sexta-feira, 24 de outubro de 2014

SISI NI KWA MUNGU



Kutafakari kutoka Is 45: 1,4-6; 1 Thes 1: 1-5; Mt 22: 15-22

Maandiko haya yanatualika kutafakari kuhusu hisia zetu za miliki ya Mungu kama wana wa watu wake na kutafakari pia kuhusu majukumu yetu na maendeleo ya Taifa la Kenya kupitia malipo ya kodi halali.
Somo la Kwanza ni tafsiri ya imani kuhusu ushindi wa Koreshi, mfalme wa Uajemi, ambaye aliwakomboa Wayahudi kutoka mamlaka ya Babeli. Kulingana na Isaya, ushindi wote wa Koreshi haukuwa uhalali wake, lakini ulikuwa tendo wa Mungu, ambaye alimchagua Koreshi kama mjumbe wake ili kufanya Jina la Bwana kujulikana kwa Mataifa yote, kuwaalika kwa imani katika Mungu mmoja tu. Kwa kweli Koreshi alipata kushinda Falme zote za Mashariki, ikiwa ni pamoja na Babeli, akiruhusu kwamba Wayahudi walirudi nyumbani na wakaishi utambulisho wao wa Watu wa Mungu na uhuru. Basi, kama ilivyotukia na Koreshi, Mungu anaweza kutumia mtu yeyote ili kufanya mipango yake.  
Paulo na wenzake wa uinjilishaji wanatambua Vipawa vya Mungu katika Jumuiya ya Wathesalonike, hasa fadhila za imani, upendo na tumaini, zinazowatambua kama wachaguliwa wa Mungu na mali yake. Katika maana hii, matendo yao yanafanywa chini ya neema ya Mungu, kulingana na Injili waliyoichukua kwa shauku. Uzoefu alioishi Paulo na Jumuiya hiyo na zengine ni kielelezo ili kufahamu bora uzoefu wa Jumuiya siku hizi.
Wapinzani wa Yesu wanamsifu kwa fadhila zake, lakini hawana nia kuwasilisha kwa hekima yake. Kulingana na wao, Yesu ni mtu wa kweli, anayefunza njia ya Mungu kwa mujibu na ukweli. Yesu ana maoni yake mwenyewe na kwa yeye mtu ni muhimu zaidi kuliko hali yake. Ingawa waliongea ukweli kuhusu Yesu, katika mazungumzu yao, inakosa imani ili kuukubali kama njia ya maisha yao. Yesu anatambua kwamba ni mazungumzu mabaya na lengo la kumnasa. Kama Yesu aliwaambia “ndio” kwa swali lao kuhusu malipo ya kodi, angechukuliwa mshirika wa utawala wa Warumi kwa Wayahudi. Ikiwa jibu lake likawa “hapana kwa malipo ya kodi” angechukuliwa mwasi. Basi, Yesu aliwaambia: “Mpeni Kaisari kilicho cha Kaisari na mpeni Mungu kilicho cha Mungu”. Jibu lake linasisitiza ukuu na kipaumbele cha Mungu juu ya wote na kila kitu.
Mahali pa kwanza katika maisha yetu ni kwa Mungu. Yeye ndiye mwenye nguvu kwa kila mtu, ikiwa ni pamoja na watawala. Sheria yake lazima iwe maarufu kwa sababu inaonyesha bora matarajio ya binadamu. Hata kama tunakabiliwa na Serikali na sheria yake, hawawezi kuchukua mahali Katika maisha yetu ambapo ni kwa Mungu na sheria ya binadamu haiwezi kuweka upinzani kwa Sheria ya Mungu. Mungu tu anastahili kuabudiwa na kutumikiwa. Hata hivyo, Yesu hakukataa umuhimu wa malipo ya  kodi halali, kwa sababu upendo kwa Mungu hautuzuii kushirikana na maendeleo ya nchi. Bali, kama Wakristu, kuchagua kwetu ni kwa uhai na kwa kila kitu kinachoshirikana na lengo hile.
Kupitia sherehe ya Eukaristia hii, tutengeneze upya ahadi yetu kama wana wa Mungu na miliki yake. Kupitia msukumo wake, tuwe mashahidi wake wa nguvu na uzuri katika mitazamo ya maendeleo ya haki na amani katika jamii.   

Fr. Ndega
Mapitio: Mwalimu Patrick

Nenhum comentário: