domingo, 21 de fevereiro de 2016

“HUYU NI MWANANGU MPENDWA, MSIKILIZENI”


Kutafakari kuhusu Lk 9, 28b-36

Tukio la kugeuka sura kwa Yesu kulitokea baada ya siku sita ya ufunuo kuhusu mateso, kufa na kufufuka kwake na mwaliko wake kwa wanafunzi wa kumfuata kulingana na njia yake mwenyewe, yaani “Kujikana mwenyewe, kuuchukua msalaba wake na kumfuata Yesu.” Habari ya kugeuka sura kwa Yesu tena inafuatwa na tangazo la pili kuhusu kifo na ufufuko wake. Kwa uzoefu huu Yesu aliwachukua wanafunzi watatu, Petro, Yakobo na Yohana. Kwa nini wafuasi hawa? Labda kwa sababu aliwapendelea kuliko wengine. Injili haiongei maana ya habari hii. Yesu aligeuka mbele ya wafuasi wake na ishara kuu zilikuwa nguo na mwili wake. Yesu aliwaonyesha kidogo utukufu wake na hali ya wakati ujao kuhusu mwili wa yeyote anayemfuata kwa uaminifu. Yesu anashiriki utukufu wake na wanafunzi wake kwa maana inampendeza kufanya hivyo ili wawe na furaha moja ya vile Mwalimu wao alivyo.

Kama illivyotokea kuhusu jangwa, Mlima pia ni mahali muhimu katika uhusiano wa Watu wa Israeli na Mungu; katika mwendo huu, Musa na Eliya wana ushiriki maalum. Katika Agano la Kale milima iliyojulikana sana ni Mlima Sinai na Horebu. Ilikuwa katika Mlima Sinai ambapo Mungu alikutana na Musa na kuwawekea Waisraeli mkataba/agano. Ilikuwa katika Mlima Horebu ambapo Eliya alijiandaa kwa muda mrefu akutane na Mungu. Katika Agano Jipya Yesu alitumia sana mahali huko mlima kama rejeo ya uhusiano wake na Baba na kama eneo kwa matukio muhimu katika kazi yake. Kulingana na utamaduni mmoja wa zamani, tukio la injili ya siku ya leo lilitokea juu ya milima Tabor.   

       Uwepo wa Musa na Eliya unaongea kuhusu rejea ya ufunuo katika Agano la Kale. Waliongea na Yesu wakionyesha kwamba hakuna mpasuko/mshipa kati ya mafundisho yao na mafundisho ya Yesu, bali uhusiano na mwendelezo. Lakini kulingana na sauti iliyosikika kutoka kwenye wingu, mwendelezo huu, ambao ni Yesu, lazima kuwa kipaumbele katika maisha ya wanafunzi kwa sababu ni Yesu peke yake kwa mamlaka aliyoyapokea kutoka kwa Baba ili kufundisha na kutafsiri kamili lile lililosemwa na mababu wa zamani.  Kusikiliza katika Biblia ni kitenzi chenye nguvu sana. Hii ni tabia ya myahudi mbele ya Neno la Mungu, akiweka vitendoni au kufanya mazoezi/vitendo kuhusu yale aliyosikia. Kusikiliza kuna uhusiano na kushika au kutenda. Baba anashuhudia kuhusu Mwana wake, anamweka kama rejeo cha maisha yetu: “Huyu ni Mwanangu mpendwa, msikilizeni”. Huu ni pia mwaliko ili tufananishe maisha yetu kulingana na Neno la Yesu. Neno la Yesu ni kipimo ili mtu awe pia mwana mpendwa wa Mungu kama Yeye. Tunashiriki katika kugeuka sura kwa Yesu kupitia kusikiliza makini kwa Neno lake.

     Kuhusu mambo hayo Mtakatifu Yohana Calabria alisema: sisi ni makini sana kwa maneno ya binadamu na kuhusu hiyo ni sawa. Lakini tunapaswa kuwa na uangalifu zaidi kwa Neno la Mungu ambalo ni – consecratory – huweka wakfu, ni kwamba, linalifanya lile linalosema.” Mtakatifu Yohane Calabria ilikuwa anasema hasa kuhusu injili ambayo ni sheria kwetu Poor Servants of Divine Providence. Katika sehemu nyingine ya maandiko yake alisema: “Ikiwa sisi huamini katika maneno ya kuapishwa kwa – consecration – katika misa, yaani “twaeni mle wote, twaeni mnywe wote”, tunapaswa kuamini pia wakati Yesu asema: “Msiwe na wasiwasi” au “Baba yeno wa mbinguni anajua kwamba mnahitaji vitu hivyo vyote” au “mtafuteni kwanza ufalme wa Mungu na matakwa yake, na hayo yote mtapewa kwa ziada.” katika maneno mengine, kutokana na Maneno ya Yesu tunaalikwa kuwa “Injili hai.” Hiki ni kipimo kwetu ili tuweze kumtambua uso uliogeukwa wa Yesu katika nyuso zenye mateso za ndugu wengi miongoni mwetu. Neema ya Mungu itusaidie kulisikiliza Neno lake kwa uangalifu na kutangaza habari njema ya siri ya Mwanae kama njia ya wokovu kwa ulimwengu wote.  

Fr Ndega

Mapitio: Sara  

Nenhum comentário: