sábado, 20 de janeiro de 2018

WITO KAMA MWALIKO KWA MABADILIKO YA MAWAZO


Kutafakari kuhusu Yon 3, 1-5.10; Mk 1,14-20


          Tukiendelea tafakari yetu iliyopita, tena jambo letu ndilo la wito. Tofauti kati yao ni kwamba katika mara iliyopita tulialikwa kutembelea/kushiriki katika hali ya kawaida ya Mwalimu Yesu; mara hii ndiye yeye ambaye anakuja katika hali yetu ya kila siku kwa njia ya unyenyekevu na mvuto na kutoa pendekezo lake kwetu, hata ni ngumu kulikataa. Labda hatupati kumfuata ‘mara’ kama yeye anataka, lakini anakubali tuanze kuchukua mwendo wa kutubu kwa umakini ambao unafananisha maisha yetu pole pole kulingana na njia yake ya kuwa na kuishi. 
            Andiko la kwanza linaongea kuhusu wito wa Yona na kutubu kwa watu wa Ninive, mji mkuu wa Asiria. Yona ndiye nabii aliye na tabia siyo za kawaida. Mungu alimpa kazi, kama alivyofanya kwa ajili ya manabii wengine, lakini badala ya kuchukua kazi, Yona aliamua kuenda zake mbali sana na Mungu. Baada ya muda fulani katika tumbo la nyangumi, alichukua kazi lakini kwa upinzani ya kibinafsi dhidi ya njia ya Mungu ya kutenda. Nabii Yona ndiye Myahudi ambaye aliitwa kufanya kazi kati ya maadui wa Wayahudi. Basi, wakati Mungu alipomwomba kutangaza kutubu, Yona alitangaza kuharibu. Kwa bahati nzuri, watu walimwamini Mungu na kubadilisha tabia zao. Mungu anatarajia tabia hii tu kutoka kwa watoto wake bila kufikiria taifa gani mtu anapokuja.
        Hii ndiyo nia ya Yesu wakati alipoanza maisha yake ya umma. Wakati Yohana Mbatizaji alifungwa gerezani, yaani wakati ambao utabiri wa Neno la Mungu haukutangazwa tena, Yesu alitambua kwamba nafasi yake ilifika. Basi, yeye aliacha Uyahudi ambapo alifanya uzoefu wa ubatizo na jangwa na kwenda Galilaya akitangaza habari njema ya Mungu. Kiini ya ujumbe wake ni  ukaribu wa Ufalme wa Mungu na hivyo, mwaliko wa kutubu kama tabia muhimu ya kuukaribisha ufalme huu. Alisema: “Wakati umetimia na ufalme wa Mungu umekaribia. Tubuni na kuiamini injili!” Kupitia Kristo, wakati unapata ukamilifu wake. Wakati ambao tunaongea hapa sio kronos kama kiasi ya wakati, bali ndiyo kairos, yaani wakati mwafaka ya kukutana na Mungu na wokovu wake.
            Katika nafsi ya Kristo, ufalme unakuwa hali halisi. Kuuamini na kuukubali ufalme huu kunamaanisha kukubali kumfuata Kristo ambaye analeta pendekezo la jamii mpya kabisa na kubadilisha maisha ya walioalikwa. Hivyo, Yesu anapita na kuwaona ndugu wawili, yaani aliiangalia familia ambayo kwa kupitia mahusiano na kazi yake ya kila siku inazaa maisha na kujenga historia. Yesu anajitoa kama kipimo, akiwaita ndugu hawa kutoa maana kwa maisha yao ya kawaida. Alisema: “Mnifuateni nami nitawafanya nyinyi kuwa wavuvi wa watu.” Yesu ndiye wazi sana na pendekezo lake lina mvuto na kunasababisha uamuzi. Kutoka kwa ndugu hawa Yesu anataka kujenga dunia ya kindugu. Pendekezo lake linaalika kuacha kila kitu mara, yaani kwa upatikanaji kabisa: kuanza kwa nyavu na baadaye familia… ama mawazo ya uongo kuihusu familia...
           Kulingana na andiko hili, mwaliko wa kutubu unauhusu mwaliko wa kumfuata Yesu. Mwaliko wa msingi ulioelekezwa kwa kila mtu ndio ule wa kutembea nyuma ya Kristo na pamoja naye ili kuitoa maana ya kweli kwa maisha ya mtu mwenyewe, kama wanafunzi wa kwanza ambao waliendelea kama wavuvi lakini kwa njia tofauti. Ikiwa mimi niko na kazi ama nimefunga ndoa ama niko na wito fulani wa utumishi wa kikanisa ama tena ninautafuta wito wangu, baada ya kukutana na injili ya Kristo siwezi kubaki nilivyo kabla ya mkutano huu, yaani ninapaswa kuamua na kuishi wito na kutafuta kwangu kwa njia tofauti. Hali ya kawaida na hali ya jumuiya zilikuwa muhimu sana katika maisha ya Yesu na ya wanafunzi wa kwanza. Kwa upande wetu hali hizi ndipo mahali ambapo Mungu anatutembelea daima na kupendekeza kwetu mwendo wa metanoia, yaani mabadiliko ya mawazo, ya njia ya kutenda, ya kufikiri na kuishi.
         Kwa kuishi vizuri wito wetu ni lazima kuacha kitu fulani ama vitu vingi. “Hata hivyo ni muhimu kukumbuka pia kwamba mwanafunzi sio mtu ambaye anaacha kitu bali ndiye yeyote ambaye alimkuta Mtu. Ikiwa tunaacha kitu tunazawadiwa mno na Yule ambaye tunamkuta”. Ndivyo hivyo tukio letu na Kristo; hatujui litamalizika wapi, lakini yeye anajua. Ni lazima ujasiri kwa kumwamini yeye ambaye alipendezwa kuukabidhi ufalme wake kwa sisi. Basi, tunaalikwa kuyaungana maisha yetu na yake ili kuitoa maana ya kweli kwa maisha yetu. Kama wanafunzi wa kwanza ambao waliacha kila kitu na kwa utayari walimjibu Bwana ambaye aliwaalika, tujikabidhi katika Yesu, kwa kuacha usalama wetu wa uongo na kila kitu ambacho kinatuzuia kuishi wito wetu kwa upatikanaji kabisa kwa ajili ya ufalme wake.


Fr Ndega

Nenhum comentário: