sábado, 10 de fevereiro de 2018

MAISHA MAPYA KWA KUPITIA IMANI NA HURUMA


Kutafakari kutoka Mk 1, 40-45

       Injili hii inatusaidia kutafakari kuhusu ugonjwa katika mazingira ya Yesu. Sio baadhi ya watu tu walikuwa wagonjwa, bali jamii nzima kwa sababu ilikuwa na mazoea ya kuwatendea mbaya walio na mahitaji ya utunzaji maalum. Hasa waliokuwa na ukoma walipaswa kujitenga na wengine na kukabili hali yao. Hao waliwekwa katika kundi maalum la wenye dhambi kwa sababu walichukuliwa kama waliolaaniwa na Mungu. Mtu aliyejichanganya nao alipata dhambi yao pia.  Hata wana wa familia hawakuweza kuwa kuwakaribia kwa sababu ya hatari ya kuambukizwa. Ubaguzi wa jamii kwao ulikuwa mbaya zaidi kuliko hatari yoyote ya kuambukiza. Yesu ndiye mwangalifu kwa hali hii kwa sababu ni dhidi ya mpango wa Mungu ambaye anataka maisha mengi kwa watu wake hasa wagonjwa. Hivyo, Yesu mwenyewe hakuwa na hofu ya kuwa mchafu kwa maana ya hali ya wagonjwa. Yeye aliwakaribia wagonjwa wengi na kuwagusa akivuka mipaka iliyowekwa na jamii.   
         Hata akijua kwamba sheria ilikataza mgonjwa wa ukoma awakaribia watu, wakati mtu huyo alipomwona Yesu, alimwendea na kutambua kwamba Yesu alikuwa na uwezo wa kumtakasa. Alionyesha imani yake katika Yesu na mara Yesu alimwonea huruma. Tunaweza kutambua uhusiano maalum kati ya tabia hizi mbili, yaani, imani ya mgonjwa na huruma ya Yesu. Yesu alifunua uso wa Mungu ulio uso wa huruma. Kupitia maneno na matendo, kila kitu katika Yesu kinadhihirisha tabia hii. Ndiyo huruma ambayo inamwimarisha Yesu atende. Yeye alimponya mgonjwa kwa sababu alitaka, lakini tena alitambua na kuthamini sana tabia ya imani ya mgonjwa. Pamoja na kuponya mgonjwa, tena Yesu alisahihisha mawazo ya uongo kumhusu Mungu katika jamii ambayo yaliisaidia hali hii mbaya.
            Mtu huyo mgonjwa ni mfano wa hali yetu ya kibinadamu yenye haja ya utakaso na kuponywa na Mungu. Kwanza kabisa tunapaswa kutambua kwamba sisi tu wagonjwa. Hatuwezi kumkaribia Mungu ikiwa hatukubali mapenzi yake kwetu. Yeye ndiye wa kwanza ambaye anataka kuondoa hali mbaya ya maisha yetu, lakini hawezi kutenda maishani mwetu ikiwa hatumruhusu. Uumbaji mpya ambao Yesu alitenda katika maisha ya mgonjwa wa ukoma unatendeka katika maisha yetu wakati mapenzi yetu ndiyo kulingana na mapenzi yake. Tunaalikwa kuamini kwamba Yesu ana hisia sana mbele ya hali ya wagonjwa kwa sababu hakuja kwa walio na afya nzuri bali kwa wagonjwa. Kama mtu yule mwenye ukoma, sisi pia tunahitaji mkutano na Yesu ambao ubadilishe maisha yetu kabisa. Kutokana na hisia yake tunaalikwa kushinda mawazo ya kijamii ambayo yaendelea kuwalaani ndugu wengi waishi kutengwa na kubaguliwa. kwa kumfuata Yesu kwa kweli tunapaswa kushiriki katika hisia zake kuhusu hali ya mateso ya ndugu hawa.  

             Kuhusu hayo, majira ya kihistoria yamejaa mifano ya watu ambao walikuwa na uwezo na ujasiri wa kutenda dhidi ya mawazo wa kijamii kuhusu wagonjwa na walio na mahitaji mengi. Mfano moja kati yao ndiye Mtakatifu Yohane Calabria. Mtu huyo anaweza kutusaidia kwa maisha yake mwenyewe. Kama mfano wa utunzaji wa Mungu, yeye alikuwa na hisia sana kwa hali ya wagonjwa. Alimwona Kristo mwenyewe katika walio wagonjwa. Alikuwa na mazoea ya kuwaimarisha kwa maneno ya kutia moyo na kutenda kwa ufanisi kwa ajili ya mwili wao. Alifikiria mateso ya wagonjwa kama msaada mkubwa kwa ajili ya mtume wa Kanisa. Aliwaimarisha na kuwashauri wagonjwa kuukaribisha ugonjwa na mateso kwa uvumilivu na sala. Kristo mwenyewe aliwapenda wagonjwa na wakati wa maisha yake alikwenda mara nyingi kuwatembelea na kuwaponya. Tunaalikwa kumkaribia Yesu na kuruhusu atuponye kutoka ugonjwa wetu wa kiroho ili tuwe mwenye hisia kuhusu hali ya walio wagonjwa wa kimwili.

Fr Ndega

Nenhum comentário: