domingo, 3 de abril de 2016

KUISHI NA KUSHUHUDIA IMANI PAMOJA NA WENGINE


Kutafakari kuhusu Mdo 5,12-16; Ufu 1,9-11a.12-13.17-19; Yoh 20,19-31

            Siku ya leo ni jumapili ya huruma ya Mungu. Tunataka kujifunza kutoka kwa Kristo jinsi ya kuwa na huruma kwa wengine kama yeye alivyo kwa ajili ya Toma aliye kutokwepo katika jumuiya. Yesu mwenyewe, katika injili ya Mathayo anatuhakikishia: “Heri walio na huruma, maana watahurumiwa” (Mt 5:7). Katika somo la kwanza watu walitambua tendo la Yesu likitendeka miongoni mwao kupitia maneno na matendo ya mitume. Kwa kweli yale ambayo Mitume walifanya yaliwavutia watu, lakini walijiona kuwa vyombo peke yake, kwa sababu mabadiliko maishani mwa watu ni kazi ya Bwana aliye Mfufuka. Katika somo la pili, Yohane alipewa ufunuo wa utambulisho wa Mtu mfano wa Mwanadamu ambaye alikufa, lakini anaishi milele. Bwana huyo anamwalika Yohane kushuhudia bila hofu kwa sababu mauti yalishindwa na hayatawali tena kamwe.

Baada ya ukatili kwa Bwana wao, wanafunzi wa Yesu waliishi katika mazingira ya hofu. Hawakutaka kuwa na mwisho sawa na mwalimu wao, lakini waliendelea wanakutana hata kwa siri. Mambo mengi ambayo walijifunza kutoka kwa Yesu yalikuwa maana kwa utambulisho wao. Basi, ingawa walikuwa na hofu hawakuwa wasio na tumaini. Lakini walikuwako na shida kwa maana yeyote ambaye anafunga milango inawezekana awe na upinzani kwa tendo la Bwana ama ugumu ili awe mashahidi. Kristo aliingia bila kufungua milango kwa sababu, baada ya ufufuko, ana mwili mtukufu, yaani hakuna kitu ambacho kiweze kuweka mpaka kwa mwili wa Yesu. Hali hii mpya ya mwili wake ni tangazo la wakati ujao wa miili ya wafuasi wake walio waaminifu. Yesu aliingia na kusimama katikati. Anajua vizuri hali ya utisho ambayo wanafunzi walikuwa wakiishi. Yeye anapaswa kuwa rejeo maishani mwa wanafunzi na, kwa hivyo, alikuja kuwasaidia katika udhaifu wao akiondoa hofu na mashaka mengi maishani mwao ambayo yanawazuia kumshuhudia kwa kweli.

Matokeo ya kwanza ya uzoefu wa Bwana Mfufuka ni furaha, kuthibitisha kwamba kuwa mwanafunzi wa Yesu ni kuwa mwenye furaha. Furaha inaifungua milango ya moyo kwa kuzipokea zawadi zingine. Nazo zawadi zifuatazo zinadhihirisha ukarimu wa Bwana Mfufuka kwa manufaa ya jumuiya ya wanafunzi wake. Bwana anaijalia jumuiya amani kama utambulisho na Bwana wao aliye “Nabii asiye na ukatili”. Kama Bwana mfufuka yu katikati ya uzoefu wa jumuiya, wana wa jumuiya wanakuwa vyombo vya amani. Zawadi ya Roho Mtakatifu ni uhakika kwamba hatutembei peke yetu. Msaada wake unatukumbusha kwamba lengo la utambulisho wetu kama wanafunzi ni kuusaidia uzoefu wa ushirika na upatanisho. Huyo Roho Mt ndiye Roho wa umoja na kutenda ili tuweze kushinda mgawanyiko na ugumu wa uhusiano miongoni mwetu. Toma hakuwapo katika mkutano wa ufunuo wa Bwana Mfufuka kwa sababu alipendelea uzoefu tofauti. Huyo ni mfano wa wale ambao wana ugumu wa kushiriki pamoja katika jumuiya na kuchagua kuomba radhi kuliko mabadiliko ya tabia yao. Pamoja na imani haba, watu hawa wanaweka vikwazo katika imani ya wengine. Kwa kweli uwepo wao ni hatari kwa imani ya jumuiya.


Lakini Yesu anatenda kwa utulivu na kumsaidia Toma kupitia ishara halisi za ushindi wake. Kama hitimisho, Yesu anampa zawadi ya imani na kumdai aishi imani hii pamoja na wengine, kupendana na kusaidiana kama matokeo ya maisha mapya kutokana na ufufuko wa Bwana wao. Mtu ana ugumu wa kuamini ikiwa anaamini peke yake, yaani, imani yake si kweli. Imani ya mtu lazima kuwa matokeo ya uzoefu wa ushiriki wake katika Kanisa, yaani jumuiya ya upendo, kwa sababu imani ya kanisa inaitangulia, inaizaa na kuilisha imani ya mtu huyo. Bila ushiriki kwa hamu katika Kanisa lililo jumuiya ya wafuasi wa Bwana Mfufuka, tuna ugumu wa kutambua ishara za uwepo wake miongoni mwetu na imani yetu ni haba. Andiko hili linatusaidia kutambua umuhimu wa kushiriki pamoja katika jumuiya. Bwana Mfufuka alitaka kujifunua kwetu kupitia msaada wa wengine. Tunapaswa kuwa macho kwa mwelekeo wa ubinafsi katika jamii ambao unaambukiza uhusiano wetu kutuzuia kuishi kwa ndugu ya kweli. Kupitia ubinafsi uovu mwingi unawezekana kutokea. Yesu anapaswa kuwa katikati ya jumuiya nayo jumuiya inapaswa kuwa na nafasi muhimu katika maisha yetu ili tuweze kushinda hofu na hali mbaya ambayo inatuzuia kuwa mashahidi wa kweli. 

Fr Ndega
Mapitio na marekebisho: Sarah

Nenhum comentário: