quinta-feira, 11 de junho de 2015

FUMBO LA MWILI NA DAMU YA KRISTU


Kutafakari toka Kutoka 24: 3-8; Ebr 9: 11-15; Mk 14: 12-16, 22-26

       Siku ya leo tunaalikuwa kuadhimisha sikukuu ya Mwili na Damu ya Kristu, fumbo la imani yetu. Hii ni nafasi maalum kuonyesha shukrani yetu na upendo wetu kwa zawadi kuu ya Ekaristi takatifu. Hii ni siku ili kutafakari kuhusu uwepo wa kweli wa kristu katika maumbo ya mkate na divai. Ekaristi takatifu ni fumbo la kujisalimisha kwake kwa upendo kwa wokovu wa ulimwengu. Ekaristi ni adhimisho la fumbo la Mungu ambaye anatumikia, yupo karibu nasi na ndani yetu. Hilo ni fumbo la ushirika ambao tunahusishwa kama washirika katika uhai wake. Ekaristi ni sakramenti ya Agano jipya na milele kupitia hilo Kristu anatuunganisha naye na miongoni mwetu wenyewe kama wana wa watu wapya wa Mungu, Kanisa.

       Masono ya leo yanaongea kuhusu hali halisi hii. Kulingana na somo la kwanza, umuhimu wa agano ambalo Mungu anaanzisha na watu wake ni Amri kumi. Amri ni mwongozo, zawadi zake Mungu kwa watu ili waishi kulingana na matarajio yake. Musa ni mpatanishi mwema ili maneno ya Mungu yatangazwe kwa watu kikamilifu yakiwahamasisha kuchukwa Amri hizi kwa uaminifu. Damu ya wanyama  waliomchinjia Mungu ikanyunyizwa juu ya watu ikithibitisha ahadi ya kubadilishana kati ya Mungu na watu wake. Somo la pili linaongea kwamba Yesu ni Kuhani wa agano jipya na milele. Ukuhani wake ni mkubwa zaidi kuliko ukuhani wa agano la kale  kwa sababu una asili ya Mungu. Yeye hakuhitaji kumtolea Mungu sadaka, bali alijitoa kama sadaka kamili na, kupitia damu yake alipata wokovu kwa ubinadamu wote.

       Hali halisi ambayo Injili linatutafakarisha ni Ekaristi ambayo ina mizizi katika ibada ya Wayahudi. Yesu alitaka kusherehekea pasaka na wanafunzi wake. Basi, akihisi wenye uhuru kabisa, "Alitwaa mkate, akashukuru, akaumega, akawapa...” “Kisha akatwaa kikombe akifanya vivyo hivyo na wote wakakinywea”. Vitendo hivi vya Yesu na wanafunzi wake vilivyofanyika katika hali ya familia na kujiamini, vilikuwa mwaliko wa uzoefu wa kushiriki pamoja na makubaliano. Mkataba kati ya Mungu na watu wake katika agano la Sinai ulishindwa na Yesu ambaye alifanya mkataba mpya, Agano jipya kati ya Mungu na Watu wake wapya  - ambalo ni Kanisa. Akitumia Ibada ya Wayahudi, Yesu alianzisha Ibada mpya, ni kwamba, Mlo wa Ekaristi, akitangaza kwa Wafuasi wake ukombozi kamili ambao ulikuwa ukija na kwamba alitamani kwa shauku kushiriki na rafiki zake. Katika karamu hii ya mwisho, Yesu alijitoa kama chakula na kinywaji, akionyesha maana ya kujisalimisha kwake kwa uhuru na kwamba pia lazima kuwa tabia ya maisha ya wafuasi wake. Wao lazima kuendelea mwendo huu kwa kumkumbuka Yesu.

       Hili ni fumbo la imani yetu:  tunaalikwa kuadhimisha fumbo la Mwili na Damu ya Kristu kwa upendo na unyenyekevu na kumjua Mungu kama yeye ndiye. Hili ni Fumbo la Paska, ambalo linajumuisha mateso, kifo na ufufuko wa Yesu. Yeye alianzisha Ekaristi akiutoa mwili na damu yake katika ibada, akiandaa wanafunzi wake kwa kujisalimisha kwake msalabani. Katika sakramenti hi jumuiya ya kikristu inaalikwa kuhisi mmoja na Kristu, kuchukua naye tangazo la ushindi wake juu ya mauti ambao unakamilika na maisha mapya yanapatikana kwa wote.


      Katika Ekaristi uwepo wa Yesu ni hai, wenye nguvu, una maana ufanisi, wenye uwezo wa kutoa matokeo mazuri. Yesu katika Ekaristi huleta mabadiliko katika maisha yetu. Kama hii, katika Ekaristi tunabadilishwa katika fumbo tunaloadhimisha, kukubali ukweli wa Fumbo la pasaka kama “Pasaka ya Kristu katika Pasaka yetu na Pasaka yetu katika Pasaka ya Kristo”. Hivyo baada ya kila adhimisho ya Ekaristi tuna changamoto kurudia shughuli za kila siku kama mashahidi wa Kristo anayetoa maisha yake kwa upendo kwa wote kuwe na maisha kamili. Basi, tumshukuru Mungu kwa uzoefu wa udugu tunaoishi katika kila misa takatifu tunayoadhimisha. Ili tuweze kulima uhusiano wa ndani na Yesu ili kutumikia wengine kwa ukarimu.

Fr Ndega 
Mapitio: Sara

Nenhum comentário: