sábado, 9 de outubro de 2021

UCHAGUZI UNAOTULETEA FURAHA KAMILI

 


Tafakari kuhusu Hek 7, 7-11; Wab 4, 12-13; Mk 10, 17-30

 


    Mada kuu ya tafakari hii ni Hekima. Asili yake ni Mungu naye ilijifanya kuonekana katika nafsi ya Yesu Kristo, ambaye alijitambulisha kama "Mkate ulioshuka kutoka mbinguni", yaani Hekima ya Mungu iliyofanyika mwili katika hali ya kibinadamu. Kwa maana hii, mtu mwenye hekima kweli ni mtu tu ambaye anashikilia kabisa mafundisho ya Yesu Kristo, kipimo cha furaha kamili.

    Somo la kitabu cha Hekima, kwa sambamba na Injili, inaleta ushuhuda wa Sulemani, ambaye alichagua hekima badala ya nguvu na utajiri. Hekima haiwezi kulinganishwa na kitu chochote kilichopo hapa duniani. Ni zawadi kutoka Juu na hupewa kwa mtu yeyote anayeitafuta na kuipendelea kuliko vitu vingine. Tunapaswa kuiomba kwa unyenyekevu na uvumilivu, tukijua kuwa ni nia ya Mungu mwenyewe kutuipatia ili tuweze kufanya uchaguzi kulingana na mapenzi yake, kama vile Sulemani mwenyewe alivyofanya.

    Kifungu kutoka kwa Waraka kwa Waebrania ni wimbo kwa Neno la Mungu. Hili ni hai na wenye ufanisi na kwa sababu hii, ina uwezo wa kuingia ndani yetu kwa kina, ikituwezesha kufanya kila kazi njema. Uwezo wa kupambanua unatoka kwa Neno kwa sababu hili ni chanzo cha hekima. Tunapolikaribisha vizuri na kuruhusu tendo lake maishani mwetu, hubadilisha moyo wetu wa jiwe pole pole, kuufanya uwe na hisia na upatikanaji kwa mapendekezo ya kimungu.

    Wakati wa maisha ya Yesu ya umma, watu wengi walimjia, wakiruhusu kuguswa na kubadilishwa na neno lake. Mara kadhaa, Yesu aliweza kuhisi furaha na kuridhika kwa matokeo mazuri ya “kampeni” yake ya wito. Lakini kwa mtu huyo anayeonekana katika Injili ya leo, hali ilikuwa tofauti kabisa, kwa sababu, ingawa alikuwa na hamu ya uzima wa milele ndani yake, moyo wake ulikuwa umefungwa na kuhusishwa na shughuli nyingi. Kwa kweli, mtu huyo alikuwa na bidii, alipatikana, alifuata amri za zamani, lakini aliishi bila maana sana, kwa sababu maisha yake yalilenga tu kutimiza sheria na kuwa na mali.

    Yesu alimwona kwa upendo, kama anavyofanya mtu ambaye anataka kukabidhi mtu mwingine kitu cha maana sana kwa sababu anajua kuwa mtu mwingine huyo ana uwezo wa kuchukua ahadi. Mwaliko wa kumfuata Yesu, basi, unatokana na mtazamo wa upendo ambao unaingia ndani kwa kina, unamvutia mtu na kumtongoza. Mtazamo huu unafikiria muhimu uzoefu wa imani, kupitia amri na pia unapanua upeo wa macho kupitia pendekezo jipya la maisha, ambalo halitegemei kuheshimu sheria au ukali wake, bali kujinyima na kushiriki mali. Kwa maneno mengine, Yesu anatualika tumfuate kwa busara.

    Mabadiliko ya kweli lazima pia yatekelezwe kwetu, kwani Neno ambalo kwa kawaida Yesu anatuelekeza huleta pendekezo ambalo husababisha mapasuko kadhaa. Ikiwa tunamfuata Yesu, tuyakatae mawazo ya ukusanyaj ama tubaki kwa mawazo hayo na kumkataa Yesu. Mtu hawezi kuchagua Yesu na kuendelea vivyo hivyo, kwa mfano, kuendelea na tabia sawasawa mbele ya mali kama mwanzo. Bila mabadiliko ya mawazo hakuna kumfuata Yesu wa kweli.

    Kwa kawaida tuko na ngumu ya kuchagua vizuri kwa sababu tunafikiria sana juu ya kile tunachopaswa kuacha ama kukataa. Mtu wa injili alifanya chaguo mbaya sana maishani mwake kwa sababu hakutaka kukataa. "Sisi pia tusifanye makosa yale yale kwa sababu wakati Bwana anatupa jukumu kubwa hivyo ni kwa sababu, kwanza, alitufikia na muonekano umejaa upendo, akitupatia msaada kwa jibu kulingana na matarajio yake". Na hii inatutosha.

    Mbele ya mazingira ambayo yajionyesha yamejaa mapendekezo ya kuvutia ni lazima hekima nyingi na ujasiri wa kinabii kwa kuchukua ahadi muhimu kama ile ambayo Yesu anatualika leo. Nayo haijahifadhiwa kwa wengine tu... Kila mtu ameitwa kuishi njia ya maisha ya unyenyekevu na kujinyima, akiweka tumaini lake kwa Mungu zaidi kuliko vitu alivyo navyo. Kujitolea kwa utumishi wa kindugu na kushiriki mali alizo nazo kwa walio na shida kunaonyesha kwamba tunaelewa kuwa uzima wa milele unaanza hapa duniani, na kutufanya tupate furaha iliyozidishwa katika kila tendo mema kwa ajili ya wengine.

    Tujiruhusu kupendwa na Bwana na kukubali pendekezo lake ambalo linatuhakikishia uhuru wa kweli, masharti ya kimsingi ya kupata uzima wa milele ambayo unaanza tunapoamua kumwamini na kumfuata. Atupatie hekima yake ili tuweze kuwa na tabia kamili mbele ya mali na kuchukua wito wetu kama wanafunzi kwa upatikanaji kabisa kwa kumtumikia yeye kwa nafsi ya ndugu na dada zetu.


Fr Ndega

Nenhum comentário: