terça-feira, 11 de agosto de 2015

KUFUFUKA KWETU KATIKA KRISTU

Kutafakari kutoka Yoh 11: 11-27

        Tunaposherehekea uzima, tunasherehekea fumbo kuu ambalo ni zawadi yenye thamani itokayo kwa Mungu. Katika Kristu zawadi hii inapata ukamilifu na vilevile tunapata kuelewa kwamba maisha hayafikii mwisho hapa. Urithi wa maisha ya wale waliotuacha ina thamani kuu kwetu tunaoitwa kuendelea katika imani  kuishi maisha yenye maana. Ikiwa hatuwezi kuona tena wale ambao walitutangulia, yale maadili waliyoishi na kutuachia ndiyo ushuhuda wa kwamba kuwepo kwao kati yetu hayakuambulia patupu. Mtakatifu John Calabria alikuwa na mazoea ya kusema, “Ikiwa tuna Mungu ndani yetu, tutafanya yale mazuri hata kwa kupita kwetu tu”. Kusherehekea wafu, kwa mfano, ni alama kuu ya kwamba tunafahamu vile wanavyoendelea kuwa muhimu kwetu sote, kwa vile kifo sio mwisho wa maisha haya: kinadhihirisha tu mwisho wa sehemu moja ya maisha. Katika nyakati za sorrow na huzuni, tujiruhusu kusaidiwa na maombi ya marafiki na kuhamasishwa na neno la Mungu linalotuimarisha katika imani na kujitolea maishani.
           Kama Wakristo, tabia yetu kuu ni tumaini. Kwa hivyo, Mt. Paulo akasema: “Na kama Kristo hakufufuka, imani yenu ni bure”. Mungu ambaye tunaamini ni Mungu wa uhai na anapotupa uzima, yeye hujiunganisha nasi na kutufanya wanawe wapendwa. Kwa kuwa mateso katika maisha haya, hakuna kinacholinganishwa na furaha tutakayohisi na utukufu utakaotufunuliwa. Vilevile, tujifunze kutoka kwa Yesu ambaye hata katika wakati wa huzuni na mateso aliyopitia kwa njia ya msalaba, alisimamia imani yake katika tendo la riziki ya Mungu: “Ee Baba, mikononi mwako naiweka roho yangu”. Hili lazima kuwa ujasiri na kilio cha roho zetu ili kutuhakikishia kwamba Mungu hawezi kutuacha wala kunyamaza mbele ya kinachotufanyikia. Jibu kutoka kwa Mungu mbele ya kufa kwa Yesu inaandamana moja kwa moja na ufufuko wake. Hilo linatupa matarajio ya kufufuka kwetu na hivyo, yatuhakikishia maisha kamili kwani yeye si Mungu wa wafu bali wa wanaoishi. Hivyo ni kusema kwamba Mungu hataki kifo. Katika Yesu anajifunua kama ufufuko na uhai.
            Kwa nini watu  hufa? Yesu alitufundisha kukuza imani yetu katika Mungu Baba, ambaye anatuangazia kwa nguvu na sifa yake yote ya pendo lake lenye huruma na ukombozi. Yeye hutuvuta kwake kwa dhamana za huruma na anatamani kuwa mmoja nasi. Kwa wakati huo huo, yeye huja kwa mwelekeo kwetu na hutarajia kukaribishwa. Maisha yetu humu duniani hupita tu sehemu moja. Lazima kuendelea safari yake katika sehemu nyingine, kwa sababu twaitwa kwa ukamilifu. Katika maana hii, Agostino asema: “Ee Mungu ulituumba tuwe wako na moyo wetu unahangaika hadi tunapopumzika kwako”. Kwa Yule mwenye imani, kifo ni pumziko katika Mungu ambako sisi sote lazima kupitia ili kuwa wakamilifu. Wakati muhimu sana maishani mwetu  utakuja na tutakutana na Mungu kwa njia ya kipekee. Tutakapokuwa mbele yake hatutaulizwa iwapo tulishiriki katika dini yoyote wala mara ngapi tulienda kanisani bali kiasi cha tulivyoweza kupenda. Chaguo tunayochagua katika mkondo wa safari yetu itadhihirisha mwelekeo ambao maisha yetu yatachukua. Kulingana na mapenzi ya Mungu, maisha yetu yanafaa kupata ukamilifu uanzao na uangalifu wa kila siku katika ishara za upendo nyumbani na kujitolea kwa jumuiya. Kwa hivyo tunapata kuungana na Mungu aliye mwanzo na chanzo cha uzima na asiyepungukiwa kamwe.

Fr Ndega

Mapitio: Sara

Nenhum comentário: