segunda-feira, 9 de fevereiro de 2015

UHITAJI WA MAFUNDISHO MAPYA

Kutafakari kutoka Kumbukumbu la Sheria 18: 15-20; 1Wak 7: 32-35; Marko 1: 21-28

Masomo haya ni mwaliko kwa sisi sote kukaribisha mafundisho ya Neno la Mungu ambalo lina uwezo wa kubadili maisha ya watu, kuwapa uwezo ili kuwa wajumbe wa wakati mpya. Kulingana na Somo la Kwanza, nabii ni mtu aliyeitwa kutoka kati ya watu ili kuongea nao tu ambayo Mungu anamwuliza kusema. Msukumu wa Mungu, pamoja na upatikanaji wa nabii, ulifanya utofauti mkubwa katika maisha ya watu wa Israeli, ukiwaongoza kupitia maisha mapya. Mtakatifu Paulo anasifu mtu anayejituma kwa huduma ya Bwana na anawamotisha wengine wote wa jumuiya kuendelea kumtumikia kwa kujisalimisha kabisa bila rizavu.

Yesu anaanza kazi yake kwa umma kutangaza Ufalme wa Mungu na kuwaalika kwa kitubio. Kama hii, aliwaita wanafunzi wa kwanza, kulingana na kutafakari kwetu wiki iliyopita. Yesu anawaalika wanafunzi wake kukaa pamoja naye na anawafundisha kupitia uzoefu wa maisha. Sehemu nyingi ya miujiza ambayo yeye hufanya, yeye anafanya mbele ya wanafunzi wake. Tangu mwanzo, wanafunzi wake wamealikwa kushiriki katika kazi yake na kushiriki hisia zake kuhusu hali halisi ya watu, hasa hao maskini. Yesu hupenda kutembelea na kufundisha katika masinagogi kwa sababu katika mahali hapo kwa kawaida watu husanyika kusikiliza Neno la Mungu na kukubali mapenzi yake. Hali hii ilikuwa pia nafasi nzuri kuwafundisha wanafunzi wake, kuwasaidia watu kufungua mioyo kwa mapitio ya Mungu.

Mamlaka yaliyopewa Yesu na Baba mwenyewe yanaonyesha ubora wa mafundisho yake kabla ya njia ya mwandishi. Kidogo kidogo watu walikuwa wakielewa kwamba mtu huyo Yesu, ambaye alizungumza kwa upendo na ukweli, alikuwa mjumbe wa Mungu. Maneno yake yenye uhai kabisa na yanaongoza kwa kitubio. Njia yake ya kuzungumza ilizaa katika moyo shauku kwa ajili ya Ufalme. Kama mjumbe wa Mungu, yeye ni wa kipekee na mamlaka ya kufundisha watu. Wale ambao wana kazi ya kuongoza watu, lazima kusikiliza sauti yake. Hata pepo wachafu wanatambua utambulisho na mamlaka ya Yesu, lakini hawashiriki ahadi yake kwa ajili ya ubinadamu. Kwa hivyo, Yesu hazungumzi nao; yeye tu anawamuru, kuwanyamazisha. Pepo wachafu hawa ni ishara ya nguvu za upinzani kwa mpango wa Mungu, kudhoofisha watu na kuwazuia kuonyesha uwezo wao kwa njia kamili. Kabla ya nguvu hizi, Yesu anaweka mamlaka na anatenda kama Mkombozi.

Uwepo wa Yesu kati ya binadamu unatawaza wakati mpya, ni kwamba, wakati wa wokovu wa Mungu. Wokovu uliowasilihswa kupitia kinywa cha Yesu kinaongozwa na ishara halisi ya ukombozi. Kulingana na matendo ya Yesu, nguvu ya Neno la Mungu haitoki kwa tafsiri ya binadamu, lakini inatoka kwa msukumu wa Mungu. Kwa hivyo mafundisho yake yanachukuliwa mapya sana. Lakini haitoshi kutambua utambulisho wa Yesu kama Masihi wa Mungu, kwa sababu hata pepo wachafu wanafanya hivyo. Ni muhimu kukubali pendekezo lake la kitubio, kuruhusu uwezo wake kuondoa pingu ambayo inatuzuia kufanya uhusiano mzuri na Mungu na wengine. Upinzani dhidi ya Yesu ni upinzani kwa utambuzi wa Ufalme wa Mungu. Kwa hali hii, tunatenda kama wapinzani wa Mungu, kutoweza kufuata kwa uaminifu nyayo za Mwana wake ambaye, wakati anatangaza habari njema ya Ufalme, anauliza kwa ushiriki wa bure na jumla ya kila mtu. Kwa upande wetu, kutafuta Ufalme huu lazima uwe kipaumbele, kwa sababu juu yake maana ya maisha na kazi zetu huweka.


Ujumbe wa injili hii ni pendekezo la uanafunzi upya. Ni mwaliko kwa sisi kupitia uwezo wetu wa kujisalimisha kwa mtu ambaye ametuita na anataka kwamba tuwe wajumbe wake. Yeye anatambua mwenyewe na wale waliomfuata yeye, Yesu anaendelea kutenda dhidi ya nguvu yoyote au mawazo ambayo yanaonea maisha ya watu. Kwa maneno mengine, kupitia matendo yetu, ishara za ukombozi wa Kristo bado zinatokea katika maisha ya watu wengi. Kutoka kwake tunapokea mamlaka kuwa watu halisi ili kusema ukweli. Hakika kwamba Yesu anaambatana nasi katika safari yetu, inatumotisha kupigana dhidi ya maovu na dhambi zote ambazo zinatuzuia kumtumikia Mungu kwa ukarimu na bure. Neema yake itusaidie kufanya kusudi hili.

Fr. Ndega
Mapitio: Mwalimu Patrick 

Nenhum comentário: