domingo, 2 de agosto de 2015

MUNGU ANAENDELEA KUONYESHA UPENDO NA UTUNZAJI WAKE


Kutafakari toka Kutoka 16: 2-4, 12-15; Efe. 4: 17, 20-24; Yn. 6: 24-35

         Mungu anawapatia watu wake chakula ishara ya uzima wa milele ambao tunaupokea katika kila Ekaristi takatifu tunayoadhimisha.
       
        Ingawa wana wa Israeli walikuwa watumwa katika Misri, wakawa na vyakula vingi ili wale hata kushiba. Walipoacha Misri na nguvu ya Mungu, wakapata utambulisho mpya kama Watu wenye uhuru.  Utambulisho huu mpya ulileta baadhi ya changamoto kama kuishi jangwani, kuwa na chakula kidogo au kutokuwa na chakula, kutokuwa na maji, uvamizi/utekaji na watu wengine, na kadhalika. Hali hii ya kutokuwa na chakula iliwafanya kulalamika dhidi ya Musa na Mungu. Mungu Aliyasikiliza malalamiko yao, kupitia upatanishi wa Musa na akionyesha upendo na utunzaji kwao, akawapa mkate kwa kila siku, yaani, mana. Wakala wakashiba.

       Mt. Paulo anafanya tofauti wazi kati ya maisha ya mtu kabla ya ubatizo na kutoka ubatizo. Kabla ya ubatizo mtu huishi maisha ya dhambi na bila ahadi. Kupitia ubatizo mtu anabadilishwa kabisa na kualikwa kuishi maisha mapya, yaliyojaa na maana. Mbele ya majaribio ya kuishi kama kabla ya utambulisho huu mpya, Mt Paulo anatuonya tuishi kama wautu wapya, yaani tuishi kitakatifu. Hii ni hali ya mtu aliyepokewa kuzaliwa kupya katika kristo.

       Yesu alitenda ishara kuu, kupitia kushirikiana kwa mikate na samaki kwa umati wa watu, akiwaonyesha unyeti mbele ya mahitaji yao na uamuzi kuhusu hali ya wenye njaa. Baada ya kula hata kushiba watu walitaka kumfanya Yesu mfalme wao. Yeye akijua mpango wao alitoroka akienda mlimani peke yake. Lakini watu walimtafuta na walimkuta na wanafunzi wake katika kapernaumu. Kulingana na Yesu hawakufahamu ishara na hawakuwa na maana kamili ili kumtafuta. Kwa hitimisho aliwaalika kumkubali kama mkate wa kweli kutoka kwa Mungu ambao unaupa ulimwengu uzima. Yeyote ambaye anakuja kwake na kumwamini hataona njaa na kiu kamwe.

        Yesu alikuwa na unyeti mbele ya mahitaji ya watu na alijaribu kuutoa mwelekeo upya kwa maisha yao kupitia uzoefu wa huruma na kushirikiana, lakini maana ya tumbo lao, wakawa vipofu na wasio na imani. Hawakufikia mafanikio katika kumtafuta Yesu kwao kwa sababu ya Kutokuwa na maana kamili. Kwa kweli nia ya Yesu akiwalisha watu ilikuwa kuwaandaa kwa mafundisho yake kuhusu mkate tofauti na kweli. Yeye anatutolea chakula kinachodumu mpaka uzima wa milele ambacho ni yeye mwenyewe. Anadhihirisha pia kwamba siyo Musa ambaye aliwapa watu mana, lakini ni Mungu. Mana ni mfano wa zawadi kuu ambayo Mungu aliitoa kwa uzima wa ulimwengu, ambaye ni  Mwanawe wa pekee. Kupitia Neno lake na kujitoa kwake Mwanao katika Ekaristi, Mungu anaendelea kuwalisha watu wake na kuwaonyesha upendo na utunzaji wake.

        Basi, Ekaristi ni ishara kubwa ya upendo wa Mungu na maonyesho ya kujitoa kwake Kristo kwa bure. Ekaristi ina maana tu ikiwa ni maonyesho ya upendo na udugu. wale tu wanaopenda kwa kweli wanaweza kwenda mpaka matokeo ya mwisho kama Kristo alivyo. Upendo tu unazaa ushirika na “vitu tu vinavyofanywa kwa upendo vina ushupavu”. Kupitia Ekaristi tunabadilishwa kamili katika Yule tunayeadhimisha, kukubali ahadi ya kuishi maisha mapya yanayozaliwa kutokana na mkutano naye. Hivyo Baada ya kila adhimisho ya Ekaristi sisi hukubali changamoto ya kurudia shughuli za kila siku kama mashahidi wa Kristo ambaye anayatoa maisha yake kwa upendo ili watu wote wawe na uzima wa milele.

Fr Ndega

Mapitio: Sara

Nenhum comentário: