quinta-feira, 29 de outubro de 2015

MTAKATIFU YOHANA CALABRIA NA WAGONJWA

Kutafakari kuhusu Is 49: 14-15; Mt 6: 24-34

        Liturujia inatujulisha mifano miwili yenye nguvu kuhusu Mungu. Katika Somo la kwanza Mungu analinganishwa kwa mama na katika injili Mungu analinganishwa kwa baba. Mungu anawapenda watu wote na hamsahau yeyote wa wana wake. Yeye anakijali kila kitu ambacho wana wake wanahitaji. Mtakatifu Yohana Calabria aliishi kwa uzoefu huu kwa mkazo na aliweza kuushuhudia kwa wengine. 

   Watu wa Israeli walikuwa watumwa katika Babeli na wakajihisi walioachwa na kusahauliwa. Nabii Isaya aliwasaidia kutambua kwamba Mungu alikuwapo miongoni mwao na hakuwasahau. Yeye ni Mungu mpole ambaye anawapenda na kuwalinda watu wake zaidi kuliko mama ampendaye mtoto wake anyonyaye. Basi, uwepo wake ni dhamana ya utunzaji na ulinzi. Katika injili Yesu anawafundisha wanafunzi wake kuhusu umuhimu zaidi wa maisha. Anaongea kuhusu hatari ya utajiri na miliki yote ambayo inaweza kumshika mtu hivi hata asiweze kifikiria mambo yanayomhusu Mungu. Nia kuu ya Yesu ni kuongea kuhusu Mungu kama Baba aliye na wasiwasi kwa utunzaji wa upendo kwa kila kitu. Baba huyu anatarajia jibu la ukarimu kutoka kwa wanadamu ambao wana thamani zaidi kuliko viumbe vingine vyote. Kuwa mwanafunzi wa kweli wa Yesu ni kutafuta kwanza Ufalme wa Mungu Baba na haki yake kama rejea ya maisha. Kwa maneno mengine, anatualika kujisalimisha mikononi mwa Mungu ambaye anayajua mahitaji yetu na yuko tayari daima kutusaidia.

       Injili hii inafikiriwa msingi wa kiroho ya Mt. Yohane Calabria kwa sababu kupitia injili hii aliufanya ugunduzi mkubwa. Aligundua jinsi ya kuishi kwa njia halisi ubaba wa Mungu na kuwa ishara ya riziki yake kwa watu. Kutokana na andiko hili alichukua mistari 33 kama ahadi kwake: “Mtafuteni kwanza Ufalme wa Mungu na haki yake; na hayo yote mtapewa kwa ziada.” Kulingana naye “Injili anatuongelea kwamba Mungu ni Baba, anatujali zaidi kuliko ndege wa angani na maua ya mashamba hata atatujalia kile ambacho tunahitaji kwa chakula na kwa mavazi, lakini tunapaswa kuutafuta kwanza Ufalme wake na haki yake”. Mt Calabria alifahamu kwamba ililazimu kuifufua imani duniani kwa Mungu Baba wa wanadamu wote, kupitia kujisalimisha kabisa kwa Riziki yake. Kwake imani kweli na asili inafikiria Mungu si kama Muumba na Bwana tu, bali kwanza kama Baba”. Mungu ni Baba, hutujali na wote ambao tunawapenda; macho yake ni makini sana kwa kila kitu na kila kitu kinapangwa na kuongozwa na hekima, nguvu na wema wake pasipo mwisho.

      Mt. Yohana Calabria alikuwa mtu mwenye unyeti mno kuuhusu ugumu na mateso ya wengine.  Aliweza kuweka matendoni maneno yake kuhusu wema na utunzaji wa Mungu katika Riziki yake, akisema, “Riziki ni Mama mpole ambaye hupatia kila kitu kwa wema wetu, hata kwa wema wetu mkubwa. Tunapaswa kuhisi tumebebwa kwa mikono yake ya mama”. Yohana Calabria aliamini katika ukweli huo na hata aliyapanga maisha na kazi zake zote kulingana na hali hii. Kama ishara ya utunzaji wa Mungu alikuwa na unyeti mkubwa kwa uhusiano na wagonjwa. Alimwona Kristo mwenyewe katika walio wagonjwa. Alifikiria mateso ya wagonjwa kama thamani na msaada mkubwa kwa mtume wa kanisa. Aliwahamasisha na kuwaonya wagonjwa kuukaribisha ugonjwa na mateso kwa utulivu na sala. magonjwa kwao yana maana kwa wokovu wao na wokovu ulimwenguni. Kristu mwenyewe aliwapenda wagonjwa na wakati wa maisha yake alikwenda mara nyingi kuwatembelea na kuwaponya. Kwa njia Mtakatifu Yohana Calabria, tumwombe Mungu kwa ajili ya wagonjwa wote, hasa kwa hawa ndugu zetu wapo katika misa hii ili neema ya Mungu iimarishe imani na nguvu zao. Maisha yenu yawe ushuhuda wa wema wa Mungu kwa sisi sote.

Fr Ndega
Mapitio: Sara

Nenhum comentário: