domingo, 16 de agosto de 2015

CHANZO CHA UZIMA WA KWELI NA FURAHA MILELE

Kutafakari kutoka Mithali 9, 1-6; Waefeso 5: 15-20; Yoh 6, 51-58

     Kulingana na Somo la kwanza, Hekima ni nafsi ya Mungu ambaye anawaalika watu wote kwa sikukuu yake. Kwa watu, Kukubali kushiriki katika karamu hii, ambayo Mungu mwenyewe alitengeneza ilikuwa mwaliko ili kuacha ujinga na kupata kuishi, wakifuata njia ya akili. Mwaliko huu ni ishara ya Ekaristi takatifu ambayo ni Yesu mwenyewe. Yeye anatualika kwenye karamu, kushiriki furaha yake kubwa na uzima wa milele. Mt Paulo anatualika kuishi kama wenye hekima, kutumia kwa njia ya hekima kila nafasi inayotokea. Kulingana naye njia ya hekima ni kugundua na kufanya mapenzi ya Mungu. Roho Mt. ndani ya kila mtu anazaa upatikanaji kwa sauti ya Mungu na uhusiano wema na wengine. 
     
   Kristu aliwaalika wasikilizaji wake kwa uzoefu wa ndani ambao ni ufunuo kuhusu utambulisho wake kama chakula kilichoshuka kutoka mbinguni si kwa binadamu tu bali kwa ajili ya uhai wa ulimwengu wote. “Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu hata alimtoa Mwana wake wa pekee, ili kila amwaminiye asipotee, bali awe na uhai wa milele (Jo 3, 16)”. Mwana anajitoa kama chakula kinachodumu hadi uzima wa milele kwa sababu ya mapenzi ya Baba ambaye ni uhai na anasababisha uzima ndani ya kila mtu anayempokea Mwanawe. Maneno haya ni awali ya mafundisho ya Yesu kuhusu ujumbe wake kama mwokozi na mkombozi wa ulimwengu. Yesu alijaribu kuwathibitishia wasikilizaji wake kuhusu hali hii, lakini hapati mafanikio maana ya mawazo yao yaliyofungwa. Ishara zilizotumiwa na Yesu – “kama mkate unaoshuka kutoka mbinguni” na “mkate huu ni mwili wangu wenyewe” -  zilikuwa ngumu sana kwa wale ambao walikuwa na kujua kwa awali kuhusu mwelekeo wa binadamu wa Yesu. Walijua Yusufu baba yake, Maria, mama yake na walishiriki pamoja shuleni moja. Hakika hawaweza kukubali kwamba mwenzao huyu alishuka mbinguni. Lakini ugumu huu haukumzuia Yesu awadhihirishie njia tofauti na iliyojaa ya maana kwa maisha yao.

    Yesu anaongea kuhusu uzima bila mwisho na kwamba uko kwa wote ambao ni yeye mwenyewe. Inawezekana kuupokea uzima huu kwa kuula mwili wake na kuinywa damu yake, kwa sababu yeye ni hai – hawezi kufa - na anaishi ndani ya wale ambao wanampokea. Yesu halazimishwi kufanya hivyo. Haya ni maonyesho ya kujisalimisha kwake kwa bure, kuendeleza uwepo wake miongoni mwa wanadamu na kufundisha njia ya utimizaji uliojaa. Hiyo ni Ekaristi kama zawadi kubwa ya Mungu ambaye hataki kuwapo mbali ya binadamu. Ekaristi ni hazina ya kanisa, uwepo maalum ya mume wake na awali ya uzoefu wa kiroho yake kama mke wa mume Kristu. Linaishi kwa sababu ya Kristu. Vivyo hivyo ni kwa wote ambao wanashiriki mkate mmoja na kikombe kimoja. Uzoefu huu ni ukamilifu wa ushirika wetu na Mungu, chanzo cha uzima wa kweli na furaha milele.


      Tunapokula chakula cha kawaida miili yetu huweza kuingiza chakula hiki ili uwe na afya nzuri. Kama hii, chakula kinaingizwa na miili yetu. Kuhusu Ekaristi, chakula cha uzima, matokeo ni tofauti: wakati tunampokea Yesu, ni sisi tunaoingizwa naye. Katika maneno mengine, Yesu anatuingiza, anatuchukua kwake ili tuishi naye. Yeye anakaa ndani yetu nasi ndani yake. Anatuunganisha naye, kutuhusisha katika ushirika sawa kati ya yeye na Baba. Bila shaka kwamba matokeo ni pia udugu wenye nguvu na mwafaka miongoni mwetu. Tumwombe Mungu, kupitia sacrament hii takatifu, neema ya kuishi kwa ndani uzoefu wetu na Mwanawe ili tufikie ushirika sawa upo katika Utatu Mtakatifu.

Fr Ndega 
Mapitio: Sara

Nenhum comentário: