domingo, 6 de março de 2016

MUNGU ANAFURAHI TUNAPOMRUDIA YEYE


Kutafakari kuhusu Lk 15, 1-3.11-32

Sura ya kumi na tano ya toleo la Luka ni maarufu miongoni mwa mifano ya Yesu. Hii inaitwa sura ya Mifano ya huruma. Tuna mifano mitatu (Kondoo aliyepotea: 4-7; Sarafu iliyopotea: 8-10; Mwana mpotevu: 11-32). Lakini siku ya leo liturjia inatujulisha moja peke yake, yaani, mfano wa mwana mpotevu. Mfano huu unaonyesha tabia ya huruma ya Mungu kuhusu wenye dhambi na furaha ya kukutana tena na yule ambaye alipotea. Kwa kufahamu nia ya Yesu kwa uhusiano na mifano hii tunahitaji kutafakari kwanza kuhusu mazingira ambayo Yesu aliishi. Katika muktadha huo, baadhi ya watu walijiona wanastahili upendo wa Mungu zaidi kwa ajili ya uaminifu wao kwa Sheria. Walichukua mamlaka ya kuwatenganisha watu, wakiwapanga kama wema au wabaya. Mamlaka haya hayatoki kwa Mungu kwa sababu kipimo ni ubaguzi. Walisahau kwamba mbele ya Mungu watu wote ni sawa. Mungu habagui katika upendo wake. Kwa upande wake watoza ushuru na wenye dhambi ni watoto wake sawa na Mafarisayo na Waandishi wa Sheria. Ikiwa hao wanaweza kuzaa ndugu, tena wanaweza kuishi katika ushirika na Mungu, anayekaribisha kila mtu ili awaokoe wote.
      Ingawa yako matukio mengi katika Agano la Kale, ambayo yanaonyesha njia maalum ya Mungu ya kutenda, ni “katika Yesu Kristo kwamba huruma ya Mungu imepata kuwa hai na yenye kuonekana, na hata ilifikia kilele chake katika Yeye... Yesu ni uso wa huruma ya Baba. Kila kitu ndani yake kinaongelea huruma. Hakuna chochote kwake kinachopungukiwa na huruma (Baba Mt Francisco).”  Kama alama ya huruma ya Mungu, Yesu ana chaguo wazi sana, yaani, “Mwanamume huyu anawakaribisha wenye dhambi naye hata anakula nao”. Maneno haya yalisemwa na wale waliompinga Yesu. Kwa kweli, Yesu aliongea kuhusu huruma ya Mungu si kwa maneno tu, bali “kwa neno lake, matendo yake na kwa nafsi yake yote.” Yeye alitumia ishara nyingi za makaribisho, akithibitisha lengo la ujumbe wake na ukweli wa mafundisho yake. Kwa kweli, watozaushuru wengi, makahaba na wengine waliokataliwa na jamii walijihisi wamekaribishwa na Yesu na, kwa hivyo, kubadilishwa kwa mkutano na huruma ya Mungu.
      Ingawa katika mfano wa mwana mpotevu tunasikia tukio la kijana mdogo na hisia za kijana mkubwa, lakini ni baba wa vijana hawa wawili ndiye aliye mhusika mkuu wakati wote. Uhusiano wake wa mapendo kwa vijana wake, ambao wote ni wapotevu kwa njia tofauti ndio umuhimu wa tukio hili. Kulingana na Yesu, baba huyo ni kama Mungu ambaye ana watoto tofauti na kushiriki nao zawadi zake kwa njia sawa. Yeye anawapenda wote na kutaka kwamba watu wote wajihisi wakiwa katika familia, kushiriki kwa furaha yake kama Baba. Katika familia hii anautoa utunzaji na ulinzi ili wawe na maana nzuri ili kubaki naye daima. Wakati yeyote anaamua kutenda kinyume naye na kubaki mbali sana naye, sio kwa maana mtu huyo hajihisi kupendwa, bali ni kwa sababu anajiona mwenye uhuru. Kama huu ni uzoefu wa upendo wa Baba: huu ni huria na kuuzaa uhuru. Sisi pia tunahisi mbali sana na Mungu wakati sisi hutenda kinyume naye, yaani, tunapomkosea. Yeye anajihisi ameachwa na kusalitiwa, lakini haachi kutupenda. Kama yule baba, Mungu anashughulika sana na maisha yetu. Anakuja kututafuta ili kutupa sisi ulinzi na utunzaji wake. Kwa hivyo tunahisi majuto na kivutio ya kuishi tena uzoefu wa ushirika tumeopoteza. Ingawa mara niyingi tunakataa utambulisho wetu wa wana, kupitia dhambi zetu, Mungu haukatai utambulisho wake wa Baba kamwe.

      Katika mfano huu yuko pia mwana mkubwa ambaye hajihisi mwana kwa sababu anajiona kuwa ni mfanyakazi wala anajihisi ndugu, kwa sababu anatojali ndugu yake mdogo. Tabia ya huyo mwana mkubwa inaizuia furaha kamili ya Baba na ukamilifu wa sikukuu. Kumrudia Mungu ni maana ya furaha kubwa kwake. Lakini furaha yake haiwezekani kuwa kabisa ikiwa hatushiriki katika hisia zake kuhusu wengine. Hataki kwamba tuwe wivu kuhusu njia yake ya kupenda; anataka kwamba tutende kama yeye alivyo. Kwa hivyo Yesu alisema, “Muwe na huruma kama Baba yenu alivyo.” Upatanisho na wengine ni kipimo ili uhusiano wetu na Mungu uwe kweli. Hii ni njia ya kweli ya toba iliyo mwendo wa muda mrefu na huanza mioyoni mwetu. Kupitia Ekaristi hii, turuhusu kuguswa na huruma ya Mungu ili tuweze kuwa vyombo vya huruma hii kwa wale wanaohitaji msamaha wetu.

Fr Ndega
Mapitio na marekebisho: Sara

Nenhum comentário: