sexta-feira, 29 de janeiro de 2016

MAPENDEKEZO YA YESU YALISABABISHA UMWINGILIO KWA WENZAKE


Kutafakari kuhusu Yer 1, 4-5. 17-19; 1Kor 12,31. 13,1-13; Lk 4, 21-30

Liturjia ya jumapili hii inaongea kuhusu umuhimu na hatari za unabii. Kwa kuchukua kazi hii ngumu ni lazima ujasiri na utayari, hasa katika mazingira magumu kama yale ya Yeremia na Yesu. Somo la kwanza anasimulia wito wa Yeremia kama historia ya upendo. Mungu mwenyewe anamwita ili awe mjumbe wake. Mungu anajua kuhusu ugumu na udhaifu wa Yeremia na, kwa hivyo, anaahidi utunzaji na ulinzi. Wito wa Yeremia ni matokeo ya uzoefu wa Neno la Mungu ambalo linampa uwezo wa kuongea na kushauri kwa jina la Bwana. Nabi wa kweli hasemi katika jina lake mwenyewe, bali asema tu yale ambayo Bwana anamwamuru kusema. Kulingana na somo la pili msingi wa uzoefu wa binadamu ni upendo. Upendo lazima kuwa hamasa ya matendo yetu kwa sababu bila upendo kila kitu tunachofanya ni bila maana. Kama sisi ni manabii tangu ubatizo, wito wetu ni pia historia ya upendo na mafanikio katika safari yetu inawezekana tu kupitia upendo. Upendo ni maana ya utambulisho wetu kama wakristo.    
Kulingana na kutafakari kwetu kuhusu injili ya jumapili iliyopita, Yesu alienda kijijini mwake Nazareti na kutangaza Neno la Mungu kama mpango wake wa maisha. Watu walishangazwa sana kwa sababu ya maneno ya neema yaliyotoka kinywani mwake. Kwa kweli Yesu aliishi kwa furaha na shauku utambulisho wake kama aliyechaguliwa na Mungu ili atangaze mpango wa upendo na wokovu wake. Uzoefu wake miongoni mwa wenzake ungalikuwa mzuri ikiwa Yesu angalisema tu yale ambayo walitaka kusikiliza. Lakini Yesu hana hofu na neno la Mungu halina mipaka. Aliwapendekezea njia mpya ya maisha na mabadiliko ya mawazo. Pendekezo la Yesu si ngumu; yeye anatarajia tabia tofauti tu. Hii ndiyo ni maana ya umwingilio wao/kukasirika kwao. Mara nyingi maneno ya Yesu yalisababisha mabadiliko maishani mwa watu wengi kwa sababu maneno yake yana nguvu yenyewe. Kwa hivyo alipata wafuasi wengi. Ikiwa mabadiliko yaliyotarajiwa hayatokei kwa baadhi ya watu, shida siyo kwa upande wa Yesu.  
Watu wa kijiji cha Yesu walijua kila kitu kumhusu yeye na walitumia hiki kama kipimo cha hukumu au utambuzi. Kujua kwao kwa awali kumhusu Yesu kuliwazuia kumjua nani ndiye. Yesu kama wokovu wa Mungu, ndiye utimizaji wa maandiko, lakini alikataliwa na wale wanajiona waliojua maandiko. Labda walikuwa na mazoea ya kukubali tu yale yaliyokuwa rahisi kwao, wakirekebisha Neno la Mungu kulingana na njia yao ya maisha, bila kuwa tayari ya kuishi kwa mapitio yanayotokana na Neno hili. Walimkataa Yesu kwa sababu walijifunga kwa upya wa Mungu uliodhihirishwa na Mwana wake. Ilikuwa ngumu sana kwao kufahamu kwamba ingawa Yesu alikuwa mwana wa Yosufu ndiye Mungu kweli. Je! Kujua kwetu kuhusu Yesu kumetusaidia kukua katika imani na kuimarisha uhusiano wetu naye?

Wakati Yesu alichukua hali yetu ya binadamu, alijitambulisha na hali hii, lakini akatambua pia kwamba vitu vingi vilipaswa kubadilika. Kwa hivyo alijulisha pendekezo mpya la maisha. Kwa upande wetu, kuishi kwa uhusiano wa kweli na Yesu hautoshi mshangao mbele ya hekima ya maneno yake kama wenzake walivyo, bali tunapaswa kuruhusu kwamba ujumbe wake wa upendo na ahadi uwe hai ndai yetu. Kama watu kutoka Nazareti, mara nyingi sisi pia tumelipinga Neno la Yesu ambalo linauliza maswali kuhusu tabia na matendo yetu ya kila siku. Kushiriki katika utume wa Yesu ni kuchukua pamoja naye hali ya wengine, hasa watu maskini. Hatuwezi kufikiri kwamba habari tumepokea kuhusu Yesu yatosha kwa safari yetu ya wito. Ni muhimu kuruhusu kwamba yeye mwenyewe ajidhihirishe kwetu kwa nguvu yote ya upendo wake siku zote za maisha yetu. Kama ilivyotokea na Yesu, sisi pia tunapaswa kuwa watu ambao wanalenga mapendekezo ya Neno la Mungu. Turuhusu kwamba maneno haya yatuongoze ili tufanye mapenzi ya Mungu. 

Fr Ndega
Mapitio: Sara

Nenhum comentário: