sexta-feira, 24 de junho de 2016

MUNGU ANATUPATIA YALE TUNAYOHITAJI


Kutafakari kuhusu Mt 6, 24-34

Kifungu hiki cha injili ni andiko la msingi wa kiroho ya Mt. Yohane Calabria. Huyu ni mwanzilishi wa Shirika letu, yaani, Poor Servants of Divine Providence. Alianza kuwajali watoto maskini na yatima kwa sababu alitambua kwamba tendo hili lilikuwa mapenzi ya Mungu. Nambari ya watoto iliongezeka daima na vyakula havikutosha kwa wote. Lakini Mungu aliyekuwa makini sana kwa hali hii, akapatia daima yale ambayo Yohane Calabria na watoto waliyahitaji kwa kuishi. Hali hili ilidhihirisha maneno ya injili ambayo tunatafakari.
Kwa upande wa Mungu, yeye anajua kwamba tunahitaji mambo hayo yote. Kwa upande wa binadamu ni lazima kuwa na imani na kujisalimisha mikononi mwa Mungu ambaye ni Baba na Mtoaji. Mtakatifu Yohane Calabria alikuwa na uhakika kuhusu hali hii kwa sababu “aliishi injili na kwa injili”. Kupitia Injili aliugundua ubaba wa Mungu kwa njia halisi sana. Ugunduzi huu mkubwa ulisimuliwa na Askofu aliyeitwa Chiot kutoka Jimbo la Verona - Uitalia ambaye alitembelewa na Mt Calabria kwa kumjulisha kuhusu tukio muhimu. Huu ni msukumo katika safari yetu kama watoto wa Mungu.
“Usiku mmoja, padre Calabria aliandika na kuituma barua kwa baba askofu Chiot akisema, “ningojee kesho saa nne asubuhi maana nahitaji kuongea nawe. Wakati padre Calabria alipofika nyumbani mwa Askofu Chiot, baba huyo alimwuliza swali: Je, bahati mbaya gani ilitokea? Barua yako ilinisumbusha. Padre Calabria akamwambia, “hapana bahati mbaya; hili ni jambo la ajabu.” - “La ajabu!”, aliuliza baba Chiot. Naye padre Calabria aliendelea kwa kusema, “Alisoma injili nzima!” Baba askofu alisema, “Hili si jambo la ajabu!” Je, inawezekana kuwepo padre ambaye hajasoma injili nzima?” Padre Calabria alisema, “Tafadhali, niruhusu kueleza. Mimi pia nimekwisha soma na kuihubiri injili, lakini juzi baada ya kuishi kwa ugumu mchana kutwa na bila kupata utulivu kwa kulala usingizi, nilichukua inijili na kuisoma nzima pamoja na kitabu cha Matendo ya Mitume. Nilipata kusoma kila kitu kwa usiku mmoja peke yake. Jambo hili lilisababisha uzoefu wa ajabu maishani mwangu. Kweli injili ni jambo kubwa! Nimestaajabia. Hebu, sikiliza! “Msiwe na wasiwasi kuhusu maisha yenu: mtakula nini au mtakunywa nini, au kuhusu miili yenu, mtavaa nini. Waangalieni ndege wa angani, wao hawapandi wala hawavuni au kuweka ghalani, lakini Baba yenu wa mbinguni huwalisha hao. Fikirini maua ya shambani yameavyo. Hayafanyi kazi wala hayafumi. Lakini nawaambia, hata mfalme Solomoni katika fahari yake yote hakuvikwa kama mojawapo ya hayo maua.”
Padre Calabria ailikuwa amesisitiza yaliyomhakikishia maana ya kweli ya kuishi na kutangaza, yaani Mungu ni Baba nasi tu watoto wake. Alichukua kama ahadi na mpango wa maisha kwake na kwa shirika lake zima maneno ya mstari wa 23, yaani, “Mtafuteni kwanza Ufalme wa Mungu na haki yake na hayo yote mtapewa kwa ziada.”
Je, Maneno haya yana maana gani katika safari yetu siku ya leo? Kulingana na Yesu hatuwezi kuwatumikia mabwana wawili, yaani Mungu na mali. Mali inaweza kuvuruga uangalifu wetu kwenye njia ya Mungu ya kutenda na kuwajali watoto wake. Yesu hakanushi kwamba sisi tunahitaji mambo mengi. Lakini anajua kwamba kosa la utambuzi linatuongoza kuishi kwa wasiwasi na kusumbukika kuweka uangalifu katika yale yasiyo muhimu sana.
Kulingana na mafundisho tumepokea kutoka kwa Yesu Mungu ni Baba kabla ya kuwa Muumba. Yeye si kama baba yeyote bali yu Baba Mwema ambaye anashughulika sana na hali ya wana wake. Yeye analinda na kutunza bila kulala. Yeye anajua mahitaji ya wana kabla ya wamwombe kitu. Kwa utunzaji wa upendo Mungu anashiriki zawadi zake na wana wake, kutarajia kwamba tufanye vivyo hivyo kwa ajili ya wengine ili undugu kati yetu uwe maonyesho ya ubaba wake. Matatizo yote yapaswa kufikiriwa na kusomeka kwa maelewano na ubaba wa Mungu.” Mungu hamsahau hata mmoja wa wana wake.

Tunaalikwa kumwelekea kwa imani na kuwa na uhakika kwamba tumepokea sana. Mungu hatupatii daima yale tunayomwomba, bali anatupatia daima tunayohitaji. Ikiwa hatupokei yale tunayomwomba yeye ni kwa sababu hatuombi ipasavyo. Tufanye upya imani yetu katika riziki yake kuwa na tabia kamili katika ushusiano wetu naye.  

Fr Josuel Ndega
Mapitio na marekebisho: Sarah

Nenhum comentário: