segunda-feira, 15 de fevereiro de 2016

ALITUONYESHA NJIA KAMILI JINSI YA KUYASHINDA MAJARIBU YOTE

Kutafakari kuhusu Kum 26, 4-10; Rum 10, 8-13; Lk 4, 1-13 

Kwaresima ni siku arobaini za maandalizi kwa adhimisho la fumbo la Pasaka ya Kristo. Wakati wa kwaresima unalenga kuwa uzoefu wa jangwa. Kwa upande wa viongozi wengi katika biblia jangwa palikuwa mahali pa mkutano na Mungu kwa hamu na uzoefu wa utakaso. Walitafuta mahali huko kabla ya matukio muhimu maishani mwao ili waweze kuchukua ahadi kwa nguvu na uaminifu. Vivyo hivyo, ni Kwaresma kama maandalizi kwa tukio muhimu sana la imani yetu, yaani Ufufuko wa Yesu. Wakati huu unatukumbusha siku arobaini ambazo Musa alibaki milimani Sinai ili azipokee Amri Kumi; na tena miaka arobaini ya utakaso wa Wana wa Israeli jangwani; tena siku arobaini za Eliya akitembea mpaka milima Horebi ili akutane na Mungu na kuyapokea maelekezo ya kazi yake kama nabii; kuna pia uhusiano na uzoefu wa Yesu wakati wa siku arobaini jangwani kabla ya kwanza kazi yake. Basi, kwaresima ni wakati maalum ya kuikuta maana kwa kuyashinda majaribu yote katika safari yetu, kwa sababu ya Kristo kwanza aliyashinda.
Somo la kwanza linaongea kwamba kumbukumbu ya historia ya Wana wa Israeli ni maana ya utambulisho wao na msaada wakumbuke daima mamba makuu ya Mungu katika safari yao. Walifurahi sana kwa sababu, katika nchi mpya walipokuwa wakiishi, wakapata kupanda na kuvuna malimbuko ya mazao. Musa anawaongoza kuungana tukio hili na mambo yote yaliyotokea katika safari yao ya ukombozi, wakimshukuru Mungu kwa sababu ya uaminifu wake na riziki yake kwa ajili yao. Sadaka ya watu ni mwendo wa kumrudishia Mungu zawadi ambazo zinatokana na ukarimu wake. Somo la pili linaongea kuhusu ukaribu wa Mungu kupitia neno lake ambaye ni Yesu Kristo. Kwa upande wake Kristo amekwisha tuokoa, lakini imani ni kipimo muhimu kwa kupata wokovu huu. Bwana wetu yuko tayari kutusaidia wakati tumwitapo ili tushinde majaribu ya kuishi mbali sana naye. Uaminifu wake ni maana ya nguvu yetu na utajiri wetu.   
Katika injili, Yesu aliongozwa jangwani na nguvu ya Roho Mtakatifu. Kama jangwa ni mahali pa uzoefu mzuri wa Mungu, Yesu alienda huko kwa sababu alitaka kutambua vizuri mpango wa Mungu. Uzoefu huu ulimhamasisha sana ili aanze kazi yake aliyomkabidhi Baba yake. Wakati huu pia alijaribiwa na Shetani ili akate tamaa kuhusu kila kitu ambacho kilikuwa maana ya utambulisho wa Yesu. Alimshawishi Yesu atumie uwezo wake kwa manufaa yake binafsi. Yesu alijaribiwa pia kutumia mamlaka badala ya upendo, huruma na utumishi. Tena Yesu alishawishiwa kusifiwa badala ya kutangaza Mungu na Ufalme wake. Majaribu matatu ya Yesu yanamaanisha majaribio yote ambayo yalikuwapo maishani mwake wakati wa kazi yake. Hata hivyo, alipata kushinda majaribu yote kwa sababu akaongozwa na Roho Mtakatifu na kuwa mtiifu kwa Baba yake. Hakuna kilichomvuruga kutokana na muhimu sana kwa sababu alikuwa mtu mwenye kupatikana na hatia.

Majaribu ya mali, nguvu na utukufu aliyokabili Yesu hayakumzuia kufanya mapenzi ya Mungu. Kama ilivyotokea naye, mitego ya mshawishi yanatuongoza kuacha ahadi yetu katika kanisa/jumuiya ama kutumia nguvu zaidi kuliko utumishi ama kuongea zaidi kuliko kusikiliza ama kuamuru zaidi kuliko kutii ama kudanganya kuliko kusaidia ama kulazimisha kuliko kupendekeza ama kutafuta upendeleo zaidi kuliko kupenda. Lakini, kulingana na Mtakatifu Agostino “Ikiwa katika Kristo tumeshawishiwa, katika yeye tunashinda shetani. Kristo angeweza kumtupa mshawishi mbali sana nawe; lakini ikiwa yeye hakuwa ameshawishiwa hangetufundisha jinsi ya kushinda juu ya majaribu.” Mfano wa Yesu katika uaminfu wake kwa Baba ni mwaliko kwa uaminifu pia. yeyote ambaye anazifuata nyayo zake, na kufunguliwa kwa msaada wa Roho wake anapata kufanya mapenzi ya Mungu kama yeye alivyo. Ushindi wake unafufua tumaini letu la kufikia mafanikio katika mapigano yetu dhidi ya kila kitu kinachotuvuruga kutokana na muhimu sana katika safari yetu ya watumishi wa Mungu.

Fr Ndega
Mapitio: Sara

Nenhum comentário: