sábado, 25 de fevereiro de 2023

MAFUNDISHO YATOKAYO JANGWANI

 

Kutafakari kuhusu Mwanzo 2, 7-9; 3,1-7; Waroma 5, 12-19; Mathayo 4, 1-11



 

 

Binadamu alifanyika kwa mavumbi ya ardhi ili kupokea uhai wa Mungu ndani yake. Pamoja na mahali pazuri pa kuishi, binadamu alipewa pia zawadi zote alizohitaji aishe kwa ushirika na Mungu na kwa maelewano na ardhi iliyo sehemu ya maisha yake. Lakini majaribio ya kutumia zawadi zake kwa ajili ya nafsi yake mwenyewe yalimwongoza binadamu kuacha ushirika na Mungu na kupanga maisha yake tofauti kabisa na mpango wa Mungu kwake.

Binadamu wa kwanza alipendelea kumtii “nyoka”, aliye mfano wa “yule mwovu,” kuliko kumtii Mungu. Hali hii ilisababisha mauti kwa watu wote. Ndiye Yesu “Adamu mpya na wa kweli” aliyegundua tena mpango Mungu na kushinda uovu akimtii Baba yake. Chaguo lake lilifanya tofauti, yaani, lilikuwa muhimu mno kwa sababu ikawaletea wote uzima.  

Mambo yote ambayo Yesu aliweza kufanya alipata mafanikio kwa msaada wa Roho Mtakatifu. Ndiye huyo Roho ambaye alimwongoza nyikani na huko pia alijaribiwa na shetani. Kweli Yesu alionyesha ahadi na hali yetu ya kibinadamu. Mfano, yeye alienda jangwani baada ya ubatizo. Ingawa hakuhitaji kubatizwa alikubali uzoefu huu kwa ajili ya mshikamano nasi tulio wenye dhambi na ya kuiheshimu kazi ya Yohane. Vivyo hivyo, alikubali kushawishiwa jangwani.

Kupitia uzoefu huu, Yesu anatuonyesha kwamba “baada ya ubatizo majaribio mengi yanatujia.” Kwa upande wake, ingawa alijaribiwa jangwani, “alichagua kubaki mwaminifu kwa Mungu.” Kila mtu anakabiliana na njia mbili ya kufuata na kupaswa kuchagua moja tu ili kufanya mapenzi ya Mungu. Ndiye Yesu mfano wa chaguo kamili. Yeye alijua wazi sana kwamba ndiye Mwana wa Mungu aliyekuja duniani si kwa ajili ya kufanya mapenzi yake mwenywe bali ya Baba.

Katika uzoefu wake wa jangwa, Yesu alifunga kwa siku arobaini na akaona njaa. Arobaini ni namba ya mfano iliyomaanisha “muda mrefu.” Kabla ya Yesu tuko na baadhi ya mifano ya Viongozi wa kibiblia ambao, kabla ya kuchukua kazi ya kuwaongoza watu ama kabla ya tukio muhimu, waliruhusu kuongozwa jangwani na kubaki bila kula chakula wakati wa muda mrefu ili waweze kujiandaa wenywe vizuri kwa ajili ya kazi aliyowakabidhi Mungu.

Tukumbuke ile muda ya siku arobaini ambayo Musa alibaki mlimani Sinai ili azipokee Amri Kumi; na pia siku arobaini wa Eliya akitembea mpaka mlima Horeb ili akutane na Mungu na kupokea kutoka kwake maelekezo ya kazi yake kama nabii. Namba arobaini inatumika pia kwa ajili ya kuongea kuhusu kiasi ya miaka ambayo Waisraeli walibaki jangwani kabla ya kuingia katika nchi ya ahadi. Kwa watu hawa wakati huu ulikuwa wa utakaso na kukomaa kulingana na ufundishaji wa Mungu. Lakini hawakuwa na uaminifu kama Yesu alivyo.

Uzoefu jangwani ni maalum kwa ajili ya upweke, utakaso na kukomaa. Lakini jangwa ni pia maisha yetu ya kawaida ambapo tumeongozwa na Roho Mtakatifu, lakini pia tunajaribiwa kukata tamaa kwa sababu ya majaribio ya yule mwovu, kama ilivyotokea na Yesu. Mshawishi alianza kutoka mambo madogo akichukua nafasi ya kosa la nguvu mwilini mwa Yesu kwa sababu ya kufunga. Matarajio yote yalikuwa dhidi ya namna ya utume wa masihi ambao Yesu alichagua.

 Yesu alishawishiwa kutumia uwezo wake kwa manufaa ya kibinafsi badala ya kwa ajili ya upendo, ya huruma na ya kuwahudumia wengine. Tena Yesu alishawishiwa kujisifa mwenyewe badala ya kumtangaza Mungu na Ufalme wake. Majaribu matatu ya Yesu yamaanisha majaribio yote ambayo yalikuwapo maishani mwake nyakati zote za kazi yake. Hata hivyo, alipata kushinda yote kwa sababu akaongozwa na Roho Mtakatifu na kuwa mtiifu kwa Baba yake.

Majaribu ya mali, nguvu na utukufu Yesu aliyokabiliana nayo hayakumzuia kufanya mapenzi ya Mungu. Kama ilivyotokea na Yesu, na Adam na Waisraeli, sisi pia tunashawishiwa kuishi bila kumwamini Mungu. Mitego ya mshawishi inatuongoza kupendelea kutumia mamlaka kuliko utumishi, kuamuru kuliko kutii, kudanganya kuliko kusaidia, kulazimisha kuliko kupendekeza, kutafuta upendeleo kuliko kupenda, kuwa wanafiki kuliko kuwa binadamu wa kweli.

Kama Yesu amekwisha kumshinda adui ya Mungu, ndilo chaguo lake msukumo ili chaguzi zetu ziweze kufanya tofauti, yaani kuwa muhimu sana. Kulingana na Mt. Agustino “Ikiwa katika Kristo tumeshawishiwa, katika yeye tutamshinda shetani. Kristo angeweza kumtupa mshawishi mbali sana naye; lakini ikiwa yeye hangalikuwa ameshawishiwa hangetufundisha jinsi ya kushinda juu ya majaribu.” Kweli yeyote ambaye anaufuata mfano wake wa kumtii Baba na kufunguliwa kwa msaada wa Roho Mtakatifu anapata kufanya mapenzi ya Mungu na kushinda majaribio yote.


Fr Ndega

Nenhum comentário: