualcosa che non va bene a causa del nostro desiderio di avere sempre più ricchezze. Gesù non sta dicendo che il denaro non è importante, ma dice che non possiamo lasciarci prendere e schiavizzare dal denaro. Gesù vuole che ognuno comprenda che i soldi non possono garantirci i valori che generano vita e felicità. Noi possiamo usare i soldi per servire Dio, ma non possiamo usare Dio per trovare soldi. Su questo dobbiamo essere vigili perché questo può accadere e spesso senza che ce ne rendiamo conto. Il denaro è pericoloso perché può farci insensibili all’amore di Dio e ai bisogni degli altri.

     Il denaro ci aiuta a vivere, ma mette anche persone lontane tra loro. Il denaro può costruire una casa ma anche può distruggere famiglie. Attraverso il denaro possiamo comprare vestiti, cibo e così via, ma possiamo anche produrre privilegi, corruzione e discriminazione. Non possiamo permettere che i soldi siano motivo di differenza tra di noi, conducendoci a discriminare gli altri. Per le comunità cristiane il denaro è stato importante in quanto istrumento per l'edificazione e manutenzione degli spazi di incontri e celebrazioni e per le molte attività della evangelizzazione. Ringraziamo Dio per l'uso del denaro come espressione di generosità per il bene delle nostre comunità. Chiediamo la grazia di usare il denaro che abbiamo non come strumento di discriminazione, ma piuttosto come uno strumento di solidarietà, costruendo fraternità. 

Fr Ndega

sábado, 14 de setembro de 2019

LA GIOIA DI PERDONARE E DI ESSERE PERDONATO



Riflessione a partir di Lc 15, 1-32


      Il quindicesimo capitolo del vangelo di Luca è molto famoso tra le parabole di Gesù. Questo è chiamato capitolo delle parabole di misericordia, vale a dire la parabola del pastore che perde la pecora (4-7), della donna che perde la moneta (8-10) e del padre che perde il figlio (11-32). Queste parabole mostrano l’atteggiamento compassionevole di Dio verso i peccatori e la gioia di trovare nuovamente quello che si era perduto.

     “Gesù è il volto della misericordia del Padre” e ha rivelato questa misericordia non soltanto con parole ma anche e soprattutto con i gesti. Per questo, dice il brano, si avvicinavano a lui tutti i pubblicani e i peccatori. Non avrebbero fatto questo passo se non avessero avuto la certezza di essere bene accolti da Gesù. Dall’altra parte abbiamo un secondo gruppo, formato dai farisei e dagli scribi, che preferiscono la critica, la lamentela, la resistenza.

        Tutti i due gruppi, anche se hanno un’esperienza diversa di Dio e atteggiamenti diversi nei suoi confronti sono figli e sono amati. Nessuno dei due conosceva il vero volto di Dio poiché un gruppo si considerava dei giusti e condannava l’altro che a sua volta portava, per assimilazione e rassegnazione, il nome di peccatori pubblici, cioè, un caso perduto. Nell’incontro con Gesù hanno trovato l’abbraccio della misericordia e, quindi, un nuovo orizzonte per la loro vita. Questo è stato lo scenario di fondo usato da Gesù per comporre e raccontare queste bellissime parabole.

        Nella parabola del pastore che perde sua pecora, abbiamo l’immagine di Dio Padre che ha un’attenzione speciale verso tutti, va in ricerca del peccatore e non ‘riposa’ finché non lo incontra e lo coinvolge nuovamente nella sua comunione. Nella parabola della donna che perde una moneta, Dio è come una madre che usa tutta la tenerezza e cura per ricongiungere nuovamente a sé ogni persona che si è allontanata dalla sua comunione e fa festa per la gioia di averla trovata.

       Nella parabola del padre che perde il figlio, la centralità punta sul modo del padre di amare i due figli, ambedue prodigi, anche se in modi diversi. Secondo Gesù, Dio nei nostri confronti è come un padre di famiglia che ha due figli e condivide i suoi doni in parti uguali con tutti. Vuole che vivano lo spirito di famiglia partecipando alla sua gioia di padre. In questa famiglia lui cerca di offrire il suo amore, la sua cura e protezione, affinché i suoi due figli abbiano buone ragione per vivere sempre in comunione con lui. Quando qualcuno decide di abbandonarlo e andare via, non è impedito di farlo perché questo padre rispetta la libertà di ciascuno. Questo suo modo di amare permette di andare via ma assicura anche una buona accoglienza a chi ritorna da lui.

      Deve essere più o meno così la nostra esperienza. Dio non impone la sua autorità, preferendo rivolgersi a noi con legami di tenerezza, trattandoci da adulti, cioè “accettando il terribile rischio educativo di lasciarci andare per la nostra strada”. Allo stesso tempo è sempre vigilante, aspettando il più piccolo segno di ritorno per darci l’abbraccio della misericordia e fare festa con noi. Tante volte ci sentiamo lontani da Dio a causa dei nostri peccati. Certamente Egli si sente abbandonato e tradito, ma non smette di amarci. Così sentiamo rimorso e la certezza di essere bene accolti ci motiva a tornare da Lui e riprendere la comunione con Lui. Anche se spesso non ci comportiamo come figli, Dio rimane sempre fedele alla sua missione di Padre. La sua misericordia è più grande e potente dei nostri errori. Abbiamo bisogno di riscoprire questo vero volto di Dio.

      Un altro momento molto duro per quel padre della parabola è stato l’indurimento di cuore del figlio maggiore verso suo fratello e riguardo al gesto di accoglienza del Padre. Veramente, questo figlio maggiore non si sente figlio, visto che tratta il padre da padrone, e quindi si sente un impiegato; e non si sente neanche fratello, perché rifiuta il proprio fratello. Il comportamento del figlio maggiore mette a rischio la gioia e la bellezza della festa.

     Quando qualcuno prende sul serio un cammino di conversione è motivo di grande gioia per il Padre. Però gli causiamo un grande dolore quando non condividiamo dei suoi sentimenti nei confronti degli altri, cioè quando siamo indifferenti nei confronti di coloro che ritornano alla comunità. Come ha parlato ai discepoli una volta, Gesù ripete a noi oggi: “Siate misericordiosi come vostro Padre.” La riconciliazione con gli altri è la condizione perché il nostro rapporto con Dio sia vero. Questa è la via della vera conversione, che è un lungo cammino e comincia nel nostro cuore. Lasciamoci colpire dal modo misericordioso di Dio di agire e una volta toccati dalla sua misericordia possiamo essere strumenti di essa per coloro che hanno bisogno del nostro perdono.

Fr Ndega

sexta-feira, 13 de setembro de 2019

FURAHA YA KUSAMEHE NA KUSAMEHEWA



Kutafakari kuhusu Lk 15, 1-32




Sura ya kumi na tano ya toleo la Luka inajulikana sana miongoni mwa mifano ya Yesu. Hii inaitwa sura ya Mifano ya huruma. Tuko na mifano mitatu, yaani mfano wa Kondoo aliyepotea (4-7), wa Sarafu iliyopotea (8-10) na Mwana mpotevu (11-32). Mifano hii inaonyesha tabia ya huruma ya Mungu kwa wenye dhambi na furaha ya kupata tena kitu kilichopotea. Kwa kufahamu nia ya Yesu alipoisimulia mifano hii tunahitaji kutafakari kwanza kuhusu mazingira ambayo Yesu aliishi.

Katika muktadha ule, baadhi ya watu walijiona waliostahili wokovu wa Mungu kuliko wengine kwa sababu ya uaminifu wao kwa Sheria. Walichukua mamlaka ya kuwatenganisha watu, wakiwapanga kama wema au wabaya. Mamlaka haya hayatoki kwa Mungu kwa sababu kipimo ni ubaguzi. Walisahau kwamba mbele ya Mungu hakuna yeyote aliye na haki kuliko mwingine. katika njia yake ya kupenda Mungu hakuna ubaguzi. Kwa upande wake watoza ushuru na wenye dhambi ni watoto wake kama vile ndio Mafarisayo na Waandishi. Kipimo cha kuishi kwa ushirika na Mungu sio sheria bali uzoefu wa undugu.
        
         Ingawa yako matukio mengi katika Agano la Kale, ambayo yanaonyesha njia maalum ya Mungu ya kutenda, ni “katika Yesu Kristo kwamba huruma ya Mungu imepata kuwa hai na yenye kuonekana, na hata ilifikia kilele chake katika Yeye... Yesu ni uso wa huruma ya Baba. Kila kitu ndani yake kinaongelea huruma. Hakuna chochote kwake kinachopungukiwa na huruma (Baba Mt Francisco).”  Kama alama ya huruma ya Mungu, Yesu ana chaguo wazi sana, kulingana na maneno ya waliompinga yeye, yaani “Mtu huyu huwakaribisha wenye dhambi, tena hula nao”.

       Kweli, Yesu alikuwa na njia maalum ya kuongelea huruma ya Mungu, yaani katika Yesu jambo la huruma lilionyeshwa “kwa neno lake, matendo yake na kwa nafsi yake yote.” Yeye alitumia ishara nyingi za makaribisho, akithibitisha lengo la ujumbe wake na ukweli wa mafundisho yake. Kwa kweli, watozaushuru wengi, makahaba na wengine waliokataliwa na jamii, walijiona kukaribishwa na Yesu na tena kubadilishwa kwa sababu ya mkutano na huruma ya Mungu.

      Mfano wa mchungaji anayepoteza kondoo wake tuko na ishara ya Mungu Baba ambaye ana macho maalum kwa kila mtu naye hapumziki mpaka kukutana na aliyepotea na kumhusisha tena katika ushirika wake. Katika mfano wa sarafu iliyopotea Mungu ni kama mama mmoja anayetumia juhudi na nguvu zote ili kukuta kitu alichopoteza naye anapopata hiki anafanya sikukuu. Katika mfano wa mwana mpotevu, macho yetu yamlenga baba aliye mhusika mkuu wakati wote. Uhusiano wake wa mapendo kwa vijana wake ndio umuhimu wa tukio hili. Kulingana na Yesu, Mungu ni kama baba mmoja aliye na watoto wawili na kushiriki nao zawadi zake kwa njia sawa. Yeye anawapenda wote na kutaka wajione katika uzoefu  wa familia kwa kushiriki katika furaha yake ya baba. Utunzaji na ulinzi wake ni maana nzuri ili wabaki pamoja naye daima.

    Yule ndogo alichukua nafasi ya kuenda zake akiacha ushirika wa baba yake. Yeye alifanya hivyo sio kwa sababu hajihisi kupendwa bali kwa sababu alihisi mwenye uhuru. Ndio hivyo uzoefu ya upendo wa Mungu Baba, yaani unaheshimu kila mtu na kumruhusu kuchagua kwa uhuru kabisa njia yenyewe ya maisha yake. Tunapotenda dhidi ya Mungu kupitia dhambi, Yeye anajihisi ameachwa na kusalitiwa, lakini hashindwi kutupenda. Yeye anashughulika sana kwa ajili ya maisha yetu kwa kutupa ulinzi na utunzaji wake. Kwa hivyo kwa kufikiria upendo wake kwetu tunahisi majuto na hamu ya kurudi tena kwake. Ingawa tunashindwa kuishi kama wana, Mungu hashindi kuishi na kutenda kama Baba mwema kamwe.

       Katika mfano huu yuko pia mwana mkubwa ambaye hajihisi mwana wala ndugu. Kosa la utoto ni kwa sababu anajiona kuwa ni mfanyakazi; kosa la undugu ni kwa sababu anamkataa ndugu yake mdogo. Tabia ya huyo mwana mkubwa inaizuia furaha kamili ya baba na ukamilifu wa sikukuu. Kumrudia Mungu ni maana ya furaha kubwa kwake. Lakini furaha yake itakuwa kubwa zaidi ikiwa wale ambao wanajiona watoto wake waweze kushiriki katika hisia zake kuwahusu wengine. Hataki kwamba tuwe na wivu kuhusu njia yake ya kupenda bali tutende kama yeye alivyo. Kwa hivyo Yesu alisema, “Muwe na huruma kama Baba yenu alivyo.” Upatanisho na wengine ni kipimo ili uhusiano wetu na Mungu uwe kweli. Hii ni njia ya kweli ya toba iliyo mwendo wa muda mrefu na huanza mioyoni mwetu. Turuhusu kuguswa na huruma ya Mungu ili tuweze kuwa vyombo vya huruma hii kwa wale wanaohitaji msamaha wetu.

sábado, 7 de setembro de 2019

MASHARTI YA KUMFUATA KRISTO


               
Kutafakari kuhusu Lk 14: 25-33



     Umati wa watu waliandamana na Yesu, lakini sio wote waliokubaliana naye. Alipoitambua hali ya kutokuwa na ahadi na makubaliano, aligeuka na kuwalekeza baadhi ya maneno. Maneno yake yalikuwa nafasi ya kutafakari kwa kweli maana ya safari yao. Ingawa Yesu alikuwa maarufu, kwa sababu ya mambo mema aliyofanya kwa ajili ya watu, utume ambao Yesu alichagua kutimiza mapenzi ya Mungu hauleti umaarufu. Watu walichanganyikiwa kuhusu Yesu kwa sababu hawakumjua bado na kumfuata kwa njia yoyote.

      Kama Yesu hakuwa na nia ya kumdanganya yeyote, aliongea nao kwa uwazi sana kuhusu maana ya kumfuata na matokeo ya uamuzi huu. Njia hii ya kusema ilikuwa tabia yake ya kawaida kama alivyofanya kwa ajili ya wale kumi na wawili, yaani aliwajulisha masharti ili wawe wanafunzi wake wa kweli. Kutoka kwao, Yesu hakutarajia werevu ama upumbavu, bali kupatikana na hatia. Hawawezi kumfuata Yesu kwa sababu walipokea habari tu ya kuwa ni vizuri kufanya hivyo. Yesu anatarajia zaidi, yaani mabadiliko ya ndani.

        Andiko hili ni mwaliko wa kuchukua ahadi ya kumfuata Kristo kwa kupanga mambo ya kesho, yaani kuwa na uwezo wa kuona mbele ili kuepuka kufaragua. Ni vizuri kuota ndoto lakini ndoto hii inapaswa kuihusu hali halisi mtu anayoishi, vinginevyo itakuwa udanganyifu tu. Yesu anataka kuepuka kwamba safari ya wafuasi wake iwe pasipo maana ama ya udanganyifu. Ni lazima utambuzi, hekima, kupanga na uamuzi.

     Mungu mwenyewe anatupa mfano wa kuwa na mipango ya muda mrefu ili tupate mafanikio katika safari yetu kama wafuasi wa Yesu. Yeye Mungu alipanga kumtuma mkombozi, kulingana na yaliyoandikwa: “... wakati maalum ulipotimia, Mungu alimtuma Mwanawe aliyezaliwa na mwanamke... ili apate kuwakomboa waliokuwa chini ya sheria.” (Wagalatia 4: 4-5). “Hata baadhi ya wakulima hutegemea mvua inyeshe hata kama hawajaandaa shamba mahali pa kupanda mbegu kama za mahindi au maharagwe.” Kupanga mambo ya kesho ni muhimu.

       Yesu alisema, “Basi, kadhalika kila mmoja wenu asiyeacha vyote alivyo navyo, hawezi kuwa mwanafunzi wangu.” Kama ilivyotekea katika vifungu vingine, Yesu aliwapendekezea watu mpango wa maisha unaojumuisha kujinyima, kwa sababu yeyote anayekutana na Yesu kwa kweli amekwisha pata hazina ya kweli kwa maisha yake wala hawezi kubaki alivyo, yaani mambo mengine hayana maana tena kama kwanza. Kwa maneno mengine, Yesu anataka kuwa kipaumbele maishani mwa wanaoamua kumfuata. Hakuna jambo lingine ambalo liweze kuitoa maana ya kweli kwa maisha yao ila Yesu peke yake.

    Wanafunzi wa Yesu wa kweli walimtegemea Mungu katika mambo yote kama Yesu alivyo. Yeye alishiriki na wanafunzi wake ufalme wa mbinguni na kuwajulisha njia ya msalaba ili waweze kufanya mapenzi ya Baba yake. Kupitia njia hii, tunatambua kwamba Kumfuata Yesu hakuuleti upendeleo au hadhi, bali mateso na kujisalimisha kwa ajili ya ufalme wa Mungu. Basi, yeyote anayetaka kuishi bila ahadi hawezi kumfuata Yesu. Tena yeyote ambaye anatamani kumfuata Kristo bila msalaba hatapata kumfuata kwa kweli kamwe.

       Kupitia njia ya unyenyekevu na utupu Yesu alipata utukufu. Utambulisho wa wanafunzi wa mwalimu Yesu unapaswa kufuata njia sawasawa naye. Kwa upande wa Kristo msalaba ulikuwa sehemu muhimu katika mwendo wa kufanya mapenzi ya Mungu na kudhihirisha kwa mpango wa upendo wake. Kwa upande wetu kama wanafunzi, kuchukua msalaba ni ishara ya utayari wetu kwa mapenzi ya Mungu kwa kujitolea kama Kristo. Kwa kufikia lengo hili tunapaswa kujikana nafsi yetu, yaani kujisahau sisi wenyewe ili wengine waweze kukumbukwe. Tunapaswa kujikana sisi wenyewe ili Mungu aweze kujifunua kwa nguvu yote ya upendo wake. Tunapaswa pia kujiondoka kutoka katikati/mahali muhimu ili wengine waweze kuwa na nafasi ya kwanza. Kwa maneno mengine, tunapaswa kuwafikiria wengine ni wamuhimu kuliko sisi wenyewe. Kama haiwezekani kumfuata Kristo bila msalaba, mfano wake wa uaminifu kwa mpango wa Mungu utuimarishe katika safari yetu ya yetu ya kujitolea kwa ajili ya ufalme wa Mungu.

Fr Ndega