sexta-feira, 20 de setembro de 2019

AMMINISTRATORI FEDELI DEI DONI DI DIO



Riflessione su Am 8, 4-7; 1Tm 2, 1-8; Lc 16, 1-13



      Dio desidera per il suo popolo lunga vita e dignità. Tutte le cose che non vanno in questa direzione vengono da lui rifiutate. Così, tramite il profeta Amos, nella prima lettura, Dio ha condannato tutte le forme di oppressione che impediscono di vivere come popolo di Dio, soprattutto la situazione di violenza contro i poveri e gli affamati. La loro sofferenza è una dimostrazione che abbiamo una società ingiusta dove esistono persone potenti, che hanno proprietà e ricchezze, mentre altre non hanno il sufficiente per vivere.

      Come il peccato della società il risultato di un accumulo di peccati personali, bisogna che siamo attenti per non contribuire ancora di più con questa ingiustizia sociale. A proposito di questo, Papa Francesco dice: “Il consumismo ci ha indotti ad abituarci al superfluo e allo spreco quotidiano di cibo... Ricordiamo bene, però, che il cibo che si butta via è come se venisse rubato dalla mensa di chi è povero, di chi ha fame!” La situazione di queste persone era una priorità nella missione di Gesù che ha preso l’impegno di essere povero per arricchire tutti con la sua povertà.

      Nella seconda lettura, San Paolo ci consiglia di pregare per tutti gli uomini specie per coloro che hanno la responsabilità di condurre e di governare: ministri della Chiesa, capi di governo e così via, affinché possano fare il loro lavoro bene, così che tutti possiamo vivere una vita di serenità e di pace. Noi siamo di Dio, e pertanto, l’autorità che i capi hanno sulle nostre vite è solo una partecipazione nella missione di Dio stesso che vuole che tutti gli uomini siano salvati e che conoscano la verità. È anche nostra responsabilità che facciano un buon lavoro e questo è gradito a Dio.

    Continuando la nostra riflessione, abbiamo una parabola in cui Gesù ci parla della necessità di essere fedeli nel compito che abbiamo ricevuto da Dio. Ciò che abbiamo appartiene a Dio, per cui ogni bene viene da lui. Lui ci affida la custodia di tutto e aspetta che noi agiamo secondo la sua volontà. Non siamo i proprietari, ma gli amministratori dei doni di Dio, per questo dovremmo usare i soldi non come fine nella vita, ma come strumento per produrre buone condizioni per tutti.

      Viviamo in una società dove il denaro è la misura di tutto e tutto dipende dal denaro. Si tratta di un potente mezzo di vita per molte persone. I cristiani, che comportamenti devono avere di fronte alla ricchezza? Coloro che seguono Cristo dovrebbero essere onesti in tutte le cose e avere il giusto comportamento in relazione alla ricchezza. La mancanza di un giusto rapporto con questa ci conduce a dimenticare la cura per la famiglia, l’attenzione alla propria salute, una vera relazione con Dio e con gli altri.

      Spesso nel rapporto con Dio c’è qualcosa che non va bene a causa del nostro desiderio di avere sempre più ricchezze. Gesù non sta dicendo che il denaro non è importante, ma dice che non possiamo lasciarci prendere e schiavizzare dal denaro. Gesù vuole che ognuno comprenda che i soldi non possono garantirci i valori che generano vita e felicità. Noi possiamo usare i soldi per servire Dio, ma non possiamo usare Dio per trovare soldi. Su questo dobbiamo essere vigili perché questo può accadere e spesso senza che ce ne rendiamo conto. Il denaro è pericoloso perché può farci insensibili all’amore di Dio e ai bisogni degli altri.

     Il denaro ci aiuta a vivere, ma mette anche persone lontane tra loro. Il denaro può costruire una casa ma anche può distruggere famiglie. Attraverso il denaro possiamo comprare vestiti, cibo e così via, ma possiamo anche produrre privilegi, corruzione e discriminazione. Non possiamo permettere che i soldi siano motivo di differenza tra di noi, conducendoci a discriminare gli altri. Per le comunità cristiane il denaro è stato importante in quanto istrumento per l'edificazione e manutenzione degli spazi di incontri e celebrazioni e per le molte attività della evangelizzazione. Ringraziamo Dio per l'uso del denaro come espressione di generosità per il bene delle nostre comunità. Chiediamo la grazia di usare il denaro che abbiamo non come strumento di discriminazione, ma piuttosto come uno strumento di solidarietà, costruendo fraternità. 

Fr Ndega

sábado, 14 de setembro de 2019

LA GIOIA DI PERDONARE E DI ESSERE PERDONATO



Riflessione a partir di Lc 15, 1-32


      Il quindicesimo capitolo del vangelo di Luca è molto famoso tra le parabole di Gesù. Questo è chiamato capitolo delle parabole di misericordia, vale a dire la parabola del pastore che perde la pecora (4-7), della donna che perde la moneta (8-10) e del padre che perde il figlio (11-32). Queste parabole mostrano l’atteggiamento compassionevole di Dio verso i peccatori e la gioia di trovare nuovamente quello che si era perduto.

     “Gesù è il volto della misericordia del Padre” e ha rivelato questa misericordia non soltanto con parole ma anche e soprattutto con i gesti. Per questo, dice il brano, si avvicinavano a lui tutti i pubblicani e i peccatori. Non avrebbero fatto questo passo se non avessero avuto la certezza di essere bene accolti da Gesù. Dall’altra parte abbiamo un secondo gruppo, formato dai farisei e dagli scribi, che preferiscono la critica, la lamentela, la resistenza.

        Tutti i due gruppi, anche se hanno un’esperienza diversa di Dio e atteggiamenti diversi nei suoi confronti sono figli e sono amati. Nessuno dei due conosceva il vero volto di Dio poiché un gruppo si considerava dei giusti e condannava l’altro che a sua volta portava, per assimilazione e rassegnazione, il nome di peccatori pubblici, cioè, un caso perduto. Nell’incontro con Gesù hanno trovato l’abbraccio della misericordia e, quindi, un nuovo orizzonte per la loro vita. Questo è stato lo scenario di fondo usato da Gesù per comporre e raccontare queste bellissime parabole.

        Nella parabola del pastore che perde sua pecora, abbiamo l’immagine di Dio Padre che ha un’attenzione speciale verso tutti, va in ricerca del peccatore e non ‘riposa’ finché non lo incontra e lo coinvolge nuovamente nella sua comunione. Nella parabola della donna che perde una moneta, Dio è come una madre che usa tutta la tenerezza e cura per ricongiungere nuovamente a sé ogni persona che si è allontanata dalla sua comunione e fa festa per la gioia di averla trovata.

       Nella parabola del padre che perde il figlio, la centralità punta sul modo del padre di amare i due figli, ambedue prodigi, anche se in modi diversi. Secondo Gesù, Dio nei nostri confronti è come un padre di famiglia che ha due figli e condivide i suoi doni in parti uguali con tutti. Vuole che vivano lo spirito di famiglia partecipando alla sua gioia di padre. In questa famiglia lui cerca di offrire il suo amore, la sua cura e protezione, affinché i suoi due figli abbiano buone ragione per vivere sempre in comunione con lui. Quando qualcuno decide di abbandonarlo e andare via, non è impedito di farlo perché questo padre rispetta la libertà di ciascuno. Questo suo modo di amare permette di andare via ma assicura anche una buona accoglienza a chi ritorna da lui.

      Deve essere più o meno così la nostra esperienza. Dio non impone la sua autorità, preferendo rivolgersi a noi con legami di tenerezza, trattandoci da adulti, cioè “accettando il terribile rischio educativo di lasciarci andare per la nostra strada”. Allo stesso tempo è sempre vigilante, aspettando il più piccolo segno di ritorno per darci l’abbraccio della misericordia e fare festa con noi. Tante volte ci sentiamo lontani da Dio a causa dei nostri peccati. Certamente Egli si sente abbandonato e tradito, ma non smette di amarci. Così sentiamo rimorso e la certezza di essere bene accolti ci motiva a tornare da Lui e riprendere la comunione con Lui. Anche se spesso non ci comportiamo come figli, Dio rimane sempre fedele alla sua missione di Padre. La sua misericordia è più grande e potente dei nostri errori. Abbiamo bisogno di riscoprire questo vero volto di Dio.

      Un altro momento molto duro per quel padre della parabola è stato l’indurimento di cuore del figlio maggiore verso suo fratello e riguardo al gesto di accoglienza del Padre. Veramente, questo figlio maggiore non si sente figlio, visto che tratta il padre da padrone, e quindi si sente un impiegato; e non si sente neanche fratello, perché rifiuta il proprio fratello. Il comportamento del figlio maggiore mette a rischio la gioia e la bellezza della festa.

     Quando qualcuno prende sul serio un cammino di conversione è motivo di grande gioia per il Padre. Però gli causiamo un grande dolore quando non condividiamo dei suoi sentimenti nei confronti degli altri, cioè quando siamo indifferenti nei confronti di coloro che ritornano alla comunità. Come ha parlato ai discepoli una volta, Gesù ripete a noi oggi: “Siate misericordiosi come vostro Padre.” La riconciliazione con gli altri è la condizione perché il nostro rapporto con Dio sia vero. Questa è la via della vera conversione, che è un lungo cammino e comincia nel nostro cuore. Lasciamoci colpire dal modo misericordioso di Dio di agire e una volta toccati dalla sua misericordia possiamo essere strumenti di essa per coloro che hanno bisogno del nostro perdono.

Fr Ndega

sexta-feira, 13 de setembro de 2019

FURAHA YA KUSAMEHE NA KUSAMEHEWA



Kutafakari kuhusu Lk 15, 1-32




Sura ya kumi na tano ya toleo la Luka inajulikana sana miongoni mwa mifano ya Yesu. Hii inaitwa sura ya Mifano ya huruma. Tuko na mifano mitatu, yaani mfano wa Kondoo aliyepotea (4-7), wa Sarafu iliyopotea (8-10) na Mwana mpotevu (11-32). Mifano hii inaonyesha tabia ya huruma ya Mungu kwa wenye dhambi na furaha ya kupata tena kitu kilichopotea. Kwa kufahamu nia ya Yesu alipoisimulia mifano hii tunahitaji kutafakari kwanza kuhusu mazingira ambayo Yesu aliishi.

Katika muktadha ule, baadhi ya watu walijiona waliostahili wokovu wa Mungu kuliko wengine kwa sababu ya uaminifu wao kwa Sheria. Walichukua mamlaka ya kuwatenganisha watu, wakiwapanga kama wema au wabaya. Mamlaka haya hayatoki kwa Mungu kwa sababu kipimo ni ubaguzi. Walisahau kwamba mbele ya Mungu hakuna yeyote aliye na haki kuliko mwingine. katika njia yake ya kupenda Mungu hakuna ubaguzi. Kwa upande wake watoza ushuru na wenye dhambi ni watoto wake kama vile ndio Mafarisayo na Waandishi. Kipimo cha kuishi kwa ushirika na Mungu sio sheria bali uzoefu wa undugu.
        
         Ingawa yako matukio mengi katika Agano la Kale, ambayo yanaonyesha njia maalum ya Mungu ya kutenda, ni “katika Yesu Kristo kwamba huruma ya Mungu imepata kuwa hai na yenye kuonekana, na hata ilifikia kilele chake katika Yeye... Yesu ni uso wa huruma ya Baba. Kila kitu ndani yake kinaongelea huruma. Hakuna chochote kwake kinachopungukiwa na huruma (Baba Mt Francisco).”  Kama alama ya huruma ya Mungu, Yesu ana chaguo wazi sana, kulingana na maneno ya waliompinga yeye, yaani “Mtu huyu huwakaribisha wenye dhambi, tena hula nao”.

       Kweli, Yesu alikuwa na njia maalum ya kuongelea huruma ya Mungu, yaani katika Yesu jambo la huruma lilionyeshwa “kwa neno lake, matendo yake na kwa nafsi yake yote.” Yeye alitumia ishara nyingi za makaribisho, akithibitisha lengo la ujumbe wake na ukweli wa mafundisho yake. Kwa kweli, watozaushuru wengi, makahaba na wengine waliokataliwa na jamii, walijiona kukaribishwa na Yesu na tena kubadilishwa kwa sababu ya mkutano na huruma ya Mungu.

      Mfano wa mchungaji anayepoteza kondoo wake tuko na ishara ya Mungu Baba ambaye ana macho maalum kwa kila mtu naye hapumziki mpaka kukutana na aliyepotea na kumhusisha tena katika ushirika wake. Katika mfano wa sarafu iliyopotea Mungu ni kama mama mmoja anayetumia juhudi na nguvu zote ili kukuta kitu alichopoteza naye anapopata hiki anafanya sikukuu. Katika mfano wa mwana mpotevu, macho yetu yamlenga baba aliye mhusika mkuu wakati wote. Uhusiano wake wa mapendo kwa vijana wake ndio umuhimu wa tukio hili. Kulingana na Yesu, Mungu ni kama baba mmoja aliye na watoto wawili na kushiriki nao zawadi zake kwa njia sawa. Yeye anawapenda wote na kutaka wajione katika uzoefu  wa familia kwa kushiriki katika furaha yake ya baba. Utunzaji na ulinzi wake ni maana nzuri ili wabaki pamoja naye daima.

    Yule ndogo alichukua nafasi ya kuenda zake akiacha ushirika wa baba yake. Yeye alifanya hivyo sio kwa sababu hajihisi kupendwa bali kwa sababu alihisi mwenye uhuru. Ndio hivyo uzoefu ya upendo wa Mungu Baba, yaani unaheshimu kila mtu na kumruhusu kuchagua kwa uhuru kabisa njia yenyewe ya maisha yake. Tunapotenda dhidi ya Mungu kupitia dhambi, Yeye anajihisi ameachwa na kusalitiwa, lakini hashindwi kutupenda. Yeye anashughulika sana kwa ajili ya maisha yetu kwa kutupa ulinzi na utunzaji wake. Kwa hivyo kwa kufikiria upendo wake kwetu tunahisi majuto na hamu ya kurudi tena kwake. Ingawa tunashindwa kuishi kama wana, Mungu hashindi kuishi na kutenda kama Baba mwema kamwe.

       Katika mfano huu yuko pia mwana mkubwa ambaye hajihisi mwana wala ndugu. Kosa la utoto ni kwa sababu anajiona kuwa ni mfanyakazi; kosa la undugu ni kwa sababu anamkataa ndugu yake mdogo. Tabia ya huyo mwana mkubwa inaizuia furaha kamili ya baba na ukamilifu wa sikukuu. Kumrudia Mungu ni maana ya furaha kubwa kwake. Lakini furaha yake itakuwa kubwa zaidi ikiwa wale ambao wanajiona watoto wake waweze kushiriki katika hisia zake kuwahusu wengine. Hataki kwamba tuwe na wivu kuhusu njia yake ya kupenda bali tutende kama yeye alivyo. Kwa hivyo Yesu alisema, “Muwe na huruma kama Baba yenu alivyo.” Upatanisho na wengine ni kipimo ili uhusiano wetu na Mungu uwe kweli. Hii ni njia ya kweli ya toba iliyo mwendo wa muda mrefu na huanza mioyoni mwetu. Turuhusu kuguswa na huruma ya Mungu ili tuweze kuwa vyombo vya huruma hii kwa wale wanaohitaji msamaha wetu.

sábado, 7 de setembro de 2019

MASHARTI YA KUMFUATA KRISTO


               
Kutafakari kuhusu Lk 14: 25-33



     Umati wa watu waliandamana na Yesu, lakini sio wote waliokubaliana naye. Alipoitambua hali ya kutokuwa na ahadi na makubaliano, aligeuka na kuwalekeza baadhi ya maneno. Maneno yake yalikuwa nafasi ya kutafakari kwa kweli maana ya safari yao. Ingawa Yesu alikuwa maarufu, kwa sababu ya mambo mema aliyofanya kwa ajili ya watu, utume ambao Yesu alichagua kutimiza mapenzi ya Mungu hauleti umaarufu. Watu walichanganyikiwa kuhusu Yesu kwa sababu hawakumjua bado na kumfuata kwa njia yoyote.

      Kama Yesu hakuwa na nia ya kumdanganya yeyote, aliongea nao kwa uwazi sana kuhusu maana ya kumfuata na matokeo ya uamuzi huu. Njia hii ya kusema ilikuwa tabia yake ya kawaida kama alivyofanya kwa ajili ya wale kumi na wawili, yaani aliwajulisha masharti ili wawe wanafunzi wake wa kweli. Kutoka kwao, Yesu hakutarajia werevu ama upumbavu, bali kupatikana na hatia. Hawawezi kumfuata Yesu kwa sababu walipokea habari tu ya kuwa ni vizuri kufanya hivyo. Yesu anatarajia zaidi, yaani mabadiliko ya ndani.

        Andiko hili ni mwaliko wa kuchukua ahadi ya kumfuata Kristo kwa kupanga mambo ya kesho, yaani kuwa na uwezo wa kuona mbele ili kuepuka kufaragua. Ni vizuri kuota ndoto lakini ndoto hii inapaswa kuihusu hali halisi mtu anayoishi, vinginevyo itakuwa udanganyifu tu. Yesu anataka kuepuka kwamba safari ya wafuasi wake iwe pasipo maana ama ya udanganyifu. Ni lazima utambuzi, hekima, kupanga na uamuzi.

     Mungu mwenyewe anatupa mfano wa kuwa na mipango ya muda mrefu ili tupate mafanikio katika safari yetu kama wafuasi wa Yesu. Yeye Mungu alipanga kumtuma mkombozi, kulingana na yaliyoandikwa: “... wakati maalum ulipotimia, Mungu alimtuma Mwanawe aliyezaliwa na mwanamke... ili apate kuwakomboa waliokuwa chini ya sheria.” (Wagalatia 4: 4-5). “Hata baadhi ya wakulima hutegemea mvua inyeshe hata kama hawajaandaa shamba mahali pa kupanda mbegu kama za mahindi au maharagwe.” Kupanga mambo ya kesho ni muhimu.

       Yesu alisema, “Basi, kadhalika kila mmoja wenu asiyeacha vyote alivyo navyo, hawezi kuwa mwanafunzi wangu.” Kama ilivyotekea katika vifungu vingine, Yesu aliwapendekezea watu mpango wa maisha unaojumuisha kujinyima, kwa sababu yeyote anayekutana na Yesu kwa kweli amekwisha pata hazina ya kweli kwa maisha yake wala hawezi kubaki alivyo, yaani mambo mengine hayana maana tena kama kwanza. Kwa maneno mengine, Yesu anataka kuwa kipaumbele maishani mwa wanaoamua kumfuata. Hakuna jambo lingine ambalo liweze kuitoa maana ya kweli kwa maisha yao ila Yesu peke yake.

    Wanafunzi wa Yesu wa kweli walimtegemea Mungu katika mambo yote kama Yesu alivyo. Yeye alishiriki na wanafunzi wake ufalme wa mbinguni na kuwajulisha njia ya msalaba ili waweze kufanya mapenzi ya Baba yake. Kupitia njia hii, tunatambua kwamba Kumfuata Yesu hakuuleti upendeleo au hadhi, bali mateso na kujisalimisha kwa ajili ya ufalme wa Mungu. Basi, yeyote anayetaka kuishi bila ahadi hawezi kumfuata Yesu. Tena yeyote ambaye anatamani kumfuata Kristo bila msalaba hatapata kumfuata kwa kweli kamwe.

       Kupitia njia ya unyenyekevu na utupu Yesu alipata utukufu. Utambulisho wa wanafunzi wa mwalimu Yesu unapaswa kufuata njia sawasawa naye. Kwa upande wa Kristo msalaba ulikuwa sehemu muhimu katika mwendo wa kufanya mapenzi ya Mungu na kudhihirisha kwa mpango wa upendo wake. Kwa upande wetu kama wanafunzi, kuchukua msalaba ni ishara ya utayari wetu kwa mapenzi ya Mungu kwa kujitolea kama Kristo. Kwa kufikia lengo hili tunapaswa kujikana nafsi yetu, yaani kujisahau sisi wenyewe ili wengine waweze kukumbukwe. Tunapaswa kujikana sisi wenyewe ili Mungu aweze kujifunua kwa nguvu yote ya upendo wake. Tunapaswa pia kujiondoka kutoka katikati/mahali muhimu ili wengine waweze kuwa na nafasi ya kwanza. Kwa maneno mengine, tunapaswa kuwafikiria wengine ni wamuhimu kuliko sisi wenyewe. Kama haiwezekani kumfuata Kristo bila msalaba, mfano wake wa uaminifu kwa mpango wa Mungu utuimarishe katika safari yetu ya yetu ya kujitolea kwa ajili ya ufalme wa Mungu.

Fr Ndega

sexta-feira, 30 de agosto de 2019

MAANA YA KUWA MWENYE HERI WA KWELI



Kutafakari kutoka Luka 14,1.7-14



       Yesu alialikwa kula chakula nyumbani mwa Mfarisayo mmoja na, kwanza kabisa, yeye alisababisha usumbufu kwa sababu alimponya mtu mmoja siku ya Sabato. Sheria ya Wayahudi inakataza hali hii, lakini Yesu anapendelea kuwatunza watu kuliko kuifuata sheria ambayo haikufuata nia ya Mungu ya asili. Akitarajia waweze kufikiri kama yeye aliwauliza swali: “Je, ni halali au la kumponya mtu siku ya Sabato?” Lakini walinyamaza. Tukumbuke kwamba Mafarisayo na Waandishi waliondoa maana ya kinabii ya sheria, wakitafsiri kulingana na mawazo yao ya upungufu. Hao wanapenda sana kujiinua na kupendezwa na watu. Mara nyingi Yesu alipokutana nao hakufikia mafanikio kuhusu mapendekezo yake ya maisha mapya kwa sababu hao ni wanafiki na kupendelea kumjaribu Yesu kuliko kubadilisha mawazo yao kulingana na matarajio yake. Kwa hivyo mara nyingi mkutano wa Yesu nao ni maana ya mapambano.

        Yesu yupo karamuni. Injili ya Luka inaonyesha kwamba kushiriki katika milo mbalimbali kulikuwa muhimu sana kwa Yesu aliyetumia vipindi hivi kama nafasi ya kuwafundisha watu. Karamu miongoni mwa Wayahudi inathaminiwa sana. Pamoja na maana ya uzoefu wa familia, kielelezo cha urafiki, mshikamano na hamu ya kukuwa pamoja, karamu pia ni mfano wa uhusiano wa upendo kati ya Mungu na watu wake (Hos 2:1-23, Isa 54:4-8, Eze 16:7-8). Katika mafundisho ya Agano la Kale, kushiriki katika Ufalme wa Mungu, mara nyingi hulinganishwa na kushiriki katika karamu (Isa 34:5-7, Zek 9:15,1 Nya 12:38, Zek 14:15-24). “Karamu za namna hiyo mara nyingi zilikuwa na ujumbe wa kimasiha. Zilisherehekea ushindi wa Mungu dhidi ya nguvu za uovu (Isa 25: 6-8), zikaimarisha uhusiano kati ya Mungu na watu wake, na kuwaunganisha watu kati yao.” Huu ni kweli, mfano kwenye karamu ya arusi. “Upendo wa Mungu ni kama ule wa Bwana arusi, jinsi alivyolipenda na kulichagua Taifa la Israeli kama mali yake mwenyewe. Wakristo wa kwanza, walifikiria pia juu ya uhusiano wao na Kristo kama mfano (Yoh 3:39, 2Kor 11:2, Efe 5:23-32).”

       Basi, katika injili ya leo, Yesu alishangaa kwa sababu ya mashindano ya watu kwa ajili ya kuchukua mahali pa kwanza katika karamu naye aliwapendekezea tabia tofauti. Mtu akipendelea kuwa wa mwisho, alichagua kuwa mtumishi kama vile Kristo aliyeja sio kutumikiwa bali kutumikia.  Katika jamii, kutafuta mahali pa kwanza, msimamo, upendeleo na umaarufu ni hali ya kawaida inayosababisha mapambano, chuki na ukatili kati ya watu. Hata katika Kanisa na jumuiya zetu tunaweza kukuta hali sawasawa na hii. Yesu alikwisha ameonya kuhusu hatari za hali hii na kufundisha unyenyekevu kama njia kamili. Unyenyekevu ni fadhila ambayo inampendeza Mungu na watu. Kuwa mnyenyekevu ni kuchukua hali ya udhaifu ya kibinafsi kwa kushinda mwelekeo wa kujiona mwema kuliko wengine. Inamaanisha kutumia nguvu zote za kibinafsi ili kuwatumikia wengine kwa ukarimu na upendo hasa wakiwa ni maskini na walio na shida ya kimwili ambao hawana cha kutulipa. Hii ni kipimo cha furaha ya kweli kwetu. Hii ni njia ya kuonyesha kwamba upendo wa Mungu unatolewa kwa hiari kwa ajili ya watu wote. Katika karamu ya arusi mbinguni, yeye atawakaribisha wale wanaomwelekea kupitia matendo ya upendo.

       Lengo la Yesu ni kuzaa ubinadamu mpya na aina mpya ya uhusiano miongoni mwa watu. Msingi wa ubinadamu mpya ni unyenyekevu na upendo. Thamani hizi zinapaswa kusaidiwa zaidi miongoni mwetu. Kupitia utumishi wa kindugu na wa kinyenyekevu tunaweza kufikia lengo la Yesu ambaye ana mawazo tofauti na yale ya jamii. Kwa Yesu, mtu ni mkuu ikiwa yeye ni mdogo; tena mtu ni wa kwanza ikiwa yeye ni wa mwisho; pia mtu anakwezwa ikiwa yeye anajishusha. Katika jumuiya zetu za wafuasi wa Yesu muhimu ni kutumikia wenzetu kama Mwalimu Yesu alivyo. Yeye anatuhakikishia kwamba yoyote tunayofanya kwa ajili ya walio na shida yatasahauliwa na Mungu. Maisha yake ya mtumishi ni kipimo kwetu. Hatuhitaji mahali pa kwanza, bali kutumikia kwanza kwa unyenyekevu na ukarimu. Tujifunze kutoka kwa Kristo aliyefahamika kama Mtumishi wa Bwana kwa namna ya kipekee ili utumishi wetu uwe bila unafiki na kuweze kumpendeza Mungu.

Fr Ndega  

domingo, 25 de agosto de 2019

KATIKA UFALME WALIO WA MWISHO WATAKUWA WA KWANZA



Kutafakari kuhusu Lk 13, 22-30



    Wakati wa safari ya kwenda Yerusalemu, Yesu alitumia nafasi ya kuwafundisha wanafunzi wake hasa kuhusu masharti ya kuingia katika ufalme wa mbinguni. Kwanza kabisa haitoshi kuwa wanafunzi wake ili kupata wokovu. Hivyo, aliwapendekezea mlango mwembamba kama changamoto. Ikiwa Yesu anajulisha mlango mwembamba ni kwa sababu pia kuna mlango mpana.

     Wakati Mt. Yohane Paulo wa II alipoongea na vijana katika mwaka wa 1993, alitofautisha vizuri njia hizi mbili, akisema: “kataeni barabara rahisi: barabara ya anasa, uhalifu, kudharau mazuri, na kukwepa wajibu. Ulevi na matumizi ya madawa ya kulevya na uasherati visiwe na nafasi katika maisha yenu. Pitieni mlango mwembamba. Chagua barabara ielekeayo kwenye uzima wa milele na furaha pamoja na Mungu.” Katika kifungu kingine Yesu alisema kwamba mlango mwembamba ni njia ambayo inaongoza kwenye uzima na wachache tu wanaoweza kuigundua njia hiyo. “Huu ni mlango wa uvumilivu, busara, kujitoa, ukarimu, wema, shukrani na kazi”. Kuhusu mlango mpana, hii ni njia rahisi inayoongoza kwenye maangamizi na waendao njia hiyo ni wengi. Basi, ili wanafunzi wa Yesu waweze kupata mafanikio katika safari yao wapaswa kupitia mlango mwembamba.   

     Katika mazingira yetu mlango mwembamba ni ishara ya juhudi yetu ya kushinda mwelekeo mbaya wa maisha yetu na kuwatendea watu mema. Katika mwendo huu ndio sisi wa kwanza wa kupata mafanikio ama bahati mbaya, kwa sababu lile tunalofanya kwa ajili ya wengine linasababisha hali nzuri ama mbaya kwetu pia. Hadithi fulani inatusaidia kuelewa vizuri hali hii. “Siku moja mwandishi wa habari alimhoji mwenye shamba ambaye ameshinda mara ya tano mashindano kuhusu mahindi mazuri zaidi katika eneo hilo. Mwandishi alimwuliza swali akisema, “unapataje kuzaa mahindi bora kuliko wengine?” Mwenye shamba alijibu, mwendo huu ni rahisi sana; nina mazoea ya kushiriki mbegu zangu nzuri na majirani wangu.” Mwandishi aliendelea kwa swali akisema, “Kwa nini unashiriki mbegu zako nzuri na majirani wako ikiwa hao wanashindana pia katika mashindano haya pamoja?” “kwa sababu ni upepo ambao unasambaza poleni ya mahindi na tena ni upepo ambao unaweka poleni mashambani na unafanya mbegu zikue. Ikiwa majirani wangu watakuwa na mahindi mabaya, upepo utasambaza poleni mbaya shambani kwangu nayo mahindi yangu yatakua mbaya. Basi ili mahindi yangu yawe mazuri ninapaswa kuwasaidia majirani wangu wote ili wawe na mbegu nzuri.”

     Basi, lile zuri ambalo tunatarajia kwa maisha yetu tunapaswa kusaidia kwa ajili ya wengine. Katika mwendo huu hatuwezi kuitafuta furaha kwa njia ya ubinafsi. Ikiwa tunataka kuwa wenye furaha, tunapaswa kuisaidia hali hii nzuri kwa wale wanaoishi karibu nasi nao wako na shida sawasawa nasi. Tunapaswa kushinda mwelekeo wa jamii wa kufikiria wengine kama washindani nasi. Wengine sio washindani, bali ni ndugu. Kujaribu kupata upendeleo tukiwavuruga wengine ni udhalimu na kutuacha mbali sana na pendekezo la Yesu. Ikiwa tuko mbali na pendekezo la Yesu, matokeo yatakuwa mbali sana na yale tuliyotarajia kwa maisha yetu. Tunaweza kuongea vizuri sana kuhusu Yesu ili kuonyesha kwamba tunamjua Yeye na Biblia pia. Tunaweza hata kufikiri kwamba kuongea bora kuliko wengine kunatuhakikishia faida ili tupokee baadhi ya tuzo kutoka kwa Mungu. Lakini, kulingana na andiko hili, maneno hayatoshi kuingia katika ufalme wa Mungu. Wokovu si astahili yetu, lakini hii ni zawadi ya ukarimu wa Mungu.

        Je, inawezekanaje tuseme kwamba tunamjua Yesu naye aseme kwamba hatujui sisi?” Hii ni kwa sababu katika biblia kitenzi kujua kinamaanisha uhusiano wa ndani, uzoefu wa kina ambao ni muhimu sana katika safari yetu ya wanafunzi wa Yesu. Ikiwa yeye anasema kwamba hatujui sisi ni kwa sababu sisi hatumjui yeye. Katika mwendo huu hakuna makubaliano kati yetu na pendekezo lake, hakuna utambulisho. Hatuwezi kuwa wanafunzi wa Yeu kupitia maneno peke yake. Ushuhuda wa maisha unathamini zaidi kuliko maneno. Tukijifikiria bora kuliko wengine hatuuhakikishii wokovu. Kila kitu tunachofanya kinasababisha matokeo makubwa kwetu na katika hali iliyo kandokando yetu. Kwa maneno mengine, kufikia mafanikio ama bahati mbaya kwa maisha yetu kunatutegemea sisi wenyewe; huu ni uamuzi wetu. Kwa upande wa Mungu tunaumbwa ili kushiriki katika maisha yake, yaani ili kuokokewa. Neema ya Mungu ituongoze ili tuweze kufanya mapenzi yake na kupata uhai.

Fr Ndega

domingo, 7 de julho de 2019

LA GIOIA DI ESSERE DISCEPOLO/A



Riflessione a partire di Is 66, 10-14; Gl 6, 14-18; Lc 10, 1-12


     
       Quello che riassume il messaggio di questi testi è la certezza che siamo chiamati alla gioia e che questa gioia è condizionata dalla fedeltà al Dio fedele. “Egli vuole plasmare in noi il cuore del suo Figlio” e per questo ci vuole disponibili e generosi.

      Usando un linguaggio materno, Isaia fa un invito alla gioia a motivo di quello che il Signore sta per compiere nella vita del suo popolo. La presenza costante di Dio in mezzo al suo popolo fa superare i momenti di disagi e delusione aprendo spazi alla speranza e alla gioia anche se tutto sembra perduto. Come al popolo della Antica Alleanza, anche a noi viene chiesta una instancabile fiducia nell’azione misteriosa del Signore perché è sempre fedele Colui che promette.

       La seconda lettura presenta una grande polemica: alcuni giudeo-cristiani, che rimanevano ancora legati alle loro tradizioni giudaiche, volevano costringere i pagani ad essere circoncisi come loro. Per questo motivo Paolo dice che se giudichiamo così rendiamo vana la croce di Cristo. Tramite la croce Cristo ha vinto la morte e anche il mondo vecchio è stato crocifisso! "Se uno è in Cristo, è una creatura nuova; le cose vecchie sono passate, ecco ne sono nate di nuove". Ci viene chiesto di vivere da risorti, abbandonando i vecchi atteggiamenti le vecchie mentalità, tutto ciò che contraddice la nostra nuova condizione.

Il brano del Vangelo ci presenta Gesù che oltre gli apostoli chiama ed invia altre 72 persone ad evangelizzare. L’evangelizzazione non è compito solo dei preti e suore ma coinvolge tutti. Gesù li manda a due a due mettendo al centro della loro attività l’esperienza comunitaria; essa è la prima testimonianza che devono dare al mondo. La missione è un impegno che non si assume da solo. Abbiamo bisogno del supporto comunitario per l’esito della nostra missione.

I discepoli devono essere persone di preghiera come esperienza fondante, cioè, come base che mantiene l’edificio della loro esistenza. Devono essere consapevoli che la messe ha il suo padrone, un Padre buono e generoso, che sa dei bisogni dei suoi figli prima che gli chiedano qualcosa. Dio non ha bisogno della nostra preghiera; siamo noi che abbiamo bisogno di pregare poiché quando preghiamo cresciamo nella consapevolezza di essere figli e discepoli molto amati; diventiamo quello che già siamo per vocazione. I discepoli sono come agnelli in mezzo a lupi, entrando nella dinamica del vero Agnello, Colui che toglie i peccati del mondo perché è in grado di donare la propria vita per i suoi amici. È in questa logica – dell’amore, del dono di sé - che la loro vita trova il suo vero senso.

Essi devono abbandonare le false sicurezze e tutto ciò che impedisce un abbandono fiducioso alla provvidenza, poiché tali sicurezze tendono a occupare nella nostra vita il posto che appartiene a Dio. La vita semplice e distaccata del discepolo è un annuncio profetico dell’amore e della cura di Dio per i suoi figli. Vivere in sovrabbondanza, invece, oltre a negare la nostra identità di discepolo, mette a rischio la credibilità del messaggio che portiamo essendo ostacolo alla fede altrui. Chiediamo al Signore la grazia di vivere gli atteggiamenti del vero discepolo, secondo il desiderio di Cristo affinché a partire dalla nostra testimonianza la fede nella Provvidenza cresca sempre di più.

Fr Ndega
Revisione dell'italiano: Giusi