quinta-feira, 27 de novembro de 2014

MUNGU NA HAO AMBAO NI MASIKINI




Tafakari kutoka Ezekieli 14: 11-12.15-17; 1Kor 15: 20-26.28; Mt 25: 31-46

      Maandiko haya inaongea kwamba Mungu ni Mfalme-mchungaji ambaye anawahifadhi na anajitambulisha na hao ambao ni masikini. Upendo na huruma kwa wengine ni kigezo ili kuingia ufalme wake. Kwa maana hii, tukaribishe ujumbe wa Liturujia hii kwa shukrani na uwazi, kutafakari kuhusu fumbu la Ufalme wa Mungu na utendaji wake kupitia kazi ya Kristu.

    Nabii Ezekieli anashutumu kutowajibika ya viongozi wa Watu wa Israeli ambayo ilisababisha uhamisho, kipindi cha huzuni na mateso kwa watu. Lakini katika ujumbe huu, nabii anatangaza pia kwamba Mungu ni busara na makini sana kwa watu wake. Anachukua ubinafsi hali ya watu wake kama mchungaji wa kweli, kuongoza wao kwa hali halisi mpya. Unabii huu hufanya mafanikio yake katika Yesu Kristu, Mchungaji Mwema. Kulingana na Mtakatifu Paulo, Yesu anashinda nguvu zote duniani, kupitia kifo chake na ufufuo wake, kuokoa ubinadamu na kuanzisha Ufalme wa Mungu Baba yake. Wanadamu wote wanaoalikwa ni kwa ufalme huu. Muungano na Kristu ni usemi wa ushiriki huu na unaongoza kwa uzima wa milele. Hivyo, kuwa miliki ya Kristu ni kuwa wa Ufalme wa Mungu, dhamana ya uzima wa milele

     Andiko hili ya Injili linajulikana kama “Hukumu ya mwisho” na wengi wetu hufikiri kwamba Yesu ni “hakimu” anayehukumu vitendo vya binadamu, kuwatuza wengi na kuwaadhibu wengine. Lakini tulijifunza kupitia maneno yake yenyewe kwamba “Mungu hakumtuma Mwana ulimwenguni ili kuwa hakimu wake, lakini kwa kuwa mkombozi wake” (Yohane 3, 17). Hivyo, lengo lake si kuhukumu bali kuokoa. Hukumu huanzishwa kwa vitendo vya watu. Kulingana na andiko hili, Yesu ni Mfalme-mchungaji. Mfalme huyo ana nia ya kukusanya watu wote karibu na yeye mwenyewe na huduma maalum kwa watu hao masikini. Anajitambulisha nao na anawaanzisha kama rejea kuokoa wengine. Anawahamasisha watu wengine kufanya matendo mema kwao na anawapa zawadi kwa hao ambao hukumbatia sababu hiyo. Hivyo, huduma ya upendo tunayo kwa masikini ni kigezo kuingia Ufalme. 
       
     Wainjilisti wanaonyesha kwamba Yesu alikataa cheo cha mfalme katika wakati wa utukufu, na akakubali katika wakati wa ushinde. Upinzani wake kwa cheo hiki ulikuwa kwa sababu mawazo ya kisiasa ya watu kuhusu suala hili. Lakini yeye mwenyewe anatumia cheo cha mfalme katika andiko hili ili kutusaidia kuelewa maana haki ya Ufalme na lengo lake kama Mfalme. Ufalme wake si kutoka ulimwengu huu na hauwezi kuonekana (ni huko au ni hapa). Yesu anaufafanua kamwe Ufalme wa Mungu, lakini alisema kwamba huo ni tayari sasa kati yetu na tunaweza kuhisi tukio lake. Katika mafanikio yake ya kidunia, hali halisi ya Ufalme wa Mungu si mbali sana toka hali halisi ya binadamu. inaishiwa kupitia thamani nzuri za tamaduni zetu na unazishinda.

    Kiini ya ujumbe wa Yesu ni tangazo la Ufalme wa Mungu, kwa sababu hatangazi mwenyewe lakini anatangaza Ufalme. Katika Yesu, Ufalme unakuwa ukweli halisi. Mjadala wa uzinduzi kuhusu tukio hili maalum unafanyika kwa wakataliwa na jamii, hao ambao ni maskini. Katika nyuso zao, Yesu alitufundisha kutambua uso wake wenyewe. Ufalme ni wao na wao ni wamiliki wa Ufalme. Katika matendo yake mema na watu hao, Yesu anaushahidi kwamba wakati mpya umekwishaanza, kubadilisha hali nyingi katika dunia, kama vile: wagonjwa wanapona, bubu wanaongea, vipofu wanaona, maskini wanahubiriwa Habari njema na watu wenye dhambi wamepata msamaha wa Mungu . Upendo na huruma wa Yesu kwao ni mwanzo wa wakati huo mpya. Ni lazima kufikia mafanikio yake katika Ufalme ufafanuzi wakati upendo kwa Mungu na kwa jirani wataishiwa kwa ukamilifu wake.

     Tunaalikwa kutambua katika ishara za ukombozi za Kristu hatua ya wokovu wa Mungu na kufuata nyayo zake kwa uaminifu, kutangaza habari njema ya Ufalme. Kwetu, kutafuta Ufalme huo ni lazima kipaumbele, kwa sababu katika kutafuta hii tunakuta maana ya maisha na kazi zetu. Yesu ametukabidhi Ufalme wake na tumekabidhi maisha yetu kwake. Ni kukabidhiana. Kumfuata Yesu ni kukubali ufalme; upinzani dhidi ya Yesu ni upinzani kwa utendaji wa Ufalme. Wakati sisi hupatikana kwa mipango ya Yesu, yeye hututumia kama wapatanishi wake ili kuendelea kutangaza kiinua mgongo cha Ufalme wake, kuwakaribisha watu wengine kujiunga na nguvu pamoja naye katika uanafunzi wakarimu na halisi milele. Ingawa yeye huweza kufanya kila kitu peke yake, alitaka yetu kwa sababu anajua kwamba tunamhitaji sana, kwa hivyo anasema, "Bila mimi hamwezi kufanya chochote" (Yohane 15: 5).

Fr. Ndega
Mapitio: Rose Mong'are

Nenhum comentário: