domingo, 26 de junho de 2016

KUJIKANA NA KUJINYIMA KAMA MASHARTI KUMFUATA YESU NA KUPATA UZIMA


Kutafakari kutoka Lk 9, 51-62


     Baada ya Petro kumkiri Yesu kama Kristu, aliye Masiya wa Mungu, Yesu aliwalika Thenashara wote wamfuate katika kujisalimisha kwake ili wapate uzima. Yesu alitambua kwamba walihitaji kujua zaidi kuhusu maana ya umasiha wake na kuyafahamu vizuri mapendekezo yake. Kwa hivyo, alitumia wakati wa safari hadi Yerusalemu kuwafundisha kamili. Mambo mengi yanatokea wakati wa safari hii na hayo yote yalikuwa nafasi ya mafundisho, hasa kuhusu njia kamili ya kutenda mbele ya kukataliwa. Safari kwenda Yerusalemu siyo safari ya kimwili tu bali ni hasa ya kiroho. Mwanzoni mwa injili inasemekana kwamba “wakati siku za kupaa kwake zilipokuwa karibu kutimia...” Basi, hii ni safari kuelekea mbinguni. Mti wa Yerusalemu unafahamiwa kama “Mti wa Mungu” ulio makao ya dini ya kiyahudi. Ingawa Yesu anajua kwamba mti huu ni mahali pa kuwaua manabii, kama ishara ya upinzani kwa mavutio ya Mungu, hata hivyo anataka kwenda huko ili mapenzi ya Mungu ya kuwaokoa watu wake yatimie.

      Kwa kufika mahali huko Yerusalemu ilikuwa lazima kupitia katika eneo la Samaria. Basi, Yesu aliwatumia baadhi ya wanafunzi wamtangulie katika Samaria wamtengenezea mahali pa kupumzika kidogo kwa sababu ya safari ya muda mrefu. Wanafunzi wa Yesu walikuwa na mazoea ya kushughulika kwa mawazo na tabia tofauti na mwalimu wao. Hii ndiyo maana ya kupatwa na hasira sana walipokataliwa wakipita katika Samaria, na kutaka Mungu aliteketeze eneo hilo. Katika safari hii kwenye Yerusalemu Yesu alikuwa akiwaongoza wanafunzi wake katika njia ya upatanisho na amani. Kwa hivyo hakubali pendekezo lao na kuwapendekezea kwenda kijiji kingine, yaani, njia nyingine. Kumfuata Yesu si rahisi sana. Wakati uliopita tulitafakari kuhusu masharti matatu ya kumfuata kwa uaminifu, yaani, “kujikana mwenyewe, kuuchukua msalaba wa kila siku na kumfuata Yesu.” Siku ya leo masharti yanaendelea kuwa matatu, lakini hapo ni kama onyo, shauri. Yesu hataki kuwadanganya wafuasi wake kupitia ahadi pasipo maana. Katika mapendekezo yake, Yesu ni wazi sana. Yeye anauheshimu uhuru wa watu, lakini anayajulisha masharti kwa wale ambao wanataka kumfuata. Vingenevyo hawatapata kumfuata kwa uaminifu.

      Wanafunzi wa Yesu walitaka kutenda kwa njia ya kibinafsi, yaani bila utambuzi na kutafakari (ishara ya kutokwepo kwa Kristo moyoni mwao). Walikuwa waaminifu kwa mwelekeo wa kibinadamu wa kisasi kuliko njia aliyopendezwa Yesu. Mwaliko waa Yesu wa kuenda mahali pengine ni uthibitisho kwamba ni lazima kuheshimu uhuru wa watu. Kumfuata Yesu ni kuchagua kuishi na kutenda tofauti. Mtu hawezi kutazama nyuma ili aongozwe kulingana na hali ya zamani kukanusha utambulisho mpya ulio matokeo ya mkutano na Kristo. Katika mwendo wa kumfuata Yesu mtu anakuwa mtumishi wa ufalme wa Mungu. Katika mwendo huu masharti hayatoki kwa mtu bali yatoka kwa Yesu. Kutazama nyuma kunaweza kuwa hatari kwa safari kwa sababu katika safari hii muhimu sana sio tulichoacha nyuma bali tutakachopokea mbele kwa sababu ya uamuzi wa kumfuata Yesu. Bila kujikana na kujinyima mtu hawezi kumfuata Yesu na kupata uzima. 


Yesu halazimishi uhuru wa wanafunzi wake, lakini anaanzisha masharti ili waweze kumfuata kweli. “Kama wafuasi, wakristo tunaweza kukosa uvumilivu na kuwadharau watu wa makanisa, dini na imani nyingine. Kama Wayahudi na Wasamaria, Wakristo wa Afrika kutoka makabila mbalimbali wanaweza kuwa na chuki kubwa kati yao, kiasi cha kushiriki katika mapigano ya kikabila. Huu siyo mwelekeo wa Yesu.”  Kutokana na mfano wa Kristo, anayeitwa pia mtu asiye na ukatili, njia ya kipekee ya kuushinda ukatili ni kujibu kwa ishara za amani. Yesu anataka kwamba tabia zetu zishinde mwelekeo wa jamii kwenye kisasi, ukatili na ukabila. Ukabila unauharibu undugu, kukanusha utambulisho wetu wa wakristo. Yesu anatualika kufahamu kuwa uovu hauwezi kuondoa uovu, bali ni wema tu unaoweza kufanya hivi. Ekaristi hii takatifu itusaidie kupenda kama Yesu alivyo na, kupitia upendo huu, tuweze kuijenga jamii inayotarajiwa na Mungu.

Fr Ndega
Mapitio na marekebisho: Sarah

Nenhum comentário: