quinta-feira, 4 de setembro de 2014

KUHUSU MAISHA YANGU



Mimi ni Josuel dos Santos Boaventura, lakini ninapenda zaidi kuitwa Ndega kwamba inaazimu “Mtu mwema”. Nilizaliwa tarehe ishirini na sita mwezi wa saba mwaka wa elfu moja mia tisa sabini na tatu. Nimetoka Brazil. Jimbo langu ni Bahia na Jina la mji nilipozaliwa ni “Cachoeira”, lakini niliishi daima katika “Conceição da Feira”, kwamba unaitwa pia “Cidade Ternura”, ni kwamba, “Mji wa Huruma”. Niliishi Utoto wangu wote Mjini huo mpaka kwenda seminarini katika mji mwingine, unaoitwa “Feira de Santana”. Shule yangu ya msingi iliitwa “Grupo Escolar Hermilo Cardoso” na Centro Educacional Yeda Barradas Carneiro. Shule yangu ya sekondari iliitwa “Colegio Estadual”. Nilianza kuenda shuleni kuandamana na binamu yangu. Baada ya wakati huo, nikaweza kuenda peke yangu. Nilisoma na nilifanya kazi ngumu sana. Hata hivyo nilipata muda pia kujifunza na kucheza mchezo wa “capoeira”.
Nina familia kubwa kwamba inaitwa “familia ya kasisi”. Baba yangu anaitwa Martins Santos Boaventura. Kazi yake ni kuviweka tayari vyuma kwa kujenga nyumba kubwa. Yeye anapenda kucheza “capoeira” na anacheza ala za muziki vizuri sana. Mama yangu anaitwa Clementina dos Santos Boaventura na anapenda kushona na kutumikia kanisani. Wazazi wangu wangaliendelea wenye nguvu na wananiangalia na upendo muhimu. Nina dada mmoja na kaka sita. Dada yangu anaitwa Joelma na anafanya kazi mkahawani. Kaka yangu mkubwa anaitwa Jose Roque na anafanya kazi kama bawabu wa benki. Kaka yangu Josemir ni polisi. Kaka yangu Josafaa ni mwalimu wa mchezo wa “capoeira” na mchezo wa ndondi. Kaka yangu Josival anafanya kazi katika kiwanda cha karatasi. Kaka yangu Juvandro anafanya kazi katika jiko la watawala wa mji wetu. Mzaliwa wa mwisho Josias ni bawabu wa Kampuni inayochukua pesa.
Katika familia yangu nilikuwa daima mtu maarufu katika sanaa, hasa sanaa ya muziki na kusoma. Kaka zangu na dada yangu walisoma mpaka shule ya sekondari. Nilitaka kuendelea kusoma zaidi ya kaka na dada zangu kwa sababu tangu mtoto mdogo wito wangu ukawa kuwa kasisi, na ili kuwa kasisi ni lazima kusoma sana. Jumapili nikapenda kuenda kanisani kwa misa na kutumikia kama mvulana wa madhabahu. Kama hii, niligundua wito wangu. Wakati mkuu wa maisha yangu ulikuwa nilipoingia seminarini. Kabla ya kuingia seminarini, Nilikuwa nimesitawi tayari vipaji vingi vya muziki kama kuimba na kupiga ngoma. Katika seminari nilipata nafasi kujifunza ujuzi mwingine ambao umenisaidia katika kazi yangu halisi.
Mimi ni kasisi wa Shirika “Poor Servants of Divine Providence”. Nilikuwa kasisi katika terehe ishirini na sita mwezi wa kwanza mwaka wa elfu mbili na mbili. Niliondoka kutoka kwa familia yangu katika Brazil na ninaishi katika Ongata Rongai tangu terehe kumi na nane mwezi wa kuanza mwaka wa elfu mbili kumi na tatu. Nilikuja hapa kwa kufanya kazi katika nyumba ya malezi. Jiukumu hilo linanihitajia busara na uangalivu daima. Zaidi ya jukumu hilo, ninapenda muziki na “capoeira” kwa sababu inafaa kwa afya, mizani na fikira.

Fr. Ndega
Mapitio: Mwalimu Patrick


Nenhum comentário: