quarta-feira, 13 de maio de 2015

KUPENDA KAMA MUNGU ANAVYOPENDA


Mdo. 10: 25-26, 34-35, 44-48; 1Yoh. 4: 7-10; Yo 15: 9-17

     Mungu hawabagui watu kwa maana anapenda na katika upendo hakuna ubaguzi. Mungu anawakaribisha wale wanaomwabudu na wanaishi kwa udugu. Kuabudu na udugu ni uhusiano na wale ambao wanamwabudu kwa njia hii, wanaabudu kwa Roho na ukweli. Roho Mtakatifu aliwashukia wale ambao wakalisikiliza Neno la Mungu kupitia kinywa chake Petro, akidhibitisha kwamba Mungu anawatendea wote kwa usawa. Mbele ya Mungu hakuna mtu wa heshima zaidi kuliko mwingine. Mungu hakuzi upendeleo na hakubali umaarufu, bali anatarajia ahadi kwa njia yake ya kufikiri na kutenda. Maana kwa njia hii ni upendo wake wa uhuru kwa wote.      
      Mtakatifu Yohana katika waraka wake anawaalika watu kupendana kwa sababu upendo kutoka kwa Mungu na wale wanaopenda wanamjua Mungu. Basi, kupenda ni kujua. Kujua katika Biblia si uzoefu wa akili, lakini ni uzoefu wa ndani. Mungu anajua kwa sababu anapenda. Kumjua Mungu ni kumpenda, kufanya naye uzoefu wa ndani. Mungu ni upendo na aliwapenda sana wanadamu kwamba alimtuma Mwanawe pekee kama maonyesho makuu ya upendo huu ili kuwafundisha watu jinsi ya kupenda kwa kweli. Kutokana uzoefu huu tulipata maisha kwa maana upendo tu unayazaa maisha na wale ambao wanakubali kuhusishwa katika uhusiano wa upendo kati ya Baba na Mwana, wanaishi maisha mapya.
      “Mwana alitupenda kama Baba anavyompenda”. Andiko hili la injili ni sehemu ya ujumbe wa maagano ya Yesu. Yaliyomo ya ujumbe huu ni urithi wake Mwalimu, aliokuwa na kama muhimu zaidi ili kuacha kwa wale ambao lazima waendeleze kazi yake. Umuhimu wa mafundisho ya Yesu ni kupenda. Upendo una chanzo chake katika Mungu kwa sababu Mungu ni upendo na anampenda Mwana. Uwepo wa Mwana miongoni mwa wanadamu uliufanya upendo huu kujulikana. Upendo ni ndani ya Mungu; ni maana ya ushirikiano wake. Wanadamu ni matokeo ya ushirikiano huu na wanaalikwa kujihusisha katika ushirikiano huu sawa, kukaa katika upendo wa Kristu. Kigezo ili kukaa katika upendo wake ni kuishi mafundisho yake, ni kwamba, kupendana kama alivyotupenda na akajitoa kwetu. Yesu halazimishwi kutupenda. Upendo wake ni maonyesho ya furaha yake yote: furaha ya ushirikiano wake na Baba, furaha ya kuwa miongoni mwa wanadamu, furaha ya kuwachagua wanadamu kama washirika katika kazi yake, furaha ya kuutoa uhai kwao. Kuushiriki upendo wake nasi, Yesu anayajaa maisha yetu kwa furaha kubwa kwa sababu kwa yeye upendo na furaha inatembea pamoja. Kama hii, mtu tu anayependa kwa kweli ni wenye furaha ya kweli.  
      Upendo ni maana ya wokovu wa ulimwengu, kwa sababu ilikuwa kwa upendo kwamba Mwana wa Mungu aliutoa uhai wake. Kulingana na Yesu thamani ya urafiki wa kweli hupimwa kwa uwezo wa kuyasalimisha maisha kwa upendo. Yesu ni rafiki yetu kwa sababu alifanya hivyo vizuri sana. Alituchagua na alituteua kuenda na kuyazaa matunda, na matunda yanayodumu. Tutakuwa marafiki zake ikiwa tuna ujasiri wa kupenda kama yeye alivyopenda. Anajitambua na wale wanaotumwa katika jina lake. Utambulisho huu ni matokeo ya upendo wake ndani yetu kwa sababu ni sahihi/tabia ya upendo kuumba utambulisho na hisia ya miliki. Ikiwa tunakaa pamoja naye tutakuwa watu wa ushirika na tutaweza kusaidia ushirika katika jumuiya zetu. Huu ni ushahidi wetu  wa kwanza: Mwone kama wanavyopendana”! Ilikuwa maoni kuhusu Wakristu wa Kwanza. Upendo wao ulionyeshwa kupitia ridhaa wao kwa wao, kushiriki pamoja, uvumilivu katika maombi pamoja na unyenyekevu wa moyo. Je, maisha yako ni maonyesho ya yale wewe huamini? Itawezekanaje jumuiya zetu kuonyesha hali halisi hii ya Jumuiya za Kwanza?
      Badala ya kuuzaa ushirikiano katika jumuiya, upendo hutufungua kwa watu wengine nje, wanaohitaji kukaribishwa pia. Wale wanaopenda kweli hawabagui watu na ni makini kwa hali halisi maalum, kujifunza kutoka kwa Mungu, anayewapenda wote, lakini anapendelea maskini na wale hawana nguvu. Kama hii pia mama, anawapenda watoto wake wote, lakini ana utunzaji maalum kwa mtoto mgonjwa. Basi, tufikiri kuhusu upendo wetu kwa wale wanaohitaji zaidi katika jumuiya.    

Fr Ndega
Mapitio: Sara

Nenhum comentário: