quarta-feira, 24 de fevereiro de 2016

HALI YA MASKINI INA UHUSIANO NASI


Kutafakari kuhusu Lk 16, 19-31

     Kama tujuavyo, mifano ni sehemu ya ajabu ya ufundishaji wa Yesu. Kupitia mfano yeye anaweka rahisi na kupatikana kwa wote siri za Ufalme wa Mungu. Siku ya leo Yesu anasimulia mfano wa mtu tajiri na Lazaro maskini anawaonya wasikilizaji wake kuhusu hali ijayo na kama matokeo ya chaguzi za watu katika wakati huu. Mtu tajiri ni ishara ya walio na mazoea ya kuitumainia mali bila unyeti kuhusu kile kinachotokea kandokando yao. Wao walichagua kwa nafsi yao njia ambayo itawaongozea mauti. Lazaro ni ishara ya walio maskini ambao wameachwa bila ulinzi na utunzaji; wanapiga kelele ili wapate nafasi ya kuishi kwa heshima. Kwa wakati sawa, Lazaro pia ni pendekezo la kuishi tofauti, kuyalenga maisha katika thamani za kweli. Huyo ni ishara ya uvumilivu, ya mapigano na mwaliko wa kumtumainia Mungu ambaye katika riziki yake hawaachi wale ambao wanamwamini.
      Kupitia mfano huu Yesu anatukumbusha hali katili ipo katika jamii yetu, yaani kukosekana kwa usawa kati ya watu. Katika Amerika Latina, kanisa lilikuwa limekwisha shutumu baadhi ya miaka iliyopita kwamba “Hali mbaya ya jeuri imezaa matajiri waliokuwa na utajiri zaidi daima juu ya maskini waliokuwa maskini zaidi daima.” Hali hii ni tofauti kabisa na matarajio ya Mungu ambaye, kulingana na wema wake, ananyesha mvua kwa wenye haki na wasio na haki, tena kwa walio wema na mabaya ili vitu vyote alivyoumba kwa wote vipatikane kwa wote.. wimbo wa Bikira Maria unashuhudia hali hii kwa njia ya ajabu na furaha kubwa kwa sababu ya njia ya Mungu ya kutenda, yaani yeye huwashusha wakuu na kuwapandisha wadogo ili waweze kuishi pamoja kama ndugu na kwa usawa wa haki na heshima.  
     Mungu anajitambulisha na hali ngumu ya wasio na nguvu na ya maskini. Udhalimu wote unaofanyika kwao unamfikia Mungu ndiye yumo ndani yao. Katika wakati ujao, baada ya hali ya dunia, hali itakuwa tofauti, yaani waliopokea mambo mema katika maisha yao bila ahadi na unyeti kuhusu hali ya wengine wataumizwa na wale waliopata mabaya kama Lazaro alivyo, watafarijiwa. Yeyote ambaye anatumia mali yake awadharau wengine anatupa maisha yake takatakani kwa sababu maisha hayamaanishi mali mengi bali uwezo wa kutenda mema. Kuhusu mambo haya Mt Yohana Calabria asema: “Maskini wako ili matajiri waokoke/waokolewe”. 

     Kipindi cha Kwaresima kinatukumbusha kwamba hali ya maskini ina uhusiano nasi, kwa sababu dhambi ya jamii ni matokeo ya kiasi cha dhambi kibinafsi. Basi, ni lazima toba sio kwa dhambi za kibinafsi tu, bali kuchukua jukumu kuhusu dhambi ya jamii pia. Mwendo huu unaweza kwanza kupitia kuacha njia ya ukuzaji na ukusanyaji ambayo kwa kawaida inatuongoza kwa kutofautiana ili tuchukue njia ya unyenyekevu ya maisha ambayo inakihusu kitu kidogo na kutufanya wenye unyeti kuwahusu wale wasio na kitu. Mungu anatuokoa kwa sababu ya upendo wake, lakini anathamini sana juhudi zetu kama alisema Baba Mt Benedito wa kumi na sita: “kwa kweli, wokovu ni zawadi iliyo neema ya Mungu, lakini ili uwe ufanisi katika maisha yangu unakudai kukubalika kwangu kuonyeshwa kupitia matendo, yaani kupitia utayari wa kuishi kama Yesu alivyo na kutembea baada yake.”

Fr Ndega
Mapitio: Sara 

Nenhum comentário: