segunda-feira, 24 de agosto de 2015

MANENO YA UHAI WA MILELE


Kutafakari kuhusu Yohana 6: 60-69

     Katika injili, tuko mbele ya maneno ya mwisho ya Yesu katika sura hii ya sita ya Yohane, baada ya mwujiza wa mikate na samaki. Kile Yesu alichoongea mpaka sehemu hii ya mwisho kilikuwa kigumu sana kwa wasikilizaji wake kufahamu na kukubali. Tumetafakari kwamba Yesu alijaribu kuwathibitishia kuhusu utambulisho wake kama mkate unaoshuka kutoka mbinguni na mkate ambao ni mwili wake wenyewe,  lakini hakupata mafanikio maana ya mawazo yao yaliyofungwa. Ishara zilizotumiwa na Yesu zilikuwa ngumu sana kwa wale ambao walikuwa na kujua awali kuhusu mwelekeo wa binadamu wake. Walijua Yusufu baba yake, Maria, mama yake na walishiriki pamoja shule moja. Hakika hawakuweza kukubali kwamba mwenzao huyu alishuka mbinguni. Lakini ugumu huu wao haukumzuia Yesu awadhihirishie njia tofauti na iliyojaa ya maana kwa maisha yao.

       Yesu alipoongea na watu akaongea kuhusu hali ya milele, ambayo ni mwisho wa safari ya maisha yetu. Anataka kusikika kwa sababu Neno lake lenye nguvu, linachoma mioyo na kusababisha uamuzi. Hakuna hata mmoja asikilize neno hili na kubaki alivyo. Miongoni mwa wale waliosikiliza Yesu walikuwapo wanafunzi kumi na wawili. Ingawa maneno haya yalikuwa magumu pia kwa wao, wanatambua kitu ambacho hakikutambuliwa na wengine. Hali hii ilionyeshwa kupitia tangazo la Petro: “Bwana, tutakwenda kwa nani? Wewe unayo maneno ya uhai wa milele. Sisi tunaamini na tunajua kwamba wewe ndiwe yule Mtakatifu wa Mungu.” Tunajua kwamba ingawa wanafunzi kumi na wawili walikuwapo pamoja na Yesu tangu mwanzo wa huduma yake kwa umma, hawakuweza kuingiza jumla maana ya utambulisho na ujumbe wa Mwalimu, lakini maneno haya ya Petro yanaonyesha ridhaa ya ndani kwa mtu na mpango wa Yesu. Maneno ya Yesu yaliyapigia chapa maishani mwao njia maalum kwamba hawawezi kupata maana mbali na Mwalimu.

     Kama hii lazima kuwa utambulisho wetu na mtu wa Yesu. Baba Mtakatifu Francisco amesisitiza sana kuhusu mahitaji ya “mkutano wa binafsi na Yesu” ili aliyemfuata aweze kumshuhudia kwa uaminifu. Yesu ni Neno lililofanyika mwili na Neno hili linayatoa maana kwa maisha yetu. Kwa hivyo tunaalikwa kuchukua tangazo la Petro kama rejea ili tuwe na tabia kamili mbele ya Neno la Mungu. Kuhusu mambo hayo Mtakatifu Yohana Calabria alisema: sisi ni makini sana kwa maneno ya binadamu na kuhusu hiyo ni sawa. Lakini sisi lazima kuwa na uangalifu zaidi kwa Neno la Mungu ambalo ni – consecratory – linafanya wakfu, ni kwamba, linalifanya lile linalosema.” Mtakatifu Yohane Calabria alikuwa anasema hasa kuhusu injili ambayo ni sheria kwetu - Poor Servants of Divine Providence. Katika sehemu nyingine ya maandiko yake alisema: “Ikiwa sisi huamini katika maneno ya kuapishwa kwa – consecration – katika misa: “twaeni mle wote, twaeni mnywe wote”, sisi lazima kuamini pia wakati Yesu asema: “Msiwe na wasiwasi” au “Baba yeno wa mbinguni anajua kwamba mnahitaji vitu hivyo vyote” au mtafuteni kwanza juu ya ufalme wa Mungu na matakwa yake, na hayo yote mtapewa kwa ziada.” katika maneno mengine, kutokana na Maneno ya Yesu tunaalikuwa kuwa “Injili hai.” Hili ni lengo la Maneno ya uhai wa milele.


      Kupitia adhimisho la Ekaristi tunalishwa na mkate wa Neno na mkate wa Ekaristi. Katika uzoefu huu Yesu anajitoa jumla kwetu, kuchoma mioyo yetu na kutushibisha ili tuwe na hamasa na shauku katika kazi zetu. Eukaristi hii itusaidie kufikia lengo hili.

Fr Ndega
Mapitio: Sara

Nenhum comentário: