sexta-feira, 29 de maio de 2020

KUJENGA MAISHA YETU KULINGANA NA THAMANI ZA KWELI


       Msomaji mpendwa, kwa Tafakari hii, ningependa kuwasilisha maono ya kidini ya thamani. Kwanza kabisa, nimeshangaa kwa sababu nikienda kwenye kamusi ya Kiitaliano kwa kutafuta maana ya thamani nimepata maana 17 tofauti. Bila shaka, Nilichagua moja ambayo inaihusu tafakari iliyopendekezeka, yaani: thamani kama fadhila, heshima ya roho. Thamani zina mengi ya kuhusiana na hisia ambazo tunahisi katika uzoefu wetu. Thamani “ni kama alama za vidole: ni tofauti kwa kila mmoja wetu na tunaziachia popote tulipo kwenda.” Hebu tufikiri kuhusu wapendwa wetu ambao walikutangulia katika uzima ya milele: thamani ambazo waliishi na kutuacha hushuhudia kwamba safari yao miongoni mwetu haikuwa bila maana. Basi, kwa upande wetu, thamani tunazoishi, ni hizi kweli tunazotaka kuzitoa kama urithi kwa vizazi vijavyo?

    Dunia yetu inakabiliana na mgogoro mkubwa wa thamani. Hizi (thamani) zimeshindwa kupata nafasi zao za kweli, yaani sisi hatuwezi tena kufahamu tofauti kati ya kile kilicho muhimu sana na kilicho muhimu kidogo tu. Kila mtu anahitaji mzani wa thamani ambao ni wa msingi ambao kupitia juhudi za mtu unaweza kutoa mwelekeo kamili kwa maisha yake mwenyewe. Wengi wetu hatujui thamani za msingi za maisha yetu wenyewe kwa sababu tunaathiriwa kwa urahisi na mazingira ambayo tunaishi: familia, shule, marafiki, jamii, nk. Bila shaka haya ni msaada wa kwanza ambao kila mmoja wetu anahitaji. Lakini ni lazima tujiulize: ni thamani gani zinazoyahusu maisha yangu sasa? Ni nini muhimu sana? Kwa njia hii, tunaanza kupanga mzani wetu wa thamani.

     Kuwa na mzani wa thamani ni muhimu sana hata tunaweza kumwambia mtu, “nionyeshe mzani wako wa thamani nami nitamwambia wewe ni nani!” Kwa maana hii, “mzani wa Thamani ungepaswa kuwa kwa sikuzote za maisha nao hauwezi kusukumwa na ulimwengu, lakini uwe matokeo ya utafutaji makini, kwa sababu ubora wa maisha yetu na chaguo tunazochukua zinautegemea mzani wa thamani wetu. Wale wanaoishi imani ya Kikristo anakiri kwamba ndiye Kristo ambaye anaonyesha mzani wa kweli wa thamani. Mambo aliyotenda na kuyafundisha, yaani thamani za injili, kinakuwa kipimo kwa ajili ya uzoefu wa mtu yeyote duniani, hata kwa wasioamini.

    Ninapodhani kuhusu Mtakatifu Yohane Calabria, kwa mfano, ninamwona yeye kama mtu wa imani kuu, ambaye aliupanga mzani wake wa thamani kutoka mpango fulani, yaani: “Utafuteni kwanza ufalme wa Mungu na haki yake, na hayo yote mtazidishiwa.” Hii ni usemi mmoja wa injili wa Mathayo (Mt 6:33). Mambo yote Mtakatifu huyo aliyodhani kwa ajili ya maisha yake na ya Shirika lake linaloitwa Familia ya Kikalabria (Poor Servants of Divine Providence) hupata msingi na uthabiti yake katika mpango huu. Kutokana na mpango huu tuko na thamani kama ubaba wa Mungu, utunzaji, uaminifu, imani, ujasiri, utambuzi, uamuzi, nk.

   Tunapofikiri kuhusu thamani ya mtu mwenyewe, hatuwezi kutumia kipimo cha kijamii, vinginevyo tutashawishiwa kumfikiria kutoka uwezo wake wa kujitokeza, kuwa bora kuliko wengine, kushindana. Katika injili, mashindano kwa ajili ya nafasi ya kwanza, kwa upendeleo na kwa umaarufu, yalimfanyisha Yesu kusema, "kati yenu isitukie hivyo.” Kutoka kwake Yesu Tunaelewa njia kamili ya uhusiano kati ya watu mambo muhimu ya kutafuta ili kutoa maana ya kweli kwa maisha yenyewe. Mawazo ya Yesu ni mawazo tofauti na mawazo ya kitupu ya binadamu, yaani kuwa wa mwisho ili kuwa wa kwanza; kuwa mtumwa wa wote ili kuwa wakuu; kupoteza maisha ili kuyapokea tena; kufa ili kuishi. Mambo yote yazitegemea chaguzi zetu.

     Mwandishi fulani asema kwamba “njia ya furaha na kutimiza kwa kibinafsi lazima inazihusu chaguzi tunazochukua.” Hatutaki kuishi kwa kulalamika milele kwa sababu ya kile hatunacho, bali tuweze kutambua vizuri kabla ya kuuchukua uamuzi wowote kwa sababu kila uamuzi huleta hasara na faida. Heri aliyejifunza kulima maishani mwake thamani za kweli; hatavunjika moyo katika wakati wa msingi wa kuwepo kwake. Nataka kumalizia kwa kuonyesha kwako, msomaji, thamani zingine ambazo Maandiko Matakatifu hutupatia na ambazo zinaweza kutusaidia sana katika mpango wa mzani wa thamani wetu ambao utatia msukumo kwa maisha yetu, kwa mfano:

- AMINI: Mithali 3.5: "Mtumaini Bwana kwa moyo wako wote.” Kuamini ni kuwa na hakika kwamba Mungu anatulinda na kwamba Yeye huyaongoza maisha yetu.

- UKARIMU: Methali ya 11.17: “Wale ambao ni wakarimu hupata faida daima.”

- UWAZI: Mithali 11, 20: “Bwana hapendi wale ambao mioyo yao si ya haki, lakini anafurahia wale ambao njia zao ni halali.” Mungu hapendi uwongo, anataka tuwe waaminifu, wa hiari, na wa kweli.

- UKWELI: Mathayo 7:12: “Yoyote myatakayo mtendewe na watu, nanyi watendeeni vivyo hivyo.”

- IMANI: Mathayo 9:29: "kisha Aliyagusa macho yake na kusema, ' kwa kadiri ya imani yenu mpate!”

- UPATIKANAJI: Luka 1:38: “Mimi ndiye mtumishi wa Bwana, na iwe kwangu kama ulivyosema.”

- UNYENYEKEVU: Matendo 2:46: “Wao walimega mkate nyumba kwa nyumba na kushiriki chakula chao kwa furaha na kwa unyenyekevu wa moyo."

- MSHIKAMANO: Matendo 4.32: “Walioamini walikuwa na moyo mmoja na roho moja; walikuwa na vitu vyote shirika.”

- UPENDO: Matendo 9.36: “Yeye alikuwa amejaa matendo mema na sadaka alizozitoa.”

- KUHUDUMIANA: 1Petro 4.10: “kila mmoja wenu kwa kadiri alivyoipokea karama, itumieni kwa kuhudumiana.”


Fr Ndega


Nenhum comentário: