sábado, 19 de outubro de 2019

KUSALI KWA NJIA KAMILI



Kutafakari kuhusu Lk 18, 1-8

                                       
       Uwepo wa Yesu ni mahali maalum pa mkutano kati ya Mungu na binadamu. Mara nyingi yeye hukutana na Baba yake kwa mazungumzo ya ndani akiwapa watu mfano wa sala ya kweli na yule ambaye anajua kila kitu na ndiye makini daima kwa maombi ya wanao. Tunapoimba: Baba, sikia wanao, sikia sauti zao, sikia dunia nzima”, tunataka kumaanisha kwamba Mungu ni Baba na kutarajia tuweze kumhutubia sala zetu kwa imani kama wenye uhakika kwamba tumepokea sana. Basi, Yesu aliwafundisha wafuasi wake wafanye kama Yeye alivyo, yaani, kusali daima bila kukata tamaa kamwe. Ili wafuasi wake wafahamu vizuri mahitaji haya alisimulia mfano mmoja kulingana na ufundishaji wake wa ajabu.

       Hakimu mmoja wakati wa muda mrefu alikataa kumsikiliza ombi la mama mjane dhidi ya adui yake na hatimaye alimsikiliza kwa sababu ya kusisitiza kwake. Mfano wa mama huyo ni lazima kuwa rejeo kwa maombi yetu. Mama huyo alikuwa na hakika kwamba yule hakimu akawa na uwezo wa kumtetea kwa hivyo alikuwa na uvumilivu kuhusu ombi lake. Mama huyo anatujulisha kipimo ili kufikia mafanikio katika mpango wowote hasa kuhusu uzoefu wa sala.

     Kuna hamu falani ndani yetu ambayo inatuvutia kwa Mungu. Kupitia hamu hii tunatambua kwamba maana ya maisha ni kukutana naye, kulishwa na uhai wake na kuongozwa naye kwa sababu bila yeye hatuwezi kufanya chochote. Ikiwa Mungu anachelewa kuhusu dua zetu ni kwa sababu wakati wake ni tofauti na wetu. Kulingana na kifungu cha nabii Isaya (55, 6.8), tunaalikwa kumtafuta Mungu daima kwa sababu anapatikana naye yupo karibu. Changamoto kwetu ni kusali na kusubiri kulingana na wakati na njia za Mungu.

       Basi, kusali ni uzoefu wa ndani; ni kumhisi Mungu karibu sana nasi, kwa kuongea kwa masikio yetu kila siku na siku zote. Kusali ni mazungumzo na Mungu, kwa kutumia muda wa ubora kuliko wa kiasi. Tunaposali kwa kweli tunahisi kwamba vitu vingi huanza kubadilisha ndani yetu na tunapata mtazamo tofauti kuhusu hali kandokando yetu. Ingawa hali hii inaendelea kwa ugumu wake na changamoto zake, mtazamo na tabia yetu itakuwa tofauti kwa sababu tunaimarishwa sio na udhaifu wetu bali na nguvu ya yule ambaye ana mazoea ya kubadilisha hali mbaya ili iwe hali mzuri na hali ya mauti ili iwe ya uzima.

        Pamoja na shauri kuhusu mahitaji ya kusali daima Yesu alitupa sala yake mwenyewe, sala iliye na yaliyomo ya mazungumzo yake na Baba, yaani Baba Yetu. Sala hii tafsiri hisia za wana ambao wanatambua ukuu na ukaribu wa Baba yao na kwa hivyo wana uhusiano wa ndani naye. Kwao sala si sharti, bali mahitaji ambayo yanatokana na ndani yao. Kwao sala ni uhusiano wa upendo kwa sababu wanapata kujiona wapendwa. Wanapenda kufanya kama mwalimu wao ambaye alisali kutokana na moyo kwa moyo.

        Labda tunahitaji tabia hii kamili kwa sababu tunamwomba Baba mmoja aliye mwema na kujua mahitaji yetu. Ana macho na masikio yenye hisia kuhusu kile kinachotokea nasi na yupo tayari daima ya kututendea mema kwa sababu pia hiyo ni njia yake. Kwa upande wetu tuwe na imani zaidi na kujisalimisha kabisa mikononi mwake kama Mwanao wa pekee. Katika sala aliyotufundisha tunasali si kwa mahitaji yetu tu, bali kwa mahitaji ya wote. Hivyo, ikiwa tunasema “Baba Yetu” ni kwa sababu tunasadiki kwamba sisi ni ndugu wa wengine wengi.

      Mungu hawabagui watu wala kusahau yeyote wa wana wake. Hapendezwi na sala ambayo haifikirii ndugu wengine. Mungu hatupatii daima vitu ambavyo tunamwomba, bali anatupatia daima vitu ambavyo tunahitaji. Ikiwa mara nyingi hatupokei vitu ambavyo tunamwomba ni kwa sababu hatuombi ipasavyo. Labda tunashindwa kuwa na tabia na nia kamili zilizodaiwa na Yesu wakati aliwafundisha wafuasi wake kusali... Mfano wa mama mjane uwe utuimarishe kuanza tena kusali kwa njia kamili.

Fr Ndega

Nenhum comentário: