domingo, 1 de outubro de 2017

MAPENZI YA MUNGU YAWE CHAKULA CHA MAISHA YETU


Kutafakari kuhusu Mt 21, 28-32


        Tunaendelea na habari kuhusu mwaliko wa Mungu ili watu wote wafanye kazi katika shamba lake la mizabibu. Uamuzi wetu sio daima kulingana na matarajio yake, hata hivyo, anaendelea kutualika. Katika kifungu cha leo Yesu anausimulia mfano mwingine ambao unaleta kama wahusika wakuu familia fulani ambapo baba mmoja alikuwa na watoto wawili na kumwomba kila mmoja mfanye kazi katika shamba lake la mzabibu. Kila mmoja alijibu kwa njia tofauti na baadaye alibadili jibu lake. Yule ambaye alijibu ‘hapana’, alifikiri vizuri, akatubu na kuamua kufanya kazi. Yule ambaye alijibu ‘ndio’, hakuenda baadaye. Yule aliyefanya mapenzi ya baba ndiye yule ambaye alienda kufanya kazi, hata baada ya wakati fulani.

         Akisimulia mfano huu, Yesu anaongelea tabia tofauti mbele ya mapenzi ya Mungu. Mwana mmoja anawakilisha viongozi wa Wayahudi na mwana mwingine anamaanisha watoza ushuru na makahaba. Hotuba wa Yohana ilikuwa na nguvu ya kuwathibitishia wasikilizaji wake. Bila shaka kwamba kama ilivyotokea na manabii wa zamani, uwezo huu wa kuthibitishia ulitokana na uzoefu wa kweli wa Neno la Mungu. Miongoni mwa wasikilizaji wa Yohane walikuwapo watoza ushuru na makahaba na viongozi wa Wayahudi. Kikundi cha kwanza ingawa walikataliwa na jamii kwa sababu ya maisha yao ya wenye dhambi, watakuwa wa kwanza wa kukaribishwa katika maisha mapya maana walimwamini Yohane na kuyakubali mapendekezo yake.

           Tabia ya viongozi wa Wayahudi ilikuwa tofauti, yaani, walimpinga Yohana Mbatizaji na pendekezo lake la kutubu. Yohane alikuwa mpatanishi tu. Ndilo Neno la Mungu ambalo lina nguvu lenyewe ili kuugusa moyo wa watu na kuubadilisha. Uhusiano ambao vikundi hivi viliishi na Yohana unaendelea vivyo hivyo na Yesu. Mimi nataka kusisitiza kwamba Yesu haidhinishi maisha ya dhambi ya watoza ushuru na makahaba, bali tabia yao ya kukaribisha vizuri ujumbe wake, wakitambua ukweli wa hali yao na kuuomba msamaha. Hilo ndilo jibu ambalo linampendeza Mungu na kuwapa nafasi ya kuokolewa.

       Wakati wa Yesu, namna hii ya watu waliwekwa katika kikundi maalum la wenye dhambi. Kuchanganyika nao kulimfanya mtu apate dhambi yao pia. Yesu alichanganyika nao, akivuka mipaka iliyowekwa na watu kwa sababu kwake mapenzi ya Mungu ni muhimu zaidi kuliko sheria ya usafi/uchafu. Wakati tunajifikiriwa ubora au waliostahili zaidi kuliko wengine tunaweka mipaka kwa mafanikio ya mapenzi ya Mungu na hali yetu inakuwa mbaya zaidi kuliko kabla. Kupitia Neno lake tunaweza kugundua mapenzi yake na kuyapanga maisha yetu kulingana na mapenzi haya.  

      Ndiye Mungu ambaye anachukua nafasi ya kuwalika watu, lakini anangoja na kuheshimu jibu la kila mtu. Kufanya kazi katika shamba la mzabibu kunamaanisha kuingia katika ufalme. Mapenzi ya Mungu ni kuwaokoa wote lakini uamuzi ndio wa watu. Mtu ambaye anajiona wa kwanza atakuwa wa mwisho. Mungu anataka kwamba maneno na chaguzi zetu ziwe kulingana na mapenzi yake kwa sababu hataki mtu akufe bali atubu na kuwa na uzima wa milele. Hasa kwa wale ambao wanamfuata Yesu, mapenzi ya Mungu yapaswa kuwa kama chakula cha kila siku kama yalivyo kwa Yesu mwenyewe. Ikiwa mapenzi ya Mungu ni kipimo cha wokovu hakuna mtu ambaye astahili kuliko wengine. Yeye atupe unyenyekevu ili tutambue hali yetu kama wenye dhambi na mapenzi yake yawe chakula cha maisha yetu kama ilivyotokea na Mwanae.    


Fr Ndega

Nenhum comentário: