sábado, 4 de agosto de 2018

TUJIFANYE “CHAKULA” KWA AJILI YA WENGINE



Kutafakari kuhusu Kut 16: 2-4, 12-15; Waef. 4: 17, 20-24; Yoh. 6: 24-35


       Ingawa wana wa Israeli walikuwa watumwa katika Misri, wakawa na vyakula vingi hata washibe. Walipoacha utumwa kwa nguvu ya Mungu, wakapata utambulisho mpya kama Watu wenye uhuru. Utambulisho huu mpya ulileta baadhi ya changamoto kama kuishi jangwani, kuwa na chakula kidogo ama kutokuwa na chakula, kutokuwa na maji, utekaji wa watu wengine, na kadhalika. Kwa hivyo, walikuwa na mwelekeo wa kulalamika. Lakini, katika mazingira haya magumu Waisraeli hawakuwa peke yao, kwa sababu Mungu aliyewakomboa aliendelea kuandamana nao maana yeye ndiye mwaminifu kwa ahadi zake. Aliwalisha kwa mana sio kwa sababu ya malalamiko yao tu bali hasa kwa maana yeye ndiye macho kwa mahitaji ya watu wake hata kabla ya kumwombe kitu. Hakika walikuwa na ugumu wa kuelewa ufundishaji wa kimungu. Akitoa mana, Mungu aliwaonyesha upendo na utunzaji wake na kutangaza zawadi kubwa zaidi itakayotimizwa na Mwana wake aliye “Mana ya kweli”.

     Mt. Paulo anafanya tofauti wazi kati ya maisha ya mtu kabla ya ubatizo na ya kutoka ubatizo. Kabla ya ubatizo mtu huishi kama mtumwa kwa maisha ya zamani na njia ya ubatili. Kupitia ubatizo mtu anabadilishwa kabisa kwa kupokea maisha mapya katika Kristo, yamejaa maana. Ndiyo hali ya ubatizo wetu. Mbele ya jaribio ya kuishi kama kabla ya utambulisho huu, tunasaidiwa na neema ya Mungu ili kufananisha maisha yetu kulingana na njia ya kuishi ya Mwanawe aliyeweza kutoa maana ulimwenguni kwa kujitolea kwake.  

     Yesu alitenda ishara kubwa ya kuzidisha mikate na samaki kwa ajili ya kuwalisha watu, akiwaonyesha hisia mbele ya mahitaji yao. Baada ya kula hata kushiba watu walitaka kumfanya Yesu mfalme wao. Kulingana na mawazo ya jamii matokeo hayo ni ishara ya mafanikio ya kazi na njia kamili ya mtu ambaye anakuwa maarufu. Lakini Yeye akijua mpango wao alitoroka akienda mlimani peke yake. Kisha watu walimtafuta na walimkuta na wanafunzi wake katika Kapernaumu. Kulingana na Yesu hawakufahamu ishara na hawakuwa na nia kamili ya kumtafuta. Hatimaye, aliwaalika kumkubali yeye kama mkate wa kweli kutoka kwa Mungu ambaye anautoa uzima kwa ulimwengu. Yeyote ambaye anakuja kwake na kumwamini yeye hataona njaa na kiu kamwe.

     Yesu alikuwa na hisia mbele ya mahitaji ya watu na kujaribu kuutoa mwelekeo mpya kwa maisha yao kupitia uzoefu wa huruma na kushirikiana, lakini maana ya tumbo lao, wakawa kama “vipofu” na bila uwezo ili kuelewa maana ya ishara. Hawakupata mafanikio katika kumtafuta Yesu kwa sababu ya kosa la maana kamili. Kweli nia ya Yesu akiwalisha watu ilikuwa kuonyesha hisia yake na kuwaandaa kwa mafundisho yake kuhusu mkate tofauti na kweli. Yeye anatoa chakula kinachodumu mpaka uzima wa milele ambacho ndiye yeye mwenyewe. Anadhihirisha pia kwamba siyo Musa ambaye aliwapa watu mana, lakini ndiye Mungu. Mana ni mfano tu wa zawadi kubwa iliyo Mwana wake ambaye Mungu alimtoa kwa uzima wa ulimwengu. Kweli “zamani, Mungu alitoa mana, leo hii Yesu mwenyewe amejifanya mkate, chakula chetu na chemchemi ya uzima.”

    Basi, chakula hiki ndicho Ekaristi takatifu iliyo ishara kubwa ya upendo wa Mungu na maonyesho ya kujitolea kwake Kristo kwa hiari. Maadhimisho ya Ekaristi ni ufanisi maishani mwetu ikiwa tunasherehekea kama maonyesho ya upendo. Wale tu wanaopenda kweli wanaweza kujitolea kwa ajili ya wengine kama Kristo alivyo. Upendo tu unazaa ushirika na “vitu tu vinavyofanyika kwa upendo vinadumu”. Kupitia Ekaristi tunabadilishwa kabisa kuwa kama Yule tunayeadhimisha kwa kukubali ahadi ya kuishi maisha mapya yaliyo matokeo ya mkutano naye. Hivyo, baada ya kila maadhimisho ya Ekaristi tunapewa changamoto ya kurudia shughuli za kila siku kama mashahidi wa Yule ambaye anayatoa maisha yake kwa upendo ili watu wote wawe na uzima wa milele.

    Kupitia Neno la Mwanawe na kujitoa kwake katika Ekaristi, Mungu anaendelea kuwalisha watu wake na kuwaonyesha upendo na utunzaji wake. “Yesu ni mkate unaotushibisha, maji yatulizayo kiu yetu, ni Yesu pekee awezaye kutuliza hamu ya mioyo yetu” inayotamani milele. Tunapaswa kujiuliza daima ikiwa tunamtafuta Yesu na nia hii ama na mvuto wowote. Hatuwezi kupata mafanikio katika kumtafuta Yesu ikiwa lengo letu ndilo kumkawisha katika uhusiano umefungwa ili atumikie mivuto yetu ya ubinafsi bali tunapaswa kumtafuta kwa ajili ya kumjua nzuri na kumpeleka kwa wengine. Kulingana na Papa Francisco, “furaha ya mkutano yetu na Bwana haitakuwa kamili ikiwa hatuishiriki na wengine”. Tunaalikwa kuongoza kutafuta kwetu kuhusu Yesu kulingana na mawazo yake yaliyo mawazo ya kujitolea, ya ukarimu na ya upendo. Basi, tuendeni kukutana na Yesu ili kujifunza kutoka kwake jinsi ya kujifanya “chakula” kwa ajili ya wengine.

Fr Ndega

Nenhum comentário: