segunda-feira, 13 de outubro de 2014

JIRANI YANGU NI NANI?



Kutafakari kutoka Luka 10, 25-37

Sehemu ya kwanza ya injili hii inatukumbusha kuhusu andiko la mtu mmoja tajiri anayekuja kwa Yesu na swali sawa: Nifanye nini ili kupokea uzima wa milele? Jibu la Yesu linafanya kumbukumbu ya amri ya Sheria, kuonyesha kuwa yeye anathamini sana Mwelekeo huu kwa maisha. Yesu anapendekeza amri hizi kwa sababu haziende kinyume cha uhuru, lakini zinahusiana kwa hamu ya ndani ya binadamu katika kutafuta kwake kwa mafanikio ya binafsi. Kulingana na Yesu, amri si orodha ya sheria kukariri, lakini ni uongozi kwa kuishi vizuri, kumpenda Mungu na kukua katika udugu kupitia upendo halisi kwa jirani.
Swali: jirani yangu ni nani? linaonyesha kwamba kitu fulani si kizuri sana katika ufahamu wa amri. Labda mtu aliyeuliza swali kwa Yesu alidhani kwamba ukumbusho wa Sheria ulikuwa wa kutosha kwa kumsifu Mungu. Hali hio inaweza tukia pia na sisi kwa sababu, wakati mwingine, sisi hukaa na wasiwasi sana katika kutii sheria na sisi husahau muhimu zaidi katika uhusiano na watu wengine. Wakati tunauliza: jirani yetu ni nani?, kumbukumbu ni daima sisi wenyewe na uradhi wa mahitaji yetu. Lakini mfano ambao Yesu anaongea kuhusu unaweka kumbukumbu nje yetu, unabadili swali: unawezaje kuwa jirani kwa wengine?
Kuwa jirani si rahisi sana kwa sababu tuna shughuli daima na kufanya vitu kwa haraka. Tulivyo na shughuli ndivyo tuna upunguvu wa uwezo kujali mahitaji ya wengine. Ni lazima tubadilishe mawazo yetu na kukaribisha mfano wa Yesu ambaye ni Msamaria Mwema kwa ubora. Yeye anatufundisha kwamba uzima wa milele unawezekana tu kama upendo kwa Mungu unaishiwa mazoea ya upendo kwa wengine. Kwa Yesu, upendo ni halisi na kweli wakati unaeleza kupitia ishara za upole na huruma. Kanuni ya kawaida kuishi vizuri katika maisha ya shirika katika kazi ni sisi wenyewe kutumika bora kwa wema wa wengine, kusaidia katika mahitaji yao, kwenda mbele ya mpango imara.
Yesu anajitambulisha na wale ambao "wameanguka kando ya njia". Je, tunaweza kutambua uwepo wake katika watu ambao kwa kawaida hukutana nao? Jinsi gani tunaitikia mahitaji ya wengine wakati tuna haraka?
"Ee Bwana, fungua macho yetu ili kuona mahitaji ya ndugu zetu. Tuhamasishe maneno na vitendo katika huduma kwao". Amina.

Fr. Ndega
Mapitio: Mwalimu Patrick

Nenhum comentário: