segunda-feira, 2 de novembro de 2015

KIFO KWAKE KRISTO NDICHO USHINDI WETU

Kutafakari kutoka Yoh 11: 11-27

        Tunaposherehekea uzima, tunasherehekea fumbo kuu ambalo ni zawadi itokayo kwa Mungu. Katika Kristu zawadi hii inapata ukamilifu na vile vile tunapata kuelewa kwamba maisha hayafikii mwisho hapa duniani. Urithi wa maisha ya wale waliotuacha ina thamani kuu kwetu tunaoitwa kuendelea katika imani  kuishi maisha yenye maana. Ikiwa hatuwezi kuwaona tena wale ambao walitutangulia, yale maadili waliyoishi na kutuachia ndiyo ushuhuda wa kwamba uwepo wao kati yetu haukuwa utupu. Mtakatifu John Calabria alikuwa na mazoea ya kusema, “Ikiwa tuna Mungu ndani yetu, tutafanya yale mazuri hata kwa kupita kwetu tu”. Kusherehekea wafu ni alama kuu ya jinsi wanavyoendelea kuwa muhimu kwetu sote, kwa hivyo kifo sio mwisho wa maisha: hiki kinadhihirisha tu mwisho wa sehemu moja ya maisha. Katika nyakati za sorrow na huzuni, tujiruhusu kusaidiwa na maombi ya marafiki na kuhamasishwa na neno la Mungu linaloimarisha imani yetu na uwezo wetu wa kujitolea .
           Kama Wakristo, tabia yetu kuu ni tumaini. Kwa hivyo, Mt. Paulo akasema: “Na kama Kristo hakufufuka, imani yenu ni bure na tumaini letu pasipo maana”. Mungu ambaye tunaamini ni Mungu wa uhai na anapotupa uzima, yeye hujiunganisha nasi na kutufanya wanawe wapendwa. Kwa kuwa mateso katika maisha haya, hayawezi kulinganishwa na furaha tutakayohisi na utukufu utakaotufunuliwa. Vilevile, tujifunze kujisalimisha kutoka kwa kielelezo cha Yesu ambaye hata katika wakati wa huzuni na mateso, aliyohisi kupitia msalaba, aliilenga imani yake katika tendo la riziki ya Mungu: “Ee Baba, mikononi mwako naiweka roho yangu”. Hili lazima kuwa kilio cha roho zetu ili tuhakikishie kwamba Mungu hawezi kutuacha wala kunyamaza mbele ya kinachotufanyikia. Mbele ya kufa kwake Yesu Jibu la Mungu ni ufufuko wa Mwanawe. Hilo linatupa matarajio ya kufufuka kwetu na hivyo, yatuhakikishia maisha kamili kwani yeye si Mungu wa wafu bali wa wanaoishi. Hivyo ni lazima kutangaza kwamba Mungu hataki kifo. Katika Yesu anajifunua kama ufufuko na uhai.
            Kwa nini watu  hufa? Yesu alitufundisha kulenga imani yetu katika Mungu Baba, ambaye anatujali kwa nguvu yote ya pendo lake lenye huruma na ukombozi. Yeye hutuvuta kwake kwa dhamana za huruma na anatamani kuwa mmoja nasi. Kwa wakati huo huo, yeye huja kwetu daima na hutarajia kukaribishwa. Maisha yetu duniani hupitia sehemu moja tu. Yanapaswa kuendelea safari yake katika sehemu nyingine, kwa sababu twaitwa kwa ukamilifu. Katika maana hii, Agostino asema: “Ee Mungu ulituumba tuwe wako na mioyo yetu inahangaika hadi tunapopumzika kwako”. Kwa Yule mwenye imani, kifo ni pumziko katika Mungu ambako sisi sote lazima kupitia ili tukuwe wakamilifu. Wakati muhimu sana maishani mwetu  utakuja na tutakutana na Mungu kwa njia ya kipekee. Tutakapokuwa mbele yake hatutaulizwa iwapo tulishiriki katika dini yoyote wala mara ngapi tulienda kanisani bali kiasi cha tulivyoweza kupenda. Chaguo tunayochagua katika mkondo wa safari yetu itadhihirisha mwelekeo ambao maisha yetu yatachukua. Kulingana na mapenzi ya Mungu, maisha yetu yanafaa kupata ukamilifu uanzao na uangalifu wa kila siku katika ishara za upendo nyumbani na kujitolea kwa jumuiya. Kwa hivyo tupate kuunganishwa na Mungu aliye mwanzo na chanzo cha uzima na asiyepungukiwa kamwe.


Fr Ndega

Nenhum comentário: