sexta-feira, 7 de novembro de 2014

UMUHIMU ZAIDI WA MAISHA



Kutafakari toka Kutoka 22, 21-27; 1Thes 1, 5-10; Mathayo 22, 34-40

       Kulingana na Maandiko, Mungu ana uhusiano maalum na watu wa Israeli. Anaanzisha agano na watu hao kuwapa miongozo kadhaa ili watende vyeme, kuhifadhi maisha yao. Ni katika hali hiyo kwamba Amri ziliibuka/patikana. Kuishi katika Amri kumekuwa umuhimu zaidi katika safari ya Watu wa Israeli kwa ambao Sheria ni Neno la Mungu na Neno la Mungu ni Sheria. Wakati wao husema “Sheria ya Mungu ni kamilifu, faraja kwa roho”, wanamaanisha kwa Neno la Mungu. Kuna uwiano wa kina kati ya Sheria na Neno, kwa sababu amri za Sheria zinaonyesha huduma ya upendo wa Mungu anayeongea kuonyesha njia za ukombozi na kisha zinadhihirisha pia utambulisho wa kweli wa watu ambao wanatii, kukuza hisia za miliki ya Mungu wao. Utiivu kwa amri ni chanzo cha baraka kinachoelekeza kwa uhai, wakati uasi kwa hizo unaelekeza kwa kifu. 
       
     Katiku Sheria kuu, Wayahudi wameweka sheria nyingi kwamba hatimaye zilibadilisha lengo kutoka iliyokuwa muhimu zaidi. Amri kumi za awali zilikuwa mia sita kumi na tatu. Watu maskini walichukuliwa wenye dhambi kwa sababu hawakuweza kukariri amri hizi zote na kwa hiyo, hawakuziweka vitendoni. Hata hivyo, sehemu hii ya idadi ya watu walijua na walikuza umuhimu zaidi wa Sheria. Hilo ni jibu la Yesu anaposema: “upende Bwana Mungu wako na moyo wako wote, na akili yako yote, na nguvu zako zote” (Dt 6: 4-5) “na jirani wako kama unavyojipenda mwenyewe” (Lev. 19: 18).     
         Kumpenda Mungu ni amri ya kwanza ya zote, lakini Yesu aliiunganisha na upendo kwa jirani, kuonyesha kwamba haiwezekani kumpenda Mundo bila kumpenda jirani. Yakobo katika waraka wake anamfikiria kama mtu mwongo anayesema kwamba anampenda Mungu na hampendi jirani. Kutoka amri ya kumpenda Mungu inabubujika kumpenda jirani kama matokeo. Chanzo ni Mungu daima kwa sababu alikuwa aliyetupenda wa kwanza. Ni kutokana na upendo kwamba Mungu anao kwetu – kwa njia ya ukarimu na bure – ambayo inawezekana kuwapenda wengine na uhalisi. “hiyo ni changamoto kwa tamaduni zote ikiwa ni pamoja na  hizo katika Afrika, ambapo uaminifu kwa familia na mila unakuzwa mara nyingi kama amri ya kwanza.”       
      Yesu aliyefanika mwili, ni upendo wa huruma wa Mungu na maisha yake yakasalimika kwa wote yanaonyesha kwamba kupitia upendo tu binadamu anaweza fikia mafanikio yake binafsi. Bila shaka, kwamba kuwa ndani ya dini na ushiriki misani ni ishara ya upendo kwa Mungu kama kipaumbele katika maisha yetu. Hata hivyo, katika mwisho wa maisha yetu ombi letu halitakuwa “Je, ulikuwa wa dini gani?” au “Je, mara ngapi ulienda misani?”, lakini swali kamili litakuwa, “ulikuwaje upendo wako kwa wengine?” kiwango cha upendo wetu kwa Mungu kinaonyeshwa katika njia kama tunavyowapenda wengine. Anapenda kweli mtu ambaye anatamani tu wema kwa mtu mpendwa, hata kama hastahili. Hivi ndivyo Mungu anavyotupenda, kwa ukarimu na bure. Uzoefu huu lazima utuongoze kufanya anavyofanya. 
      Muhimu zaidi kwa Yesu ni kumpenda Mungu, kupenda pia jirani. ufundishaji wake wa ajabu yako ulifanya amri hizo mbili hata kupatikana zaidi, akitoa ushauri kwamba inatosha tupendana kama alivyotupenda. kama vile Mungu ametupenda katika Kristu, sisi lazima tupende kutoka kwa Kristu. Yeyote anayependa katika njia hiyo amefahamu umuhimu zaidi wa Sheria na maisha, kwa sababu yeyote anayefuata Yesu hafuati sheria au mafundisho, lakini anafuata Mtu.
    Kwa hiyo, kigezo tu Wakristu wanacho kushuhudia upendo wa Mungu duniani ni kupenda wengine kama ndugu. Tunampenda Mungu wakati tunampa mahali pa kwanza katika maisha yetu, kutafuta kwanza ufalme wake na haki yake, wakati sisi ni waminifu katika sala zetu kila siku, tunaposhiriki kwa makini katika sherehe ya sakramenti. Sisi huonyesha upendo kwa jirani wakati tunaweza kuhisi huruma mbele ya hali halisi ya huzuni na mateso ya wengine na tunapatikana kuwasaidia katika mahitaji yao. Katika maana hii, ilisemwa kuhusu Jimuiya za kwanza: “Oneni wanavyopendana”. Hata hivyo, iliwezekana tu kwa sababu walibaki pamoja katika upendo wa Mtu aliyewaita. Hitaji hilo lingalipo katika siku zetu na linaaminisha nguvu za uhai ya kazi yetu kama Wakristu.    

Fr. Ndega
Mapitio: Mwalimu Patrick

Nenhum comentário: