domingo, 28 de junho de 2015

KUZALISHA NA KUSAIDIA UZIMA MIONGONI MWA WATU


Hek 1: 13-15; 2: 23-24; 2Kor 8: 7.9.13-15; Mk 5: 21-43

      Kulingana na mpango wa upendo wake Mungu, tuliumbwa kwa uzima. Kupitia Yesu Kristu, amezalisha na kusaidia uzima miongoni mwa watu. Tunapitia mauti wakati hatupendi, kuonyesha upinzani dhidi ya mipango ya Mungu.  

      Somo la kwanza kutoka kitabu cha Hekima linaongea kwamba Mungu ni Mungu wa uhai. Aliviumba vitu vyote na ameongoza kila kitu kwa hekima na wema. Hakuyaumba mauti, na kila kitu anafanya ni kwa wema wa wana wake ili wawe na maisha mengi. Ulikuwa mpango wa Mungu kuumba binadamu kama yeye mwenyewe na kuwakabidhi utunzaji wa vitu vyote. Mungu aliwapa zawadi ya maisha ya milele, akionyesha furaha yake yote na uradhi kuhusu tendo maalum la mikono yake. Kuwepo kwa mauti si mpango wa Mungu; mauti hayatoki kwa yeye. Yalianzishwa duniani na shetani kwa sababu ya wivu na upinzani wake dhidi ya mapenzi ya Mungu. Yeye ni adui wa Mungu na wale tu ambao wameamua kumtumikia shetani, wakifanya upinzani dhidi ya Mungu, watayapitia mauti.   

     Kabla ya mahitaji ya wakristu wa kanisa la Yerusalemu, Mt Paulo anauliza usaidizi kutoka jumuiya zingine za kikristu, ambazo zinajibu mara moja. Katika andiko hili tuna kielelezo kizuri cha jumuiya ya Wakorinto. Mt Paulo anatambua na anasifu zawadi za jumuiya hii, hasa zawadi za imani na huduma ya ukarimu. Kupitia tabia hizi wanatenda kulingana na ukarimu na utupu wa Kristu ambaye, ingawa alikuwa tajiri, akajifanya maskini ili awatajirishe watu kutokana na umaskini wake. Huu ni mwaliko kwa kushiriki na wengine zawadi zilizopokewa, kuishi kwa njia ya halisi umoja wa Mwili wa Kristu.

     Wanafunzi walikubali changamoto ya kulivuka ziwa tena hata baada ya uzoefu wa kutisha wa dhoruba (kulingana na Injili ya wiki iliyopita). Lakini sasa, kwa kutambua uwepo na nguvu ya Yesu, wana maana nzuri kulivuka ziwa na kuyachukua matokeo ya kuishi na Yesu katika upande mwingine, ni kwamba, kufikiri, kuhisi na kutenda tofauti. Lengo la ujumbe wa Kristu ni kuusaidia uzima miongoni mwa watu. Anafanya hili kwa nguvu yote ya upendo wake. Kama hili lilitokea kupitia miujiza miwili iliyojulishwa katika injili siku ya leo. Yesu anayatoa maisha mapya kwa mwanamke aliyeteseka kwa kutokwa na damu kwa miaka kumi na miwili, na anafufua binti wa Yairu. Katika miujiza hii miwili ilikuwa muhimu sana tabia ya imani ya watu hawa wawili ambayo ilitambuliwa na Yesu na kuwekwa kama kigezo cha msingi ili kuruhusu tendo la Mungu ambaye anataka kuokoa na kutoa maisha mapya.


      Watu wengi walikuwa karibu na Yesu, lakini mwanamke huyo tu alimgusa kwa imani. Kwa hivyo Yesu anauliza maswali, “Nani aliyegusa mavazi yangu?” swali hili linatufanya kutafakari kuhusu utambulisho wetu kama wakristu, ambao tunaishi karibu na Yesu, kushiriki kwa sakramenti, hasa Ekaristi takatifu, lakini pasipo imani au kwa imani ndogo. Hali halisi hii inatuzuia kufikia mabadiliko ambayo tunahitaji kwa maisha yetu. Hiyo ni kama kulivyotokea katika Nazareth ambapo Yesu hakuweza kufanya mwujiza kwa sababu ya kutokuwa na imani ya watu. Binti Yairo ni ishara ya maisha yetu ambayo yanahitaji kuhamasishwa na kufufuliwa. Imani ya Yairo ni imani ya jumuiya yetu, ambayo lazima kuwa macho ili itambue Yesu na imruhusu kushiriki nguvu za uhai zake nasi. Anajua kwamba bila kitendo chake maishani mwetu hatuwezi kufanya chochote. Yeye afufue imani yetu ndogo ili tutangaze kwa shauku uhai wake wa ufufuko na ushiriki wetu naye. Ili ushiriki wetu katika kila Ekaristi takatifu uwe maonyesho ya uhusiano wetu wa ndani naye. 

Fr Ndega
Mapitio: Sara

Nenhum comentário: